< Nahum 1 >

1 The burden of Nineueh. The booke of the vision of Nahum the Elkeshite.
Maono kuhusu Ninawi. Kitabu cha maono ya Nahumu, Mwelkoshi.
2 God is ielous, and the Lord reuengeth: the Lord reuengeth: euen the Lord of anger, the Lord will take vengeance on his aduersaries, and he reserueth wrath for his enemies.
Yehova ni Mungu mwenye wivu na analipa kisasi; Yehova hulipa kisasi na amejaa ghadhabu; Yohova analipiza kisasi kwa adui zake, na huiendeleza hasira yake kwa adui zake.
3 The Lord is slow to anger, but he is great in power, and will not surely cleare the wicked: the Lord hath his way in ye whirlewind, and in the storme, and the cloudes are the dust of his feete.
Yehova ni mwenye nguvu nyingi na mpole wa hasira; hatakuwa na namna ya kuacha kuwahesabia hatia adui zake. Yehova hufanya njia yake kwenye upepo wa kisulisuli na dhoruba, na mawingu ni mavumbi ya miguu yake.
4 He rebuketh the sea, and dryeth it, and he dryeth vp all the riuers: Bashan is wasted and Carmel, and the floure of Lebanon is wasted.
Huikemea bahari na kuifanya ikauke; hukausha mito yote. Bashani ni dhaifu, na Karmeli pia; maua ya Lebanoni ni dhaifu.
5 The mountaines tremble for him, and the hilles melt, and the earth is burnt at his sight, yea, the worlde, and all that dwell therein.
Milima hutetema kwenye uwepo wake, na vilima huyeyuka; dunia huanguka mbele zake, kabisa, dunia na watu wote wanaoishi ndani yake.
6 Who can stande before his wrath? or who can abide in the fiercenesse of his wrath? his wrath is powred out like fire, and the rockes are broken by him.
Ni nani anaweza kusimama mbele ya ghadhabu yake? Nani anaweza kuzuia ukali wa hasira yake? Ghadhabu yake imemwagwa kama moto, na miamba ameibomoa mbalimbali.
7 The Lord is good and as a strong hold in the day of trouble, and he knoweth them that trust in him.
Yehova ni mwema, boma katika siku ya taabu; na yeye ni mwaminifu kwa wale wanaomkimbilia.
8 But passing ouer as with a flood, he will vtterly destroy the place thereof, and darknesse shall pursue his enemies.
Lakini atafanya mwisho wa adui zake kwa mafuriko ya kutisha; atawawinda kwenye giza.
9 What doe ye imagine against the Lord? he wil make an vtter destruction: affliction shall not rise vp the seconde time.
Watu wanapanga nini dhidi ya Yehova? Yeye atakomesha; taabu haitainuka mara ya pili.
10 For he shall come as vnto thornes folden one in another, and as vnto drunkards in their drunkennesse: they shall be deuoured as stubble fully dryed.
Maana watakuwa wamevurugika kama michongoma; wataloweshwa katika kinywaji chao mwenyewe; wataharibiwa kabisa kwa moto kama mashina ya mabua.
11 There commeth one out of thee that imagineth euill against the Lord, euen a wicked counsellour.
Mtu mmoja aliinuka miongoni mwenu, Ninawi, aliyepanga ubaya dhidi ya Yehova, mtu ambaye aliimarisha uovu.
12 Thus saith the Lord, Though they be quiet, and also many, yet thus shall they be cut off when he shall passe by: though I haue afflicted thee, I will afflict thee no more.
Hivi ndivyo anavyosema Yehova, “Hata kama wananguvu zao timilifu na idadi timilifu, hata hivyo watanyolewa, watu wao hawatakuwepo tena. Bali wewe, Yuda: Ingawa nimekutesa, sitakutesa tena.
13 For nowe I will breake his yoke from thee, and will burst thy bonds in sunder.
Sasa nitaivunja ile nira ya watu kutoka kwako; nitaikata minyororo yako.
14 And the Lord hath giuen a commandement concerning thee, that no more of thy name be sowen: out of the house of thy gods will I cut off the grauen, and the molten image: I will make it thy graue for thee, for thou art vile.
Yehova ametoa amri juu yako, Ninawi: “Hakutakuwa na kizazi tena chenye kubeba jina lako. Nitazizuia sanamu zilizochongwa na kuziondoa sanamu za chuma kutoka kwenye nyumba za miungu yenu. Nitachimba makaburi yenu, kwa kudharauliwa kwenu.”
15 Beholde vpon the mountaines the feete of him that declareth, and publisheth peace: O Iudah, keepe thy solemne feastes, perfourme thy vowes: for the wicked shall no more passe thorowe thee: he is vtterly cut off.
Tazama, juu ya milima kuna miguu ya mtu aletaye habari njema, anayetangaza amani! Sherehekeeni sikukuu zenu, Yuda, na tunzeni nadhiri zenu, kwa maana mwovu hatawavamia tena; ameondolewa kabisa.

< Nahum 1 >