< Matthew 6 >
1 Take heede that ye giue not your almes before men, to be seene of them, or els ye shall haue no reward of your Father which is in heaue.
Zingatia kutotenda matendo ya haki mbele ya watu ili kujionyesha, vinginevyo hutapata thawabu kutoka kwa Baba aliye mbinguni.
2 Therefore when thou giuest thine almes, thou shalt not make a trumpet to be blowen before thee, as the hypocrites doe in the Synagogues and in the streetes, to be praysed of men. Verely I say vnto you, they haue their rewarde.
Hivyo basi unapotoa usipige tarumbeta na kujisifu mwenyewe kama wanafiki wanavyofanya katika masinagogi na katika mitaa, ili kwamba watu wawasifu. Kweli nawaambia, wamekwisha kupokea thawabu yao.
3 But when thou doest thine almes, let not thy left hand knowe what thy right hand doeth,
Lakini wewe unapotoa, mkono wako wa kushoto usijue kinachofanywa na mkono wa kulia,
4 That thine almes may be in secret, and thy Father that seeth in secret, hee will rewarde thee openly.
ili kwamba zawadi yako itolewe kwa siri. Ndipo Baba yako aonaye sirini atakupatia thawabu yako.
5 And when thou prayest, be not as the hypocrites: for they loue to stand, and pray in the Synagogues, and in the corners of the streetes, because they would be seene of men. Verely I say vnto you, they haue their rewarde.
Na unapokuwa ukiomba, usiwe kama wanafiki, kwa kuwa wanapenda kusimama na kuomba kwenye masinagogi na kwenye kona za mitaani, ili kwamba watu wawatazame. Kweli nawaambia, wamekwishapokea thawabu yao.
6 But when thou prayest, enter into thy chamber and when thou hast shut thy doore, pray vnto thy Father which is in secret, and thy Father which seeth in secret, shall rewarde thee openly.
Lakini wewe, unapo omba, ingia chumbani. Funga mlango, na uombe kwa kwa Baba yako aliye sirini. Ndipo Baba yako aonaye sirini atakupatia thawabu yako.
7 Also when ye pray, vse no vaine repetitions as the Heathen: for they thinke to be heard for their much babbling.
Na unapokuwa ukiomba, usirudie rudie maneno yasiyo na maana kama mataifa wanavyofanya, kwa kuwa wanafikiri kwamba watasikiwa kwa sababu ya maneno mengi wanayosema.
8 Be ye not like them therefore: for your Father knoweth whereof ye haue neede, before ye aske of him.
Kwa hiyo, usiwe kama wao, kwa kuwa Baba yako anatambua mahitaji yako hata kabla hujaomba kwake.
9 After this maner therefore pray ye, Our father which art in heauen, halowed be thy name.
Hivyo basi omba hivi: Baba yetu uliye mbinguni, ulitukuze jina lako.
10 Thy Kingdome come. Thy will be done euen in earth, as it is in heauen.
Ufalme wako uje, mapenzi yako yafanyike hapa duniani kama huko mbinguni.
11 Giue vs this day our dayly bread.
Utupatiye leo mkate wetu wa kila siku.
12 And forgiue vs our dettes, as we also forgiue our detters.
utusamehe deni zetu, kama nasi tunavyowasamehe wadeni wetu.
13 And leade vs not into tentation, but deliuer vs from euill: for thine is the kingdome, and the power, and the glorie for euer. Amen.
Na usitulete katika majaribu, lakini utuepushe kutoka kwa yule mwovu.'
14 For if ye doe forgiue men their trespasses, your heauenly Father will also forgiue you.
Ikiwa mtawasemehe watu makosa yao, Baba yako aliye mbinguni pia atawasamehe ninyi.
15 But if ye do not forgiue men their trespasses, no more will your father forgiue you your trespaces.
Lakini ikiwa hamtawasamehe makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe makosa yenu.
16 Moreouer, when ye fast, looke not sowre as the hypocrites: for they disfigure their faces, that they might seeme vnto men to fast. Verely I say vnto you, that they haue their rewarde.
Zaidi ya yote, unapokuwa umefunga, usioneshe sura ya huzuni kama wanafiki wanavyofanya, kwa kuwa wanakunja sura zao ili kwamba watu wawatambue wamefunga. Kweli ninakuambia, wamekwisha kupokea thawabu yao.
17 But when thou fastest, anoint thine head, and wash thy face,
Lakini wewe, unapokuwa umefunga, paka mafuta kichwa chako na uoshe uso wako.
18 That thou seeme not vnto men to fast, but vnto thy Father which is in secret: and thy Father which seeth in secret, will rewarde thee openly.
Hivyo haitakuonesha mbele ya watu kuwa umefunga, lakini tu itakuwa kwa Baba yako aliye sirini. Na Baba yako aonaye sirini, atakupa thawabu yako.
19 Lay not vp treasures for your selues vpon the earth, where the mothe and canker corrupt, and where theeues digge through and steale.
Usijitunzie hazina yako mwenyewe hapa duniani, ambapo nondo na kutu huharibu, ambapo wezi huvunja na kuiba.
20 But lay vp treasures for your selues in heauen, where neither the mothe nor canker corrupteth, and where theeues neither digge through, nor steale.
Badala yake, jitunzie hazina yako mwenyewe mbinguni, ambapo wala nondo wala kutu hawezi kuharibu, na ambapo wezi hawawezi kuvunja na kuiba.
21 For where your treasure is, there will your heart be also.
Kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo na moyo wako utakapokuwepo pia.
22 The light of the body is the eye: if then thine eye be single, thy whole body shall be light.
Jicho ni taa ya mwili. Kwa hiyo, ikiwa jicho lako ni zima, mwili wote utajazwa na nuru.
23 But if thine eye be wicked, then all thy body shalbe darke. Wherefore if the light that is in thee, be darkenes, howe great is that darkenesse?
Lakini ikiwa jicho lako ni bovu, mwili wako wote umejaa giza totoro. Kwahiyo, ikiwa nuru ambayo imo ndani yako ni giza hasa, ni giza kubwa kiasi gani!
24 No man can serue two masters: for eyther he shall hate the one, and loue the other, or els he shall leane to the one, and despise the other. Ye cannot serue God and riches.
Hakuna hata mmoja anayeweza kuwatumikia mabwana wawili, kwa kuwa atamchukia mmoja na kumpenda mwingine, au la sivyo atajitoa kwa mmoja na kumdharau mwingine. Hamuwezi kumtumikia Mungu na mali.
25 Therefore I say vnto you, be not carefull for your life, what ye shall eate, or what ye shall drinke: nor yet for your body, what ye shall put on. Is not the life more worth then meate? and the bodie then raiment?
Kwa hiyo nakuambia, usiwe na mashaka kuhusu maisha yako, kuwa utakula nini au utakunywa nini, au kuhusu mwili wako, utavaa nini. Je! Maisha si zaidi ya chakula na mwili zaidi ya mavazi?
26 Behold the foules of the heauen: for they sowe not, neither reape, nor carie into the barnes: yet your heauenly Father feedeth them. Are ye not much better then they?
Tazama ndege walioko angani. Hawapandi na hawavuni na hawakusanyi na kutunza ghalani, lakini Baba yenu wa mbinguni huwalisha wao. Je ninyi si wa thamani zaidi kuliko wao?
27 Which of you by taking care is able to adde one cubite vnto his stature?
Na ni nani miongoni mwenu kwa kujihangaisha anaweza kuongeza dhiraa moja kwenye uhai wa maisha yake?
28 And why care ye for raiment? Learne howe the lilies of the fielde doe growe: they are not wearied, neither spinne:
Na kwa nini mna kuwa na wasiwasi kuhusu mavazi? Fikiria kuhusu maua kwenye mashamba, jinsi yanavyokua. Hayafanyi kazi na hayawezi kujivisha.
29 Yet I say vnto you, that euen Salomon in all his glorie was not arayed like one of these.
Bado ninawaambia, hata Sulemani katika utukufu wake wote hakuvikwa kama mojawapo ya haya.
30 Wherefore if God so clothe the grasse of the fielde which is to day, and to morowe is cast into the ouen, shall he not doe much more vnto you, O ye of litle faith?
Ikiwa Mungu anayavalisha majani katika mashamba, ambayo yadumu siku moja na kesho yanatupwa katika moto, je ni kwa kiasi gani atawavalisha ninyi, ninyi wenye imani ndogo?
31 Therefore take no thought, saying, What shall we eate? or what shall we drinke? or where with shall we be clothed?
Kwa hiyo msiwe na wasiwasi nakusema, 'Je tutakula nini?' au “Je tutakunywa nini?” au “Je tutavaa nguo gani?”
32 (For after all these things seeke the Gentiles) for your heauenly Father knoweth, that ye haue neede of all these things.
Kwa kuwa mataifa wanatafuta mambo haya, na Baba yenu wa mbinguni anajua kuwa mnahitaji hayo.
33 But seeke ye first the kingdome of God, and his righteousnesse, and all these things shall be ministred vnto you.
Lakini kwanza tafuteni ufalme wake na haki yake na haya yote yatakabidhiwa kwako.
34 Care not then for the morowe: for the morowe shall care for it selfe: the day hath ynough with his owne griefe.
Kwa hiyo, usione shaka kwa ajili ya kesho, kwa kuwa kesho itajishughulikia yenyewe. Kila siku inatosha kuwa na tatizo lake yenyewe.