< Matthew 4 >

1 Then was Iesus led aside of the Spirit into the wildernes, to be tempted of the deuil.
Kisha Yesu akaongozwa na Roho Mtakatifu kwenda nyikani ili akajaribiwe na ibilisi.
2 And when he had fasted fourtie dayes, and fourtie nights, he was afterward hungrie.
Baada ya kufunga siku arobaini usiku na mchana, hatimaye akaona njaa.
3 Then came to him the tempter, and said, If thou be the Sonne of God, commande that these stones be made bread.
Mjaribu akamjia na kumwambia, “Ikiwa wewe ndiye Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yawe mikate.”
4 But he answering said, It is written, Man shall not liue by bread onely, but by euery worde that proceedeth out of the mouth of God.
Lakini Yesu akajibu, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.’”
5 Then the deuil tooke him vp into the holy Citie, and set him on a pinacle of the temple,
Ndipo ibilisi akamchukua Yesu mpaka mji mtakatifu na kumweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu,
6 And said vnto him, If thou be the Sonne of God, cast thy selfe downe: for it is written, that he wil giue his Angels charge ouer thee, and with their hands they shall lift thee vp, lest at any time thou shouldest dash thy foote against a stone.
akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini. Kwa kuwa imeandikwa: “‘Atakuagizia malaika zake, nao watakuchukua mikononi mwao ili usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’”
7 Iesus saide vnto him, It is written againe, Thou shalt not tempt the Lord thy God.
Yesu akamjibu, “Pia imeandikwa: ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”
8 Againe the deuil tooke him vp into an exceeding hie mountaine, and shewed him all the kingdomes of the world, and the glory of them,
Kwa mara nyingine, ibilisi akamchukua Yesu mpaka kwenye kilele cha mlima mrefu na kumwonyesha falme zote za dunia na fahari zake,
9 And sayd to him, All these will I giue thee, if thou wilt fall downe, and worship me.
kisha akamwambia, “Nitakupa hivi vyote kama ukinisujudia na kuniabudu.”
10 Then sayd Iesus vnto him, Auoyde Satan: for it is written, Thou shalt worship the Lord thy God, and him onely shalt thou serue.
Yesu akamwambia, “Ondoka mbele yangu, Shetani! Kwa maana imeandikwa, ‘Mwabudu Bwana Mungu wako, na umtumikie yeye peke yake.’”
11 Then the deuill left him: and beholde, the Angels came, and ministred vnto him.
Ndipo ibilisi akamwacha, nao malaika wakaja na kumhudumia.
12 And when Iesus had heard that Iohn was committed to prison, he returned into Galile.
Yesu aliposikia kwamba Yohana Mbatizaji alikuwa ametiwa gerezani, alirudi Galilaya.
13 And leauing Nazareth, went and dwelt in Capernaum, which is neere the sea in the borders of Zabulon and Nephthalim,
Akaondoka Nazareti akaenda kuishi Kapernaumu, mji ulioko karibu na bahari, katika mipaka ya nchi ya Zabuloni na Naftali,
14 That it might be fulfilled which was spoken by Esaias the Propet, saying,
ili kutimiza unabii wa nabii Isaya, kama alivyosema:
15 The land of Zabulon, and the land of Nephthalim by the way of the sea, beyond Iordan, Galile of the Gentiles:
“Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, kwenye njia ya kuelekea baharini, ngʼambo ya Yordani, Galilaya ya watu wa Mataifa:
16 The people which sate in darkenes, sawe great light: and to them which sate in the region, and shadowe of death, light is risen vp.
watu wale waliokaa gizani wameona nuru kuu; nao wale walioishi katika nchi ya uvuli wa mauti, nuru imewazukia.”
17 From that time Iesus began to preach, and to say, Amende your liues: for the kingdome of heauen is at hand.
Tangu wakati huo, Yesu alianza kuhubiri akisema: “Tubuni, kwa maana Ufalme wa Mbinguni umekaribia.”
18 And Iesus walking by the sea of Galile, sawe two brethren, Simon, which was called Peter, and Andrew his brother, casting a net into the sea (for they were fishers.)
Yesu alipokuwa anatembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea ndugu yake. Walikuwa wakizitupa nyavu zao baharini kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
19 And he sayd vnto them, Follow me, and I will make you fishers of men.
Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
20 And they straightway leauing the nets, folowed him.
Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
21 And when he was gone forth from thence, he saw other two brethren, Iames the sonne of Zebedeus, and Iohn his brother in a ship with Zebedeus their father, mending their nets, and he called them.
Alipoendelea mbele kutoka pale, akawaona ndugu wengine wawili, Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa wamekaa kwenye mashua pamoja na baba yao Zebedayo, wakizitengeneza nyavu zao. Yesu akawaita.
22 And they without tarying, leauing the ship, and their father, folowed him.
Nao mara wakaiacha mashua yao, pamoja na baba yao, wakamfuata.
23 So Iesus went about all Galile, teaching in their Synagogues, and preaching the Gospel of the kingdome, and healing euery sicknesse and euery disease among the people.
Yesu akapita katika Galilaya yote, akifundisha katika masinagogi yao, akihubiri habari njema za Ufalme, na akiponya kila ugonjwa na kila aina ya maradhi miongoni mwa watu.
24 And his fame spread abroad through all Syria: and they brought vnto him all sicke people, that were taken with diuers diseases and torments, and them that were possessed with deuils, and those which were lunatike, and those that had the palsey: and he healed them.
Kwa hiyo sifa zake zikaenea sehemu zote za Shamu, nao watu wakamletea wote waliokuwa na magonjwa mbalimbali na maumivu, waliopagawa na pepo wachafu, wenye kifafa na waliopooza, naye akawaponya.
25 And there folowed him great multitudes out of Galile, and Decapolis, and Hierusalem, and Iudea, and from beyond Iordan.
Makutano makubwa ya watu yakawa yanamjia kutoka Galilaya, Dekapoli, Yerusalemu, Uyahudi na kutoka ngʼambo ya Mto Yordani.

< Matthew 4 >