< Matthew 27 >
1 When the morning was come, all the chiefe Priests, and the elders of the people tooke counsell against Iesus, to put him to death,
Muda wa asubuhi ulipofika, wakuu wote wa makuhani na wazee wa watu walikula njama dhidi ya Yesu wapate kumuua.
2 And led him away bounde, and deliuered him vnto Pontius Pilate the gouernour.
Walimfunga, walimwongoza, na kumfikisha kwa Liwali Pilato.
3 Then when Iudas which betraied him, sawe that hee was condemned, hee repented himselfe, and brought againe the thirtie pieces of siluer to the chiefe Priestes, and Elders,
Kisha wakati Yuda, ambaye alikuwa amemsaliti, aliona kwamba Yesu amekwisha kuhukumiwa, alijuta na kurudisha vipande thelathini vya fedha kwa mkuu wa makuhani na wazee,
4 Saying, I haue sinned, betraying the innocent bloud. But they sayde, What is that to vs? see thou to it.
na akasema, “Nimefanya dhambi kwa kuisaliti damu isiyo na hatia.” Lakini wakajibu, “Inatuhusu nini sisi? Yaangalie hayo mwenyewe.”
5 And when hee had cast downe the siluer pieces in the Temple, hee departed, and went, and hanged himselfe.
Kisha alivirusha chini vile vipande vya fedha katika hekalu, na kuondoka zake na kujinyonga mwenyewe.
6 And the chiefe Priestes tooke the siluer pieces, and sayde, It is not lawfull for vs to put them into the treasure, because it is the price of bloud.
Mkuu wa makuhani alivichukua vile vipande vya fedha na kusema, “Si halali kuiweka fedha hii katika hazina, kwa sababu ni gharama ya damu.”
7 And they tooke counsell, and bought with them a potters fielde, for the buriall of strangers.
Walijadiliana kwa pamoja na fedha ikatumika kununulia shamba la mfinyazi la kuzika wageni.
8 Wherefore that field is called, The field of bloud, vntill this day.
Kwa sababu hii shamba hilo limekuwa likiitwa, “Shamba la damu” hadi leo hii.
9 (Then was fulfilled that which was spoken by Ieremias the Prophet, saying, And they tooke thirtie siluer pieces, ye price of him that was valued, whom they of ye children of Israel valued.
Kisha lile neno lililokuwa limenenwa na nabii Yeremia lilitimia, kusema, “Walitwaa vipande thelathini vya fedha, gharama iliyopangwa na watu wa Israel kwa ajili yake,
10 And they gaue them for the potters fielde, as the Lord appointed me.)
na waliitumia kwa shamba la mfinyanzi, kama Bwana alivyokuwa amenielekeza.”
11 And Iesus stood before ye gouernour, and the gouernour asked him, saying, Art thou that King of the Iewes? Iesus said vnto him, Thou sayest it.
Sasa Yesu alisimama mbele ya liwali, na liwali akamwuliza, “Je! Wewe ni mfalme wa Wayahudi?” Yesu alimjibu, “Wewe wasema hivyo.”
12 And when he was accused of the chiefe Priestes, and Elders, he answered nothing.
Lakini wakati aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu chochote.
13 Then saide Pilate vnto him, Hearest thou not howe many things they lay against thee?
Kisha Pilato alimwambia, “Hujayasikia mashitaka yote dhidi yako?”
14 But he answered him not to one worde, in so much that the gouernour marueiled greatly.
Lakini hakumjibu hata neno moja, hivyo liwali alijawa na mshangao.
15 Nowe at the feast, the gouernour was wont to deliuer vnto the people a prisoner whom they would.
Sasa katika sikukuu ilikuwa desturi ya liwali kumfungua mfungwa mmoja anayechaguliwa na umati.
16 And they had then a notable prisoner, called Barabbas.
Wakati huo walikuwa na mfungwa sugu jina lake Baraba.
17 When they were then gathered together, Pilate said vnto the, Whether will ye that I let loose vnto you Barabbas, or Iesus which is called Christ?
Hivyo wakati walipokuwa wamekusanyika pamoja, Pilato aliwauliza, “Ni nani mnataka tumfungue kwa ajili yenu?” Baraba au Yesu anayeitwa Kristo?”
18 (For he knewe well, that for enuie they had deliuered him.
Kwa sababu alijua kwamba wamekwisha kumkamata kwa sababu ya chuki.
19 Also when he was set downe vpon the iudgement seate, his wife sent to him, saying, Haue thou nothing to do with that iust man: for I haue suffered many things this day in a dreame by reason of him.)
Wakati alipokuwa akiketi kwenye kiti chake cha hukumu, mke wake alimtumia neno na kusema, “Usitende jambo lolote kwa mtu huyo asiye na hatia. Kwani nimeteswa mno hata leo katika ndoto kwa sababu yake.”
20 But the chiefe Priestes and the Elders had persuaded the people that they shoulde aske Barabbas, and should destroy Iesus.
Ndipo wakuu wa makuhani na wazee waliwashawishi makutano wamwombe Baraba, na Yesu auawe.
21 Then the gouernour answered, and said vnto them, Whether of the twaine will ye that I let loose vnto you? And they said, Barabbas.
Liwali aliwauliza, “Ni yupi kati ya wawili mnataka mimi nimwachie kwenu?” Walisema, “Baraba.”
22 Pilate said vnto them, What shall I do then with Iesus, which is called Christ? They all said to him, Let him be crucified.
Pilato akawaambia, “Nimtendee nini Yesu anayeitwa Kristo?” Wote wakajibu, “Msulibishe”
23 Then saide the gouernour, But what euill hath he done? Then they cryed the more, saying, Let him be crucified.
Naye akasema, “Kwa nini, ni kosa gani ametenda?” Lakini walizidi kupaza sauti hata juu mno, “Msulibishe.”
24 When Pilate saw that he auailed nothing, but that more tumult was made, he tooke water and washed his hands before the multitude, saying, I am innocent of the blood of this iust man: looke you to it.
Hivyo wakati Pilato alipoona hawezi kufanya lolote, lakini badala yake vurugu zilikuwa zimeanza, alitwaa maji akanawa mikono yake mbele ya umati, na kusema, “Mimi sina hatia juu ya damu ya mtu huyu asiye na hatia. Yaangalieni haya wenyewe.”
25 Then answered all the people, and saide, His bloud be on vs, and on our children.
Watu wote wakasema, “Damu yake iwe juu yetu na watoto wetu.”
26 Thus let he Barabbas loose vnto them, and scourged Iesus, and deliuered him to be crucified.
Kisha akamfungulia Baraba kwao, lakini alimpiga mijeredi Yesu na kumkabidhi kwao kwenda kusulibiwa.
27 Then the souldiers of the gouernour tooke Iesus into the common hall, and gathered about him the whole band,
Kisha askari wa liwali wakamchukua Yesu mpaka Praitorio na kundi kubwa la maaskari wote wakamkusanyika.
28 And they stripped him, and put about him a skarlet robe,
Wakamvua nguo zake na kumvika kanzu ya rangi nyekundu.
29 And platted a crowne of thornes, and put it vpon his head, and a reede in his right hand, and bowed their knees before him, and mocked him, saying, God saue thee King of the Iewes,
Kisha wakatengeneza taji ya miiba na kuiweka juu ya kichwa chake, na walimwekea mwanzi katika mkono wake wa kuume. Walipiga magoti mbele yake na kumkejeri, wakisema, “Salamu, Mfalme wa Wayahudi?”
30 And spitted vpon him, and tooke a reede, and smote him on the head.
Na walimtemea mate, na walitwaa mwanzi na kumpiga kichwani.
31 Thus when they had mocked him, they tooke the robe from him, and put his owne rayment on him, and led him away to crucifie him.
Wakati walipokuwa wakimkejeri, walimvua ile kanzu na kumvika nguo zake, na kumwongoza kwenda kumsulibisha.
32 And as they came out, they found a man of Cyrene, named Simon: him they compelled to beare his crosse.
Walipotoka nje, walimwona mtu kutoka Krene jina lake Simeoni, ambaye walimlazimisha kwenda nao ili apate kuubeba msalaba wake.
33 And when they came vnto the place called Golgotha, (that is to say, the place of dead mens skulles)
Walipofika mahali paitwapo Galigotha, maana yake, “Eneo la fuvu la Kichwa.”
34 They gaue him vineger to drinke, mingled with gall: and when he had tasted thereof, he would not drinke.
Walimpa siki iliyochanganywa na nyongo anywe. Lakini alipoionja, hakuweza kuinywa.
35 And when they had crucified him, they parted his garments, and did cast lottes, that it might be fulfilled, which was spoken by the Prophet, They deuided my garments among them, and vpon my vesture did cast lottes.
Wakati walipokuwa wamemsulibisha, waligawana mavazi yake kwa kupiga kura.
36 And they sate, and watched him there.
Na waliketi na kumwangalia.
37 They set vp also ouer his head his cause written, THIS IS IESVS THE KING OF THE IEVVES.
Juu ya kichwa chake waliweka mashitaka dhidi yake yakisomeka, “Huyu ni Yesu, mfalme wa Wayahudi.”
38 And there were two theeues crucified with him, one on the right hand, and another on the left.
Wanyang'anyi wawili walisulibiwa pamoja naye, mmoja upande wa kulia wake na mwingine wa kushoto.
39 And they that passed by, reuiled him, wagging their heades,
Wale waliokuwa wakipita walimdhihaki, wakitikisa vichwa vyao
40 And saying, Thou that destroyest ye Temple, and buildest it in three dayes, saue thy selfe: if thou be ye Sonne of God, come downe from ye crosse.
na kusema, “Wewe uliyekuwa unataka kuliharibu hekalu na kulijenga katika siku tatu, jiokoe mwenyewe! Kama ni Mwana wa Mungu, shuka chini utoke msalabani!”
41 Likewise also the hie Priests mocking him, with the Scribes, and Elders, and Pharises, said,
Katika hali ile ile wakuu wa makuhani walikuwa wakimkashifu, pamoja na waandishi na wazee, na kusema,
42 He saued others, but he cannot saue him selfe: if he be ye King of Israel, let him now come downe from ye crosse, and we will beleeue in him.
“Aliokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe. Yeye ni Mfalme wa Wayahudi. Na ashuke chini toka msalabani, ndipo tutakapomwamini.
43 He trusted in God, let him deliuer him nowe, if he will haue him: for he saide, I am the Sonne of God.
Alimtumaini Mungu. Acha Mungu amwokoe sasa kama anataka, kwa sababu alisema, 'Mimi ni Mwana wa Mungu.'”
44 The selfe same thing also ye theeues which were crucified with him, cast in his teeth.
Na wale wanyang'anyi waliokuwa wamesulibiwa pamoja naye pia walisema maneno ya kumdhihaki.
45 Now from ye sixt houre was there darkenesse ouer all the land, vnto the ninth houre.
Sasa kutoka saa sita kulikuwa na giza katika nchi yote hadi saa tisa.
46 And about ye ninth houre Iesus cryed with a loud voyce, saying, Eli, Eli, lamasabachthani? that is, My God, my God, why hast thou forsaken me?
Ilipofika saa tisa, Yesu akalia kwa sauti kuu, “Eloi, Eloi, lama thabakithan?” akimaanisha, “Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?”
47 And some of them that stoode there, when they heard it, said, This man calleth Elias.
Wakati huo baadhi yao waliokuwa wamesimama pale walisikia, wakasema, “Anamwita Eliya.”
48 And straightway one of them ran, and tooke a spondge, and filled it with vineger, and put it on a reede, and gaue him to drinke.
Mara moja mmoja wao alikimbia kuchukua sifongo na kuijaza kinywaji kichungu, akaiweka juu ya mti na kumpa apate kunywa.
49 Other said, Let be: let vs see, if Elias wil come and saue him.
Nao waliosalia wakasema, “Mwacheni peke yake, acheni tuone kama Eliya atakuja kumwokoa.”
50 Then Iesus cryed againe with a loude voyce, and yeelded vp the ghost.
Kisha Yesu akalia tena kwa sauti kuu na akaitoa roho yake.
51 And behold, the vayle of the Temple was rent in twaine, from the top to the bottome, and the earth did quake, and the stones were cloue.
Tazama, Pazia la hekalu lilipasuka sehemu mbili kutokea juu hadi chini. Na ardhi ikatetemeka na miamba ikapasuka vipande.
52 And the graues did open themselues, and many bodies of the Saintes, which slept, arose,
Makaburi yalifunguka, na miili ya watakatifu wengi waliokuwa wamelala usingizi walifufuliwa.
53 And came out of the graues after his resurrection, and went into the holy citie, and appeared vnto many.
Walitoka kwenye makaburi baada ya ufufuo wake, waliingia mji mtakatifu, na wakaonekana na wengi.
54 When the Centurion, and they that were with him watching Iesus, saw the earthquake, and the thinges that were done, they feared greatly, saying, Truely this was the Sonne of God.
Basi yule akida na wale ambao walikuwa wakimtazama Yesu waliona tetemeko na mambo yaliyokuwa yakitokea, walijawa na woga sana na kusema, “Kweli huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”
55 And many women were there, beholding him a farre off, which had folowed Iesus from Galile, ministring vnto him.
Wanawake wengi waliokuwa wakimfuata Yesu kutoka Galilaya ili kumhudumia walikuwa pale wakitazama kutoka kwa mbali.
56 Among whom was Marie Magdalene, and Marie the mother of Iames, and Ioses, and the mother of Zebedeus sonnes.
Miongini mwao walikuwa Mariamu Magdarena, Mariamu mama yake Yakobo na Joseph, na mama wa watoto wa Zebedayo
57 And when the euen was come, there came a riche man of Arimathea, named Ioseph, who had also himselfe bene Iesus disciple.
Ilipofika jioni, alikuja mtu tajiri kutoka Arimathayo, aliyeitwa Yusufu, ambaye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
58 He went to Pilate, and asked ye body of Iesus. Then Pilate commanded ye body to be deliuered.
Alimwendea Pilato na kuuomba mwili wa Yesu. Kisha Pilato aliagiza apate kupewa.
59 So Ioseph tooke the body, and wrapped it in a cleane linnen cloth,
Yusufu aliuchukua mwili akaufunga na nguo ya sufi safi,
60 And put it in his new tombe, which he had hewen out in a rocke, and rolled a great stone to the doore of the sepulchre, and departed.
na akaulaza katika kaburi jipya lake alilokuwa amelichonga mwambani. Kisha akavingirisha jiwe kubwa likafunika mlango wa kaburi na akaenda zake.
61 And there was Marie Magdalene, and the other Marie sitting ouer against the sepulchre.
Mariamu Magdalena na Mariamu mwingine walikuwa pale, wamekaa kuelekea kaburi.
62 Nowe the next day that followed the Preparation of the Sabbath, the hie Priestes and Pharises assembled to Pilate,
Siku iliyofuata ambayo ilikuwa siku baada ya maandalio, wakuu wa makuhani na Mafarisayo walikusanyika pamoja kwa Pilato.
63 And said, Syr, we remember that that deceiuer saide, while he was yet aliue, Within three dayes I will rise.
Wakamwambia, “Bwana, tunakumbuka kuwa wakati yule mdanganyifu alipokuwa hai, alisema, 'Baada ya siku tatu atafufuka tena.'
64 Command therefore, that the sepulchre be made sure vntill the third day, lest his disciples come by night, and steale him away, and say vnto the people, He is risen from the dead: so shall the last errour be worse then the first.
Kwahiyo, agiza kwamba kaburi lilindwe salama mpaka siku ya tatu. Vinginevyo, wanafunzi wake wanaweza kuja kumwiba na kusema kwa watu, 'Amefufuka kutoka wafu.' Na udanganyifu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa kwanza.”
65 Then Pilate saide vnto them, Ye haue a watch: goe, and make it sure as ye knowe.
Pilato akawaambia, “Chukueni walinzi. Nendeni mkafanye hali ya usalama kama muwezavyo.”
66 And they went, and made the sepulchre sure with the watch, and sealed the stone.
Hivyo walikwenda na kufanya kaburi kuwa salama, jiwe liligongwa mhuri na kuweka walinzi.