< Matthew 20 >
1 For the kingdome of heauen is like vnto a certaine, housholder, which went out at the dawning of the day to hire labourers into his vineyarde.
“Ufalme wa mbinguni unafanana na mtu mwenye shamba la mizabibu, ambaye alitoka asubuhi na mapema kuwaajiri wafanyakazi katika shamba lake.
2 And he agreed with the labourers for a peny a day, and sent them into his vineyard.
Akapatana nao kuwalipa dinari moja kwa siku, kisha akawapeleka katika shamba lake la mizabibu.
3 And he went out about the third houre, and sawe other standing idle in the market place,
Akatoka mnamo saa tatu asubuhi, akaona watu wengine wamesimama sokoni, hawana kazi.
4 And sayd vnto them, Goe ye also into my vineyard, and whatsoeuer is right, I will giue you: and they went their way.
Akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu, nami nitawapeni haki yenu.
5 Againe he went out about the sixt and ninth houre, and did likewise.
Basi, wakaenda. Huyo mwenye shamba akatoka tena mnamo saa sita na saa tisa, akafanya vivyo hivyo.
6 And he went about the eleuenth houre, and found other standing idle, and sayd vnto them, Why stand ye here all the day idle?
Hata mnamo saa kumi na moja jioni, akatoka tena; akakuta watu wengine wamesimama pale sokoni. Basi, akawauliza, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?
7 They sayd vnto him, Because no man hath hired vs. He sayd to them, Goe ye also into my vineyard, and whatsoeuer is right, that shall ye receiue.
Wakamjibu: Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Yeye akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu.
8 And when euen was come, the master of the vineyard sayd vnto his steward, Call the labourers, and giue them their hire, beginning at the last, till thou come to the first.
“Kulipokuchwa, huyo mwenye shamba alimwambia mtunza hazina wake, Waite wafanyakazi ukawalipe mshahara wao, ukianzia na wale walioajiriwa mwisho, na kumalizia na wale wa kwanza.
9 And they which were hired about ye eleuenth houre, came and receiued euery man a penie.
Basi, wakaja wale walioajiriwa mnamo saa kumi na moja, wakapokea kila mmoja dinari moja.
10 Nowe when the first came, they supposed that they should receiue more, but they likewise receiued euery man a penie.
Wale wa kwanza walipofika, walikuwa wanadhani watapewa zaidi; lakini hata wao wakapewa kila mmoja dinari moja.
11 And when they had receiued it, they murmured against the master of the house,
Wakazipokea fedha zao, wakaanza kumnung'unikia yule bwana.
12 Saying, These last haue wrought but one houre, and thou hast made them equall vnto vs, which haue borne the burden and heate of the day.
Wakasema, Watu hawa walioajiriwa mwisho walifanya kazi kwa muda wa saa moja tu, mbona umetutendea sawa na wao hali sisi tumevumilia kazi ngumu kutwa na jua kali?
13 And hee answered one of them, saying, Friend, I doe thee no wrong: didst thou not agree with me for a penie?
“Hapo yule bwana akamjibu mmoja wao, Rafiki, sikukupunja kitu! Je, hukupatana nami mshahara wa denari moja?
14 Take that which is thine owne, and go thy way: I will giue vnto this last, as much as to thee.
Chukua haki yako, uende zako. Napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe.
15 Is it not lawfull for me to do as I will with mine owne? Is thine eye euil, because I am good?
Je, sina haki ya kufanya na mali yangu nipendavyo? Je, unaona kijicho kwa kuwa mimi ni mwema?”
16 So the last shalbe first, and the first last: for many are called, but fewe chosen.
Yesu akamaliza kwa kusema, “Hivyo, walio wa mwisho watakuwa wa kwanza na wa kwanza watakuwa wa mwisho.”
17 And Iesus went vp to Hierusalem, and tooke the twelue disciples apart in the way, and said vnto them,
Yesu alipokuwa anakwenda Yerusalemu, aliwachukua wale wanafunzi kumi na wawili faraghani, na njiani akawaambia,
18 Beholde, wee goe vp to Hierusalem, and the Sonne of man shall bee deliuered vnto the chiefe priestes, and vnto the Scribes, and they shall condemne him to death,
“Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu, na huko Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa makuhani wakuu na walimu wa Sheria, nao watamhukumu auawe.
19 And shall deliuer him to the Gentiles, to mocke, and to scourge, and to crucifie him, but the third day he shall rise againe.
Watamkabidhi kwa watu wa mataifa mengine ili adhihakiwe, apigwe viboko na kusulubiwa; lakini siku ya tatu atafufuliwa.”
20 Then came to him the mother of Zebedeus children with her sonnes, worshipping him, and desiring a certaine thing of him.
Hapo mama yao wana wa Zebedayo alimjia Yesu pamoja na wanawe, akapiga magoti mbele yake na kumwomba kitu.
21 And he said vnto her, What wouldest thou? She said to him, Graunt that these my two sonnes may sit, the one at thy right hand, and the other at thy left hand in thy kingdome.
Yesu akamwuliza, “Unataka nini?” Huyo mama akamwambia, “Ahidi kwamba katika Ufalme wako, hawa wanangu wawili watakaa mmoja upande wako wa kulia na mwingine upande wako wa kushoto.”
22 And Iesus answered and said, Ye know not what ye aske. Are ye able to drinke of the cup that I shall drinke of, and to be baptized with the baptisme that I shalbe baptized with? They said to him, We are able.
Yesu akajibu, “Hamjui mnaomba nini. Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa mimi?” Wakamjibu, “Tunaweza.”
23 And he said vnto them, Ye shall drinke in deede of my cup, and shall be baptized with the baptisme, that I am baptized with, but to sit at my right hande, and at my left hand, is not mine to giue: but it shalbe giuen to them for whome it is prepared of my Father.
Yesu akawaambia, “Kweli mtakunywa kikombe changu, lakini kuketi kulia au kushoto kwangu si kazi yangu kupanga; jambo hilo watapewa wale waliowekewa tayari na Baba yangu.”
24 And when the other ten heard this, they disdained at the two brethren.
Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakawakasirikia hao ndugu wawili.
25 Therefore Iesus called them vnto him, and saide, We knowe that the lordes of the Gentiles haue domination ouer them, and they that are great, exercise authoritie ouer them.
Hivyo Yesu akawaita, akawaambia, “Mnajua kwamba watawala wa mataifa hutawala watu wao kwa mabavu na wakuu hao huwamiliki watu wao.
26 But it shall not be so among you: but whosoeuer will be great among you, let him be your seruant.
Lakini kwenu isiwe hivyo, ila yeyote anayetaka kuwa mkuu kati yenu sharti awe mtumishi wa wote;
27 And whosoeuer will be chiefe among you, let him be your seruant.
na anayetaka kuwa wa kwanza kati yenu sharti awe mtumishi wenu.
28 Euen as the Sonne of man came not to be serued, but to serue, and to giue his life for the ransome of many.
Jinsi hiyohiyo, Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, bali kutumikia na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi.”
29 And as they departed from Iericho, a great multitude followed him.
Yesu alipokuwa anaondoka mjini Yeriko, umati wa watu ulimfuata.
30 And beholde, two blinde men, sitting by the way side, when they heard that Iesus passed by, cryed, saying, O Lord, the Sonne of Dauid, haue mercie on vs.
Basi, kulikuwa na vipofu wawili wameketi kando ya njia, na waliposikia kwamba Yesu alikuwa anapitia hapo, walipaaza sauti: “Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!”
31 And the multitude rebuked them, because they should holde their peace: but they cried the more, saying, O Lord, the Sonne of Dauid, haue mercie on vs.
Ule umati wa watu ukawakemea na kuwaambia wanyamaze. Lakini wao wakazidi kupaaza sauti: “Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!”
32 Then Iesus stoode still, and called them, and said, What will ye that I should do to you?
Yesu akasimama, akawaita na kuwauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
33 They saide to him, Lord, that our eyes may be opened.
Wakamjibu, “Mheshimiwa, tunaomba macho yetu yafumbuliwe.”
34 And Iesus mooued with compassion, touched their eyes, and immediatly their eyes receiued sight, and they followed him.
Basi, Yesu akawaonea huruma, akawagusa macho yao, na papo hapo wakaweza kuona, wakamfuata.