< Matthew 16 >
1 Then came the Pharises and Sadduces, and did tempt him, desiring him to shew them a signe from heauen.
Mafarisayo na Masadukayo wakamjia Yesu na kumjaribu kwa kumwomba awaonyeshe ishara kutoka mbinguni.
2 But he answered, and said vnto them, When it is euening, ye say, Faire wether: for ye skie is red.
Yesu akawajibu, “Ifikapo jioni, mnasema, ‘Hali ya hewa itakuwa nzuri, kwa kuwa anga ni nyekundu.’
3 And in the morning ye say, To day shall be a tempest: for the skie is red and lowring. O hypocrites, ye can discerne the face of the skie, and can ye not discerne the signes of the times?
Nanyi wakati wa asubuhi mnasema, ‘Leo kutakuwa na dhoruba, kwa sababu anga ni nyekundu na mawingu yametanda.’ Mnajua jinsi ya kupambanua kule kuonekana kwa anga, lakini hamwezi kupambanua dalili za nyakati.
4 The wicked generation, and adulterous seeketh a signe, but there shall no signe be giuen it, but that signe of the Prophet Ionas: so hee left them, and departed.
Kizazi kiovu na cha uzinzi kinatafuta ishara, lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ishara ya Yona.” Yesu akawaacha, akaenda zake.
5 And when his disciples were come to the other side, they had forgotten to take bread with them.
Wanafunzi wake walipofika ngʼambo ya bahari, walikuwa wamesahau kuchukua mikate.
6 Then Iesus said vnto them, Take heede and beware of the leauen of the Pharises and Sadduces.
Yesu akawaambia, “Jihadharini. Jilindeni na chachu ya Mafarisayo na ya Masadukayo.”
7 And they reasoned among themselues, saying, It is because we haue brought no bread.
Wakajadiliana wao kwa wao, wakisema, “Ni kwa sababu hatukuleta mikate.”
8 But Iesus knowing it, saide vnto them, O ye of litle faith, why reason you thus among your selues, because ye haue brought no bread?
Yesu, akifahamu majadiliano yao, akauliza, “Enyi wa imani haba! Mbona mnajadiliana miongoni mwenu kuhusu kutokuwa na mikate?
9 Doe ye not yet perceiue, neither remember the fiue loaues, when there were fiue thousand men, and how many baskets tooke ye vp?
Je, bado hamwelewi? Je, hamkumbuki ile mikate mitano iliyolisha watu 5,000 na idadi ya vikapu vingapi vya mabaki mlivyokusanya?
10 Neither the seuen loaues when there were foure thousande men, and howe many baskets tooke ye vp?
Au ile mikate saba iliyolisha watu 4,000 na idadi ya vikapu vingapi vya mabaki mlivyokusanya?
11 Why perceiue ye not that I said not vnto you concerning bread, that ye shoulde beware of the leauen of the Pharises and Sadduces?
Inakuwaje mnashindwa kuelewa kwamba nilikuwa sisemi nanyi habari za mikate? Jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.”
12 Then vnderstood they that he had not said that they should beware of the leauen of bread, but of the doctrine of the Pharises, and Sadduces.
Ndipo wakaelewa kwamba alikuwa hasemi juu ya chachu ya kutengeneza mikate, bali juu ya mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo.
13 Nowe when Iesus came into the coastes of Cesarea Philippi, hee asked his disciples, saying, Whome doe men say that I, the sonne of man am?
Basi Yesu alipofika katika eneo la Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake, “Watu husema kwamba mimi Mwana wa Adamu ni nani?”
14 And they said, Some say, Iohn Baptist: and some, Elias: and others, Ieremias, or one of the Prophets.
Wakamjibu, “Baadhi husema ni Yohana Mbatizaji; wengine husema ni Eliya; na bado wengine husema ni Yeremia au mmojawapo wa manabii.”
15 He said vnto them, But whome say ye that I am?
Akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?”
16 Then Simon Peter answered, and said, Thou art that Christ, the Sonne of the liuing God.
Simoni Petro akamjibu, “Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.”
17 And Iesus answered, and saide to him, Blessed art thou, Simon, the sonne of Ionas: for flesh and blood hath not reueiled it vnto thee, but my Father which is in heauen.
Naye Yesu akamwambia, “Heri wewe, Simoni Bar-Yona, kwa maana hili halikufunuliwa kwako na mwanadamu, bali na Baba yangu aliye mbinguni.
18 And I say also vnto thee, that thou art Peter, and vpon this rocke I will builde my Church: and ye gates of hell shall not ouercome it. (Hadēs )
Nami nakuambia, wewe ndiwe Petro na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu, hata malango ya Kuzimu hayataweza kulishinda. (Hadēs )
19 And I will giue vnto thee the keyes of the kingdome of heauen, and whatsoeuer thou shalt binde vpon earth, shalbe bound in heauen: and whatsoeuer thou shalt loose on earth, shall be loosed in heauen.
Nitakupa funguo za Ufalme wa mbinguni, na lolote utakalolifunga duniani litakuwa limefungwa Mbinguni, nalo lolote utakalofungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.”
20 Then hee charged his disciples, that they should tell no man that he was Iesus that Christ.
Kisha akawakataza wanafunzi wake wasimwambie mtu yeyote kwamba yeye ndiye Kristo.
21 From that time foorth Iesus beganne to shewe vnto his disciples, that he must goe vnto Hierusalem, and suffer many thinges of the Elders, and of the hie Priestes, and Scribes, and be slaine, and be raised againe the thirde day.
Tangu wakati huo, Yesu alianza kuwaeleza wanafunzi wake kwamba hana budi kwenda Yerusalemu na kupata mateso mengi mikononi mwa wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa sheria, na kwamba itampasa auawe lakini siku ya tatu kufufuliwa.
22 Then Peter tooke him aside, and began to rebuke him, saying, Master, pitie thy selfe: this shall not be vnto thee.
Petro akamchukua kando, akaanza kumkemea akisema, “Haiwezekani, Bwana! Jambo hili kamwe halitakupata!”
23 Then he turned backe, and said vnto Peter, Get thee behinde me, Satan: thou art an offence vnto me, because thou vnderstandest not the thinges that are of God, but the thinges that are of men.
Lakini Yesu akageuka na kumwambia Petro, “Rudi nyuma yangu, Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu. Moyo wako hauwazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.”
24 Iesus then saide to his disciples, If any man will follow me, let him forsake himselfe: and take vp his crosse, and follow me.
Ndipo Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.
25 For whosoeuer will saue his life, shall lose it: and whosoeuer shall lose his life for my sake, shall finde it.
Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu atayapata.
26 For what shall it profite a man though he should winne the whole worlde, if hee lose his owne soule? or what shall a man giue for recompence of his soule?
Kwa maana, je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akayapoteza maisha yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?
27 For the Sonne of man shall come in the glory of his Father with his Angels, and then shall he giue to euery man according to his deedes.
Kwa maana Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake, naye ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.
28 Verely I say vnto you, there bee some of them that stande here, which shall not taste of death, till they haue seene the Sonne of man come in his kingdome.
Nawaambia kweli, baadhi yenu hapa hawataonja mauti kabla ya kumwona Mwana wa Adamu akija katika Ufalme wake.”