< Matthew 15 >

1 Then came to Iesus the Scribes and Pharises, which were of Hierusalem, saying,
Ndipo baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria wakamjia Yesu kutoka Yerusalemu na kumuuliza,
2 Why do thy disciples transgresse the tradition of the Elders? for they wash not their hands when they eate bread.
“Mbona wanafunzi wako wanakiuka mapokeo ya wazee? Kwa maana wao hawanawi mikono yao kabla ya kula!”
3 But he answered and said vnto them, Why doe yee also transgresse the commandement of God by your tradition?
Yesu akawajibu, “Mbona ninyi mnavunja amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu?
4 For God hath commanded, saying, Honour thy father and mother: and he that curseth father or mother, let him die the death.
Kwa maana Mungu alisema, ‘Waheshimu baba yako na mama yako,’ na, ‘Yeyote amtukanaye baba yake au mama yake, na auawe.’
5 But ye say, Whosoeuer shall say to father or mother, By the gift that is offered by me, thou maiest haue profite,
Lakini ninyi mwafundisha kwamba mtu akimwambia baba yake au mama yake, ‘Kile ambacho ningeweza kukusaidia kimewekwa wakfu kwa Mungu,’
6 Though hee honour not his father, or his mother, shalbe free: thus haue ye made the commandement of God of no aucthoritie by your tradition.
basi hana tena sababu ya kumheshimu baba yake nacho. Basi kwa ajili ya mafundisho yenu mnavunja amri ya Mungu.
7 O hypocrites, Esaias prophecied well of you, saying,
Ninyi wanafiki! Isaya alikuwa sawa alipotabiri juu yenu kwamba:
8 This people draweth neere vnto me with their mouth, and honoureth me with the lips, but their heart is farre off from me.
“‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami.
9 But in vaine they worship me, teaching for doctrines, mens precepts.
Huniabudu bure; nayo mafundisho yao ni maagizo ya wanadamu tu.’”
10 Then hee called the multitude vnto him, and said to them, Heare and vnderstand.
Yesu akaita ule umati wa watu, akawaambia, “Sikilizeni na mwelewe:
11 That which goeth into the mouth, defileth not the man, but that which commeth out of the mouth, that defileth the man.
kinachomfanya mtu kuwa najisi mbele za Mungu si kile kiingiacho kinywani mwake, bali ni kile kitokacho kinywani mwake.”
12 Then came his disciples, and saide vnto him, Perceiuest thou not, that the Pharises are offended in hearing this saying?
Kisha wanafunzi wake wakamjia na kumuuliza, “Je, unajua kwamba Mafarisayo walichukizwa sana waliposikia yale uliyosema?”
13 But hee answered and saide, Euery plant which mine heauenly Father hath not planted, shalbe rooted vp.
Akawajibu, “Kila pando ambalo Baba yangu wa mbinguni hakulipanda, litangʼolewa.
14 Let them alone, they be the blinde leaders of the blinde: and if the blinde leade ye blinde, both shall fall into the ditche.
Waacheni; wao ni viongozi vipofu, wanaoongoza vipofu. Kama kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili watatumbukia shimoni.”
15 Then answered Peter, and said to him, Declare vnto vs this parable.
Petro akasema, “Tueleze maana ya huu mfano.”
16 Then said Iesus, Are ye yet without vnderstanding?
Yesu akawauliza, “Je, bado ninyi hamfahamu?
17 Perceiue ye not yet, that whatsoeuer entreth into the mouth, goeth into the bellie, and is cast out into the draught?
Je, hamwelewi kwamba chochote kiingiacho kinywani huenda tumboni, na hatimaye hutolewa nje kikiwa uchafu?
18 But those thinges which proceede out of the mouth, come from the heart, and they defile the man.
Lakini kitokacho kinywani hutoka moyoni, na hiki ndicho kimtiacho mtu unajisi.
19 For out of the heart come euil thoughts, murders, adulteries, fornications, thefts, false testimonies, slaunders.
Kwa maana ndani ya moyo hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushahidi wa uongo na masingizio.
20 These are the things, which defile the man: but to eat with vnwashen hands, defileth not ye man.
Haya ndiyo yamtiayo mtu unajisi; lakini kula bila kunawa mikono hakumtii mtu unajisi.”
21 And Iesus went thence, and departed into the coastes of Tyrus and Sidon.
Yesu aliondoka mahali pale, akaenda sehemu za Tiro na Sidoni.
22 And beholde, a woman a Cananite came out of the same coasts, and cried, saying vnto him, Haue mercie on me, O Lord, the sonne of Dauid: my daughter is miserably vexed with a deuil.
Mwanamke mmoja Mkanaani aliyeishi sehemu jirani na hizo akaja kwake akilia, akasema, “Nihurumie, Ee Bwana, Mwana wa Daudi! Binti yangu amepagawa na pepo mchafu, na anateseka sana.”
23 But hee answered her not a worde. Then came to him his disciples, and besought him, saying, Sende her away, for she crieth after vs.
Lakini Yesu hakumjibu neno. Hivyo wanafunzi wake wakamwendea na kumsihi sana, wakisema, “Mwambie aende zake, kwa maana anaendelea kutupigia kelele.”
24 But he answered, and said, I am not sent, but vnto the lost sheepe of the house of Israel.
Yesu akajibu, “Nimetumwa tu kwa ajili ya kondoo wa Israeli waliopotea.”
25 Yet she came, and worshipped him, saying, Lord, helpe me.
Lakini yule mwanamke akaja, akapiga magoti mbele ya Yesu, akasema, “Bwana, nisaidie!”
26 And he answered, and said, It is not good to take the childrens bread, and to cast it to whelps.
Yesu akajibu, “Si haki kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.”
27 But she said, Trueth, Lord: yet in deede the whelpes eate of the crommes, which fall from their masters table.
Yule mwanamke akajibu, “Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yanayoanguka kutoka kwenye meza za bwana zao.”
28 Then Iesus answered, and saide vnto her, O woman, great is thy faith: be it to thee, as thou desirest. And her daughter was made whole at that houre.
Ndipo Yesu akamwambia, “Mwanamke, imani yako ni kubwa! Iwe kwako kama unavyotaka.” Naye binti yake akapona tangu saa ile.
29 So Iesus went away from thence, and came neere vnto the sea of Galile, and went vp into a mountaine and sate downe there.
Yesu akaondoka na kwenda kando ya Bahari ya Galilaya. Kisha akapanda mlimani, akaketi huko.
30 And great multitudes came vnto him, hauing with them, halt, blinde, dumme, maymed, and many other, and cast them downe at Iesus feete, and he healed them.
Umati mkubwa wa watu ukamjia, wakiwaleta vilema, vipofu, viwete, bubu na wengine wengi, wakawaweka miguuni pake; naye akawaponya.
31 In so much that the multitude wondered, to see the dumme speake, the maimed whole, the halt to goe, and the blinde to see: and they glorified the God of Israel.
Hao watu wakashangaa walipoona bubu wakisema, vilema wakipona, viwete wakitembea na vipofu wakiona, wakamtukuza Mungu wa Israeli.
32 Then Iesus called his disciples vnto him, and said, I haue compassion on this multitude, because they haue continued with mee already three dayes, and haue nothing to eate: and I wil not let them depart fasting, least they faint in the way.
Kisha Yesu akawaita wanafunzi wake, akawaambia, “Ninauhurumia huu umati wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa pamoja nami kwa muda wa siku tatu, na hawana chakula chochote. Nami sipendi kuwaaga wakiwa na njaa, wasije wakazimia njiani.”
33 And his disciples saide vnto him, Whence should we get so much bread in the wildernes, as should suffice so great a multitude!
Wanafunzi wake wakasema, “Tutapata wapi mikate ya kutosha kuwalisha umati huu wa watu mkubwa namna hii, nasi tuko nyikani?”
34 And Iesus said vnto them, How many loaues haue ye? And they said, Seuen, and a few litle fishes.
Yesu akawauliza, “Mnayo mikate mingapi?” Wakamjibu, “Tunayo mikate saba na visamaki vichache.”
35 Then he commanded the multitude to sit downe on the ground,
Yesu akawaambia ule umati wa watu waketi chini.
36 And tooke the seuen loaues, and the fishes, and gaue thankes, and brake them, and gaue to his disciples, and the disciples to the multitude.
Kisha akachukua ile mikate saba na wale samaki, naye akiisha kumshukuru Mungu, akavimega na kuwapa wanafunzi wake, nao wakawapa ule umati wa watu.
37 And they did all eate, and were sufficed: and they tooke vp of the fragments that remained, seuen baskets full.
Wote wakala na kushiba. Baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu saba.
38 And they that had eaten, were foure thousand men, beside women, and litle children.
Idadi ya watu walikuwa wanaume 4,000, bila kuhesabu wanawake na watoto.
39 Then Iesus sent away the multitude, and tooke ship, and came into the partes of Magdala.
Baada ya kuaga ule umati wa watu, Yesu aliingia katika mashua, akaenda sehemu za Magadani.

< Matthew 15 >