< Mark 9 >
1 And he saide vnto them, Verely I say vnto you, that there be some of them that stande here, which shall not taste of death till they haue seene the kingdome of God come with power.
Yesu akaendelea kuwaambia, “Amin, nawaambia, kuna watu waliosimama hapa ambao hawataonja mauti kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu ukija kwa nguvu.”
2 And sixe dayes after, Iesus taketh vnto him Peter, and Iames, and Iohn, and carieth them vp into an hie mountaine out of the way alone, and his shape was changed before them.
Baada ya siku sita, Yesu akawachukua Petro, Yakobo na Yohana, akawapeleka juu ya mlima mrefu, mahali walipokuwa faraghani. Huko, Yesu akageuka sura mbele yao.
3 And his rayment did shine, and was very white, as snowe, so white as no fuller can make vpon the earth.
Mavazi yake yakawa na weupe wa kuzima macho, meupe kuliko ambavyo mtu yeyote duniani angaliweza kuyangʼarisha.
4 And there appeared vnto them Elias with Moses, and they were talking with Iesus.
Mose na Eliya wakawatokea, wakawa wanazungumza na Yesu.
5 Then Peter answered, and said to Iesus, Master, it is good for vs to be here: let vs make also three tabernacles, one for thee, and one for Moses, and one for Elias.
Petro akamwambia Yesu, “Rabi, ni vyema sisi tukae hapa. Turuhusu tujenge vibanda vitatu: kimoja chako, kingine cha Mose na kingine cha Eliya.”
6 Yet hee knewe not what he saide: for they were afraide.
Petro hakujua aseme nini kwa maana yeye na wenzake walikuwa wameogopa sana.
7 And there was a cloude that shadowed them, and a voyce came out of the cloude, saying, This is my beloued Sonne: heare him.
Ndipo pakatokea wingu, likawafunika, nayo sauti kutoka lile wingu ikasema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa. Msikieni yeye.”
8 And suddenly they looked roud about, and sawe no more any man saue Iesus only with them.
Mara walipotazama huku na huku, hawakuona tena mtu mwingine yeyote pamoja nao isipokuwa Yesu.
9 And as they came downe from the mountaine, he charged them, that they should tell no man what they had seene, saue when the Sonne of man were risen from the dead againe.
Walipokuwa wakishuka kutoka mlimani, Yesu akawakataza wasimwambie mtu yeyote mambo waliyoona, mpaka Mwana wa Adamu atakapokuwa amefufuka kutoka kwa wafu.
10 So they kept that matter to themselues, and demaunded one of another, what the rising from the dead againe should meane?
Wakalihifadhi jambo hilo wao wenyewe, lakini wakawa wanajiuliza, “Huku kufufuka kwa wafu maana yake nini?”
11 Also they asked him, saying, Why say the Scribes, that Elias must first come?
Wakamuuliza, “Kwa nini walimu wa sheria husema kwamba ni lazima Eliya aje kwanza?”
12 And he answered, and said vnto them, Elias verely shall first come, and restore all things: and as it is written of the Sonne of man, hee must suffer many things, and be set at nought.
Yesu akawajibu, “Ni kweli, Eliya yuaja kwanza ili kutengeneza mambo yote. Mbona basi imeandikwa kwamba Mwana wa Adamu ni lazima ateseke sana na kudharauliwa?
13 But I say vnto you, that Elias is come, (and they haue done vnto him whatsoeuer they would) as it is written of him.
Lakini ninawaambia, Eliya amekwisha kuja, nao wakamtendea walivyopenda, kama ilivyoandikwa kumhusu yeye.”
14 And when he came to his disciples, he saw a great multitude about them, and the Scribes disputing with them.
Walipowafikia wale wanafunzi wengine, wakawakuta wamezungukwa na umati mkubwa wa watu na baadhi ya walimu wa sheria wakibishana nao.
15 And straightway all the people, when they behelde him, were amased, and ranne to him, and saluted him.
Mara wale watu walipomwona Yesu, wakastaajabu sana, wakamkimbilia ili kumsalimu.
16 Then hee asked the Scribes, What dispute you among your selues?
Akawauliza wanafunzi wake, “Mnabishana nao kuhusu nini?”
17 And one of the companie answered, and said, Master, I haue brought my sonne vnto thee, which hath a dumme spirit:
Mtu mmoja miongoni mwa ule umati wa watu akajibu, “Mwalimu, nilimleta kwako mwanangu ambaye ana pepo mchafu anayemfanya asiweze kuongea.
18 And wheresoeuer he taketh him, he teareth him, and he fometh, and gnasheth his teeth, and pineth away: and I spake to thy disciples, that they should cast him out, and they could not.
Kila mara huyo pepo mchafu ampagaapo mwanangu, humwangusha chini na kumfanya atokwe povu mdomoni na kusaga meno, kisha mwili wake hukauka. Niliwaomba wanafunzi wako wamtoe huyo pepo mchafu, lakini hawakuweza.”
19 Then he answered him, and said, O faithlesse generation, how long now shall I be with you! how long now shall I suffer you! Bring him vnto me.
Yesu akawaambia, “Enyi kizazi kisicho na imani! Nitakuwa pamoja nanyi mpaka lini? Nitawavumilia mpaka lini? Mleteni mvulana kwangu.”
20 So they brought him vnto him: and assoone as the spirit sawe him, hee tare him, and hee fell downe on the ground walowing and foming.
Nao wakamleta yule mvulana. Yule pepo mchafu alipomwona Yesu, mara akamtia yule mvulana kifafa, akaanguka, akagaagaa chini huku akitokwa na povu kinywani.
21 Then he asked his father, How long time is it since he hath bin thus? And he said, Of a childe.
Yesu akamuuliza baba yake, “Mwanao amekuwa katika hali hii tangu lini?” Akamjibu, “Tangu utoto wake.
22 And oft times he casteth him into the fire, and into the water to destroy him: but if thou canst do any thing, helpe vs, and haue compassion vpon vs.
Mara kwa mara huyo pepo mchafu amekuwa akimwangusha kwenye moto au kwenye maji ili kumwangamiza. Lakini kama unaweza kufanya jambo lolote, tafadhali tuhurumie utusaidie.”
23 And Iesus said vnto him, If thou canst beleeue it, al things are possible to him that beleeueth.
Yesu akamwambia, “Kama ukiweza kuamini, yote yawezekana kwake yeye aaminiye.”
24 And straightway the father of the childe crying with teares, saide, Lord, I beleeue: helpe my vnbeliefe.
Mara baba yake yule mvulana akapiga kelele akisema, “Ninaamini. Nisaidie kutokuamini kwangu!”
25 When Iesus saw that the people came running together, he rebuked the vncleane spirit, saying vnto him, Thou domme and deafe spirit, I charge thee, come out of him, and enter no more into him.
Yesu alipoona kwamba umati wa watu unakusanyika pamoja mbio, akamkemea yule pepo mchafu, akimwambia, “Wewe pepo bubu na kiziwi, nakuamuru umtoke, wala usimwingie tena!”
26 Then the spirit cried, and rent him sore, and came out, and he was as one dead, in so much that many said, He is dead.
Yule pepo mchafu akiisha kupiga kelele, akamtia kifafa kwa nguvu, na akamtoka. Yule mvulana alikuwa kama maiti, hivyo watu wengi wakasema, “Amekufa.”
27 But Iesus tooke his hande, and lift him vp, and he arose.
Lakini Yesu akamshika mkono, akamwinua, naye akasimama.
28 And when hee was come into the house, his disciples asked him secretly, Why could not we cast him out?
Baada ya Yesu kuingia ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamuuliza wakiwa peke yao, “Mbona sisi hatukuweza kumtoa huyo pepo mchafu?”
29 And he saide vnto them, This kinde can by no other meanes come foorth, but by prayer and fasting.
Yesu akawajibu, “Hali hii haiwezi kutoka isipokuwa kwa kuomba na kufunga.”
30 And they departed thence, and went together through Galile, and hee would not that any should haue knowen it.
Wakaondoka huko, wakapitia Galilaya. Yesu hakutaka mtu yeyote afahamu mahali walipo,
31 For he taught his disciples, and saide vnto them, The Sonne of man shalbe deliuered into the handes of men, and they shall kill him, but after that he is killed, he shall rise againe the third day.
kwa maana alikuwa anawafundisha wanafunzi wake. Akawaambia, “Mwana wa Adamu atasalitiwa na kutiwa mikononi mwa watu. Nao watamuua, lakini siku tatu baada ya kuuawa atafufuka.”
32 But they vnderstoode not that saying, and were afraide to aske him.
Lakini wao hawakuelewa kile alimaanisha, nao waliogopa kumuuliza maana yake.
33 After, he came to Capernaum: and when he was in the house, he asked them, What was it that ye disputed among you by the way?
Basi wakafika Kapernaumu na baada ya kuingia nyumbani akawauliza, “Mlikuwa mnabishana nini kule njiani?”
34 And they helde their peace: for by the way they reasoned among themselues, who should bee the chiefest.
Lakini hawakumjibu, kwa sababu njiani walikuwa wakibishana kuhusu nani miongoni mwao alikuwa mkuu zaidi ya wote.
35 And he sate downe, and called the twelue, and said to them, If any man desire to be first, the same shalbe last of all, and seruant vnto all.
Akaketi chini, akawaita wote kumi na wawili, akawaambia: “Kama mtu yeyote akitaka kuwa wa kwanza, hana budi kuwa wa mwisho na mtumishi wa wote.”
36 And he tooke a litle childe, and set him in the middes of them, and tooke him in his armes, and sayd vnto them,
Kisha akamchukua mtoto mdogo, akamsimamisha katikati yao. Akamkumbatia, akawaambia,
37 Whosoeuer shall receiue one of such litle children in my Name, receiueth me: and whosoeuer receiueth mee, receiueth not me, but him that sent me.
“Mtu yeyote amkaribishaye mmoja wa hawa watoto wadogo kwa Jina langu, anikaribisha mimi. Naye anikaribishaye mimi, amkaribisha Baba yangu aliyenituma.”
38 Then Iohn answered him, saying, Master, we sawe one casting out deuils by thy Name, which followeth not vs, and we forbade him, because he followeth vs not.
Yohana akamwambia, “Mwalimu, tumemwona mtu akitoa pepo wachafu kwa jina lako, nasi tukamkataza, kwa sababu yeye si mmoja wetu.”
39 But Iesus sayd, Forbid him not: for there is no man that can doe a miracle by my Name, that can lightly speake euill of me.
Yesu akasema, “Msimkataze, kwa kuwa hakuna yeyote atendaye miujiza kwa Jina langu ambaye baada ya kitambo kidogo aweza kunena lolote baya dhidi yangu.
40 For whosoeuer is not against vs, is on our part.
Kwa maana yeyote asiye kinyume chetu, yuko upande wetu.
41 And whosoeuer shall giue you a cup of water to drinke for my Names sake, because ye belong to Christ, verely I say vnto you, he shall not lose his rewarde.
Amin, nawaambia, yeyote awapaye ninyi kikombe cha maji kwa Jina langu kwa sababu ninyi ni mali ya Kristo, hakika hataikosa thawabu yake.”
42 And whosoeuer shall offend one of these litle ones, that beleeue in me, it were better for him rather, that a milstone were hanged about his necke, and that he were cast into the sea.
“Kama mtu yeyote akimsababisha mmojawapo wa wadogo hawa wanaoniamini kutenda dhambi, ingekuwa bora kwake afungiwe jiwe kubwa la kusagia shingoni mwake, na kutoswa baharini.
43 Wherefore, if thine hand cause thee to offend, cut it off: it is better for thee to enter into life, maimed, then hauing two hands, to goe into hell, into the fire that neuer shalbe quenched, (Geenna )
Kama mkono wako ukikusababisha kutenda dhambi, ukate. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa na mkono mmoja, kuliko kuwa na mikono miwili lakini ukaingia jehanamu, mahali ambako moto hauzimiki. [ (Geenna )
44 Where their worme dyeth not, and the fire neuer goeth out.
Mahali ambako funza wake hawafi wala moto wake hauzimiki.]
45 Likewise, if thy foote cause thee to offend, cut it off: it is better for thee to go halt into life, then hauing two feete, to be cast into hell, into the fire that neuer shalbe quenched, (Geenna )
Kama mguu wako ukikusababisha kutenda dhambi, ukate. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili lakini ukaingia jehanamu. [ (Geenna )
46 Where their worme dyeth not, and the fire neuer goeth out.
Mahali ambako funza wake hawafi wala moto hauzimiki.]
47 And if thine eye cause thee to offende, plucke it out: it is better for thee to goe into the kingdome of God with one eye, then hauing two eyes, to be cast into hell fire, (Geenna )
Nalo jicho lako likikusababisha kutenda dhambi, lingʼoe. Ni afadhali kwako kuingia katika Ufalme wa Mungu ukiwa na jicho moja, kuliko kuwa na macho mawili lakini ukatupwa jehanamu, (Geenna )
48 Where their worme dyeth not, and the fire neuer goeth out.
mahali ambako “‘funza wake hawafi, wala moto wake hauzimiki.’
49 For euery man shalbe salted with fire: and euery sacrifice shalbe salted with salt.
Kila mmoja atatiwa chumvi kwa moto.
50 Salt is good: but if the salt be vnsauerie, wherewith shall it be seasoned? haue salt in your selues, and haue peace one with another.
“Chumvi ni nzuri, lakini ikipoteza ladha yake utaifanyaje ili iweze kukolea tena? Mwe na chumvi ndani yenu, mkaishi kwa amani, kila mmoja na mwenzake.”