< Mark 15 >

1 And anon in the dawning, the hie Priestes helde a Councill with the Elders, and the Scribes, and the whole Council, and bound Iesus, and led him away, and deliuered him to Pilate.
Asubuhi na mapema, viongozi wa makuhani, pamoja na wazee, walimu wa sheria na Baraza lote, wakafikia uamuzi. Wakamfunga Yesu, wakamchukua na kumkabidhi kwa Pilato.
2 Then Pilate asked him, Art thou the King of the Iewes? And hee answered, and sayde vnto him, Thou sayest it.
Pilato akamuuliza, “Je, wewe ndiye Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”
3 And the hie Priestes accused him of many things.
Viongozi wa makuhani wakamshtaki kwa mambo mengi.
4 Wherefore Pilate asked him againe, saying, Answerest thou nothing? beholde howe many things they witnesse against thee.
Pilato akamuuliza tena, “Je, huna la kujibu? Tazama ni mashtaka mangapi wanayaleta juu yako.”
5 But Iesus answered no more at all, so that Pilate marueiled.
Lakini Yesu hakujibu lolote, hivyo Pilato akashangaa.
6 Nowe at the feast, Pilate did deliuer a prisoner vnto them, whomesoeuer they woulde desire.
Ilikuwa desturi wakati wa Sikukuu ya Pasaka kumfungulia mfungwa yeyote ambaye watu wangemtaka.
7 Then there was one named Barabbas, which was bounde with his fellowes, that had made insurrection, who in the insurrection had committed murder.
Wakati huo, mtu aliyeitwa Baraba alikuwa amefungwa gerezani pamoja na waasi wengine waliokuwa wametekeleza uuaji wakati wa maasi.
8 And the people cried aloude, and began to desire that he woulde doe as he had euer done vnto them.
Ule umati wa watu ukamjia Pilato na kumwomba awafanyie kama ilivyokuwa desturi yake.
9 Then Pilate answered them, and said, Will ye that I let loose vnto you the King of ye Iewes?
Pilato akawauliza, “Mnataka niwafungulie huyu Mfalme wa Wayahudi?”
10 For he knewe that the hie Priestes had deliuered him of enuie.
Kwa maana yeye alitambua kuwa viongozi wa makuhani walikuwa wamemtia Yesu mikononi mwake kwa ajili ya wivu.
11 But the high Priestes had moued the people to desire that he would rather deliuer Barabbas vnto them.
Lakini viongozi wa makuhani wakauchochea ule umati wa watu wamwombe awafungulie Baraba badala yake.
12 And Pilate answered, and said againe vnto them, What will ye then that I doe with him, whom ye call the King of the Iewes?
Pilato akawauliza tena, “Basi mnataka nifanye nini na huyu mtu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
13 And they cried againe, Crucifie him.
Wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe!”
14 Then Pilate said vnto them, But what euill hath he done? And they cryed the more feruently, Crucifie him.
Pilato akawauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakapiga kelele kwa nguvu zaidi, wakisema, “Msulubishe!”
15 So Pilate willing to content the people, loosed them Barabbas, and deliuered Iesus, when he had scourged him, that he might be crucified.
Pilato, akitaka kuuridhisha ule umati wa watu, akawafungulia Baraba. Naye baada ya kuamuru Yesu achapwe mijeledi, akamtoa ili asulubishwe.
16 Then the souldiers led him away into the hall, which is the common hall, and called together the whole band,
Askari wakampeleka Yesu hadi kwenye ukumbi wa ndani wa jumba la kifalme, ndio Praitorio, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
17 And clad him with purple, and platted a crowne of thornes, and put it about his head,
Wakamvalisha Yesu joho la zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani.
18 And began to salute him, saying, Haile, King of the Iewes.
Wakaanza kumsalimu kwa dhihaka, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!”
19 And they smote him on the head with a reede, and spat vpon him, and bowed the knees, and did him reuerence.
Wakampiga kwa fimbo ya mwanzi tena na tena kichwani na kumtemea mate. Wakapiga magoti mbele yake, wakamsujudia kwa kumdhihaki.
20 And whe they had mocked him, they tooke the purple off him, and put his owne clothes on him, and led him out to crucifie him.
Walipokwisha kumdhihaki, wakamvua lile joho la zambarau, wakamvika tena nguo zake. Kisha wakamtoa nje ili wakamsulubishe.
21 And they compelled one that passed by, called Simon of Cyrene (which came out of the countrey, and was father of Alexander and Rufus) to beare his crosse.
Mtu mmoja kutoka Kirene, jina lake Simoni, baba yao Aleksanda na Rufo, alikuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shamba, nao wakamlazimisha kuubeba ule msalaba.
22 And they brought him to a place named Golgotha, which is by interpretation, the place of dead mens skulles.
Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha (maana yake ni Mahali pa Fuvu la Kichwa).
23 And they gaue him to drinke wine mingled with myrrhe: but he receiued it not.
Nao wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini hakuinywa.
24 And when they had crucified him, they parted his garments, casting lots for them, what euery man should haue.
Basi wakamsulubisha, nazo nguo zake wakagawana miongoni mwao kwa kuzipigia kura ili kuamua ni gani kila mtu ataichukua.
25 And it was the third houre, when they crucified him.
Ilikuwa yapata saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
26 And ye title of his cause was written aboue, THAT KING OF THE JEWES.
Tangazo likaandikwa la mashtaka dhidi yake lenye maneno haya: “Mfalme wa Wayahudi.”
27 They crucified also with him two theeues, the one on ye right hand, and the other on his left.
Pamoja naye walisulubiwa wanyangʼanyi wawili, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wa kushoto. [
28 Thus the Scripture was fulfilled, which sayth, And he was counted among the wicked.
Nayo maandiko yakatimizwa, yale yasemayo, “Alihesabiwa pamoja na watenda dhambi.]”
29 And they that went by, railed on him, wagging their heads, and saying, Hey, thou that destroyest the Temple, and buildest it in three dayes,
Watu waliokuwa wakipita njiani wakamtukana huku wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe ambaye utalivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu,
30 Saue thy selfe, and come downe from the crosse.
basi shuka kutoka msalabani na ujiokoe mwenyewe!”
31 Likewise also euen the hie Priests mocking, said among themselues with the Scribes, He saued other men, himselfe he cannot saue.
Vivyo hivyo, viongozi wa makuhani pamoja na walimu wa sheria wakamdhihaki miongoni mwao wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe!
32 Let Christ the King of Israel nowe come downe from the crosse, that we may see, and beleeue. They also that were crucified with him, reuiled him.
Basi huyu Kristo, huyu Mfalme wa Israeli, ashuke sasa kutoka msalabani, ili tupate kuona na kuamini.” Wale waliosulubiwa pamoja naye pia wakamtukana.
33 Nowe when the sixt houre was come, darkenesse arose ouer all the land vntill the ninth houre.
Ilipofika saa sita, giza liliifunika nchi yote hadi saa tisa.
34 And at the ninth houre Iesus cryed with a loude voyce, saying, Eloi, Eloi, lamma-sabachthani? which is by interpretation, My God, my God, why hast thou forsaken me?
Mnamo saa tisa, Yesu akapaza sauti, akalia, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?” (maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”)
35 And some of them that stoode by, when they heard it, said, Behold, he calleth Elias.
Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama karibu waliposikia hayo, wakasema, “Msikieni, anamwita Eliya.”
36 And one ranne, and filled a spondge full of vineger, and put it on a reede, and gaue him to drinke, saying, Let him alone: let vs see if Elias will come, and take him downe.
Mtu mmoja akaenda mbio, akachovya sifongo kwenye siki, akaiweka kwenye mwanzi na akampa Yesu ili anywe, akisema, “Basi mwacheni. Hebu tuone kama Eliya atakuja kumshusha kutoka hapo msalabani.”
37 And Iesus cryed with a loude voyce, and gaue vp the ghost.
Kisha Yesu akatoa sauti kuu, akakata roho.
38 And the vaile of the Temple was rent in twaine, from the toppe to the bottome.
Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili kuanzia juu hadi chini.
39 Nowe when the Centurion, which stoode ouer against him, sawe that he thus crying gaue vp the ghost, he saide, Truely this man was the Sonne of God.
Basi yule jemadari aliyekuwa amesimama hapo mbele ya msalaba wa Yesu aliposikia ile sauti yake na kuona jinsi alivyokata roho, akasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
40 There were also women, which beheld afarre off, among whom was Marie Magdalene, and Marie (the mother of Iames the lesse, and of Ioses) and Salome,
Walikuwepo pia wanawake waliokuwa wakiangalia kwa mbali. Miongoni mwao walikuwepo Maria Magdalene, na Maria mama yao Yakobo mdogo na Yose, pia na Salome.
41 Which also when he was in Galile, folowed him, and ministred vnto him, and many other women which came vp with him vnto Hierusalem.
Hawa walifuatana na Yesu na kushughulikia mahitaji yake alipokuwa Galilaya. Pia walikuwepo wanawake wengine wengi waliokuwa wamekuja pamoja naye Yerusalemu.
42 And nowe when the night was come (because it was the day of the preparation that is before the Sabbath)
Ilipofika jioni, kwa kuwa ilikuwa Siku ya Maandalizi, yaani siku moja kabla ya Sabato,
43 Ioseph of Arimathea, an honorable counsellour, which also looked for the kingdome of God, came, and went in boldly vnto Pilate, and asked the body of Iesus.
Yosefu wa Arimathaya, mtu aliyeheshimiwa katika Baraza, na ambaye alikuwa anautarajia Ufalme wa Mungu, akamwendea Pilato kwa ujasiri na kumwomba mwili wa Yesu.
44 And Pilate marueiled, if he were already dead, and called vnto him the Centurion, and asked of him whether he had bene any while dead.
Pilato alikuwa akijiuliza kama Yesu alikuwa amekwisha kufa. Hivyo akamwita yule jemadari, akamuuliza iwapo Yesu alikuwa amekwisha kufa.
45 And when he knewe the trueth of the Centurion, he gaue the body to Ioseph:
Baada ya kupata habari kutoka kwa yule jemadari kwamba kweli amekwisha kufa, Pilato akampa Yosefu ruhusa ya kuuchukua huo mwili.
46 Who bought a linnen cloth, and tooke him downe, and wrapped him in the linnen cloth, and laide him in a tombe that was hewen out of a rocke, and rolled a stone vnto the doore of the sepulchre:
Hivyo Yosefu akanunua kitambaa cha kitani safi, akaushusha mwili kutoka msalabani, akaufunga katika kile kitambaa cha kitani, na kuuweka ndani ya kaburi lililochongwa kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kwenye ingilio la kaburi.
47 And Marie Magdalene, and Marie Ioses mother, behelde where he should be layed.
Maria Magdalene na Maria mamaye Yose walipaona mahali pale alipolazwa.

< Mark 15 >