< Luke 7 >
1 When hee had ended all his sayings in the audience of the people, he entred into Capernaum.
Baada ya kusema yale aliyotaka watu wasikie, Yesu alikwenda Kafarnaumu.
2 And a certaine Ceturions seruant was sicke and readie to die, which was deare vnto him.
Huko kulikuwa na jemadari mmoja Mroma ambaye alikuwa na mtumishi wake aliyempenda sana. Huyu mtumishi alikuwa mgonjwa karibu kufa.
3 And when he heard of Iesus, hee sent vnto him the Elders of the Iewes, beseeching him that he would come, and heale his seruant.
Yule jemadari aliposikia habari za Yesu, aliwatuma wazee fulani Wayahudi waende kumwomba aje amponye mtumishi wake.
4 So they came to Iesus, and besought him instantly, saying that hee was worthy that hee should doe this for him:
Walipofika kwa Yesu, walimsihi sana, wakasema: “Huyu anastahili afanyiwe jambo hilo,
5 For he loueth, said they, our nation, and he hath built vs a Synagogue.
maana analipenda taifa letu, na ndiye aliyetujengea lile sunagogi.”
6 Then Iesus went with them: but when he was now not farre from the house, the Centurion sent friendes to him, saying vnto him, Lord, trouble not thy selfe: for I am not worthy that thou shouldest enter vnder my roofe:
Basi, Yesu akaenda pamoja nao. Alipokuwa karibu kufika nyumbani kwa yule jemadari Mroma, yule jemadari aliwatuma marafiki zake wamwambie Yesu: “Bwana, usijisumbue zaidi, maana mimi sistahili uingie nyumbani mwangu.
7 Wherefore I thought not my selfe worthy to come vnto thee: but say the word, and my seruant shalbe whole:
Ndio maana sikujiona nastahili hata kuja kwako; amuru tu, na mtumishi wangu atapona.
8 For I likewise am a man set vnder authoritie, and haue vnder mee souldiers, and I say vnto one, Goe, and he goeth: and to another, Come, and hee commeth: and to my seruant, Doe this, and he doeth it.
Mimi pia ni mtu niliye chini ya mamlaka, na ninao askari chini yangu. Namwambia mmoja, Nenda!, naye huenda; namwambia mwingine, Njoo! naye huja; na nikimwambia mtumishi wangu, Fanya hiki!, hufanya.”
9 When Iesus heard these things, he marueiled at him, and turned him, and said to the people, that followed him, I say vnto you, I haue not found so great faith, no not in Israel.
Yesu aliposikia hayo, alishangaa; halafu akauelekea ule umati wa watu uliokuwa unamfuata, akasema, “Sijaona imani kubwa namna hii hata katika Israeli.”
10 And when they that were sent, turned backe to the house, they founde the seruant that was sicke, whole.
Wale watu walipowasili nyumbani walimkuta yule mtumishi hajambo kabisa.
11 And it came to passe the day after, that he went into a citie called Nain, and many of his disciples went with him, and a great multitude.
Baadaye kidogo Yesu alikwenda katika mji mmoja uitwao Naini, na wafuasi wake pamoja na kundi kubwa la watu waliandamana naye.
12 Nowe when hee came neere to the gate of the citie, behold, there was a dead man caried out, who was the onely begotten sonne of his mother, which was a widowe, and much people of the citie was with her.
Basi, alipokuwa anakaribia lango la mji, walitokea watu wamebeba maiti ya kijana mmoja, mtoto wa pekee wa mama mjane. Watu wengi wa mji ule walikuwa pamoja na huyo mama.
13 And when the Lord sawe her, he had compassion on her, and said vnto her, Weepe not.
Bwana alipomwona mama huyo, alimwonea huruma, akamwambia, “Usilie.”
14 And he went and touched the coffin (and they that bare him, stoode still) and he said, Yong man, I say vnto thee, Arise.
Kisha akaenda, akaligusa lile jeneza, na wale waliokuwa wanalichukua wakasimama. Halafu akasema, “Kijana! Nakuamuru, amka!”
15 And he that was dead, sate vp, and began to speake, and he deliuered him to his mother.
Yule aliyekufa akaketi, akaanza kuongea. Na Yesu akamkabidhi kwa mama yake.
16 Then there came a feare on them all, and they glorified God, saying, A great Prophet is risen among vs, and God hath visited his people.
Watu wote walishikwa na hofu, wakawa wanamtukuza Mungu wakisema: “Nabii mkuu ametokea kati yetu. Mungu amekuja kuwakomboa watu wake.”
17 And this rumour of him went foorth throughout all Iudea, and throughout all the region round about.
Habari hizo zikaenea kote katika Uyahudi na katika nchi za jirani.
18 And the disciples of Iohn shewed him of all these things.
Wanafunzi wa Yohane walimpa habari Yohane juu ya mambo hayo yote. Naye Yohane, baada ya kuwaita wawili kati ya wanafunzi wake,
19 So Iohn called vnto him two certaine men of his disciples, and sent them to Iesus, saying, Art thou hee that should come, or shall we waite for another?
aliwatuma kwa Bwana wamwulize: “Wewe ndiye yule ajaye, au tumtazamie mwingine?”
20 And when the men were come vnto him, they said, Iohn Baptist hath sent vs vnto thee, saying, Art thou hee that should come, or shall we waite for another?
Wale wanafunzi walipomfikia Yesu wakamwambia, “Yohane Mbatizaji ametutuma kwako tukuulize: Wewe ndiye yule ajaye, au tumtazamie mwingine?”
21 And at that time, he cured many of their sickenesses, and plagues, and of euill spirites, and vnto many blinde men he gaue sight freely.
Wakati huohuo, Yesu alikuwa anawaponya watu wengi waliokuwa wanateseka kwa magonjwa na waliopagawa na pepo wabaya, akawawezesha vipofu wengi kuona tena.
22 And Iesus answered, and saide vnto them, Goe your wayes and shewe Iohn, what things ye haue seene and heard: that the blinde see, the halt goe, the lepers are cleansed, the deafe heare, the dead are raised, and the poore receiue the Gospel.
Basi, Yesu akawajibu, “Nendeni mkamwambie Yohane yale mliyojionea na kuyasikia: vipofu wanaona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa Habari njema.
23 And blessed is hee, that shall not be offended in me.
Heri mtu yule ambaye hana mashaka nami!”
24 And when the messengers of Iohn were departed, hee began to speake vnto the people, of Iohn, What went ye out into the wildernes to see? A reede shaken with the winde?
Hapo wajumbe wa Yohane walipokwisha kwenda zao, Yesu alianza kuyaambia makundi ya watu juu ya Yohane: “Mlikwenda kule jangwani, hivi mlitaka kuona kitu gani? Mlitaka kuona unyasi unaotikiswa na upepo?
25 But what went ye out to see? A man clothed in soft rayment? beholde, they which are gorgeously apparelled, and liue delicately, are in Kings courtes.
Basi, mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona mtu aliyevalia mavazi maridadi? La hasha! Wanaovaa mavazi maridadi na kuishi maisha ya anasa, hukaa katika majumba ya wafalme!
26 But what went ye foorth to see? A Prophet? yea, I say to you, and greater then a Prophet.
Basi, niambieni, mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona nabii? Naam, hakika ni zaidi ya nabii.
27 This is he of whom it is written, Beholde, I sende my messenger before thy face, which shall prepare thy way before thee.
Huyu Yohane ndiye anayesemwa katika Maandiko Matakatifu: Hapa ni mtumishi wangu, asema Bwana; ninamtuma akutangulie, akutayarishie njia.”
28 For I say vnto you, there is no greater Prophet then Iohn, among them that are begotten of women: neuerthelesse, hee that is the least in the kingdome of God, is greater then he.
Yesu akamalizia kwa kusema, “Nawaambieni, kati ya binadamu wote hakuna aliye mkubwa zaidi kuliko Yohane Mbatizaji. Hata hivyo, yule aliye mdogo kabisa katika ufalme wa Mungu ni mkubwa zaidi kuliko yeye.”
29 Then all the people that heard, and the Publicanes iustified God, being baptized with the baptisme of Iohn.
Waliposikia hayo watu wote na watoza ushuru waliusifu wema wa Mungu; hao ndio wale waliokuwa wameupokea ubatizo wa Yohane.
30 But the Pharises and the expounders of the Law despised the counsell of God against themselues, and were not baptized of him.
Lakini Mafarisayo na walimu wa Sheria walikataa mpango wa Mungu uliowahusu wakakataa kubatizwa na Yohane.
31 And the Lord saide, Whereunto shall I liken the men of this generation? and what thing are they like vnto?
Yesu akaendelea kusema, “Basi, nitawafananisha watu wa kizazi hiki na kitu gani? Ni watu wa namna gani?
32 They are like vnto litle children sitting in the market place, and crying one to another, and saying, We haue piped vnto you, and ye haue not daunced: we haue mourned to you, and ye haue not wept.
Ni kama vijana waliokuwa wamekaa sokoni na kuambiana, kikundi kimoja na kingine: Tumewapigieni ngoma, lakini hamkucheza! Tumeomboleza, lakini hamkulia!
33 For Iohn Baptist came, neither eating bread, nor drinking wine: and ye say, He hath the deuil.
Kwa maana Yohane alikuja, yeye alifunga na hakunywa divai, nanyi mkasema: Amepagawa na pepo!
34 The Sonne of man is come, and eateth and drinketh: and ye say, Beholde, a man which is a glutton, and a drinker of wine, a friend of Publicanes and sinners:
Akaja Mwana wa Mtu; anakula na kunywa, mkasema: Mwangalieni mlafi huyu na mlevi; rafiki ya watoza ushuru na wenye dhambi!
35 But wisdome is iustified of all her children.
Hata hivyo, hekima ya Mungu imethibitishwa kuwa njema na wote wale wanaoikubali.”
36 And one of the Pharises desired him that hee would eate with him: and hee went into the Pharises house, and sate downe at table.
Mfarisayo mmoja alimwalika Yesu kula chakula nyumbani kwake. Akaingia nyumbani mwa huyo Mfarisayo, akakaa kula chakula.
37 And beholde, a woman in the citie, which was a sinner, when she knewe that Iesus sate at table in the Pharises house, shee brought a boxe of oyntment.
Basi, katika mji ule kulikuwa na mama mmoja aliyekuwa anaishi maisha mabaya. Alipopata habari kwamba Yesu yuko nyumbani kwa huyo Mfarisayo, alichukua chupa ya alabasta yenye marashi.
38 And shee stoode at his feete behinde him weeping, and began to wash his feete with teares, and did wipe them with the heares of her head, and kissed his feete, and anoynted them with the oyntment.
Akaja, akasimama karibu na miguu yake Yesu, akilia, na machozi yake yakamdondokea Yesu miguuni. Huyo mwanamke akaipangusa miguu ya Yesu kwa nywele zake. Kisha akaibusu na kuipaka yale marashi.
39 Nowe when the Pharise which bade him, saw it, he spake within himselfe, saying, If this man were a Prophet, hee woulde surely haue knowen who, and what maner of woman this is which toucheth him: for she is a sinner.
Yule Mfarisayo aliyemwalika Yesu alipoona hayo, akawaza moyoni mwake, “Kama mtu huyu angekuwa kweli nabii angejua huyu mwanamke ni wa namna gani, ya kwamba ni mwenye dhambi.”
40 And Iesus answered, and saide vnto him, Simon, I haue somewhat to say vnto thee. And he said, Master, say on.
Yesu akamwambia huyo Mfarisayo, “Simoni, ninacho kitu cha kukwambia.” Naye Simoni akamwambia, “Ndio Mwalimu, sema.” Yesu akasema,
41 There was a certaine lender which had two detters: the one ought fiue hundreth pence, and the other fiftie:
“Watu wawili walikuwa wamemkopa mtu fedha: mmoja alikuwa amekopa dinari mia tano, na mwingine hamsini.
42 When they had nothing to pay, he forgaue them both: Which of them therefore, tell mee, will loue him most?
Waliposhindwa kulipa madeni yao, huyo mtu aliwasamehe wote wawili. Sasa ni yupi kati ya hao wawili atampenda zaidi huyo bwana?”
43 Simon answered, and said, I suppose that he, to whom he forgaue most. And he said vnto him, Thou hast truely iudged.
Simoni akamjibu, “Ni dhahiri kwamba yule aliyesamehewa deni kubwa zaidi atampenda zaidi yule bwana.” Yesu akamwambia, “Sawa.”
44 Then he turned to the woman, and said vnto Simon, Seest thou this woman? I entred into thine house, and thou gauest mee no water to my feete: but she hath washed my feete with teares, and wiped them with the heares of her head.
Halafu akamgeukia yule mwanamke na kumwambia Simoni, “Unamwona huyu mwanamke, sivyo? Basi, mimi nilipoingia hapa nyumbani kwako hukunipa maji ya kunawa miguu yangu; lakini mwanamke huyu ameniosha miguu yangu kwa machozi yake na kunipangusa kwa nywele zake.
45 Thou gauest me no kisse: but she, since the time I came in, hath not ceased to kisse my feete.
Wewe hukunisalimu kwa kunibusu, lakini huyu mwanamke tangu nilipoingia hapa amekuwa akiibusu miguu yangu.
46 Mine head with oyle thou didest not anoint: but she hath anoynted my feete with oyntment.
Wewe hukunionyesha ukarimu wako kwa kunipaka mafuta kichwani, lakini huyu mwanamke amefanya hivyo kwa kunipaka mafuta miguu yangu.
47 Wherefore I say vnto thee, many sinnes are forgiuen her: for she loued much. To whom a litle is forgiuen, he doeth loue a litle.
Kwa hiyo nakwambia amesamehewa dhambi zake nyingi kwa kuwa ameonyesha upendo mkubwa. Mwenye kusamehe kidogo, hupenda kidogo.”
48 And he saide vnto her, Thy sinnes are forgiuen thee.
Basi, Yesu akamwambia yule mwanamke, “Umesamehewa dhambi zako.”
49 And they that sate at table with him, began to say within themselues, Who is this that euen forgiueth sinnes?
Na hapo wale waliokuwa pamoja naye mezani wakaulizana, “Ni mtu wa namna gani huyu awezaye kusamehe dhambi?”
50 And he said to the woman, Thy faith hath saued thee: goe in peace.
Naye Yesu akamwambia yule mwanamke, “Imani yako imekuokoa; nenda kwa amani.”