< Luke 20 >
1 And it came to passe, that on one of those dayes, as he taught the people in the Temple, and preached the Gospel, the hie Priests and the Scribes came vpon him with the Elders,
Siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuwahubiria juu ya Habari Njema, makuhani wakuu na walimu wa Sheria pamoja na wazee walifika,
2 And spake vnto him, saying, Tell vs by what authoritie thou doest these things, or who is hee that hath giuen thee this authoritie?
wakasema, “Tuambie! Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani?”
3 And he answered, and sayde vnto them, I also will aske you one thing: tell me therefore:
Yesu akawaambia, “Na mimi nitawaulizeni swali:
4 The baptisme of Iohn, was it from heauen, or of men?
mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa Mungu au kwa watu?”
5 And they reasoned within themselues, saying, If we shall say, From heauen, he will say, Why then beleeued ye him not?
Lakini wao wakajadiliana hivi: “Tukisema yalitoka mbinguni, yeye atatuuliza: Mbona hamkumsadiki?
6 But if we shall say, Of men, all the people will stone vs: for they be perswaded that Iohn was a Prophet.
Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii.”
7 Therefore they answered, that they could not tell whence it was.
Basi, wakamwambia, “Hatujui mamlaka hayo yalitoka wapi.”
8 Then Iesus sayd vnto them, Neither tell I you, by what authoritie I doe these things.
Yesu akawaambia, “Hata mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”
9 Then began he to speake to ye people this parable, A certaine man planted a vineyarde, and let it forth to husbandmen: and went into a strange countrey, for a great time.
Yesu akaendelea kuwaambia watu mfano huu: “Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima; kisha akasafiri hadi nchi ya mbali, akakaa huko kwa muda mrefu.
10 And at the time conuenient he sent a seruant to the husbandmen, that they should giue him of the fruite of the vineyard: but the husbandmen did beate him, and sent him away emptie.
Wakati wa mavuno, mtu huyo alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima, akachukue sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga mtumishi huyo wakamrudisha mikono mitupu.
11 Againe he sent yet another seruant: and they did beate him, and foule entreated him, and sent him away emptie.
Yule bwana akamtuma tena mtumishi mwingine; lakini wao wakampiga huyo vilevile na kumtendea vibaya, wakamrudisha mikono mitupu.
12 Moreouer he sent the third, and him they wounded, and cast out.
Akamtuma tena wa tatu; huyu naye, baada ya kumwumiza, wakamfukuza.
13 Then sayd the Lord of the vineyard, What shall I doe? I will send my beloued sonne: it may be that they will doe reuerence, when they see him.
Yule mwenye shamba akafikiri: Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpenzi; labda watamjali yeye.
14 But when the husbandmen sawe him, they reasoned with themselues, saying, This is the heire: come, let vs kill him, that the inheritance may be ours.
Wale wakulima walipomwona tu, wakasemezana: Huyu ndiye mrithi. Basi, tumwue ili urithi wake uwe wetu.
15 So they cast him out of the vineyarde, and killed him. What shall the Lord of the vineyarde therefore doe vnto them?
Basi, wakamtoa nje ya lile shamba la mizabibu, wakamwua.” Yesu akauliza, “Yule mwenye shamba atawafanya nini hao wakulima?
16 He will come and destroy these husbandmen, and wil giue out his vineyard to others. But when they heard it, they sayd, God forbid.
Atakuja kuwaangamiza wakulima hao, na atawapa wakulima wengine hilo shamba la mizabibu.” Watu waliposikia maneno hayo, walisema: “Hasha! Yasitukie hata kidogo!”
17 And he beheld them, and said, What meaneth this then that is written, The stone that the builders refused, that is made the head of the corner?
Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, “Maandiko haya Matakatifu yana maana gani basi? Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi!
18 Whosoeuer shall fall vpon that stone, shall be broken: and on whomsoeuer it shall fall, it will grinde him to pouder.
Mtu yeyote akianguka juu ya jiwe hilo, atavunjika vipandevipande; na likimwangukia mtu yeyote, litamsaga kabisa.”
19 Then the hie Priests, and the Scribes the same houre went about to lay hands on him: (but they feared the people) for they perceiued that he had spoken this parable against them.
Walimu wa Sheria na makuhani wakuu walifahamu kwamba mfano huo ulikuwa unawahusu, na hivyo walitaka kumkamata palepale, ila tu waliogopa watu.
20 And they watched him, and sent forth spies, which should faine themselues iust men, to take him in his talke, and to deliuer him vnto the power and authoritie of the gouernour.
Basi, wakawa wanatafuta wakati wa kufaa. Wakawahonga watu fulani wajisingizie kuwa wema, wakawatuma wamnase Yesu kwa maswali, na hivyo waweze kumtia nguvuni na kumpeleka kwa wakuu wa serikali.
21 And they asked him, saying, Master, we know that thou sayest, and teachest right, neither doest thou accept mans person, but teachest the way of God truely.
Hao wapelelezi wakamwambia, “Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli; tunajua kwamba wewe huna ubaguzi; wewe wafundisha ukweli juu ya njia ya Mungu.
22 Is it lawfull for vs to giue Cesar tribute or no?
Basi, twambie kama ni halali, au la, kulipa kodi kwa Kaisari!”
23 But he perceiued their craftines, and sayd vnto them, Why tempt ye me?
Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
24 Shew me a penie. Whose image and superscription hath it? They answered, and sayd, Cesars.
“Nionyesheni sarafu. Je, sura na chapa ni vya nani?”
25 Then he sayd vnto them, Giue then vnto Cesar the things which are Cesars, and to God those which are Gods.
Nao wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Yesu akawaambia, “Basi, mpeni Kaisari vilivyo vyake Kaisari, na Mungu vilivyo vyake Mungu.”
26 And they could not reproue his saying before the people: but they marueiled at his answere, and helde their peace.
Hawakufaulu kumnasa kwa neno lolote pale mbele ya watu na hivyo wakakaa kimya wakilistaajabia jibu lake.
27 Then came to him certaine of the Sadduces (which denie that there is any resurrection) and they asked him,
Kisha Masadukayo, ambao husema kwamba wafu hawafufuki, wakamjia Yesu, wakasema:
28 Saying, Master, Moses wrote vnto vs, If any mans brother die hauing a wife, and hee die without children, that his brother should take his wife, and raise vp seede vnto his brother.
“Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu ya mtu fulani akifa na kumwacha mjane wake bila watoto, ni lazima ndugu yake amchukue huyo mama mjane, amzalie watoto ndugu yake marehemu.
29 Now there were seuen brethren, and the first tooke a wife, and he dyed without children.
Sasa, wakati mmoja kulikuwa na ndugu saba. Yule wa kwanza alioa na baadaye akafa bila kuacha mtoto.
30 And the second tooke the wife, and he dyed childelesse.
Yule ndugu wa pili akamwoa yule mjane, naye pia, akafa;
31 Then the third tooke her: and so likewise the seuen dyed, and left no children.
na ndugu wa tatu vilevile. Mambo yakawa yaleyale kwa wote saba—wote walikufa bila kuacha watoto.
32 And last of all the woman dyed also.
Mwishowe akafa pia yule mwanamke.
33 Therefore at the resurrection, whose wife of them shall she be? for seuen had her to wife.
Je, siku wafu watakapofufuliwa, mwanamke huyo atakuwa mke wa nani? Alikuwa ameolewa na wote saba.”
34 Then Iesus answered, and sayd vnto them, The children of this world marry wiues, and are married. (aiōn )
Yesu akawaambia, “Watu wa nyakati hizi huoa na kuolewa; (aiōn )
35 But they which shalbe counted worthy to enioy that world, and the resurrection from the dead, neither marry wiues, neither are married. (aiōn )
lakini wale ambao Mungu atawawezesha kushiriki ule wakati wa ufufuo, hawataoa wala kuolewa. (aiōn )
36 For they can die no more, forasmuch as they are equall vnto the Angels, and are the sonnes of God, since they are the children of the resurrection.
Ama hakika, hawawezi kufa tena, kwa sababu watakuwa kama malaika, na ni watoto wa Mungu kwa vile wamefufuliwa katika wafu.
37 And that the dead shall rise againe, euen Moses shewed it besides the bush, when he said, The Lord is the God of Abraham, and the God of Isaac, and the God of Iacob.
Lakini, kwamba kuna kufufuka kutoka wafu, hata Mose alithibitisha jambo hilo katika Maandiko Matakatifu. Katika sehemu ya Maandiko Matakatifu juu ya kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto, anamtaja Bwana kama Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.
38 For he is not the God of the dead, but of them which liue: for all liue vnto him.
Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa wale walio hai; maana wale aliowaita kwake, wanaishi naye.”
39 Then certaine of the Scribes answered, and sayd, Master, thou hast well sayd.
Baadhi ya wale walimu wa Sheria wakasema, “Mwalimu, umejibu vema kabisa.”
40 And after that, durst they not aske him any thing at all.
Walisema hivyo kwa sababu hawakuthubutu kumwuliza tena maswali mengine.
41 Then sayd he vnto them, Howe say they that Christ is Dauids sonne?
Yesu akawauliza, “Yasemekanaje kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
42 And Dauid himselfe sayth in the booke of the Psalmes, The Lord sayd vnto my Lord, Sit at my right hand,
Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia
43 Till I shall make thine enemies thy footestoole.
mpaka niwafanye adui zako kama kiti cha kuwekea miguu yako.
44 Seeing Dauid called him Lord, howe is he then his sonne?
Ikiwa Daudi anamwita yeye, Bwana, basi atakuwaje mwanawe?”
45 Then in the audience of all the people he sayd vnto his disciples,
Yesu aliwaambia wanafunzi wake mbele ya watu wote,
46 Beware of the Scribes, which willingly go in long robes, and loue salutations in the markets, and the highest seates in the assemblies, and the chiefe roomes at feastes:
“Jihadharini na walimu wa Sheria ambao hupenda kupitapita wamevalia kanzu. Hupenda kusalimiwa na watu kwa heshima masokoni, huketi mahali pa heshima katika masunagogi na kuchukua nafasi za heshima katika karamu.
47 Which deuoure widowes houses, and in shewe make long prayers: These shall receiue greater damnation.
Huwadhulumu wajane huku wakisingizia kuwa wema kwa kusali sala ndefu. Hao watapata hukumu kali zaidi!”