< Luke 17 >

1 Then said he to his disciples, It can not be auoided, but that offences will come, but wo be to him by whome they come.
Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mambo yanayosababisha watu watende dhambi hayana budi kutukia. Lakini ole wake mtu yule anayeyasababisha.
2 It is better for him that a great milstone were hanged about his necke, and that he were cast into ye sea, then that he should offende one of these litle ones.
Ingekuwa heri kama mtu huyo angefungiwa jiwe la kusagia shingoni na kutoswa baharini, kuliko kumsababisha mmojawapo wa hawa wadogo kutenda dhambi.
3 Take heede to your selues: if thy brother trespasse against thee, rebuke him: and if hee repent, forgiue him.
Kwa hiyo, jilindeni. “Kama ndugu yako akikukosea mwonye, naye akitubu, msamehe.
4 And though he sinne against thee seuen times in a day, and seuen times in a day turne againe to thee, saying, It repenteth mee, thou shalt forgiue him.
Kama akikukosea mara saba kwa siku moja na mara saba kwa siku moja akaja kwako akisema, ‘Ninatubu,’ msamehe.”
5 And the Apostles saide vnto the Lord, Increase our faith.
Mitume wake wakamwambia Bwana, “Tuongezee imani.”
6 And the Lord said, If ye had faith, as much as is a graine of mustard seede, and should say vnto this mulberie tree, Plucke thy selfe vp by the rootes, and plant thy selfe in the sea, it should euen obey you.
Bwana akawajibu, “Kama mkiwa na imani ndogo kama punje ya haradali, mngeweza kuuambia mti huu wa mkuyu, ‘Ngʼoka ukaote baharini,’ nao ungewatii.
7 Who is it also of you, that hauing a seruant plowing or feeding cattell, woulde say vnto him by and by, when hee were come from the fielde, Goe, and sit downe at table?
“Ikiwa mmoja wenu ana mtumishi anayelima shambani au anayechunga kondoo, je, mtumishi huyo arudipo atamwambia, ‘Karibu hapa keti ule chakula?’
8 And woulde not rather say to him, Dresse wherewith I may suppe, and girde thy selfe, and serue mee, till I haue eaten and drunken, and afterward eate thou, and drinke thou?
Je, badala yake, hatamwambia, ‘Niandalie chakula, nile, jifunge unitumikie ninapokula na kunywa; baadaye waweza kula na kunywa?’
9 Doeth he thanke that seruant, because hee did that which was commanded vnto him? I trowe not.
Je, huyo mtu atamshukuru mtumishi huyo kwa kutimiza yale aliyoamriwa?
10 So likewise yee, when yee haue done all those things, which are commanded you, say, We are vnprofitable seruants: wee haue done that which was our duetie to doe.
Vivyo hivyo nanyi mkiisha kufanya mliyoagizwa, semeni, ‘Sisi tu watumishi tusiostahili; tumefanya tu yale tuliyopaswa kufanya.’”
11 And so it was when he went to Hierusalem, that he passed through the middes of Samaria, and Galile.
Yesu alipokuwa njiani akienda Yerusalemu, alipitia mpakani mwa Samaria na Galilaya.
12 And as hee entred into a certaine towne, there met him tenne men that were lepers, which stoode a farre off.
Alipokuwa akiingia kwenye kijiji kimoja, watu kumi waliokuwa na ukoma wakakutana naye. Wakasimama mbali,
13 And they lift vp their voyces and saide, Iesus, Master, haue mercie on vs.
wakapaza sauti, wakasema, “Yesu, Bwana, tuhurumie!”
14 And when he saw them, he said vnto them, Goe, shewe your selues vnto the Priestes. And it came to passe, that as they went, they were clensed.
Alipowaona akawaambia, “Nendeni mkajionyeshe kwa makuhani.” Nao walipokuwa njiani wakienda, wakatakasika.
15 Then one of them, when hee sawe that hee, was healed, turned backe, and with a loude voyce praised God,
Mmoja wao alipoona kwamba amepona, akarudi kwa Yesu, akimsifu Mungu kwa sauti kuu.
16 And fell downe on his face at his feete, and gaue him thankes: and he was a Samaritan.
Akajitupa miguuni mwa Yesu akamshukuru. Yeye alikuwa Msamaria.
17 And Iesus answered, and said, Are there not tenne clensed? but where are the nine?
Yesu akauliza, “Je, hawakutakaswa wote kumi? Wako wapi wale wengine tisa?
18 There is none founde that returned to giue God praise, saue this stranger.
Hakuna hata mmoja aliyeonekana kurudi ili kumshukuru Mungu isipokuwa huyu mgeni?”
19 And he saide vnto him, Arise, goe thy way, thy faith hath saued thee.
Yesu akamwambia, “Inuka na uende zako, imani yako imekuponya.”
20 And when hee was demaunded of the Pharises, when the kingdome of God shoulde come, he answered them, and said, The kingdome of God commeth not with obseruation.
Yesu alipoulizwa na Mafarisayo Ufalme wa Mungu utakuja lini, yeye akawajibu, “Ufalme wa Mungu hauji kwa kuchunguza kwa bidii,
21 Neither shall men say, Loe here, or lo there: for behold, the kingdome of God is within you.
wala watu hawatasema, ‘Huu hapa,’ au ‘Ule kule,’ kwa maana Ufalme wa Mungu umo ndani yenu.”
22 And he saide vnto the disciples, The dayes will come, when ye shall desire to see one of the dayes of the Sonne of man, and ye shall not see it.
Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Wakati utafika ambapo mtatamani kuiona moja ya siku ya Mwana wa Adamu, lakini hamtaiona.
23 Then they shall say to you, Behold here, or beholde there: but goe not thither, neither follow them.
Watu watawaambia, ‘Yule kule!’ Au, ‘Huyu hapa!’ Msiwakimbilie.
24 For as the lightening that lighteneth out of the one part vnder heauen, shineth vnto the other part vnder heauen, so shall the Sonne of man be in his day.
Kwa maana kama vile umeme wa radi umulikavyo katika anga kuanzia mwisho mmoja hadi mwingine, ndivyo atakavyokuwa Mwana wa Adamu katika siku yake.
25 But first must he suffer many things, and be reprooued of this generation.
Lakini kwanza itampasa kuteseka katika mambo mengi na kukataliwa na kizazi hiki.
26 And as it was in the dayes of Noe, so shall it be in the dayes of the Sonne of man.
“Kama ilivyokuwa siku za Noa, ndivyo itakavyokuwa katika siku za Mwana wa Adamu.
27 They ate, they dranke, they married wiues, and gaue in marriage vnto the day that Noe went into the Arke: and the flood came, and destroyed them all.
Watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka siku ile Noa alipoingia katika safina. Ndipo gharika ikaja na kuwaangamiza wote.
28 Likewise also, as it was in the dayes of Lot: they ate, they dranke, they bought, they solde, they planted, they built.
“Ndivyo ilivyokuwa katika siku za Loti: Watu walikuwa wakila na kunywa, wakinunua na kuuza, wakilima na kujenga.
29 But in the day that Lot went out of Sodom, it rained fire and brimstone from heauen, and destroyed them all.
Lakini siku ile Loti alipoondoka Sodoma, ikanyesha mvua ya moto na kiberiti kutoka mbinguni ukawaangamiza wote.
30 After these ensamples shall it be in the day when the Sonne of man is reueiled.
“Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile Mwana wa Adamu atakapofunuliwa.
31 At that day hee that is vpon the house, and his stuffe in ye house, let him not come downe to take it out: and he that is in the fielde likewise, let him not turne backe to that he left behinde.
Siku hiyo, mtu yeyote aliye juu ya dari ya nyumba yake, hata vitu vyake vikiwa ndani ya hiyo nyumba, asishuke kuvichukua. Vivyo hivyo mtu aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua chochote.
32 Remember Lots wife.
Mkumbukeni mke wa Loti!
33 Whosoeuer will seeke to saue his soule, shall loose it: and whosoeuer shall loose it, shall get it life.
Mtu yeyote anayejaribu kuyaokoa maisha yake atayapoteza, na yeyote atakayeyapoteza maisha yake atayaokoa.
34 I tell you, in that night there shall be two in one bed: the one shalbe receiued, and the other shalbe left.
Nawaambia, usiku huo watu wawili watakuwa wamelala kitanda kimoja; naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa.
35 Two women shalbe grinding together: the one shalbe taken, and the other shalbe left.
Wanawake wawili watakuwa wanasaga nafaka pamoja; naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa. [
36 Two shalbe in the fielde: one shalbe receiued, and another shalbe left.
Wanaume wawili watakuwa wanafanya kazi pamoja shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.]”
37 And they answered, and saide to him, Where, Lord? And he said vnto them, Wheresoeuer the body is, thither shall also the eagles bee gathered together.
Kisha wakamuuliza, “Haya yatatukia wapi Bwana?” Akawaambia, “Pale ulipo mzoga, huko ndiko tai watakapokusanyika.”

< Luke 17 >