< Luke 13 >

1 There were certaine men present at the same season, that shewed him of the Galileans, whose blood Pilate had mingled with their sacrifices.
Kwa wakataihuo huo, kulikuwa na baadhi watu waliomtaarifu juu ya Wagalilaya ambao Pilato aliwaua na kuchanganya damu yao na sadaka zao.
2 And Iesus answered, and saide vnto them, Suppose ye, that these Galileans were greater sinners then al the other Galileans, because they haue suffered such things?
Yesu akajibu na kuwaambia, “Je mwadhani kuwa Wagalilaya hao walikuwa na dhambi kuliko Wagalilaya wengine wote ndiyo maana wamepatwa na mabaya hayo?
3 I tell you, nay: but except ye amend your liues, ye shall all likewise perish.
Hapana, nawaambia, lakini msipotubu, nanyi mtaangamia vivyo hivyo.
4 Or thinke you that those eighteene, vpon whom the tower in Siloam fell, and slewe them, were sinners aboue all men that dwel in Hierusalem?
Au wale watu kumi na nane katika Siloamu ambao mnara ulianguka na kuwaua, mnafikiri wao walikuwa wenye dhambi zaidi kuliko watu wengine katika Yerusalemu?
5 I tell you, nay: but except ye amend your liues, ye shall all likewise perish.
Hapana, mimi nasema, lakini kama msipotubu, ninyi nyote pia mtaangamia.
6 He spake also this parable, A certaine man had a figge tree planted in his vineyard: and he came and sought fruite thereon, and found none.
Yesu aliwaambia mfano huu, “Mtu mmoja alikuwa na mtini umepandwa katika shamba lake na alikwenda kutafuta matunda juu yake lakini hakupata.
7 Then said he to the dresser of his vineyard, Behold, this three yeeres haue I come and sought fruite of this figge tree, and finde none: cut it downe: why keepeth it also the ground barren?
Akamwambia mtunza bustani, 'Tazama, kwa miaka mitatu nimekuja na kujaribu kutafuta matunda kwenye mtini huu lakini sikupata. Uukate. Kwani ulete uharibifu wa ardhi?
8 And he answered, and said vnto him, Lord, let it alone this yeere also, till I digge round about it, and doung it.
Mtunza bustani akajibu na kusema, 'uache mwaka huu ili niupalilie na kuweka mbolea juu yake.
9 And if it beare fruite, well: if not, then after thou shalt cut it downe.
Kama ukizaa matunda mwaka ujao, ni vema; lakini kama hautazaa, uukate!”'
10 And he taught in one of ye Synagogues on the Sabbath day.
Sasa Yesu alikuwa akifundisha katika mojawapo ya Masinagogi wakati wa Sabato.
11 And behold, there was a woman which had a spirit of infirmitie eighteene yeeres, and was bowed together, and coulde not lift vp her selfe in any wise.
Tazama, alikuwepo mama mmoja ambaye kwa miaka kumi na minane alikuwa na rohomchafu wa udhaifu, na yeye alikuwa amepinda na hana uwezo kabisa wa kusimama.
12 When Iesus sawe her, he called her to him, and said to her, Woman, thou art loosed from thy disease.
Yesu alipomwona, alimwita, akamwambia, “Mama, umewekwa huru kutoka kwenye udhaifu wako.”
13 And he laide his handes on her, and immediately she was made straight againe, and glorified God.
Akaweka mikono yake juu yake, na mara mwili wake akajinyoosha na akamtukuza Mungu.
14 And the ruler of the Synagogue answered with indignation, because that Iesus healed on the Sabbath day, and said vnto the people, There are sixe dayes in which men ought to worke: in them therefore come and be healed, and not on the Sabbath day.
Lakini mkuu wa sinagogi alikasirika kwa sababu Yesu alikuwa amemponya siku ya Sabato. Hivyo mtawala akajibu akawambia makutano, “Kuna siku sita ambazo ni lazima kufanya kazi. Njoni kuponywa basi, si katika siku ya Sabato. '
15 Then answered him the Lord, and said, Hypocrite, doth not eche one of you on the Sabbath day loose his oxe or his asse from the stall, and leade him away to the water?
Bwana akamjibu na akasema, “wanafiki! Hakuna kila mmoja wenu kufungua punda wako au ng'ombe kutoka zizini na kuwaongoza kumpeleka kunywa siku ya Sabato?
16 And ought not this daughter of Abraham, whom Satan had bound, loe, eighteene yeeres, be loosed from this bond on the Sabbath day?
Hivyo pia binti wa Abrahamu, ambaye Shetani amemfunga kwa miaka kumi na minane, je haikumpasa kifungo chake kisifunguliwe siku ya sabato?”
17 And when he said these things, all his aduersaries were ashamed: but all the people reioyced at all the excellent things, that were done by him.
Alipokuwa akisema maneno hayo, wale wote waliompinga waliona aibu, bali makutano wote wa wengine walishangilia kwa ajili ya mambo ya ajabu aliyotenda.
18 Then said he, What is the kingdome of God like? or whereto shall I compare it?
Yesu akasema, “Ufalme wa Mungu unafanana na nini, na naweza kuulinganisha na nini?
19 It is like a graine of mustard seede, which a man tooke and sowed in his garden, and it grewe, and waxed a great tree, and the foules of the heauen made nestes in the branches thereof.
Ni kama mbegu ya haradari aliyoitwaa mtu mmoja na kuipanda shambani mwake, na ikamea ikawa mti mkubwa, na ndege wa mbinguni wakajenga viota vyao katika matawi yake.
20 And againe he said, Whereunto shall I liken the kingdome of God?
Tena akasema, “Niufananishe na nini ufalme wa Mungu?
21 It is like leauen, which a woman tooke, and hid in three peckes of floure, till all was leauened.
Ni kama chachu ambayo mwanamke aliichukua na kuchanganyakwenye vipimo vitatu vya unga hata ukaumuka.”
22 And he went through all cities and townes, teaching, and iourneying towards Hierusalem.
Yesu alitembelea kila mji na kijiji njiani akielekea Yerusalemu na kuwafundisha.
23 Then saide one vnto him, Lord, are there fewe that shalbe saued? And he said vnto them,
Mtu mmoja akauliza, “Bwana, ni watu wachache tu watakaookolewa?” Hivyo akawaambia,
24 Striue to enter in at the straite gate: for many, I say vnto you, will seeke to enter in, and shall not be able.
“Jitahidi kuingia kwa kupitia mlango mwembamba, kwa sababu wengi watajaribu na hawataweza kuingia.
25 When the good man of the house is risen vp, and hath shut to the doore, and ye begin to stand without, and to knocke at the doore, saying, Lord, Lord, open to vs, and he shall answere and say vnto you, I know you not whence ye are,
Mara baada ya mmiliki wa nyumba kusimama na kufunga mlango, basi mtasimama nje na kupiga hodi mlangoni na kusema, Bwana, Bwana, tufungulie yeye atajibu na kuwaambia, siwajui ninyi wala mtokako.'
26 Then shall ye begin to say, We haue eaten and drunke in thy presence, and thou hast taught in our streetes.
Ndipo mtasema, Tulikula na kunywa mbele yako na wewe ulifundisha katika mitaa yetu.”
27 But he shall say, I tell you, I knowe you not whence ye are: depart from me, all ye workers of iniquitie.
Lakini yeye atawajibu, `nawaambia, siwajui mtokako, ondokeni kwangu, ninyi watenda maovu!'
28 There shall be weeping and gnashing of teeth when ye shall see Abraham and Isaac, and Iacob, and all the Prophets in the kingdome of God, and your selues thrust out at doores.
Kutakuwa na kilio na kusaga meno wakati mtakapowaona Abrahamu, Isaka, Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, lakini ninyi wenyewe mumetupwa nje.
29 Then shall come many from the East, and from the West, and from the North, and from the South, and shall sit at Table in the kingdome of God.
Watafika kutoka Mashariki, Magharibi, Kaskazini na Kusini, na kupumzika katika meza ya chakula cha jioni katika ufalme wa Mungu.
30 And beholde, there are last, which shalbe first, and there are first, which shalbe last.
Na tambua hili, wa mwisho ni wa kwanza na wa kwanza atakuwa wa mwisho.”
31 The same day there came certaine Pharises, and said vnto him, Depart, and goe hence: for Herod will kill thee.
Muda mfupi baadaye, baadhi ya Mafarisayo walikuja na kumwambia, “Nenda na ondoka hapa kwa sababu Herode anataka kukuua.”
32 Then said he vnto them, Goe ye and tell that foxe, Beholde, I cast out deuils, and will heale still to day, and to morowe, and the third day I shalbe perfected.
Yesu akasema, “Nendeni mkamwambie yule mbweha, `Tazama, ninawafukuza pepo na kufanya uponyaji leo na kesho, na siku ya tatu nitatimiza lengo langu.
33 Neuerthelesse I must walke to day, and to morowe, and the day following: for it cannot be that a Prophet should perish out of Hierusalem.
Katika hali yoyote, ni muhimu kwa ajili yangu kuendelea leo, kesho, na siku iliyofuata, kwa vile haikubaliki kumuua nabii mbali na Yerusalemu.
34 O Hierusalem, Hierusalem, which killest the Prophets, and stonest them that are sent to thee, howe often would I haue gathered thy children together, as the henne gathereth her brood vnder her wings, and ye would not!
Yerusalemu, Yerusalemu, nani anawaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwenu. Mara ngapi nimetaka kuwakusanya watoto wenu kama vile kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mbawa zake, lakini humkulitaka hili.
35 Beholde, your house is left vnto you desolate: and verely I tell you, ye shall not see me vntill the time come that ye shall say, Blessed is he that commeth in the Name of the Lord.
Tazama, nyumba yako imetelekezwa. Nami nawaambia, hamuwezi kuniona hata mtakaposema 'Amebarikiwa huyo ajaye kwa jina la Bwana.'”

< Luke 13 >