< Luke 12 >

1 In the meane time, there gathered together an innumerable multitude of people, so that they trode one another: and he began to say vnto his disciples first, Take heede to your selues of the leauen of the Pharises, which is hypocrisie.
Wakati watu kwa maelfu walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu aliwaambia kwanza wanafunzi wake, “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani unafiki.
2 For there is nothing couered, that shall not bee reueiled: neither hidde, that shall not be knowen.
Kila kilichofunikwa kitafunuliwa, kila kilichofichika kitafichuliwa.
3 Wherefore whatsoeuer yee haue spoken in darkenesse, it shall be heard in the light: and that which ye haue spoken in the eare, in secret places, shall be preached on the houses.
Kwa hiyo, kila mliyosema gizani, watu watayasikia katika mwanga, na kila mliyonong'ona faraghani milango imefungwa, yatatangazwa juu ya nyumba.
4 And I say vnto you, my friendes, be not afraide of them that kill the bodie, and after that are not able to doe any more.
“Nawaambieni ninyi rafiki zangu: msiwaogope wale wanaoua mwili, wasiweze kufanya kitu kingine zaidi.
5 But I wil forewarne you, who ye shall feare: feare him which after hee hath killed, hath power to cast into hell: yea, I say vnto you, him feare. (Geenna g1067)
Nitawaonyesheni yule ambaye ni lazima kumwogopa: mwogopeni yule ambaye baada ya kuua ana uwezo wa kumtupa mtu katika moto wa Jehanamu. Naam, ninawaambieni, mwogopeni huyo. (Geenna g1067)
6 Are not fiue sparowes bought for two farthings, and yet not one of them is forgotten before God?
Inajulikana kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti kumi, au sivyo? Lakini mbele ya Mungu hasahauliki hata mmoja.
7 Yea, and all the heares of your head are nombred: feare not therefore: yee are more of value then many sparowes.
Lakini hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope, basi, ninyi mna thamani zaidi kuliko shomoro wengi!
8 Also I say vnto you, Whosoeuer shall confesse mee before men, him shall the Sonne of man confesse also before the Angels of God.
“Nawaambieni kweli, kila mtu anayekiri hadharani kwamba yeye ni wangu, Mwana wa Mtu naye atakiri mbele ya malaika wa Mungu kwamba mtu huyo ni wake.
9 But hee that shall denie mee before men, shall be denied before the Angels of God.
Lakini, mtu yeyote anayenikana mbele ya watu, naye atakanwa mbele ya malaika wa Mungu.
10 And whosoeuer shall speake a woorde against the Sonne of man, it shall be forgiuen him: but vnto him, that shall blaspheme ye holy Ghost, it shall not be forgiuen.
“Yeyote anayesema neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa; lakini anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
11 And when they shall bring you vnto the Synagogues, and vnto the rulers and Princes, take no thought howe, or what thing ye shall answere, or what yee shall speake.
“Watakapowapeleka ninyi mbele ya masunagogi na mbele ya wakuu na watawala msiwe na wasiwasi juu ya jinsi mtakavyojitetea au jinsi mtakavyosema.
12 For the holy Ghost shall teache you in the same houre, what yee ought to say.
Kwa maana wakati huo Roho Mtakatifu atawafundisheni kile mnachopaswa kusema.”
13 And one of the companie said vnto him, Master, bidde my brother deuide the inheritance with me.
Mtu mmoja katika ule umati wa watu akamwambia, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane urithi aliotuachia baba.”
14 And he said vnto him, Man, who made me a iudge, or a deuider ouer you?
Yesu akamjibu, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi mwamuzi au msuluhishi kati yenu?”
15 Wherefore he said vnto them, Take heede, and beware of couetousnesse: for though a man haue abundance, yet his life standeth not in his riches.
Basi, akawaambia wote, “Jihadharini na kila aina ya tamaa; maana uzima wa mtu hautegemei wingi wa vitu alivyo navyo.”
16 And he put foorth a parable vnto them, saying, The grounde of a certaine riche man brought foorth fruites plenteously.
Kisha akawaambia mfano: “Kulikuwa na tajiri mmoja ambaye shamba lake lilizaa mavuno mengi.
17 Therefore he thought with himselfe, saying, What shall I doe, because I haue no roume, where I may lay vp my fruites?
Tajiri huyo akafikiri moyoni mwake: Nitafanyaje nami sina mahali pa kuhifadhia mavuno yangu?
18 And he said, This wil I do, I wil pul downe my barnes, and builde greater, and therein will I gather all my fruites, and my goods.
Nitafanya hivi: nitabomoa ghala zangu na kujenga kubwa zaidi, na humo nitahifadhi mavuno yangu yote na mali yangu.
19 And I wil say to my soule, Soule, thou hast much goods laide vp for many yeeres: liue at ease, eate, drinke and take thy pastime.
Hapo nitaweza kuiambia roho yangu: sasa unayo akiba ya matumizi kwa miaka na miaka. Ponda mali, ule, unywe na kufurahi.
20 But God said vnto him, O foole, this night wil they fetch away thy soule from thee: then whose shall those things be which thou hast prouided?
Lakini Mungu akamwambia: Mpumbavu wewe; leo usiku roho yako itachukuliwa. Na vitu vile vyote ulivyojilundikia vitakuwa vya nani?”
21 So is he that gathereth riches to himselfe, and is not riche in God.
Yesu akamaliza kwa kusema “Ndivyo ilivyo kwa mtu anayejilundikia mali kwa ajili yake mwenyewe, lakini si tajiri mbele ya Mungu.”
22 And he spake vnto his disciples, Therefore I say vnto you, Take no thought for your life, what yee shall eate: neither for your body, what yee shall put on.
Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kwa sababu hiyo nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula mnachohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu.
23 The life is more then meate: and the body more then the raiment.
Kwa sababu uzima ni bora kuliko chakula, na mwili ni bora kuliko mavazi.
24 Consider the rauens: for they neither sowe nor reape: which neither haue storehouse nor barne, and yet God feedeth them: how much more are yee better then foules?
Chukueni kwa mfano, kunguru: hawapandi, hawavuni wala hawana ghala yoyote. Hata hivyo, Mungu huwalisha. Ninyi mna thamani zaidi kuliko ndege!
25 And which of you with taking thought, can adde to his stature one cubite?
Ni nani kati yenu kwa kuwa na wasiwasi anaweza kuongeza urefu wa maisha yake?
26 If yee then bee not able to doe the least thing, why take yee thought for the remnant?
Basi, kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini kuwa na wasiwasi juu ya yale mengine?
27 Consider the lilies howe they growe: they labour not, neither spin they: yet I say vnto you, that Salomon himselfe in all his royaltie was not clothed like one of these.
Angalieni maua jinsi yanavyomea. Hayafanyi kazi wala hayafumi. Hata hivyo, nawahakikishieni kwamba hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
28 If then God so clothe the grasse which is to day in the field, and to morowe is cast into the ouen, howe much more will he clothe you, O yee of litle faith?
Lakini, kama Mungu hulivika vizuri jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatawafanyia ninyi zaidi? Enyi watu wenye imani haba!
29 Therefore aske not what yee shall eate, or what ye shall drinke, neither hag you in suspense.
“Basi, msivurugike akili, mkihangaika daima juu ya mtakachokula au mtakachokunywa.
30 For all such things the people of the world seeke for: and your Father knoweth that ye haue neede of these things.
Kwa maana hayo yote ndiyo yanayohangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo.
31 But rather seeke ye after the kingdome of God, and all these things shalbe cast vpon you.
Shughulikieni kwanza Ufalme wa Mungu, na hayo yote mtapewa kwa ziada.
32 Feare not, litle flocke: for it is your Fathers pleasure, to giue you the kingdome.
“Msiogope, enyi kundi dogo! Maana Baba yenu amependa kuwapeni Ufalme.
33 Sell that ye haue, and giue almes: make you bagges, which waxe not old, a treasure that can neuer faile in heauen, where no theefe commeth, neither mothe corrupteth.
Uzeni mali yenu mkawape maskini misaada. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na jiwekeeni hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu.
34 For where your treasure is, there will your hearts be also.
Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
35 Let your loynes be gird about and your lights burning,
“Muwe tayari! Jifungeni mkanda kiunoni, na taa zenu ziwe zinawaka;
36 And ye your selues like vnto men that waite for their master, when he will returne from the wedding, that when he commeth and knocketh, they may open vnto him immediatly.
muwe kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka arusini, ili wamfungulie mara atakapobisha hodi.
37 Blessed are those seruants, whom the Lord when he commeth shall finde waking: verely I say vnto you, he will girde himselfe about, and make them to sit downe at table, and will come forth, and serue them.
Heri yao watumishi wale ambao bwana wao atakaporudi atawakuta wanakesha! Nawaambieni hakika, huyo bwana atajifunga mkanda kiunoni, atawaketisha mezani na kuwahudumia.
38 And if he come in the seconde watch, or come in the third watch, and shall finde them so, blessed are those seruants.
Heri yao watumishi hao ikiwa bwana wao atawakuta wanakesha hata ikiwa atarudi usiku wa manane au alfajiri.
39 Nowe vnderstand this, that if the good man of the house had knowen at what houre the theefe would haue come, he would haue watched, and would not haue suffered his house to be digged through.
Jueni kwamba, kama mwenye nyumba angejua saa ambayo mwizi atakuja, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
40 Be ye also prepared therefore: for the Sonne of man will come at an houre when ye thinke not.
Nanyi, kadhalika muwe tayari, maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia.”
41 Then Peter saide vnto him, Master, tellest thou this parable vnto vs, or euen to all?
Petro akamwambia, “Bwana, mfano huo ni kwa ajili yetu tu, au ni kwa ajili ya watu wote?”
42 And the Lord saide, Who is a faithfull steward and wise, whom the master shall make ruler ouer his householde, to giue them their portion of meate in season?
Bwana akajibu, “Ni nani basi, mtumishi aliye mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watumishi wake ili awape chakula wakati ufaao?
43 Blessed is that seruant, whom his master when he commeth, shall finde so doing.
Heri yake mtumishi huyo ikiwa bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
44 Of a trueth I say vnto you, that he wil make him ruler ouer all that he hath.
Hakika atampa madaraka juu ya mali yake yote.
45 But if that seruant say in his heart, My master doeth deferre his comming, and ginne to smite the seruants, and maydens, and to eate, and drinke, and to be drunken,
Lakini, kama mtumishi huyo atafikiri moyoni mwake: na kusema: Bwana wangu amekawia sana kurudi halafu aanze kuwapiga watumishi wenzake, wa kiume au wa kike, na kula, kunywa na kulewa,
46 The master of that seruant will come in a day when he thinketh not, and at an houre when he is not ware of, and will cut him off, and giue him his portion with the vnbeleeuers.
bwana wake atarudi siku asiyoitazamia na saa asiyoijua; atamkatilia mbali na kumweka fungu moja na wasioamini.
47 And that seruant that knewe his masters will, and prepared not himselfe, neither did according to his will, shalbe beaten with many stripes.
Mtumishi ambaye anajua matakwa ya bwana wake lakini hajiweki tayari kufanya anavyotakiwa, atapigwa sana.
48 But he that knewe it not, and yet did commit things worthy of stripes, shall be beaten with fewe stripes: for vnto whomsoeuer much is giuen, of him shalbe much required, and to whom men much commit, the more of him will they aske.
Lakini yule afanyaye yanayostahili adhabu bila kujua, atapigwa kidogo. Aliyepewa vingi atatakiwa vingi; aliyekabidhiwa vingi zaidi atatakiwa kutoa vingi zaidi.
49 I am come to put fire on the earth, and what is my desire, if it be already kindled?
“Nimekuja kuwasha moto duniani, laiti ungekuwa umewaka tayari!
50 Notwithstanding I must be baptized with a baptisme, and how am I grieued, till it be ended?
Ninao ubatizo ambao inanipasa niupokee; jinsi gani ninavyohangaika mpaka ukamilike!
51 Thinke ye that I am come to giue peace on earth? I tell you, nay, but rather debate.
Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? Hata kidogo; si amani bali utengano.
52 For from hencefoorth there shall be fiue in one house deuided, three against two, and two against three.
Na tangu sasa, jamaa ya watu watano itagawanyika; watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
53 The father shalbe deuided against ye sonne, and the sonne against the father: the mother against the daughter, and the daughter against the mother: the mother in lawe against her daughter in lawe, and the daughter in lawe against her mother in lawe.
Baba atakuwa dhidi ya mwanawe, mwana dhidi ya baba yake; mama dhidi ya bintiye, binti dhidi ya mama yake; mama mkwe dhidi ya mke wa mwanawe na huyo dhidi ya mama mkwe wake.”
54 Then said he to the people, When ye see a cloude rise out of the West, straightway ye say, A shower commeth: and so it is.
Yesu akayaambia tena makundi ya watu, “Mnapoona mawingu yakitokea upande wa magharibi, mara mwasema: Mvua itanyesha, na kweli hunyesha.
55 And when ye see the South winde blowe, ye say, that it wilbe hoate: and it commeth to passe.
Mnapoona upepo wa kusi unavuma, mwasema Kutakuwa na hali ya joto na ndivyo inavyokuwa.
56 Hypocrites, ye can discerne the face of the earth, and of the skie: but why discerne ye not this time?
Enyi wanafiki! Mnajua kutabiri hali ya hewa kwa kuangalia dunia na anga; kwa nini basi, hamwezi kujua maana ya nyakati hizi?
57 Yea, and why iudge ye not of your selues what is right?
“Na kwa nini hamwezi kujiamulia wenyewe jambo jema la kufanya?
58 While thou goest with thine aduersarie to the ruler, as thou art in the way, giue diligence in the way, that thou mayest be deliuered from him, least he drawe thee to the iudge, and the iudge deliuer thee to the iayler, and the iayler cast thee into prison.
Maana kama mshtaki wako anakupeleka mahakamani, ingekuwa afadhali kwako kupatana naye mkiwa bado njiani, ili asije akakupeleka mbele ya hakimu, naye hakimu akakutoa kwa polisi, nao wakakutia ndani.
59 I tell thee, thou shalt not depart thence, till thou hast payed the vtmost mite.
Hakika hutatoka huko nakwambia, mpaka utakapomaliza kulipa senti ya mwisho.”

< Luke 12 >