< Luke 10 >

1 After these thinges, the Lord appointed other seuentie also, and sent them, two and two before him into euery citie and place, whither he himselfe should come.
Baada ya hayo, Bwana akawachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawili wawili katika kila mji na kila sehemu aliyokusudia kwenda baadaye.
2 And he said vnto them, The haruest is great, but the labourers are fewe: pray therefore the Lord of the haruest to sende foorth labourers into his haruest.
Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini watendakazi ni wachache. Kwa hiyo mwombeni Bwana wa mavuno, ili apeleke watendakazi katika shamba lake la mavuno.
3 Goe your wayes: beholde, I send you foorth as lambes among wolues.
Haya! nendeni. Ninawatuma kama wana-kondoo katikati ya mbwa mwitu.
4 Beare no bagge, neither scrippe, nor shoes, and salute no man by the way.
Msichukue mkoba, wala mfuko, wala viatu, na msimsalimu mtu yeyote njiani.
5 And into whatsoeuer house ye enter, first say, Peace be to this house.
“Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza semeni, ‘Amani iwe kwenu.’
6 And if the sonne of peace be there, your peace shall rest vpon him: if not, it shall turne to you againe.
Kama kuna mtu wa amani humo, basi amani yenu itakuwa juu yake. La sivyo, itawarudia.
7 And in that house tary still, eating and drinking such things as by them shall be set before you: for the labourer is worthy of his wages. Goe not from house to house.
Kaeni katika nyumba hiyo, mkila na kunywa kile watakachowapa, kwa sababu kila mtendakazi anastahili malipo yake. Msihamehame kutoka nyumba hadi nyumba.
8 But into whatsoeuer citie ye shall enter, if they receiue you, eate such things as are set before you,
“Mkienda katika mji na watu wake wakawakaribisha, kuleni chochote kiwekwacho mbele yenu,
9 And heale the sicke that are there, and say vnto them, The kingdome of God is come neere vnto you.
waponyeni wagonjwa waliomo na waambieni: ‘Ufalme wa Mungu umekaribia.’
10 But into whatsoeuer citie ye shall enter, if they will not receiue you, goe your wayes out into the streetes of the same, and say,
Lakini mkiingia katika mji, nao hawakuwakaribisha, tokeni mwende katika barabara zake mkaseme:
11 Euen the very dust, which cleaueth on vs of your citie, we wipe off against you: notwithstanding knowe this, that the kingdome of God was come neere vnto you.
‘Hata mavumbi ya mji wenu yaliyoshikamana na miguu yetu, tunayakungʼuta dhidi yenu. Lakini mjue kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.’
12 For I say to you, that it shall be easier in that day for them of Sodom, then for that citie.
Ninawaambia, itakuwa rahisi zaidi kwa Sodoma kustahimili katika siku ile kuliko mji ule.
13 Woe be to thee, Chorazin: woe be to thee, Beth-saida: for if the miracles had bene done in Tyrus and Sidon, which haue bene done in you, they had a great while agone repented, sitting in sackecloth and ashes.
“Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwenu ingefanyika Tiro na Sidoni, miji hiyo ingekuwa imetubu zamani, kwa kuvaa magunia na kujipaka majivu.
14 Therefore it shall be easier for Tyrus, and Sidon, at the iudgement, then for you.
Lakini itakuwa rahisi zaidi kwa Tiro na Sidoni kustahimili katika siku ya hukumu, kuliko ninyi.
15 And thou, Capernaum, which art exalted to heauen, shalt be thrust downe to hell. (Hadēs g86)
Nawe, Kapernaumu, je, utainuliwa hadi mbinguni? La hasha, utashushwa mpaka kuzimu.” (Hadēs g86)
16 He that heareth you, heareth me: and he that despiseth you, despiseth me: and he that despiseth me, despiseth him that sent me.
“Yeye awasikilizaye ninyi anisikiliza mimi; naye awakataaye ninyi amenikataa mimi. Lakini yeye anikataaye mimi amkataa yeye aliyenituma.”
17 And the seuentie turned againe with ioy, saying, Lord, euen the deuils are subdued to vs through thy Name.
Wale sabini na wawili wakarudi kwa furaha, na kusema, “Bwana, hata pepo wachafu wanatutii kwa jina lako.”
18 And he said vnto them, I sawe Satan, like lightening, fall downe from heauen.
Yesu akawaambia, “Nilimwona Shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme wa radi.
19 Beholde, I giue vnto you power to treade on Serpents, and Scorpions, and ouer all the power of the enemie, and nothing shall hurt you.
Tazama nimewapa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge na juu ya nguvu zote za adui; wala hakuna kitu chochote kitakachowadhuru.
20 Neuerthelesse, in this reioyce not, that the spirits are subdued vnto you: but rather reioyce, because your names are written in heauen.
Basi, msifurahi kwa kuwa pepo wachafu wanawatii, bali furahini kwa kuwa majina yenu yameandikwa mbinguni.”
21 That same houre reioyced Iesus in the spirit, and said, I confesse vnto thee, Father, Lord of heauen and earth, that thou hast hid these things from the wise and vnderstanding, and hast reueiled them to babes: euen so, Father, because it so pleased thee.
Wakati huo Yesu akashangilia katika Roho Mtakatifu, akasema, “Nakuhimidi Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye elimu, nawe ukawafunulia watoto wadogo. Naam, Baba, kwa kuwa hivyo ndivyo ilivyokupendeza.
22 All things are giuen me of my Father: and no man knoweth who the Sonne is, but the Father: neither who the Father is, saue the Sonne, and he to whom the Sonne will reueile him.
“Nimekabidhiwa vitu vyote na Baba yangu. Hakuna mtu amjuaye Mwana ni nani ila Baba, wala hakuna amjuaye Baba ni nani ila Mwana na yeyote ambaye Mwana anapenda kumfunulia.”
23 And he turned to his disciples, and said secretly, Blessed are the eyes, which see that ye see.
Basi Yesu akawageukia wanafunzi wake akanena nao faraghani, akawaambia, “Heri macho yanayoona yale mambo mnayoyaona.
24 For I tell you that many Prophets and Kings haue desired to see those things, which ye see, and haue not seene them: and to heare those things which ye heare, and haue not heard them.
Kwa maana nawaambia, manabii wengi na wafalme walitamani kuona yale mnayoyaona lakini hawakuyaona, na walitamani kusikia yale mnayoyasikia lakini hawakuyasikia.”
25 Then beholde, a certaine Lawyer stoode vp, and tempted him, saying, Master, what shall I doe, to inherite eternall life? (aiōnios g166)
Wakati huo mtaalamu mmoja wa sheria alisimama ili kumjaribu Yesu, akamuuliza, “Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?” (aiōnios g166)
26 And he saide vnto him, What is written in the Lawe? howe readest thou?
Yesu akamjibu, “Imeandikwaje katika Sheria? Kwani unasoma nini humo?”
27 And he answered, and saide, Thou shalt loue thy Lord God with all thine heart, and with all thy soule, and with all thy strength, and with all thy thought, and thy neighbour as thy selfe.
Akajibu, “‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote’; tena, ‘Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.’”
28 Then he said vnto him, Thou hast answered right: this doe, and thou shalt liue.
Yesu akamwambia, “Umejibu vyema. Fanya hivyo nawe utaishi.”
29 But he willing to iustifie himselfe, said vnto Iesus, Who is then my neighbour?
Lakini yule mtaalamu wa sheria, akitaka kujionyesha kuwa mwenye haki, akamuuliza Yesu, “Jirani yangu ni nani?”
30 And Iesus answered, and saide, A certaine man went downe from Hierusalem to Iericho, and fell among theeues, and they robbed him of his raiment, and wounded him, and departed, leauing him halfe dead.
Yesu akamjibu akasema, “Mtu mmoja alikuwa akiteremka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko, naye akaangukia mikononi mwa wanyangʼanyi. Wakampiga, wakaondoka, wakamwacha akiwa karibu kufa.
31 Nowe so it fell out, that there came downe a certaine Priest that same way, and when he sawe him, he passed by on the other side.
Kuhani mmoja alikuwa akipitia njia ile, alipomwona huyo mtu, akapita upande mwingine, akamwacha hapo barabarani.
32 And likewise also a Leuite, when he was come neere to the place, went and looked on him, and passed by on the other side.
Vivyo hivyo, Mlawi mmoja naye alipofika mahali pale, alimwona, akapita upande mwingine, akamwacha hapo barabarani
33 Then a certaine Samaritane, as he iourneyed, came neere vnto him, and when he sawe him, he had compassion on him,
Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa akisafiri alipomwona, alimhurumia.
34 And went to him, and bound vp his wounds, and powred in oyle and wine, and put him on his owne beast, and brought him to an Inne, and made prouision for him.
Akaenda alipokuwa na akasafisha majeraha yake kwa divai na mafuta, kisha akayafunga. Ndipo akampandisha kwenye punda wake, akampeleka mpaka kwenye nyumba ya wageni na kumtunza.
35 And on the morowe when he departed, he tooke out two pence, and gaue them to the hoste, and said vnto him, Take care of him, and whatsoeuer thou spendest more, when I come againe, I will recompense thee.
Kesho yake, yule Msamaria akachukua dinari mbiliakampa yule mwenye nyumba ya wageni na kusema, ‘Mtunze, nami nirudipo nitakulipa gharama yoyote ya ziada uliyotumia kwa ajili yake.’
36 Which nowe of these three, thinkest thou, was neighbour vnto him that fell among the theeues?
“Ni yupi basi miongoni mwa hawa watatu wewe unadhani ni jirani yake yule mtu aliyeangukia mikononi mwa wanyangʼanyi?”
37 And he saide, He that shewed mercie on him. Then said Iesus vnto him, Goe, and do thou likewise.
Yule mtaalamu wa sheria akajibu, “Ni yule aliyemhurumia.” Ndipo Yesu akamwambia, “Nenda, ukafanye vivyo hivyo.”
38 Nowe it came to passe, as they went, that he entred into a certaine towne, and a certaine woman named Martha, receiued him into her house.
Ikawa Yesu na wanafunzi wake walipokuwa wakienda Yerusalemu, akaingia kwenye kijiji kimoja ambapo mwanamke mmoja aliyeitwa Martha alimkaribisha nyumbani kwake.
39 And she had a sister called Marie, which also sate at Iesus feete, and heard his preaching.
Martha alikuwa na mdogo wake aliyeitwa Maria, ambaye aliketi chini miguuni mwa Bwana akisikiliza yale aliyokuwa akisema.
40 But Martha was combred about much seruing, and came to him, and saide, Master, doest thou not care that my sister hath left me to serue alone? bid her therefore, that she helpe me.
Lakini Martha alikuwa akihangaika na maandalizi yote yaliyokuwa yafanyike. Martha akaja kwa Yesu na kumuuliza, “Bwana, hujali kwamba ndugu yangu ameniachia kazi zote mwenyewe? Basi mwambie anisaidie.”
41 And Iesus answered, and said vnto her, Martha, Martha, thou carest, and art troubled about many things:
Lakini Bwana akamjibu, “Martha, Martha, mbona unasumbuka na kuhangaika na mengi?
42 But one thing is needefull, Marie hath chosen the good part, which shall not be taken away from her.
Lakini kunahitajika kitu kimoja tu. Maria amechagua kile kilicho bora, wala hakuna mtu atakayemwondolea.”

< Luke 10 >