< Leviticus 9 >

1 And in the eight day Moses called Aaron and his sonnes, and the Elders of Israel:
Katika siku ya nane, Musa akawaita Aroni na wanawe pamoja na wazee wa Israeli.
2 Then hee sayde vnto Aaron, Take thee a yong calfe for a sinne offring, and a ram for a burnt offring, both without blemish, and bring them before the Lord.
Akamwambia Aroni, “Twaa ndama dume kutoka kundini kwa ajili ya sadaka ya dhambi zako, na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, wote wawili wasiwe na dosari, na uwatoe mbele za Yahweh.
3 And vnto the children of Israel thou shalt speake, saying, Take yee an hee goate for a sinne offring, and a calfe, and a lambe, both of a yeere olde, without blemish for a burnt offring:
Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'Twaeni beberu kwa ajili ya sadaka ya dhambi na ndama na mwana-kondoo, hawa wawili wawe na umri wa mwaka mmoja na bila dosari, ni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
4 Also a bullock, and a ramme for peace offringes, to offer before the Lord, and a meate offring mingled with oyle: for to day the Lord will appeare vnto you.
pia twaeni fahali na kondoo dume kwa sadaka za amani ili kuwatoa mbele za Yahweh, na sadaka za nafaka iliyochanganywa na mafuta, kwa sababu leo Yahweh atajidhihirisha kwenu.
5 Then they brought that which Moses commanded before the Tabernacle of the Congregation, and all the assembly drewe neere and stood before the Lord.
Kwa hiyo wakaleta kwenye hema la kukutania vyote ambavyo Musa aliagiza, nalo kusanyiko lote la Israeli likakaribia na kusimama mbele za Yahweh.
6 (For Moses had sayde, This is the thing, which the Lord commanded that ye should do, and the glory of the Lord shall appeare vnto you)
Kisha Musa akasema, “Hivi ndivyo Yahweh amewaamru nyinyi mfanye, ili kwamba utukufu wake uweze kuonekana kwenu.
7 Then Moses sayd vnto Aaron, Draw neere to the Altar, and offer thy sinne offering, and thy burnt offring, and make an attonement for thee and for the people: offer also the offring of the people, and make an atonement for them, as the Lord hath commanded.
“Musa akamwambia Aroni, “Njoo karibu na Madhabahu na uteo sadaka yako ya dhambi na sadaka ya kuteketezwa, na kufanya upatanisho kwa ajili ya watu ili kufanya upatanisho kwa ajili yao kama vile ambavyo Yahweh amekwishaamru.”
8 Aaron therefore went vnto the Altar, and killed the calfe of the sinne offring, which was for himselfe.
Kwa hiyo Aroni akaikaribia madhabahu na akamchinja yule ndama kwa ajili ya sadaka ya dhambi, ambayo ilikuwa kwa ajili yake mwenyewe.
9 And the sonnes of Aaron brought ye blood vnto him, and he dipt his finger in the blood, and put it vpon the hornes of the Altar, and powred the rest of the blood at the foote of the Altar.
Nao wana wa Aroni wakamletea hiyo damu, naye akakichofya kidole chake kwenye damu na kuiweka kwenye pembe za madhabahu, kisha akaimwaga damu chini ya kitako cha madhabahu.
10 But the fat and the kidneis and the kall of the liuer of the sinne offring, he burnt vpon the Altar, as the Lord had commanded Moses.
Hata hivyo, aliyateketeza hayo mafuta, figo, na mafuta yanafunika ini juu ya madhabahu kuwa sadaka ya dhambi, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamru Musa.
11 The flesh also and the hide hee burnt with fire without the hoste.
Na akaiteketeza hiyo nyama pamoja na ngozi nje ya kambi
12 After, he slewe the burnt offering, and Aarons sonnes brought vnto him the blood, which he sprinckled round about vpon the Altar.
Aroni akaichinja sadaka ya kuteketezwa, nao wanawe wakampa hiyo damu, ambayo aliinyunza pande zote za madhabahu.
13 Also they brought the burnt offring vnto him with the pieces thereof, and the head, and he burnt them vpon the Altar.
Kisha wakampa ile sadaka ya kuteketezwa, kipande kwa kipande, pamoja na kichwa, naye akaviteketeza juu ya madhabahu.
14 Likewise he did wash the inwardes and the legs, and burnt them vpon the burnt offring on the Altar.
Akaziosha sehemu za ndani pamoja na miguu na kuziteketeza juu ya dhabihu ya kuteketezwa juu ya Madhabahu.
15 Then he offred the peoples offring, and tooke a goate, which was the sinne offring for the people, and slewe it: and offred it for sinne, as the first:
Aroni akaleta dhabihu ya watu— mbuzi, kisha akamtoa kuwa dhabihu kwa ajili ya dhambi yao naye akamchinja, akaitoa dhabihu kwa ajili ya dhambi, kama alivyofanya kwa yule mbuzi wa kwanza.
16 So he offred the burnt offring, and prepared it, according to the maner.
Akaileta sadaka ya kuteketezwa na kuitoa kama Yahweh alivyokuwa ameamru.
17 He presented also the meate offring, and filled his hand thereof, and beside the burnt sacrifice of the morning he burnt this vpon the Altar.
Akaileta sadaka ya nafaka; akakijaza kiganja chake nafaka na kuiteketeza juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya asubuhi ya kuteketezwa.
18 He slewe also the bullock, and the ram for the peace offrings, that was for the people, and Arons sonnes brought vnto him the blood, which he sprinkled vpon the Altar round about,
Pia akamchinja fahali na yule kondoo dume, dhabihu kwa ajili ya sadaka ya amani, ambayo ilikuwa kwa ajili ya watu. Nao wana wa Aronni wakampa damu, ambayo aliinyunyiza kila upande wa mdhabahu.
19 With the fat of the bullocke, and of the ram, the rumpe, and that which couereth the inwards and the kidneis, and the kall of the liuer.
Hata hivyo, waliyakata mafuta ya fahali na ya yule kondoo dume, mafuta ya kwenye mkia, mafuta yafunikayo sehemu za ndani, figo, na yale mafuta yaliyofunika mapafu.
20 So they layed the fat vpon the breasts, and he burnt the fat vpon the Altar.
Wakazichukua hizi sehemu zilizokatwa wakaziweka juu ya vidari, na kisha Aroni akateketeza mafuta juu ya madhabahu.
21 But the breastes and the right shoulder Aaron shooke to and from before the Lord, as the Lord had commanded Moses.
Naye Aroni akavitikisa vidari na paja la kulia kuwa sadaka ya kutikiswa mbele za Yahweh, kama vile Musa alivyokuwa ameamru,
22 So Aaron lift vp his hand toward the people, and blessed them, and came downe from offring of the sinne offring, and the burnt offring, and the peace offrings.
Kisha Aroni akainua juu mikono yake mbele ya watu na kuwabariki, kisha akashuka chini kutoka mahali alipokuwa akitoa hiyo sadaka ya dhambi, sadaka ya kuteketezwa, na sadaka ya amani.
23 After, Moses and Aaron went into the Tabernacle of the Congregation, and came out, and blessed the people, and the glorie of the Lord appeared to all the people.
Musa na Aroni wakaingia ndani ya hema la kukutania, kisha wakatoka nje tena na kuwabariki watu, na utukufu wa Yahweh ukaonekana kwa watu wote.
24 And there came a fire out from the Lord and consumed vpon the Altar the burnt offring and the fatte: which when all the people sawe, they gaue thankes, and fell on their faces.
Moto ukashuka kutoka kwa Yahweh na ukairamba sadaka ya kuteketezwa na mafuta yaliyokuwa juu ya madhabahu. Watu wlipoona jambo hili, wakapiga kelele na kulala chini.

< Leviticus 9 >