< Leviticus 7 >
1 Likewise this is the lawe of the trespasse offering, it is most holy.
“‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya hatia, ambayo ni takatifu sana:
2 In the place where they kill the burnt offering, shall they kill the trespasse offering, and the blood thereof shall he sprinkle rounde about vpon the altar.
Sadaka ya hatia itachinjiwa mahali pale ambapo sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa, nayo damu yake itanyunyizwa pande zote za madhabahu.
3 All the fat thereof also shall he offer, the rumpe, and the fat that couereth the inwardes.
Mafuta yake yote yatatolewa sadaka: mafuta ya mkia na mafuta yale yanayofunika sehemu za ndani,
4 After he shall take away the two kidneis, with the fat that is on them and vpon the flankes, and the kall on the liuer with the kidneis.
figo zote mbili pamoja na mafuta yanayozizunguka yaliyo karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo yataondolewa pamoja na hizo figo.
5 Then the Priest shall burne them vpon the altar, for an offring made by fire vnto the Lord: this is a trespasse offring.
Kuhani atayateketeza juu ya madhabahu kuwa sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto. Hii ni sadaka ya hatia.
6 All the males among the Priestes shall eate thereof, it shalbe eaten in the holy place, for it is most holy.
Mwanaume yeyote katika jamaa ya kuhani aweza kuila, lakini lazima iliwe mahali patakatifu; ni takatifu sana.
7 As the sinne offring is, so is the trespasse offring, one lawe serueth for both: that wherewith the Priest shall make atonement, shalbe his.
“‘Sheria hii ya sadaka ya hatia ni sawasawa na ile ya sadaka ya dhambi: Nyama ya yule mnyama aliyetolewa sadaka ni ya yule kuhani anayesimamia ibada ya upatanisho.
8 Also the Priest that offereth any mans burnt offring, shall haue the skinne of the burnt offring which he hath offered.
Kuhani anayetoa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya mtu yeyote anaweza kuichukua ngozi ya mnyama yule aliyetolewa iwe yake.
9 And all the meate offring that is baken in the ouen, and that is dressed in the pan, and in the frying pan, shall be the Priestes that offereth it.
Kila sadaka ya nafaka iliyookwa jikoni au kupikwa katika sufuria au katika kikaangio itakuwa ya kuhani anayeitoa.
10 And euery meate offering mingled with oyle, and that is dry, shall pertaine vnto all the sonnes of Aaron, to all alike.
Nayo kila sadaka ya nafaka, iwe imechanganywa na mafuta au iko kavu, itakuwa ya wana wa Aroni, nayo itagawanywa sawa kati yao.
11 Furthermore, this is the lawe of the peace offrings, which he shall offer vnto the Lord.
“‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya amani ambayo mtu aweza kuileta kwa Bwana:
12 If he offer it to giue thankes, then he shall offer for his thankes offering, vnleauened cakes mingled with oyle, and vnleauened wafers anointed with oyle, and fine floure fryed with the cakes mingled with oyle.
“‘Ikiwa mtu atatoa sadaka ya amani kwa ajili ya kuonyesha shukrani, pamoja na sadaka hii ya shukrani, atatoa maandazi yasiyotiwa chachu yaliyochanganywa na mafuta, mikate myembamba isiyotiwa chachu iliyopakwa mafuta, maandazi ya unga laini uliokandwa vizuri na kuchanganywa na mafuta.
13 He shall offer also his offring with cakes of leauened bread, for his peace offrings, to giue thankes.
Pamoja na sadaka hii ya amani ya shukrani ataleta sadaka ya maandazi yaliyotengenezwa kwa chachu.
14 And of all the sacrifice he shall offer one cake for an heaue offering vnto the Lord, and it shalbe the Priestes that sprinckleth the blood of the peace offrings.
Ataleta moja ya kila aina ya andazi kama sadaka, matoleo kwa Bwana; hii ni ya kuhani anayenyunyiza damu ya sadaka ya amani.
15 Also the flesh of his peace offerings, for thankesgiuing, shalbe eaten the same day that it is offered: he shall leaue nothing thereof vntill the morning.
Nyama ya sadaka ya amani kwa ajili ya shukrani lazima iliwe siku iyo hiyo inapotolewa; hutabakiza kitu chochote mpaka asubuhi.
16 But if the sacrifice of his offring be a vow, or a free offering, it shalbe eaten the same day that he offreth his sacrifice: and so in the morning the residue thereof shalbe eaten.
“‘Lakini kama sadaka yake ni kwa ajili ya nadhiri au ni sadaka ya hiari, sadaka hiyo italiwa siku hiyo inapotolewa, lakini chochote kinachobakia kinaweza kuliwa kesho yake.
17 But as much of the offered flesh as remaineth vnto the third day, shalbe burnt with fire.
Nyama yoyote ya sadaka inayobaki mpaka siku ya tatu lazima iteketezwe kwa moto.
18 For if any of the flesh of his peace offrings be eaten in the third day, he shall not be accepted that offereth it, neither shall it be reckoned vnto him, but shalbe an abomination: therefore ye person that eateth of it shall beare his iniquitie.
Kama nyama yoyote ya sadaka ya amani italiwa siku ya tatu, Bwana hataikubali. Haitahesabiwa kwake huyo aliyeitoa, kwa kuwa ni najisi. Mtu atakayekula sehemu yake yoyote atahesabiwa hatia.
19 The flesh also that toucheth any vncleane thing, shall not be eaten, but burnt with fire: but of this flesh all that be cleane shall eate thereof.
“‘Nyama ile inayogusa chochote ambacho ni najisi kwa kawaida ya ibada kamwe haitaliwa, ni lazima iteketezwe kwa moto. Kuhusu nyama nyingine, mtu yeyote aliye safi kwa kawaida ya ibada anaweza kuila.
20 But if any eate of the flesh of the peace offerings that pertaineth to the Lord, hauing his vncleannesse vpon him, euen the same person shalbe cut off from his people.
Lakini kama mtu yeyote najisi akila nyama yoyote ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Bwana, huyo mtu lazima akatiliwe mbali na watu wake.
21 Moreouer, whe any toucheth any vncleane thing, as the vncleannesse of man, or of an vncleane beast, or of any filthie abomination, and eate of the flesh of the peace offrings, which pertaineth vnto the Lord, euen that person shalbe cut off from his people.
Kama mtu yeyote akigusa kitu kilicho najisi, iwe ni uchafu wa mwanadamu, au mnyama najisi, au kitu chochote kilicho najisi, kitu cha kuchukiza, kisha akala nyama yoyote ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Bwana, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.’”
22 Againe ye Lord spake vnto Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose,
23 Speake vnto the children of Israel, and say, Ye shall eate no fat of beeues, nor of sheepe, nor of goates:
“Waambie Waisraeli: ‘Msile mafuta yoyote ya ngʼombe, kondoo wala mbuzi.
24 Yet the fat of the dead beast, and the fat of that, which is torne with beastes, shalbe occupied to any vse, but ye shall not eate of it.
Mafuta ya mnyama aliyekutwa amekufa au ameraruliwa na mnyama pori yanaweza kutumika kwa kazi nyingine yoyote, lakini kamwe msiyale.
25 For whosoeuer eateth the fat of the beast, of the which he shall offer an offering made by fire to the Lord, euen the person that eateth, shalbe cut off from his people.
Mtu yeyote alaye mafuta ya mnyama ambaye ametolewa sadaka kwa Bwana kwa moto ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
26 Neither shall ye eate any blood, either of foule, or of beast in all your dwellings.
Popote mtakapoishi, kamwe msinywe damu ya ndege yeyote wala ya mnyama.
27 Euery person that eateth any blood, euen the same person shall be cut off from his people.
Ikiwa mtu yeyote atakunywa damu, mtu huyo lazima akatiliwe mbali na watu wake.’”
28 And the Lord talked with Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose,
29 Speake vnto the children of Israel, and say, Hee that offereth his peace offerings vnto the Lord, shall bring his gifte vnto the Lord of his peace offerings:
“Waambie Waisraeli: ‘Mtu yeyote aletaye sadaka ya amani kwa Bwana ataleta sehemu ya sadaka hiyo kama dhabihu yake kwa Bwana.
30 His handes shall bring the offerings of the Lord made by fire: euen the fatte with the breast shall he bring, that the breast may be shaken to and from before the Lord.
Ataleta sadaka kwa mikono yake mwenyewe iliyotolewa kwa Bwana kwa moto; ataleta mafuta ya huyo mnyama pamoja na kidari, naye atainua hicho kidari mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
31 Then the Priest shall burne the fatte vpon the Altar, and the breast shall be Aarons and his sonnes.
Kuhani atayateketeza hayo mafuta juu ya madhabahu, lakini kidari kitakuwa cha Aroni na wanawe.
32 And the right shoulder shall ye giue vnto the Priest for an heaue offering, of your peace offrings.
Paja la kulia la sadaka zako za amani utampa kuhani kama matoleo.
33 The same that offreth the blood of ye peace offrings, and the fatte, among the sonnes of Aaron, shall haue the right shoulder for his parte.
Mwana wa Aroni atoaye damu na mafuta ya sadaka ya amani ndiye atakayepewa paja hilo la kulia kuwa fungu lake.
34 For the breast shaken to and from, and the shoulder lifted vp, haue I taken of the children of Israel, euen of their peace offrings, and haue giuen them vnto Aaron the Priest and vnto his sonnes by a statute for euer from among the children of Israel.
Kutoka kwenye sadaka za amani za Waisraeli, mimi Mungu nimepokea kidari kile kilichoinuliwa pamoja na lile paja lililotolewa, nami nimevitoa kwa kuhani Aroni na wanawe kuwa fungu lao la kawaida kutoka kwa Waisraeli.’”
35 This is the anointing of Aaron, and the anointing of his sonnes, concerning the offerings of the Lord made by fire, in the day when he presented them to serue in the Priestes office vnto the Lord.
Hii ndiyo sehemu ya sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, ambazo zilitengwa kwa ajili ya Aroni na wanawe siku ile walipowekwa wakfu ili kumtumikia Bwana katika kazi ya ukuhani.
36 The which portions the Lord commanded to giue them in the day that he anointed them from among the children of Israel, by a statute for euer in their generations.
Siku ile walipotiwa mafuta, Bwana aliagiza kwamba Waisraeli wawape hili kama fungu lao la kawaida kwa vizazi vijavyo.
37 This is also the lawe of the burnt offring of the meate offring, and of the sinne offring, and of the trespasse offring, and of the consecrations, and of the peace offrings,
Basi haya ndiyo masharti kuhusu sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka, sadaka ya dhambi, sadaka ya hatia, sadaka ya kuwekwa wakfu, na sadaka ya amani,
38 Which the Lord commanded Moses in the mount Sinai, when he commanded the children of Israel to offer their giftes vnto the Lord in the wildernesse of Sinai.
ambayo Bwana alimpa Mose juu ya Mlima Sinai siku ile alipowaagiza Waisraeli walete sadaka zao kwa Bwana, katika Jangwa la Sinai.