< Leviticus 16 >

1 Fvrthermore the Lord spake vnto Moses, after the death of the two sonnes of Aaron, whe they came to offer before the Lord, and dyed:
Yahwe alizungumza na Musa - hii ni baada vifo vya wana wawili wa Haruni, walipomkaribia Yahwe na ndipo wakafa.
2 And the Lord sayd vnto Moses, Speake vnto Aaron thy brother, that he come not at all times into the Holy place within the vayle, before the Merciseate, which is vpon the Arke, that he dye not: for I wil appeare in the cloude vpon the Merciseate.
Yahwe alimwambia Musa, “Ongea na Haruni kaka yako na umwambie hapana kuja tu wakati wowote katika patakatifu pa patakatifu ndani ya pazia, mbele ya kifuniko cha upatanisho kilicho juu ya sanduku. Akifanya hivyo, anakufa, kwasababu naonekana katika wingu juu ya kifuniko cha upatanisho.
3 After this sort shall Aaron come into the Holy place: euen with a yong bullocke for a sinne offring, and a ramme for a burnt offring.
Hivi ndivyo jinsi Haruni lazima aje katika patakatifu pa patakatifu. Yeye lazima aingie pamoja na ndama kama sadaka ya dhambi, na kondoo dume kama sadaka ya dhambi.
4 He shall put on the holy linnen coate, and shall haue linnen breeches vpon his flesh, and shall be girded with a linnen girdle, and shall couer his head with a linnen miter: these are the holy garments: therefore shall hee wash his flesh in water, when he doeth put them on.
Ni lazima avae kanzu ya kitatani, na lazima avae ndani yake nguo ya kitani, na lazima avae mshipi wa kitani na kilemba cha kitani. Haya ni mavazi matakatifu. Lazima aoge mwili wake katika maji na avae mavazi haya.
5 And hee shall take of the Congregation of the children of Israel, two hee goates for a sinne offring, and a ramme for a burnt offring.
Lazima achukue kwenye umati wa watu wa Israeli mbuzi wawili waume kama sadaka ya dhambi na kondoo dume moja ikiwa ni sadaka ya kuteketezwa.
6 Then Aaron shall offer the bullocke for his sinne offring, and make an atonement for himselfe, and for his house.
Ndipo Haruni lazima alete ng'ombe kama sadaka ya dhambi, ambayo itakuwa kwaajili yake mwenyewe, kufanya upatanisho kwaajili yake mwenyewe na familia yake.
7 And he shall take the two hee goates, and present them before the Lord at the doore of the Tabernacle of the Congregation.
Ndipo lazima achukue mbuzi wawili na kuwaweka mbele ya Yahwe katika mlango wa kuingilia kwenye hema ya mkutano.
8 Then Aaron shall cast lots ouer the two hee goates: one lot for the Lord, and the other for the Scape goate.
Ndipo Haruni lazima apige kura kwaajili ya mbuzi hao wawili, kura moja kwaajili ya Yahwe, na kura nyingine kwaajili ya msingiziwa.
9 And Aaron shall offer the goat, vpon which the Lords lot shall fal, and make him a sinne offring.
Ndipo Haruni lazima awasilishe mbuzi ambaye kura imeangukia kwa Yahwe, na kumtoa mbuzi huyo kama sadaka ya dhambi.
10 But the goate, on which the lot shall fall to be the Scape goate, shalbe presented aliue before the Lord, to make reconciliation by him, and to let him go (as a Scape goate) into the wildernes.
Lakini mbuzi ambaye kura ya usingiziwa imemwangukia lazima aletwe kwa Yahwe akiwa hai, kufanya upatanisho kwa kumwachia aende porini kama, mbuzimsingiziwa.
11 Thus Aaron shall offer the bullocke for his sinne offring, and make a reconciliation for himselfe, and for his house, and shall kill the bullocke for his sinne offring.
Pia Haruni lazima alete ng'ombe kwaajili ya sadaka ya dhambi, ambayo itakuwa kwaajili yake mwenyewe, lazima afanye upatanisho kwaajili yake mwenyewe na familia yake, hivyo lazima yeye amuue huyo ng'ombe kama sadaka ya dhambi kwaajili yake mwenyewe.
12 And he shall take a censer full of burning coles from off the altar before the Lord, and his handfull of sweete incense beaten small, and bring it within the vayle,
Haruni lazima achukue chetezo iliyojaa mkaa wa moto kutoka kwenye madhabahu mbele ya Yahwe, na mikono imejaa ubani mzuri, na kuleta vitu hivi ndani ya pazia.
13 And shall put the incense vpon the fire before the Lord, that the cloude of the incense may couer the Merciseat that is vpon the Testimonie: so he shall not dye.
Hapo lazima aweke ubani juu ya moto mbele za Yahwe ili kwamba wingu kutoka kwenye ubani liweze kufunika kifuniko cha agano la imani ya upatanisho. Yeye afanye hivyo ili kwamba asife.
14 And hee shall take of the blood of the bullocke, and sprinkle it with his finger vpon the Merciseat Eastward: and before the Merciseate shall he sprinkle of the blood with his finger seuen times.
Ndipo lazima achukue kiasi cha damu ya ng'ombe na kuinyunyiza kwa kidole chake mbele ya kifuniko cha upatanisho. Lazima anyunyize kiasi cha damu kwa kidole chake mara saba mbele ya kifuniko cha upatanisho.
15 Then shall he kill the goate that is the peoples sinne offring, and bring his blood within the vaile, and doe with that blood, as he did with the blood of the bullocke, and sprinckle it vpon the Merciseate, and before the Merciseate.
Ndipo lazima aue mbuzi kwaajili ya sadaka ya dhambi ambayo ni kwaajili ya watu na kuileta damu yake ndani kwenye pazi. Hapo lazima aifanyie damu kama alivyofanya kwenye damu ya fahali: lazima ainyunyize juu ya kifuniko cha upatanisho na mbele ya kifunuko cha upatanisho.
16 So he shall purge the Holy place from the vncleannes of the children of Israel, and from their trespasses of all their sinnes: so shall he do also for the Tabernacle of the Cogregation placed with them, in the middes of their vncleannesse.
Yeye lazima afanye upatanisho kwaajili ya mahali patakatifu kwa sababu ya matendo ya unajisi ya watu wa Israeli, na kwa sababu ya uasi na dhambi zao zote. Yeye pia lazima afanye haya kwaajili ya hema ya mkutano, ambapo Yahwe anaishi kati yao, katika uwepo wa matendo yao ya unajisi.
17 And there shalbe no man in the Tabernacle of the Congregation, when he goeth in to make an atonement in the Holy place, vntill hee come out, and haue made an atonement for himselfe, and for his housholde, and for all the Congregation of Israel.
Hakuna mtu anayetakiwa kuwepo katika hema ya mkutano wakati Haruni anaingia kufanya upatanisho katika mahali patakatifu pa patakatifu, na mpaka atoke nje na amemaliza kufanya upatanisho kwaajili yake mwenyewe na kwaajili ya familia yake, na kwaajili umati wa Israeli.
18 After, he shall goe out vnto the altar that is before the Lord and make a reconciliation vpon it, and shall take of the blood of the bullocke, and of the blood of the goate, and put it vpon the hornes of the Altar round about:
Yeye lazima aende nje kwenye madhabahu hapo mbele za Yahwe na kufanya upatanisho kwaajili ya hiyo, na lazima achukue kiasi cha damu ya mbuzi na kuiweka juu ya pembe za madhabahu yote kuzunguka.
19 So shall hee sprinkle of the blood vpon it with his finger seuen times, and clense it, and halowe it from the vncleannes of the children of Israel.
Anatakiwa anyunyize kiasi cha damu juu yake kwa kidole chake mara saba kuitakasa na kuitenga maalumu kwa Yahwe, mbali kutoka matendo ya unajisi wa watu wa Israeli.
20 When he hath made an ende of purging the Holy place, and the Tabernacle of the Congregation, and the altar, then he shall bring the liue goate:
Atakapo maliza kupatanisha kwaajili ya mahali patakatifu sana, hema la mkutano, na madhabahu, lazima amlete mbuzi aliyehai.
21 And Aaron shall put both his handes vpon the head of the liue goate, and confesse ouer him al the iniquities of the children of Israel, and all their trespasses, in all their sinnes, putting them vpon the head of the goate, and shall sende him away (by the hand of a man appointed) into the wildernes.
Haruni lazima aweke mikono yake yote juu ya kichwa cha mbuzi huyu aliyehai na akiri juu yake maovu yote ya watu wa Israeli, uasi wao wote, dhambi zao zote. Ndipo lazima aweke dhambi hizo juu ya kichwa cha mbuzi na amwachie katika uangalizi wa mtu aliyetari kumwongoza mbuzi huyo porini.
22 So the goate shall beare vpon him all their iniquities into the land that is not inhabited, and he shall let the goate go into the wildernesse.
Mbuzi lazima abebe juu yake mwenyewe uovu wote kwenda mahali pakiwa. Kule msituni, huyo mtu amwache mbuzi aende huru.
23 After, Aaron shall come into the Tabernacle of the Congregation, and put off the linnen clothes, which he put on when he went into the Holy place, and leaue them there.
Ndipo Haruni anapaswa kwenda tena humo kwenye hema ya mkutano na kuvua mavazi ya kitani ambayo amayavaa kabla hajaenda mahali patakatifu sana, na anatakiwa kuyaacha mavazi hayo pale.
24 Hee shall wash also his flesh with water in the Holy place, and put on his owne rayment, and come out, and make his burnt offring, and the burnt offring of the people, and make an atonement for himselfe, and for the people.
Anapaswa aoshe mwili wake kwa maji mahali patakatifu, na avae nguo zake za kawaida; pia lazima atoke nje kutoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya kuteketezwa kwaajili ya wale watu, na kwa njia hii anafanya upatanisho kwaajili yake mwenyewe na kwaajili ya watu.
25 Also the fatte of the sinne offring shall he burne vpon the altar.
Lazima yeye achome mafuta ya sadaka ya dhambi juu ya madhabahu.
26 And he that caried forth the goat, called the Scape goat, shall wash his clothes, and wash his flesh in water, and after that shall come into the hoste.
Huyu mtu anayemwacha mbuzi msingiziwa aende huru anafua nguo zake na kuosha mwili wake katika maji; baada ya hayo, anaweza kurudi tena kambini.
27 Also the bullocke for the sinne offring, and the goate for the sinne offring (whose blood was brought to make a reconciliation in the Holy place) shall one carie out without the hoste to be burnt in the fire, with their skinnes, and with their flesh, and with their doung.
Yule fahali kwaajili ya sadaka ya dhambi na mbuzi kwaajili ya sadaka za dhambi, ambaye damu yake ililetwa kufanya upatanisho katika mahali patakatifu, lazima ipelekwe nje ya kambi. kule lazima wachome, ngozi zao, nyama yao na kinyesi chao.
28 And hee that burneth them shall wash his clothes, and wash his flesh in water, and afterward come into the hoste.
Huyu anayechoma sehemu hizo lazima afue nguo zake na aoge mwili wake katika maji; baada ya hapo, anaweza kurudi tena kwenye kambi.
29 So this shalbe an ordinance for euer vnto you: the tenth day of the seuenth moneth, yee shall humble your soules, and do no worke at all, whether it be one of the same countrey or a strager that soiourneth among you.
Hii itakuwa sharti kwaajili yenu kwamba katika mwezi wa saba, kwenye siku ya kumi ya mwezi, mtanyenyekea wenyewe na msifanye kazi, iwe mwenyeji wa kuzaliwa au mgeni anayeishi kati yenu.
30 For that day shall ye Priest make an atonement for you to clense you: ye shalbe cleane from all your sinnes before the Lord.
Hii ni kwasababu katika siku hii ya upatanisho utafanywa kwaajili yenu, kuwatakasa ninyi kutoka dhambi zenu zote ili mwe safi mbele za Yahwe.
31 This shall be a Sabbath of rest vnto you, and ye shall humble your soules, by an ordinance for euer.
Hii ni maalumu kwa Sabato ya kupumzika kwaajili yenu, na lazima mnyenyekee wenyewe na msifanye kazi. Hili litakuwa sharti kati yenu.
32 And the Priest whom he shall anoynt, and whom he shall cosecrate (to minister in his fathers steade) shall make the atonement, and shall put on the linnen clothes and Holy vestments,
Kuhani mkuu, ambaye atapakwa mafuta na kuwekwa wakfu kuwa kuhani mkuu katika nafasi ya baba yake, lazima afanye upatanisho huu na kuvaa mavazi ya kitani, hayo ni mavazi matakatifu.
33 And shall purge the Holy Sanctuarie and the Tabernacle of the Congregation, and shall clense the altar, and make an atonement for the Priests and for all the people of the Congregation.
Lazima afanye upatanisho kwaajili ya mahali patakatifu sana; lazima afanye upatanisho kwaajili ya hema ya mkutano na madhabahu, na lazima afanye upatanisho kwaajili ya makuhani na kwaajili ya kusanyiko la watu.
34 And this shalbe an euerlasting ordinance vnto you, to make an atonement for the children of Israel for all their sinnes once a yeere: and as the Lord commanded Moses, he did.
Hii daima itakuwa sharti kwaajili yako, kufanya upatanisho kwaajili ya watu wa Israeli kwasababu ya dhambi zao zote, mara moja kwa kila mwaka.” Na ilikuwa ikifanika kama Yahwe alivyomwamuru Musa.

< Leviticus 16 >