< Judges 7 >

1 Then Ierubbaal (who is Gideon) rose vp early, and all the people that were with him, and pitched beside the well of Harod, so that the hoste of the Midianites was on the Northside of them in the valley by the hill of Moreh.
Ndipo Yerub-Baali (yaani Gideoni) na lile jeshi lililokuwa pamoja naye, wakaondoka asubuhi na mapema na kupiga kambi kando ya chemchemi ya Harodi. Kambi ya Wamidiani ilikuwa kaskazini yao katika bonde karibu na kilima cha More.
2 And the Lord said vnto Gideon, The people that are with thee, are too many for me to giue the Midianites into their hands, lest Israel make their vaunt against me, and say, Mine hand hath saued mee.
Bwana akamwambia Gideoni, “Jeshi lililo pamoja nawe ni kubwa sana kwa mimi kuwatia Wamidiani mikononi mwao. Ili kwamba Israeli asije akajisifu juu yangu akisema, ‘Mkono wangu ndio ulioniokoa,
3 Now therefore proclaime in the audience of the people, and say, Who so is timerous or fearefull, let him returne, and depart earely from mount Gilead. And there returned of the people which were at mount Gilead, two and twentie thousand: so ten thousand remayned.
kwa hiyo sasa tangaza jeshi lote likiwa linasikia, kwamba: Yeyote anayeogopa na kutetemeka, yeye na arudi nyumbani, aondoke katika Mlima Gileadi.’” Hivyo watu 22,000 walirudi, wakabaki 10,000.
4 And the Lord said vnto Gideon, The people are yet too many: bring them downe vnto the water, and I will try them for thee there: and of whome I say vnto thee, This man shall goe with thee, the same shall go with thee: and of whomsoeuer I say vnto thee, This man shall not goe with thee, the same shall not go.
Lakini Bwana akamwambia Gideoni, “Idadi ya jeshi bado ni kubwa. Wapeleke chini katika maji nami nitawajaribu huko kwa ajili yako. Kama nikikuambia, ‘Huyu atakwenda pamoja nawe,’ yeye atakwenda; lakini kama nikisema, ‘Huyu hatakwenda pamoja nawe,’ yeye hatakwenda.”
5 So he brought downe the people vnto the water. And the Lord sayd vnto Gideon, As many as lap the water with their tongues, as a dog lappeth, them put by themselues, and euery one that shall bow downe his knees to drinke, put apart.
Hivyo Gideoni akalileta lile jeshi chini kwenye maji naye Bwana akamwambia Gideoni, “Watenge upande mmoja wale wote wanywao maji kwa ulimi, kama vile mbwa anywavyo, wale wote wapigao magoti ili kunywa wakipeleka mikono yao vinywani mwao, waweke upande mwingine.”
6 And the nomber of them that lapped by putting their handes to their mouthes, were three hundreth men: but all the remnant of the people kneeled downe vpon their knees to drinke water.
Idadi ya wale waliokunywa kwa kuramba ramba walikuwa 300, lakini wengine wote katika jeshi walipiga magoti ili kunywa.
7 Then the Lord sayde vnto Gideon, By these three hundreth men that lapped, will I saue you, and deliuer the Midianites into thine hand: and let all the other people go euery man vnto his place.
Bwana akamwambia Gideoni, “Kwa hao watu 300 walioramba maji nitawaokoa ninyi, nami nitawatia Wamidiani mkononi mwako. Waache hao watu wengine wote warudi kila mmoja nyumbani mwake.”
8 So the people tooke vitailes with them, and their trumpets: and he sent all the rest of Israel, euery man vnto his tent, and reteined the three hundreth men: and the hoste of Midian was beneath him in a valley.
Hivyo Gideoni akawaacha wale Waisraeli wengine kila mmoja aende kwenye hema yake. Akabakia na wale 300, ambao walichukua vyakula na tarumbeta za wale wenzao. Basi kambi ya Wamidiani ilikuwa chini yake bondeni.
9 And the same night the Lord sayde vnto him, Arise, get thee downe vnto the hoste: for I haue deliuered it into thine hand.
Usiku ule ule Bwana akamwambia Gideoni, “Ondoka, ushuke kambini, kwa kuwa nimeitia mkononi mwako.
10 But if thou feare to go downe, then go thou, and Phurah thy seruant downe to the hoste,
Lakini kama unaogopa kushambulia, shuka kambini pamoja na mtumishi wako Pura,
11 And thou shalt hearken what they say, and so shall thine handes be strong to go downe vnto the hoste. Then went he downe and Phurah his seruant vnto the outside of the souldiers that were in the hoste.
nawe sikiliza wanayosema. Hatimaye, utatiwa moyo kushambulia kambi.” Basi yeye na Pura mtumishi wake wakashuka na kufikia walinzi wa mbele wenye silaha waliokuwa mle kambini.
12 And the Midianites, and the Amalekites and all they of the East, lay in the valley like grashoppers in multitude, and their camels were without nomber, as the sande which is by the sea side for multitude.
Wamidiani, Waamaleki na mataifa mengine yote ya mashariki walikaa bondeni, nao walikuwa mfano wa nzige kwa wingi wao. Ngamia zao hazikuhesabika, wingi wao ulikuwa kama mchanga wa ufuoni mwa bahari.
13 And when Gideon was come, beholde, a man tolde a dreame vnto his neighbour, and said, Behold, I dreamed a dreame, and lo, a cake of barley bread tumbled from aboue into the hoste of Midian, and came vnto a tent, and smote it that it fell, and ouerturned it, that the tent fell downe.
Gideoni alifika wakati huo huo kukiwa na mtu mmoja aliyekuwa anamweleza mwenzake ndoto yake, akisema, “Niliota ndoto: Tazama mkate wa shayiri ulioviringana ulianguka katika kambi moja ya Wamidiani, ukaipiga na ikaanguka nao ukaipindua juu chini na hema ikaporomoka chini.”
14 And his fellow answered, and sayde, This is nothing els saue the sworde of Gideon the sonne of Ioash a man of Israel: for into his hande hath God deliuered Midian and all the hoste.
Rafiki yake akamjibu, “Habari hii si kitu kingine zaidi ya upanga wa Gideoni mwana wa Yoashi, Mwisraeli. Mungu amewatia Wamidiani na jeshi lote mkononi mwake.”
15 When Gideon heard the dreame tolde, and the interpretation of the same, he worshipped, and returned vnto the hoste of Israel, and said, Vp: for the Lord hath deliuered into your hande the hoste of Midian.
Gideoni alipoisikia hiyo ndoto na tafsiri yake, akamwabudu Mungu. Akarudi kwenye kambi ya Israeli na kusema, “Inukeni! Bwana amelitia jeshi la Wamidiani mikononi mwenu.”
16 And hee deuided the three hundreth men into three bandes, and gaue euery man a trumpet in his hande with emptie pitchers, and lampes within the pitchers.
Akawagawa wale watu 300 katika makundi matatu, akawakabidhi tarumbeta mikononi mwao wote na mitungi isiyokuwa na maji yenye mienge ndani yake.
17 And he sayd vnto them, Looke on me, and do likewise, when I come to the side of the hoste: euen as I do, so do you.
Akawaambia, “Nitazameni, fanyeni kama nitakavyofanya, nitakapofika mwisho wa kambi mfanye kama nitakavyofanya.
18 When I blowe with a trumpet and all that are with me, blowe ye with trumpets also on euery side of the hoste, and say, For the Lord, and for Gideon.
Wakati mimi na wale walio pamoja nami wote, tutakapopiga tarumbeta zetu, ninyi nanyi pigeni tarumbeta pande zote za kambi na mpige kelele, mseme, ‘Upanga wa Bwana na wa Gideoni.’”
19 So Gideon and the hundreth men that were with him, came vnto the outside of the hoste, in the beginning of the middle watche, and they raised vp the watchmen, and they blew with their trumpets, and brake the pitchers that were in their handes.
Gideoni na wale watu 100 waliokuwa pamoja naye wakafika mwisho wa kambi usiku mwanzoni mwa zamu ya kati, mara tu walipokuwa wamebadili zamu. Wakapiga zile tarumbeta zao na kuvunja ile mitungi iliyokuwa mikononi mwao.
20 And the three companies blew with trumpets and brake the pitchers, and helde the lampes in their left hands, and the trumpets in their right. handes to blowe withall: and they cryed, The sword of the Lord and of Gideon.
Yale makundi matatu yakapiga tarumbeta na kuvunja mitungi. Wakashika mienge kwa mikono yao ya kushoto na katika mikono yao ya kuume tarumbeta ili kuzipiga, wakapaza sauti zao, “Upanga wa Bwana na wa Gideoni!”
21 And they stoode, euery man in his place round about the hoste: and all the hoste ranne, and cryed, and fled.
Wakasimama kila mtu mahali pake kuizunguka kambi pande zote, Wamidiani wote wakakimbia, huku wakipiga kelele.
22 And the three hundreth blewe with trumpets, and the Lord set euery mans sworde vpon his neighbour, and vpon all the hoste: so the hoste fled to Beth-hashittah in Zererah, and to the border of Abel-meholah, vnto Tabbath.
Walipozipiga zile tarumbeta 300, Bwana akafanya watu katika kambi yote kugeuziana upanga kila mmoja na mwenziwe. Jeshi likakimbia mpaka Beth-Shita kuelekea Serera hadi mpakani mwa Abel-Mehola karibu na Tabathi.
23 Then the men of Israel being gathered together out of Naphtali, and out of Asher, and out of all Manasseh, pursued after the Midianites.
Watu wa Israeli wakaitwa kutoka Naftali, Asheri na Manase, wakawafuatia Wamidiani.
24 And Gideon sent messengers vnto all mount Ephraim, saying, Come downe against the Midianites, and take before them the waters vnto Beth-barah, and Iorden. Then all the men of Ephraim gathered together and tooke the waters vnto Beth-barah, and Iorden.
Gideoni akatuma wajumbe katika nchi yote ya vilima vya Efraimu akisema, “Teremkeni dhidi ya Wamidiani na mkazuie vivuko vya maji mbele yao hadi Beth-Bara na pia Yordani.” Hivyo watu wote wa Efraimu wakakutanika pamoja na kuzingira mto wa Yordani hadi Beth-Bara.
25 And they tooke two princes of the Midianites, Oreb and Zeeb, and slew Oreb vpon the rocke Oreb, and slewe Zeeb at the winepresse of Zeeb, and pursued the Midianites, and brought the heads of Oreb and Zeeb to Gideon beyonde Iorden.
Wakawakamata wakuu wawili wa Midiani, Orebu na Zeebu. Wakamuulia Orebu pale penye mwamba wa Orebu, na Zeebu wakamuulia penye shinikizo la kukamulia divai la Zeebu. Wakawafuatia Wamidiani na kuleta vichwa vya Orebu na Zeebu kwa Gideoni, huko ngʼambo ya Yordani.

< Judges 7 >