< Judges 6 >

1 Afterwarde the children of Israel committed wickednesse in the sight of the Lord, and the Lord gaue them into the handes of Midian seuen yeres.
Wana wa Israeli wakafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana; naye akawatia mikononi mwa Midiani kwa miaka saba.
2 And the hand of Midian preuayled against Israel, and because of the Midianites the children of Israel made them dennes in the mountaines, and caues, and strong holdes.
Uwezo wa Midiani uliwanyanyasa Israeli. Kwa sababu ya Midiani, watu wa Israeli walitengeneza makao wenyewe kutoka kwenye mabwawa katika milima, mapango, na ngome.
3 When Israel had sowen, then came vp the Midianites, the Amalekites, and they of the East, and came vpon them,
Kisha ikawa kwamba wakati wowote Waisraeli walipopanda mazao yao, Wamidiani na Waamaleki na watu kutoka mashariki waliwavamia Waisraeli.
4 And camped by them, and destroyed the fruite of the earth, euen til thou come vnto Azzah, and left no foode for Israel, neither sheepe, nor oxe, nor asse.
Waliweza kutengenezajeshi lao juu ya ardhi na kuharibu mazao, mpaka njia ya Gaza. Hawakuacha chakula huko Israeli, wala kondoo wala ng'ombe wala punda.
5 For they went vp, and their cattel, and came with their tentes as grashoppers in multitude: so that they and their camels were without number: and they came into the land to destroy it.
Kila wakati wao na mifugo yao na mahema walipokuja, walikuja kama kundi la nzige, na haikuwezekana kuhesabu watu au ngamia zao. Walivamia ardhi ili kuiharibu.
6 So was Israel exceedingly impouerished by the Midianites: therefore the children of Israel cryed vnto the Lord.
Midiani iliwadhoofisha Waisraeli sana mpaka watu wa Israeli wakamwita Bwana.
7 And when the children of Israel cryed vnto the Lord because of the Midianites,
Watu wa Israeli walipomwomba Bwana kwa sababu ya Midiani,
8 The Lord sent vnto the children of Israel a Prophet, who sayd vuto them, Thus sayth the Lord God of Israel, I haue brought you vp from Egypt, and haue brought you out of the house of bondage,
Bwana alimtuma nabii kwa wana wa Israeli. Nabii akawaambia, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nimekuleta kutoka Misri; Nilikutoa nje ya nyumba ya utumwa.
9 And I haue deliuered you out of the hand of the Egyptians, and out of the hand of all that oppressed you, and haue cast them out before you, and giuen you their land.
Naliwaokoa kutoka kwenye mikono ya Wamisri, na kutoka kwenye mkono wa wote waliokuwa wakikunyanyasa. Niliwafukuza mbele yenu, na nimewapa nchi yao.
10 And I sayde vnto you, I am the Lord your God: feare not the gods of the Amorites in whose lande you dwell: but ye haue not obeyed my voyce.
Niliwaambia, “Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu; Nimewaamuru msiabudu miungu ya Waamori, ambao mnaishi katika nchi yao. Lakini hamkuitii sauti yangu.”
11 And the Angell of the Lord came, and sate vnder the oke which was in Ophrah, that perteined vnto Ioash the father of the Ezrites, and his sonne Gideon threshed wheate by the winepresse, to hide it from the Midianites.
Basi malaika wa Bwana akaja na kukaa chini ya mwaloni huko Ofra, uliokuwa wa Yoashi (Mwabiyezeri), wakati Gidioni, mwana wa Yoashi, akitenganisha ngano katika sakafu, katika kikapu cha divai-kuificha toka kwa Wamidiani.
12 Then the Angel of the Lord appeared vnto him, and said vnto him, The Lord is with thee, thou valiant man.
Malaika wa Bwana akamtokea, akamwambia, Bwana yu pamoja nanyi, mpiganaji mwenye nguvu!
13 To whome Gideon answered, Ah my Lord, if the Lord be with vs, why then is all this come vpon vs? and where be all his miracles which our fathers tolde vs of, and sayd, Did not the Lord bring vs out of Egypt? but now the Lord hath forsaken vs, and deliuered vs into the hand of the Midianites.
Gideoni akamwambia, Oo, bwana wangu, ikiwa Bwana yu pamoja nasi, kwa nini basi yote haya yanatupata? Je, yako wapi matendo yake yote mazuri ambayo baba zetu walituambia, waliposema, 'Je! si Bwana aliyetukomboa kutoka Misri?' Lakini sasa Bwana ametuacha na kututia mikononi mwa Midiani. '
14 And the Lord looked vpon him, and sayd, Goe in this thy might, and thou shalt saue Israel out of the handes of the Midianites: haue not I sent thee?
Bwana akamtazama na kusema, “Nenda katika nguvu uliyo nayo tayari. Uiokoe Israeli kutoka mkononi wa Midiani. Je, sikukutuma?”
15 And he answered him, Ah my Lord, whereby shall I saue Israel? beholde, my father is poore in Manasseh, and I am the least in my fathers house.
Gideoni akamwambia, “Tafadhali, Bwana, nawezeje kuwaokoa Israeli? Angalia, familia yangu ni dhaifu zaidi katika Manase, na mimi si muhimu katika nyumba ya baba yangu.”
16 Then the Lord sayd vnto him, I wil therefore be with thee, and thou shalt smite the Midianites, as one man.
Bwana akamwambia, “Nitakuwa pamoja nawe, nawe utalishinda jeshi lote la Midiani kama mtu mmoja.”
17 And he answered him, I pray thee, if I haue founde fauour in thy sight, then shewe me a signe, that thou talkest with me.
Gideoni akamwambia, “Ikiwa unapendezwa na mimi, nipe basi ishara kwamba wewe ndio unenena nami.
18 Depart not hence, I pray thee, vntil I come vnto thee, and bring mine offring, and lay it before thee. And he sayde, I will tary vntill thou come againe.
Tafadhali, usiondoke hapa, mpaka nitakapokuja kwako na kuleta zawadi yangu na kuiweka mbele yako.” Bwana akasema, “Nitasubiri mpaka utakaporudi.”
19 Then Gideon went in, and made ready a kidde, and vnleauened bread of an Ephah of floure, and put the flesh in a basket, and put the broth in a pot, and brought it out vnto him vnder the oke, and presented it.
Gideoni akaenda, akaandaa mwana mbuzi, na efa moja ya unga akafanya mikate isiyotiwa chachu. Akaiweka nyama hiyo katika kikapu, na akaweka mchuzi ndani ya sufuria na kuviletea chini ya mti wa mwaloni, akavitowa.
20 And the Angell of God saide vnto him, Take the flesh and the vnleauened bread, and lay them vpon this stone, and powre out the broth: and he did so.
Malaika wa Mungu akamwambia, “Chukua nyama na mikate isiyotiwa chachu, ukaweke juu ya mwamba huu, ukamwage mchuzi juu yake.” Gideoni akafanya hivyo.
21 Then the Angell of the Lord put forth the ende of the staffe that he had in his hand, and touched the flesh and the vnleauened bread: and there arose vp fire out of the stone, and consumed the flesh and the vnleauened bread: so the Angel of the Lord departed out of his sight.
Kisha malaika wa Bwana akashika ncha ya fimbo mkononi mwake. Kwa hiyo akagusa nyama na mikate isiyotiwa chachu; moto ukatoka nje ya mwamba, ukateketeza nyama na mikate isiyotiwa chachu. Kisha malaika wa Bwana akaenda, na Gideoni hakuweza kumwona tena.
22 And when Gideon perceiued that it was an Angel of the Lord, Gideon then sayde, Alas, my Lord God: for because I haue seene an Angell of the Lord face to face, I shall die.
Gideoni alielewa kuwa yule alikuwa malaika wa Bwana. Gideoni akasema, “Ewe Bwana MUNGU! Kwa maana nimemwona malaika wa Bwana uso kwa uso!”
23 And the Lord said vnto him, Peace be vnto thee: feare not, thou shalt not die.
Bwana akamwambia, “Amani iwe kwako! Usiogope, huwezi kufa.”
24 Then Gideon made an altar there vnto the Lord, and called it, Iehouah shalom: vnto this day it is in Ophrah, of the father of the Ezrites.
Basi Gideoni akamjengea Bwana madhabahu huko. Aliiita, “Bwana ni Amani.” Hadi leo bado iko katika Ofra ya jamaa ya Waabiezeri.
25 And the same night the Lord sayd vnto him, Take thy fathers yong bullocke, and an other bullocke of seuen yeeres olde, and destroy the altar of Baal that thy father hath, and cut downe the groue that is by it,
Usiku huo, Bwana akamwambia, “Twaa ng'ombe wa baba yako, na ng'ombe wa pili wa umri wa miaka saba, ukaondoe madhabahu ya Baali, ambayo ni ya baba yako, na kukata Ashera iliyo karibu nayo.
26 And build an altar vnto the Lord thy God vpon the top of this rocke, in a plaine place: and take the seconde bullocke, and offer a burnt offringe with the woode of the groue, which thou shalt cut downe.
Jenga madhabahu kwa Bwana, Mungu wako juu ya mahali pa kukimbilia, na kuijenga njia sahihi. Toa ng'ombe ya pili kama sadaka ya kuteketezwa, ukitumia kuni kutoka Ashera uliyoikata. '
27 Then Gideon tooke tenne men of his seruants, and did as ye Lord bade him: but because he feared to doe it by day for his fathers housholde, and the men of the citie, he did it by night.
Gideoni akachukua watumishi wake kumi na kufanya kama Bwana alivyomwambia. Lakini kwa sababu aliogopa sana watu wa nyumba ya baba yake na watu wa mji hakufanya hivyo wakati wa mchana, alifanya hivyo usiku.
28 And when the men of the citie arose early in the morning, beholde, the altar of Baal was broken, and the groue cut downe that was by it, and the seconde bullocke offred vpon the altar that was made.
Asubuhi wakati watu wa mji walipoamka, madhabahu ya Baali imebomolewa, na Ashera iliyokuwa karibu nayo imekatwa, na ng'ombe wa pili ametolewa sadaka kwenye madhabahu iliyojengwa.
29 Therefore they saide one to another, Who hath done this thing? and when they inquired and asked, they saide, Gideon the sonne of Ioash hath done this thing.
Watu wa mji wakaambiana, “Ni nani aliyefanya jambo hili?” Walipokuwa wakiongea na wengine na kutafuta majibu, wakasema, 'Gidioni mwana wa Yoashi amefanya jambo hili.”
30 Then the men of the citie said vnto Ioash, Bring out thy sonne, that hee may dye: for he hath destroyed the altar of Baal, and hath also cut downe the groue that was by it.
Ndipo watu wa mji wakamwambia Yoashi, “Mtoe mtoto wako ili afe, kwa sababu ameibomoa madhabahu ya Baali, na kwa sababu ameikata Ashera karibu nayo.”
31 And Ioash said vnto all that stood by him, Will ye pleade Baals cause? or will ye saue him? he that will contend for him, let him dye or the morning. If he be God, let him pleade for himselfe against him that hath cast downe his altar.
Yoashi akawaambia wote waliompinga, “Je, ninyi mtamsihi Baali? Je, mtamuokoa? Mtu yeyote atakayemtetea, basi atauawa asubuhi hii. Ikiwa Baali ni mungu, basi atajitetea mwenyewe wakati mtu anaibomoa madhabahu yake.”
32 And in that day was Gideon called Ierubbaal, that is, Let Baal pleade for himselfe because he hath broken downe his altar.
Kwa hiyo siku hiyo wakamwita Gideoni “Yerubaali,” kwa sababu alisema, “Baali ajijitetee dhidi yake,” kwa sababu Gidioni alivunja madhabahu ya Baali.
33 Then all the Midianites and the Amalekites and they of ye East, were gathered together, aud went and pitched in the valley of Izreel.
Basi Wamidiani wote, Waamaleki, na watu wa mashariki walikusanyika pamoja. Wakavuka Yordani na wakapanga katika bonde la Yezreeli.
34 But the Spirit of the Lord came vpon Gideon, and he blew a trumpet, and Abiezer was ioyned with him.
Lakini Roho wa Bwana akaja juu ya Gideoni. Gideoni akapiga tarumbeta, akawaita jamaa ya Abiezeri, ili wapate kumfuata.
35 And he sent messengers thorowout al Manasseh, which also was ioyned with him, and he sent messengers vnto Asher, and to Zebulun and to Naphtali, and they came vp to meete them.
Aliwatuma wajumbe wote katika Manase, na wao pia, waliitwa nje kumfuata. Naye akatuma wajumbe kwa Asheri, na Zabuloni, na Naftali; nao wakaenda kumlaki.
36 Then Gideon said vnto God, If thou wilt saue Israel by mine hand, as thou hast sayd,
Gideoni akamwambia Mungu, “Ikiwa ungependa kunitumia kuokoa Israeli, kama ulivyosema,
37 Beholde, I wil put a fleece of wooll in the threshing place: if the dewe come on the fleece onely, and it be drie vpon all the earth, then shall I be sure, that thou wilt saue Israel by mine hand, as thou hast said.
tazameni, ninaweka ngozi ya samazi kwenye sakafu. Ikiwa kuna umande tu juu ya ngozi, na ni kavu duniani, basi nitajua kwamba utanitumia kuokoa Israeli, kama ulivyosema.”
38 And so it was: for he rose vp earely on the morow, and thrust the fleece together, and wringed the dew out of the fleece, and filled a bowle of water.
Hivi ndivyo ilivyotokea-Gideoni aliamka mapama asubuhi, akaikamua ngozi hiyo, na akatoa umande kwenye ngozi, wa kutosha kujaza bakuli kwa maji.
39 Againe, Gideon sayde vnto God, Be not angry with me, that I may speake once more: let me prooue once againe, I pray thee, with the fleece: let it now be drie onely vpon the fleece, and let dewe be vpon all the ground.
Gideoni akamwambia Mungu, 'Usinikasirikie, nitasema tena kwa mara nyingine. Tafadhali niruhusu nijaribu tena kwa kutumia ngozi. Wakati huu uifanye kavu, na iwe na umande juu ya ardhi yote kuzunguka.
40 And God did so that same night: for it was drie vpon the fleece onely, and there was dewe on all the ground.
Mungu alifanya kile alichoomba usiku huo. Ngozi ilikuwa kavu, na kulikuwa na umande katika ardhi yote iliyozunguka.

< Judges 6 >