< Joshua 17 >

1 This was also the lot of the tribe of Manasseh: for he was the first borne of Ioseph, to wit, of Machir the first borne of Manasseh, and the father of Gilead: nowe because he was a man of warre, he had Gilead and Bashan.
Huu ndio mgawo wa kabila la Manase kama mzaliwa wa kwanza wa Yosefu, yaani kwa ajili ya Makiri, mzaliwa wa kwanza wa Manase. Makiri alikuwa baba wa Wagileadi, ambao walipokea Gileadi na Bashani kwa sababu Wamakiri walikuwa askari wakuu.
2 And also of the rest of the sonnes of Manasseh by their families, euen of the sonnes of Abiezer, and of the sonnes of Helek, and of ye sonnes of Azriel, and of the sonnes of Shechem, and of the sonnes of Hepher, and of the sonnes of Shemida: these were the males of Manasseh, the sonne of Ioseph according to their families.
Kwa hiyo mgawo huu ulikuwa kwa ajili ya watu wa Manase waliokuwa wamebaki, ambao ni koo za Abiezeri, Heleki, Asirieli, Shekemu, Heferi na Shemida. Hawa ndio wanaume wale wengine wa uzao wa Manase mwana wa Yosefu kwa koo zao.
3 But Zelophehad the sonne of Hephir, the sonne of Gilead, the sonne of Machir, ye sonne of Manasseh, had no sonnes, but daughters: and these are the names of his daughters, Mahlah, and Noah, Hoglah, Milcah and Tirzah:
Basi Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase hakuwa na wana waume ila mabinti tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.
4 Which came before Eleazar the Priest, and before Ioshua the sonne of Nun, and before the princes, saying, The Lord commanded Moses to giue vs an inheritance among our brethren: therefore according to the commandement of the Lord he gaue them an inheritance among the brethren of their father.
Wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi, wakasema: “Bwana alimwagiza Mose atupatie urithi miongoni mwa ndugu zetu.” Kwa hiyo Yoshua akawapa urithi pamoja na ndugu wa baba yao, kufuatana na agizo la Bwana.
5 And there fell ten portions to Manasseh, beside the land of Gilead and Bashan, which is on the other side Iorden,
Fungu la Manase lilikuwa na sehemu kumi za nchi, licha ya Gileadi na Bashani mashariki mwa Yordani,
6 Because the daughters of Manasseh did inherite among his sonnes: and Manassehs other sonnes had the land of Gilead.
kwa sababu wale binti za kabila la Manase walipokea urithi miongoni mwa wana wa kiume. Nchi ya Gileadi ilikuwa mali ya wazao wa Manase waliobaki.
7 So the borders of Manasseh were from Asher to Michmethah that lieth before Shechem, and this border goeth on the right hand, euen vnto the inhabitants of En-tappuah.
Eneo la Manase lilienea kuanzia Asheri hadi Mikmeta mashariki mwa Shekemu. Mpaka ule ulielekea upande wa kusini kutoka pale kujumuisha watu walioishi En-Tapua.
8 The land of Tappuah belonged to Manasseh, but Tappuah beside the border of Manasseh belongeth to the sonnes of Ephraim.
(Nchi ya Tapua ilikuwa mali ya Manase, lakini Tapua yenyewe iliyo mpakani mwa nchi ya Manase ilikuwa ya Waefraimu.)
9 Also this border goeth downe vnto the riuer Kanah Southward to the riuer: these cities of Ephraim are among the cities of Manasseh: and the border of Manasseh is on the Northside of the riuer, and the endes of it are at the Sea,
Kisha mpaka ule uliendelea kuelekea kusini hadi Bonde la Kana. Kulikuwepo miji ya Efraimu iliyokuwa miongoni mwa miji ya Manase, lakini mpaka wa Manase ulikuwa upande wa kaskazini wa lile bonde na kuishia kwenye bahari.
10 The South perteyneth to Ephraim, and the North to Manasseh, and the Sea is his border: and they met together in Asher Northwarde, and in Issachar Eastward.
Nchi ya kusini ilikuwa ya Efraimu, na ile iliyokuwa upande wa kaskazini ilikuwa ya Manase. Eneo la Manase lilifika bahari na ikapakana na Asheri upande wa kaskazini, na Isakari upande wa mashariki.
11 And Manasseh had in Issachar and in Asher, Beth-shean, and her townes, and Ibleam, and her townes, and the inhabitants of Dor with ye townes thereof, and the inhabitants of En-dor with the townes thereof, and the inhabitants of Thaanach with her townes, and the inhabitants of Megiddo with the townes of the same, euen three countreis.
Katika Isakari na Asheri Manase alikuwa na miji pia: Beth-Shani, Ibleamu na watu wa Dori, Endori, Taanaki na Megido, pamoja na vijiji vyote vinavyohusika na miji hiyo (ya tatu katika orodha ni Nafothi).
12 Yet the children of Manasseh coulde not destroy those cities, but the Canaanites dwelled still in that land.
Lakini Wamanase hawakuweza kuimiliki miji hii, kwa kuwa Wakanaani walikazana kuishi katika maeneo hayo.
13 Neuerthelesse, when the children of Israel were strong, they put the Canaanites vnder tribute, but cast them not out wholy.
Hata hivyo, Waisraeli walivyoendelea kupata nguvu waliwatumikisha Wakanaani na kuwatia katika kazi za kulazimishwa, lakini hawakuwafukuza kabisa.
14 Then the children of Ioseph spake vnto Ioshua, saying, Why hast thou giuen me but one lot, and one portion to inherite, seeing I am a great people, for as much as the Lord hath blessed me hitherto?
Watu wa Yosefu wakamwambia Yoshua, “Kwa nini umetupa sisi mgawo mmoja tu na sehemu moja tu kuwa urithi? Sisi tu watu wengi sana, na Bwana ametubariki kwa wingi.”
15 Ioshua then answered them, If thou be much people, get thee vp to the wood, and cut trees for thy selfe there in the lande of the Perizzites, and of the gyants, if mount Ephraim be too narowe for thee.
Yoshua akajibu, “Kama ninyi ni wengi sana, na kama nchi ya vilima ya Efraimu ni ndogo sana kwenu, pandeni msituni mkafyeke eneo kwa ajili yenu wenyewe huko kwenye nchi ya Waperizi na Warefai.”
16 Then the children of Ioseph saide, The mountaine will not be ynough for vs: and all the Canaanites that dwell in the lowe countrey haue charets of yron, aswell they in Beth-shean, and in the townes of the same, as they in the valley of Izreel.
Watu wa Yosefu wakajibu, “Hiyo nchi ya vilima haitutoshi, nao Wakanaani wote wanaoishi katika tambarare wanayo magari ya vita ya chuma, wote wa Beth-Shani na miji yake, na wale walio katika Bonde la Yezreeli.”
17 And Ioshua spake vnto the house of Ioseph, to Ephraim, and to Manasseh, saying, Thou art a great people, and hast great power, and shalt not haue one lot.
Lakini Yoshua akanena na nyumba ya Yosefu, yaani Efraimu na Manase: “Ninyi ni wengi sana na wenye nguvu sana. Hamtakuwa na mgawo mmoja tu,
18 Therefore the mountaine shall be thine: for it is a wood, and thou shalt cut it downe: and the endes of it shall be thine, and thou shalt cast out the Canaanites, though they haue yron charets, and though they be strong.
bali pia nchi hii ya kilima yenye msitu. Ifyekeni, nayo mipaka yake itakuwa yenu umbali mtakaoweza kufika. Ingawa Wakanaani wana magari ya chuma, nao wana nguvu, mwaweza kuwafukuza humo.”

< Joshua 17 >