< John 4 >

1 Nowe when the Lord knew, how the Pharises had heard, that Iesus made and baptized moe disciples then Iohn,
Basi Yesu alipofahamu kuwa Mafarisayo wamesikia kuwa Yesu alikuwa anafuasa na kuwabatiza zaidi ya Yohana,
2 (Though Iesus himselfe baptized not: but his disciples)
(ingawa Yesu mwenyewe alikuwa habatizi ila wanafunzi wake),
3 Hee left Iudea, and departed againe into Galile.
alitoka Judea na akaenda Galilaya.
4 And he must needes goe through Samaria.
Hivyo ilikuwa muhimu kupitia Samaria.
5 Then came hee to a citie of Samaria called Sychar, neere vnto the possession that Iacob gaue to his sonne Ioseph.
Na akafika kwenye mji wa Samaria, unaoitwa Sikari, karibu na eneo ambalo Yakobo alimpa mwanae Yusufu.
6 And there was Iacobs well. Iesus then wearied in the iourney, sate thus on the well: it was about the sixt houre.
Na kisima cha Yakobo kilikuwa hapo. Yesu alikuwa amechoka kwa ajili ya safari na akakaa karibu na kisima. Ilikuwa muda wa mchana.
7 There came a woman of Samaria to drawe water. Iesus sayd vnto her, Giue me drinke.
Mwanamke Msamaria alikuja kuteka maji, na Yesu akamwambia, “Nipe maji ninywe.”
8 For his disciples were gone away into the citie, to buy meate.
Kwa sababu wanafunzi wake walikuwa wameenda zao mjini kununua chakula.
9 Then sayde the woman of Samaria vnto him, Howe is it, that thou being a Iewe, askest drinke of me, which am a woman of Samaria? For the Iewes meddle not with the Samaritans.
Yule mwanamke akamwambia, “Inakuaje wewe Myahudi, kuniomba mimi mwanamke Msamaria, kitu cha kunywa?” Kwa sababu Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.
10 Iesus answered and saide vnto her, If thou knewest that gift of God, and who it is that saieth to thee, Giue mee drinke, thou wouldest haue asked of him, and hee woulde haue giuen thee, water of life.
Yesu akamjibu, “Kama ungelijua karama ya Mungu, na yule anayekuambia 'Nipe maji, ' ungelimwomba, na angelikupa maji ya uzima.”
11 The woman saide vnto him, Sir, thou hast nothing to drawe with, and the well is deepe: from whence then hast thou that water of life?
Mwanamke akajibu, “Bwana hauna ndoo ya kuchotea, na kisima ni kirefu. Utayapata wapi Maji ya Uzima?
12 Art thou greater then our father Iacob, which gaue vs the well, and hee himselfe dranke thereof, and his sonnes, and his cattell?
Je wewe ni mkuu, kuliko baba yetu Yakobo, ambaye alitupa kisima hiki, na yeye mwenyewe na watoto wake pamoja na mifugo yake wakanywa maji ya kisima hiki?”
13 Iesus answered, and said vnto her, Whosoeuer drinketh of this water, shall thirst againe:
Yesu akajibu, “Yeyote anywae maji haya atapata kiu tena,
14 But whosoeuer drinketh of the water that I shall giue him, shall neuer be more a thirst: but the water that I shall giue him, shalbe in him a well of water, springing vp into euerlasting life. (aiōn g165, aiōnios g166)
lakini yeye atakaye kunywa maji nitakayompa hatapata kiu tena. Badala yake maji nitakayompa yatakuwa chemchemi inayobubujika hata milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
15 The woman said vnto him, Syr, giue me of that water, that I may not thirst, neither come hither to drawe.
Yule mwanamke akamwambia, “Bwana, nayaomba maji hayo ili nisipate kiu, na nisihangaike kuja hapa kuchota maji.”
16 Iesus said vnto her, Go, call thine husband, and come hither.
Yesu akamwambia, “Nenda kamwite mumeo, kisha urudi.”
17 The woman answered, and saide, I haue no husband. Iesus said vnto her, Thou hast well said, I haue no husband.
Mwanamke akamwambia, “Sina mume.” Yesu akajibu, “Umesema vyema, 'Sina mume;'
18 For thou hast had fiue husbands, and he whom thou nowe hast, is not thine husband: that saidest thou truely.
kwa maana umekuwa na wanaume watano, na mmoja ambaye unaye sasa sio mume wako. Katika hili umesema kweli!”
19 The woman saide vnto him, Sir, I see that thou art a Prophet.
Mwanamke akamwambia, “Bwana naona yakuwa wewe ni nabii.
20 Our fathers worshipped in this mountaine, and ye say, that in Ierusalem is the place where men ought to worship.
Baba zetu waliabudu katika mlima huu. Lakini ninyi mwasema ya kuwa Yerusalemu ndiyo sehemu ambayo watu wanapaswa kuabudu.”
21 Iesus saide vnto her, Woman, beleeue me, the houre commeth, when ye shall neither in this mountaine, nor at Hierusalem worship ye Father.
Yesu akamjibu, “Mwanamke, niamini, wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba katika mlima huu au Yerusalemu.
22 Ye worship that which ye knowe not: we worship that which we knowe: for saluation is of the Iewes.
Ninyi watu mwaabudu kile msichokijua, lakini sisi twaabudu tunachokijua, kwa sababu wokovu watoka kwa Wayahudi.”
23 But the houre commeth, and nowe is, when the true worshippers shall worship the Father in spirit, and trueth: for the Father requireth euen such to worship him.
Hatahivyo, wakati unakuja, na sasa upo hapa, wakati waabuduo kweli watamwabudu Baba katika roho na kweli, kwa sababu Baba anawatafuta watu wa namna hiyo kuwa watu wake wanao mwabudu.
24 God is a Spirite, and they that worship him, must worship him in spirit and trueth.
Mungu ni Roho, na wale wanaomwabudu wanapaswa kumwabudu kwa roho na kweli.”
25 The woman said vnto him, I knowe well that Messias shall come which is called Christ: when he is come, he will tell vs all things.
Mwanamke akamwambia, “Ninajua kuwa Masihi anakuja, (aitwaye Kristo). Huyo atakapokuja atatwambia yote.”
26 Iesus said vnto her, I am he, that speake vnto thee.
Yesu akamwambia, “Mimi unayesema nami ndiye.”
27 And vpon that, came his disciples, and marueiled that he talked with a woman: yet no man said vnto him, What askest thou? or why talkest thou with her?
Wakati huo huo wanafunzi wake wakarudi. Nao walishangaa kwa nini alikuwa akizungumza na mwanamke, lakini hakuna aliyethubutu kumuuliza, “Unataka nini?” au “Kwa nini unazungumza naye?”
28 The woman then left her waterpot, and went her way into the citie, and said to the men,
Hivyo mwanamke akauacha mtungi wake na akaenda mjini na akawambia watu,
29 Come, see a man which hath tolde me all things that euer I did: is not he that Christ?
“Njooni mwone mtu aliyeniambia mambo yangu yote niliyoyatenda, je yawezekana akawa ndiye Kristo?”
30 Then they went out of the citie, and came vnto him.
Wakatoka mjini wakaja kwake.
31 In the meane while, the disciples prayed him, saying, Master, eate.
Wakati wa mchana wanafunzi wake walimsihi wakisema, “Rabi kula chakula.”
32 But he said vnto them, I haue meate to eate that ye know not of.
lakini yeye aliwambia, “Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.”
33 Then said ye disciples betweene themselues, Hath any man brought him meate?
Wanafunzi wakaambizana, hakuna aliyemletea kitu chochotekula,”Je walileta?”
34 Iesus saide vnto them, My meate is that I may doe the will of him that sent me, and finish his worke.
Yesu akawambia, “Chakula changu ni kufanya mapenzi yake yeye aliyenituma na kutimiza kazi yake.
35 Say not ye, There are yet foure moneths, and then commeth haruest? Beholde, I say vnto you, Lift vp your eyes, and looke on the regions: for they are white alreadie vnto haruest.
Je, hamsemi, 'Bado miezi mitano na mavuno yatakuwa tayari?' Ninawambieni tazameni mashamba yalivyo tayari kwa mavuno!
36 And he that reapeth, receiueth rewarde, and gathereth fruite vnto life eternall, that both he that soweth, and he that reapeth, might reioyce together. (aiōnios g166)
Yeye avunaye hupokea mishahara na kukusanya matunda kwa ajili ya uzima wa milele, ili kwamba yeye apandaye naye avunaye wafurahi pamoja. (aiōnios g166)
37 For herein is the saying true, that one soweth, and an other reapeth.
Kwa kuwa msemo huu ni wa kweli, 'Mmoja apanda na mwingine avuna.'
38 I sent you to reape that, whereon ye bestowed no labour: other men laboured, and ye are entred into their labours.
Niliwatuma kuvuna ambacho hamkukihangaikia, Wengine wamefanya kazi na ninyi mmeingia katika furaha ya kazi yao.”
39 Nowe many of the Samaritans of that citie beleeued in him, for the saying of the woman which testified, He hath tolde me all things that euer I did.
Wasamaria wengi katika mji ule walimwani kwa sababu ya taarifa ya yule mwanamke aliyekuwa akishuhudia, “Aliyeniambia mambo yote niliyoyafanya.”
40 Then when the Samaritans were come vnto him, they besought him, that he woulde tarie with them: and he abode there two dayes.
Hivyo Wasamaria walipokuja walimsihi akae pamoja nao na akakaa kwao kwa siku mbili.
41 And many moe beleeued because of his owne word.
Na wengi zaidi wakamwamini kwa sababu ya neno lake.
42 And they said vnto the woman, Nowe we beleeue, not because of thy saying: for we haue heard him our selues, and knowe that this is in deede that Christ the Sauiour of the world.
Wakamwambia yule mwanamke, “Tunaamini sio tu kwa maneno yako, kwa sababu sisi wenyewe tumesikia, na sasa twafahamu kuwa hakika yeye ni mwokozi wa ulimwengu.”
43 So two dayes after he departed thence, and went into Galile.
Baada ya siku hizo mbili, akaondoka na kuelekea Galilaya.
44 For Iesus himselfe had testified, that a Prophet hath none honour in his owne countrey.
Kwa sababu yeye mwenyewe alikuwa ametangaza kuwa nabii hana heshima katika nchi yake mwenyewe.
45 Then when he was come into Galile, the Galileans receiued him, which had seene all the things that he did at Hierusalem at the feast: for they went also vnto the feast.
Alipokuja kutoka Galilaya, Wagalilaya walimkaribisha. Walikuwa wameona mambo yote aliyoyafanya Yerusalemu kwenye sikukuu, kwa sababu na wao pia walikuwa wamehudhuria kwenye sikukuu.
46 And Iesus came againe into Cana a towne of Galile, where he had made of water, wine. And there was a certaine ruler, whose sonne was sicke at Capernaum.
Alikuja tena Kana ya Galilaya huko alikoyabadilisha maji kuwa divai. Palikuwa na ofisa ambaye mwana wake alikuwa ni mgonjwa huko Kapernaumu.
47 When he heard that Iesus was come out of Iudea into Galile, he went vnto him, and besought him that he would goe downe, and heale his sonne: for he was euen ready to die.
Aliposikia kuwa Yesu alitoka Judea na kwenda Galilaya, alienda kwa Yesu na kumsihi atelemke amponye mwanawe, ambaye alikuwa karibu kufa.
48 Then saide Iesus vnto him, Except ye see signes and wonders, ye will not beleeue.
Ndipo Yesu akamwambia, “Ninyi msipoona ishara na maajabu hamwezi kuamini.
49 The ruler said vnto him, Syr, goe downe before my sonne dye.
Kiongozi akasema, “Bwana shuka chini kabla mwanangu hajafa.”
50 Iesus said vnto him, Go thy way, thy sonne liueth: and the man beleeued the worde that Iesus had spoken vnto him, and went his way.
Yesu akamwambia, “Nenda mwanao ni mzima.” Yule mtu akaamini neno alilolisema Yesu na akaenda zake.
51 And as he was nowe going downe, his seruants met him, saying, Thy sonne liueth.
Alipokuwa akishuka, watumishi wake walimpokea na kumwambia mwana wake alikuwa mzima.
52 Then enquired he of them the houre when he began to amend. And they said vnto him, Yesterday the seuenth houre the feuer left him.
Hivyo akawauliza ni muda gani alipata nafuu. Wakajibu, “Jana muda wa saa saba homa ilipomwacha.”
53 Then the father knew, that it was the same houre in the which Iesus had said vnto him, Thy sonne liueth. And he beleeued, and all his houshold.
Ndipo baba yake akatambua kuwa ni muda ule ule Yesu aliosema, “Mwana wako ni mzima.” Hivyo yeye na familia yake wakaamini.
54 This second miracle did Iesus againe, after he was come out of Iudea into Galile.
Hii ilikuwa ni ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipotoka Yudea kwenda Galilaya.

< John 4 >