< John 20 >
1 Nowe the first day of the weeke came Marie Magdalene, early when it was yet darke, vnto the sepulchre, and sawe the stone taken away from the tombe.
Alfajiri na mapema Jumapili, kukiwa bado na giza, Maria Magdalene alikwenda kaburini, akaliona lile jiwe limeondolewa mlangoni pa kaburi.
2 Then she ranne, and came to Simon Peter, and to the other disciple whom Iesus loued, and saide vnto them, They haue taken away the Lord out of the sepulchre, and we knowe not where they haue laid him.
Basi, akaenda mbio hadi kwa Petro na yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, akawaambia, “Wamemwondoa Bwana kaburini, na wala hatujui walikomweka.”
3 Peter therefore went forth, and the other disciple, and they came vnto the sepulchre.
Petro pamoja na yule mwanafunzi mwingine wakaenda kaburini.
4 So they ranne both together, but the other disciple did outrunne Peter, and came first to the sepulchre.
Wote wawili walikimbia lakini yule mwanafunzi mwingine alikimbia mbio zaidi kuliko Petro, akatangulia kufika kaburini.
5 And he stouped downe, and sawe the linnen clothes lying: yet went he not in.
Alipoinama na kuchungulia ndani, aliona sanda, lakini hakuingia ndani.
6 Then came Simon Peter following him, and went into the sepulchre, and sawe the linnen clothes lye,
Simoni Petro naye akaja akimfuata, akaingia kaburini; humo akaona sanda,
7 And the kerchiefe that was vpon his head, not lying with the linnen clothes, but wrapped together in a place by it selfe.
na kile kitambaa alichofungwa Yesu kichwani. Hicho kitambaa hakikuwekwa pamoja na hiyo sanda, bali kilikuwa kimekunjwa na kuwekwa mahali peke yake.
8 Then went in also the other disciple, which came first to the sepulchre, and he sawe it, and beleeued.
Kisha yule mwanafunzi mwingine aliyemtangulia kufika kaburini, akaingia pia ndani, akaona, akaaamini.
9 For as yet they knewe not the Scripture, That he must rise againe from the dead.
(Walikuwa bado hawajaelewa Maandiko Matakatifu yaliyosema kwamba ilikuwa lazima afufuke kutoka wafu).
10 And the disciples went away againe vnto their owne home.
Basi, hao wanafunzi wakarudi nyumbani.
11 But Marie stoode without at the sepulchre weeping: and as she wept, she bowed her selfe into the sepulchre,
Maria alikuwa amesimama nje ya kaburi, akilia. Huku akiwa bado analia, aliinama na kuchungulia kaburini,
12 And sawe two Angels in white, sitting, the one at the head, and the other at the feete, where the body of Iesus had laien.
akawaona malaika wawili waliovaa mavazi meupe, wameketi pale mwili wa Yesu ulipokuwa umelazwa, mmoja kichwani na wa pili miguuni.
13 And they said vnto her, Woman, why weepest thou? She said vnto them, They haue taken away my Lord, and I know not where they haue laide him.
Hao malaika wakamwuliza, “Mama, kwa nini unalia?” Naye akawaambia, “Wamemwondoa Bwana wangu, na wala sijui walikomweka!”
14 When she had thus said, she turned her selfe backe, and sawe Iesus standing, and knewe not that it was Iesus.
Baada ya kusema hayo, aligeuka nyuma, akamwona Yesu amesimama hapo, lakini asitambue ya kuwa ni Yesu.
15 Iesus saith vnto her, Woman, why weepest thou? whom seekest thou? She supposing that he had bene the gardener, said vnto him, Sir, if thou hast borne him hence, tell me where thou hast laid him, and I will take him away.
Yesu akamwuliza, “Mama, kwa nini unalia? Unamtafuta nani?” Maria, akidhani kwamba huyo ni mtunza bustani, akamwambia, “Mheshimiwa, kama ni wewe umemwondoa, niambie ulikomweka, nami nitamchukua.”
16 Iesus saith vnto her, Marie. She turned her selfe, and said vnto him, Rabboni, which is to say, Master.
Yesu akamwambia, “Maria!” Naye Maria akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, “Raboni” (yaani “Mwalimu”).
17 Iesus saith vnto her, Touch me not: for I am not yet ascended to my Father: but goe to my brethren, and say vnto them, I ascend vnto my Father, and to your Father, and to my God, and your God.
Yesu akamwambia, “Usinishike; sijakwenda bado juu kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu uwaambie: nakwenda juu kwa Baba yangu na Baba yenu, Mungu wangu na Mungu wenu.”
18 Marie Magdalene came and told the disciples that she had seene the Lord, and that he had spoken these things vnto her.
Hivyo Maria Magdalene akaenda akawapa habari wale wanafunzi kuwa amemwona Bwana, na kwamba alikuwa amemwambia hivyo.
19 The same day then at night, which was the first day of the weeke, and when the doores were shut where the disciples were assembled for feare of the Iewes, came Iesus and stoode in the middes, and saide to them, Peace be vnto you.
Ilikuwa jioni ya siku hiyo ya Jumapili. Wanafunzi walikuwa wamekutana pamoja ndani ya nyumba, na milango ilikuwa imefungwa kwa sababu waliwaogopa viongozi wa Wayahudi. Basi, Yesu akaja, akasimama kati yao, akawaambia, “Amani kwenu!”
20 And when he had so saide, he shewed vnto them his handes, and his side. Then were the disciples glad when they had seene the Lord.
Alipokwisha sema hayo, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Basi, hao wanafunzi wakafurahi mno kumwona Bwana.
21 Then saide Iesus to them againe, Peace be vnto you: as my Father sent me, so sende I you.
Yesu akawaambia tena, “Amani kwenu! Kama vile Baba alivyonituma mimi, nami nawatuma ninyi.”
22 And when he had saide that, he breathed on them, and saide vnto them, Receiue the holy Ghost.
Alipokwisha sema hayo, akawapulizia na kuwaambia, “Pokeeni Roho Mtakatifu.
23 Whosoeuers sinnes ye remit, they are remitted vnto them: and whosoeuers sinnes ye reteine, they are reteined.
Mkiwasamehe watu dhambi zao, wamesamehewa; msipowaondolea, hawasamehewi.”
24 But Thomas one of the twelue, called Didymus, was not with them when Iesus came.
Thoma mmoja wa wale kumi na wawili (aitwaye Pacha), hakuwa pamoja nao wakati Yesu alipokuja.
25 The other disciples therefore saide vnto him, We haue seene the Lord: but he said vnto them, Except I see in his handes the print of the nailes, and put my finger into the print of the nailes, and put mine hand into his side, I will not beleeue it.
Basi, wale wanafunzi wengine wakamwambia, “Tumemwona Bwana.” Thoma akawaambia, “Nisipoona mikononi mwake alama za misumari, na kutia kidole changu katika kovu hizo, na kutia mkono wangu ubavuni mwake, sitasadiki.”
26 And eight dayes after, againe his disciples were within, and Thomas with them. Then came Iesus, when the doores were shut, and stood in the middes, and said, Peace be vnto you.
Basi, baada ya siku nane hao wanafunzi walikuwa tena pamoja mle ndani, na Thoma alikuwa pamoja nao. Milango ilikuwa imefungwa, lakini Yesu akaja, akasimama kati yao, akasema, “Amani kwenu!”
27 After saide he to Thomas, Put thy finger here, and see mine hands, and put forth thine hand, and put it into my side, and be not faithlesse, but faithfull.
Kisha akamwambia Thoma, “Lete kidole chako hapa uitazame mikono yangu; lete mkono wako ukautie ubavuni mwangu. Usiwe na mashaka, ila amini!”
28 Then Thomas answered, and said vnto him, Thou art my Lord, and my God.
Thoma akamjibu, “Bwana wangu na Mungu wangu!”
29 Iesus said vnto him, Thomas, because thou hast seene me, thou beleeuest: blessed are they that haue not seene, and haue beleeued.
Yesu akamwambia, “Je, unaamini kwa kuwa umeniona? Heri yao wale ambao hawajaona, lakini wameamini.”
30 And many other signes also did Iesus in the presence of his disciples, which are not written in this booke.
Yesu alifanya mbele ya wanafunzi wake ishara nyingine nyingi ambazo hazikuandikwa katika kitabu hiki.
31 But these things are written, that ye might beleeue, that Iesus is that Christ that Sonne of God, and that in beleeuing ye might haue life through his Name.
Lakini hizi zimeandikwa ili mpate kuamini kwamba Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu; na kwa kuamini mpate kuwa na uzima kwa nguvu ya jina lake.