< John 16 >
1 These thinges haue I saide vnto you, that ye should not be offended.
Nimewaambia mambo haya ili msiweze kukwazwa.
2 They shall excommunicate you: yea, the time shall come, that whosoeuer killeth you, will thinke that he doeth God seruice.
Watawatoa nje ya masinagogi; hakika saa inakuja ambayo kila atakayewaua atafikiri kuwa anafanya kazi njema kwa ajili ya Mungu.
3 And these things will they doe vnto you, because they haue not knowen ye Father, nor me.
Watawatendea mambo haya kwa sababu hawamfahamu Baba wala hawanifahamu mimi.
4 But these things haue I tolde you, that when the houre shall come, ye might remember, that I tolde you them. And these things said I not vnto you from ye beginning, because I was with you.
Nimewaambia mambo haya ili kwamba wakati ukifika wa haya kutokea, mnaweza kuyakumbuka na jinsi nilivyowaambia muweze wao. Sikuwaambia kuhusu mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
5 But now I go my way to him that sent me, and none of you asketh me, Whither goest thou?
Japokuwa, sasa naenda kwa yule aliyenituma; lakini hakuna kati yenu anayeniuliza, “Unaenda wapi?”
6 But because I haue saide these thinges vnto you, your hearts are full of sorowe.
Kwa sababu nimesema maneno haya kwenu, huzuni imejaa mioyoni mwenu.
7 Yet I tell you the trueth, It is expedient for you that I goe away: for if I goe not away, that Comforter will not come vnto you: but if I depart, I will send him vnto you.
Hata hivyo, nawaambia ukweli: ni vyema kwenu nikiondoka; kwa maana nisipoondoka, mfariji hatakuja kwen; lakini nikienda ntamtuma kwenu.
8 And when he is come, he will reproue the worlde of sinne, and of righteousnesse, and of iudgement.
Akija, huyo mfariji ataubitisha ulimwengu kuhusiana na dhambi, kuhusiana na haki na kuhusiana na hukumu.
9 Of sinne, because they beleeued not in me:
Kuhusiana na dhambi, kwa sababu hawakuniamini mimi,
10 Of righteousnesse, because I goe to my Father, and ye shall see me no more:
kuhusiana na haki, kwa sababu naenda kwa baba, na hamtaniona tena;
11 Of iudgement, because the prince of this world is iudged.
na kuhusiana na hukumu kwa sababu mkuu wa ulimwengu huu amehukumiwa.
12 I haue yet many things to say vnto you, but ye cannot beare them nowe.
Ninayo mengi ya kuwaambia, lakini hamtayaelewa sasa.
13 Howbeit, when he is come which is the Spirit of trueth, he will leade you into all trueth: for he shall not speake of himselfe, but whatsoeuer he shall heare, shall he speake, and he will shew you the things to come.
Lakini, yeye, Roho wa kweli, akija, atawaongoza katika kweli yote; kwa kuwa hataongea kwa ajili yake mwenyewe; lakini yoyote atakayoyasikia, atayasema mambo hayo; na atayadhihirisha kwenu mambo yatakayokuja.
14 He shall glorifie me: for he shall receiue of mine, and shall shewe it vnto you.
Yeye atanitukuza mimi, kwa sababu atayachukua mambo yangu na atayatangaza kwenu.
15 All thinges that the Father hath, are mine: therefore said I, that he shall take of mine, and shewe it vnto you.
Vitu vyote alivyonavyo Baba ni vyangu; kwa hiyo, nimesema kwamba Roho atachukua mambo yangu na atayadhihirisha kwenu.
16 A litle while, and ye shall not see me: and againe a litle while, and ye shall see me: for I goe to the Father.
Bado muda mfupi, hamtaniona tena; na baada ya muda mfupi tena, mtaniona.”
17 Then said some of his disciples among them selues, What is this that he saieth vnto vs, A litle while, and ye shall not see me, and againe, a litle while, and ye shall see me, and, For I goe to the Father.
Baadhi ya wanafunzi wake wakaambizana, “Ni nini anachotuambia, “muda mfupi, na hamtaniona tena,' na, kisha, mda mfupi mtaniona,' na, 'kwa sababu naenda kwa Baba?”
18 They said therefore, What is this that he saith, A litle while? we know not what he sayeth.
Kwa hiyo wakasema, “Ni kitu gani anachosema, 'Bado mda mfupi'? Hatujui asemavyo.”
19 Now Iesus knew that they would aske him, and said vnto them, Doe ye enquire among your selues, of that I said, A litle while, and ye shall not see me: and againe, a litle while, and yee shall see me?
Yesu aliona kuwa walitamani kumuuliza, naye akawaambia, “Mnajiuliza wenyewe kuhusu hili, nilivyosema, 'Bado muda mfupi, hamtaniona tena; na baada ya muda mfupi mtaniona'?
20 Verely, verely I say vnto you, that ye shall weepe and lament, and the worlde shall reioyce: and ye shall sorowe, but your sorowe shalbe turned to ioye.
Amin, amin, nawaambia, mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utashangilia, mtakuwa na huzuni lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
21 A woman when she traueileth, hath sorowe, because her houre is come: but assoone as she is deliuered of the childe, she remembreth no more the anguish, for ioy that a man is borne into the world.
Mwanamke anakuwa na huzuni wakati anapokuwa na uchungu kwa sababu wakati wa kujifungua umefika; lakini anapojifungua mtoto, hakumbuki tena maumivu kwa sababu ya furaha yake kwamba mtoto amezaliwa duniani.
22 And ye nowe therefore are in sorowe: but I will see you againe, and your hearts shall reioyce, and your ioy shall no man take from you.
Ninyi pia mna huzuni sasa, lakini nitawaona tena; na mioyo yenu itafurahi na hakuna atakayeweza kuiondoa furaha yenu.
23 And in that day shall ye aske me nothing. Verely, verely I say vnto you, whatsoeuer ye shall aske the Father in my Name, he will giue it you.
Siku hiyo hamtaniuliza maswali. Amin, Amin, nawaambia, Mkiomba lolote kwa Baba, atawapa kwa jina langu.
24 Hitherto haue ye asked nothing in my Name: aske, and ye shall receiue, that your ioye may be full.
Mpaka sasa hamjaomba lolote kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapokea ili kwamba furaha yenu ikamilike.
25 These things haue I spoken vnto you in parables: but the time will come, when I shall no more speake to you in parables: but I shall shew you plainely of the Father.
Nimezungumza na ninyi kwa lugha isiyoeleweka, lakini saa inakuja ambapo sitazungumza kwa lugha isiyoeleweka lakini badala yake nitawaambia waziwazi kuhusu Baba.
26 At that day shall ye aske in my Name, and I say not vnto you, that I will pray vnto the Father for you:
Siku hiyo mtaomba kwa jina langu, na siwaambii kwamba nitaomba kwa Baba kwa ajili yenu;
27 For the Father himselfe loueth you, because ye haue loued me, and haue beleeued that I came out from God.
Kwa kuwa Baba mwenyewe anawapenda kwa sababu mmenipenda mimi na kwa sababu mmeniamini kuwa nimetoka kwa Baba.
28 I am come out from the Father, and came into the worlde: againe I leaue the worlde, and goe to the Father.
Nilitoka kwa Baba na nimekuja ulimwenguni; tena, naondoka ulimwenguni na ninaenda kwa Baba”.
29 His disciples saide vnto him, Loe, nowe speakest thou plainely, and thou speakest no parable.
Wanafunzi wake wakamwambia, “Unaona, sasa unaongea wazi wazi na hautumii mafumbo.
30 Nowe knowe wee that thou knowest all things, and needest not that any man should aske thee. By this we beleeue, that thou art come out from God.
Sasa, tunajua kwamba unajua mambo yote, na hauhitaji mtu yoyote akuulize maswali. Kwa sababu hii tunaamini kuwa unatoka kwa Mungu.
31 Iesus answered them, Doe you beleeue nowe?
Yesu akawajibu, “Sasa mmeamini?”
32 Beholde, the houre commeth, and is already come, that ye shalbe scattered euery man into his owne, and shall leaue me alone: but I am not alone: for the Father is with me.
Tazama, saa inakuja, ndiyo na hakika imefika, ambapo mtatawanyika kila mmoja na kwa wa kwao mtaniacha mwenyewe. Lakini siko peke yangu kwa sababu Baba yupo nami.
33 These thinges haue I spoken vnto you, that in me ye might haue peace: in the world ye shall haue affliction, but be of good comfort: I haue ouercome the world.
Nawaambia mambo haya ili kwamba ndani yangu muwe na amani. Duniani mna matatizo, lakini jipeni moyo, nimeushinda ulimwengu.