< Joel 3 >
1 For beholde, in those dayes and in that time, when I shall bring againe the captiuitie of Iudah and Ierusalem,
“Katika siku hizo na wakati huo, nitakaporejesha neema ya Yuda na Yerusalemu,
2 I will also gather all nations, and wil bring them downe into the valley of Iehoshaphat, and will pleade with them there for my people, and for mine heritage Israel, whom they haue scattered among the nations, and parted my land.
nitayakusanya mataifa yote na kuyaleta katika Bonde la Yehoshafati Hapo nitaingia kwenye hukumu dhidi yao kuhusu urithi wangu, watu wangu Israeli, kwa kuwa waliwatawanya watu wangu miongoni mwa mataifa na kuigawa nchi yangu.
3 And they haue cast lottes for my people, and haue giuen the childe for the harlot, and sold the girle for wine, that they might drinke.
Wanawapigia kura watu wangu na kuwauza wavulana ili kupata makahaba; waliwauza wasichana ili wapate kunywa mvinyo.
4 Yea, and what haue you to do with me, O Tyrus and Zidon and all the costes of Palestina? will ye render me a recompence? and if ye recompence mee, swiftly and speedily will I render your recompence vpon your head:
“Sasa una nini dhidi yangu, ee Tiro na Sidoni, nanyi nchi zote za Ufilisti? Je, mnanilipiza kwa yale niliyoyafanya? Kama mnalipa, mimi nitalipiza juu ya vichwa vyenu kwa kasi na kwa haraka yale mliyoyatenda.
5 For ye haue taken my siluer and my golde, and haue caried into your temples my goodly and pleasant things.
Kwa kuwa mlichukua fedha na dhahabu yangu pia mkabeba hazina zangu nzuri sana mkapeleka kwenye mahekalu yenu.
6 The children also of Iudah and the children of Ierusalem haue you solde vnto the Grecians, that ye might send them farre from their border.
Mliwauza watu wa Yuda na Yerusalemu kwa Wayunani, ili kwamba mpate kuwapeleka mbali na nchi yao.
7 Beholde, I will rayse them out of the place where ye haue sold them, and will render your reward vpon your owne head,
“Tazama nitawaamsha kutoka zile sehemu mlizowauza, nami nitawalipiza juu ya vichwa vyenu kile mlichofanya.
8 And I will send your sonnes and your daughters into the hande of the children of Iudah, and they shall sell them to the Sabeans, to a people farre off: for the Lord hath spoken it.
Nitawauza wana wenu na binti zenu kwa watu wa Yuda, nao watawauza kwa Waseba, taifa lililo mbali.” Bwana amesema.
9 Publish this among the Gentiles: prepare warre, wake vp the mightie men: let all the men of warre drawe neere and come vp.
Tangazeni hili miongoni mwa mataifa: Jiandaeni kwa vita! Amsha askari! Wanaume wote wapiganaji wasogee karibu na kushambulia.
10 Breake your plowshares into swords, and your sithes into speares: let the weake say, I am strong.
Majembe yenu yafueni yawe panga na miundu yenu ya kukatia iwe mikuki. Aliye dhaifu na aseme, “Mimi nina nguvu!”
11 Assemble your selues, and come all yee heathen and gather your selues together round about: there shall the Lord cast downe the mightie men.
Njooni haraka, ninyi mataifa yote kutoka pande zote, kusanyikeni huko. Shusha wapiganaji wako, Ee Bwana!
12 Let the heathen be wakened, and come vp to the valley of Iehoshaphat: for there will I sit to iudge all the heathen round about.
“Mataifa na yaamshwe; na yasonge mbele kuelekea Bonde la Yehoshafati, kwa kuwa nitaketi mahali pale kuhukumu mataifa yote yaliyoko kila upande.
13 Put in your sithes, for the haruest is ripe: come, get you downe, for the winepresse is full: yea, the winepresses runne ouer, for their wickednesse is great.
Tia mundu, kwa kuwa mavuno yamekomaa. Njooni, mkanyage zabibu, kwa kuwa shinikizo la kukamua zabibu limejaa na mapipa yanafurika: kwa kuwa uovu wao ni mkubwa!”
14 O multitude, O multitude, come into the valley of threshing: for the day of the Lord is neere in the valley of threshing.
Umati mkubwa, umati mkubwa katika bonde la uamuzi! Kwa kuwa siku ya Bwana ni karibu katika bonde la uamuzi.
15 The sunne and moone shalbe darkened, and the starres shall withdrawe their light.
Jua na mwezi vitatiwa giza, na nyota hazitatoa mwanga wake tena.
16 The Lord also shall roare out of Zion, and vtter his voyce from Ierusalem, and the heauens and the earth shall shake, but the Lord wil be the hope of his people, and the strength of the children of Israel.
Bwana atanguruma kutoka Sayuni na mshindo wa ngurumo kutoka Yerusalemu; dunia na mbingu vitatikisika. Lakini Bwana atakuwa kimbilio la watu wake, ngome imara kwa ajili ya watu wa Israeli.
17 So shall ye know that I am the Lord your God dwelling in Zion, mine holy Mountaine: then shall Ierusalem bee holy, and there shall no strangers go thorowe her any more.
“Ndipo mtakapojua kwamba Mimi, Bwana Mungu wenu, nakaa Sayuni, mlima wangu mtakatifu. Yerusalemu utakuwa mtakatifu; kamwe wageni hawatavamia tena.
18 And in that day shall the mountaines drop downe newe wine, and the hilles shall flowe with milke, and al the riuers of Iudah shall runne with waters, and a fountaine shall come forth of the House of the Lord, and shall water the valley of Shittim.
“Katika siku hiyo milima itadondosha divai mpya, na vilima vitatiririka maziwa; mabonde yote ya Yuda yatatiririka maji. Chemchemi itatiririka kutoka kwenye nyumba ya Bwana na kunywesha Bonde la Shitimu.
19 Egypt shalbe waste, and Edom shall be a desolate wildernesse, for the iniuries of the childre of Iudah, because they haue shed innocent blood in their land.
Lakini Misri itakuwa ukiwa, Edomu itakuwa jangwa tupu, kwa sababu ya jeuri waliofanya kwa watu wa Yuda, ambao katika nchi yao walimwaga damu isiyo na hatia.
20 But Iudah shall dwell for euer, and Ierusalem from generation to generation.
Yuda itakaliwa na watu milele na Yerusalemu itadumu vizazi vyote.
21 For I will clense their blood, that I haue not clensed, and the Lord will dwell in Zion.
Hatia yao ya damu, ambayo sijasamehe, nitasamehe.”