< Job 6 >

1 Bvt Iob answered, and said,
Kisha Ayubu akajibu:
2 Oh that my griefe were well weighed, and my miseries were layed together in the balance.
“Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
3 For it woulde be nowe heauier then the sande of the sea: therefore my wordes are swallowed vp.
Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 For the arrowes of the Almightie are in me, the venime whereof doeth drinke vp my spirit, and the terrours of God fight against me.
Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
5 Doeth the wilde asse bray when he hath grasse? or loweth the oxe when he hath fodder?
Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
6 That which is vnsauerie, shall it be eaten without salt? or is there any taste in the white of an egge?
Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
7 Such things as my soule refused to touch, as were sorowes, are my meate.
Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
8 Oh that I might haue my desire, and that God would grant me the thing that I long for!
“Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
9 That is, that God would destroy me: that he would let his hand go, and cut me off.
kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
10 Then should I yet haue comfort, (though I burne with sorowe, let him not spare) because I haue not denyed the wordes of the Holy one.
Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
11 What power haue I that I should endure? or what is mine end, if I should prolong my life?
“Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
12 Is my strength the strength of stones? or is my flesh of brasse?
Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
13 Is it not so, that there is in me no helpe? and that strength is taken from me?
Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
14 He that is in miserie, ought to be comforted of his neighbour: but men haue forsaken the feare of the Almightie.
“Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
15 My brethre haue deceiued me as a brook, and as the rising of the riuers they passe away.
Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
16 Which are blackish with yee, and wherein the snowe is hid.
wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
17 But in time they are dryed vp with heate and are consumed: and when it is hote they faile out of their places,
lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
18 Or they depart from their way and course, yea, they vanish and perish.
Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
19 They that go to Tema, considered them, and they that goe to Sheba, waited for them.
Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
20 But they were confounded: when they hoped, they came thither and were ashamed.
Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
21 Surely nowe are ye like vnto it: ye haue seene my fearefull plague, and are afraide.
Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
22 Was it because I said, Bring vnto me? or giue a rewarde to me of your substance?
Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
23 And deliuer me from the enemies hande, or ransome me out of the hand of tyrants?
au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
24 Teach me, and I wil hold my tongue: and cause me to vnderstande, wherein I haue erred.
“Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
25 Howe stedfast are the wordes of righteousnes? and what can any of you iustly reproue?
Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
26 Doe ye imagine to reproue wordes, that the talke of the afflicted should be as the winde?
Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
27 Ye make your wrath to fall vpon the fatherlesse, and dig a pit for your friende.
Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
28 Nowe therefore be content to looke vpon me: for I will not lie before your face.
“Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
29 Turne, I pray you, let there be none iniquitie: returne, I say, and ye shall see yet my righteousnesse in that behalfe.
Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
30 Is there iniquitie in my tongue? doeth not my mouth feele sorowes?
Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?

< Job 6 >