< Job 42 >

1 Then Iob answered the Lord, and sayd,
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
2 I knowe that thou canst doe all things, and that there is no thought hidde from thee.
“Ninajua ya kuwa unaweza kufanya mambo yote, wala hakuna mpango wako unaoweza kuzuilika.
3 Who is hee that hideth counsell without knowledge? therefore haue I spoken that I vnderstood not, euen things too wonderfull for me, and which I knew not.
Uliuliza, ‘Ni nani huyu afichaye mashauri yangu bila maarifa?’ Hakika nilisema juu ya mambo niliyokuwa siyaelewi, mambo ya ajabu mno kwangu mimi kuyajua.
4 Heare, I beseech thee, and I will speake: I will demaunde of thee, and declare thou vnto me.
“Ulisema, ‘Sikiliza sasa, nami nitanena; nitakuuliza swali, nawe yakupasa kunijibu.’
5 I haue heard of thee by the hearing of the eare, but now mine eye seeth thee.
Masikio yangu yalikuwa yamesikia habari zako, lakini sasa macho yangu yamekuona.
6 Therefore I abhorre my selfe, and repent in dust and ashes.
Kwa hiyo najidharau mwenyewe, na kutubu katika mavumbi na majivu.”
7 Now after that the Lord had spoken these wordes vnto Iob, ye Lord also said vnto Eliphaz ye Temanite, My wrath is kindled against thee, and against thy two friends: for yee haue not spoken of me the thing that is right, like my seruant Iob.
Baada ya Bwana kusema mambo haya yote na Ayubu, akamwambia Elifazi Mtemani, “Nina hasira juu yako na juu ya rafiki zako wawili, kwa sababu hamkusema yaliyo sawa kwa habari yangu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu.
8 Therefore take vnto you nowe seuen bullockes, and seuen rammes, and go to my seruant Iob, and offer vp for your selues a burnt offring, and my seruant Iob shall pray for you: for I wil accept him, least I should put you to shame, because ye haue not spoken of me the thing, which is right, like my seruant Iob.
Basi sasa chukueni mafahali saba na kondoo dume saba mkamwendee mtumishi wangu Ayubu nanyi mkatoe sadaka za kuteketezwa kwa ajili yenu wenyewe. Mtumishi wangu Ayubu ataomba kwa ajili yenu, nami nitayakubali maombi yake ili nisiwatendee sawasawa na upumbavu wenu. Ninyi hamkusema yaliyo sawa kwa habari yangu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu.”
9 So Eliphaz the Temanite, and Bildad the Shuhite, and Zophar the Naamathite went, and did according as the Lord had saide vnto them, and the Lord accepted Iob.
Kwa hiyo Elifazi Mtemani, Bildadi Mshuhi, na Sofari Mnaamathi wakafanya kama Bwana alivyowaambia; naye Bwana akayakubali maombi ya Ayubu.
10 Then the Lord turned the captiuitie of Iob, when he prayed for his friends: also the Lord gaue Iob twise so much as he had before.
Baada ya Ayubu kuwaombea rafiki zake, Bwana akamwondoa kwenye uteka, akamfanikisha tena naye akampa mara mbili ya vile alivyokuwa navyo hapo mwanzoni.
11 Then came vnto him all his brethren, and all his sisters, and all they that had bene of his acquaintance before, and did eate bread with him in his house, and had compassion of him, and comforted him for al the euil, that the Lord had brought vpon him, and euery man gaue him a piece of money, and euery one an earing of golde.
Ndipo ndugu zake wote waume kwa wake na kila mtu aliyemfahamu mwanzoni, wakaja wakala pamoja naye katika nyumba yake. Wakamfariji na kumtuliza moyo juu ya taabu yote Bwana aliyoileta juu yake, nao kila mmoja akampa kipande cha fedha na pete ya dhahabu.
12 So the Lord blessed the last dayes of Iob more then the first: for he had foureteene thousand sheepe, and sixe thousand camels, and a thousand yoke of oxen, and a thousand shee asses.
Bwana akaibariki sehemu ya mwisho ya maisha ya Ayubu kuliko ile ya kwanza. Alikuwa na kondoo elfu kumi na nne, ngamia elfu sita, jozi za mafahali elfu moja, na punda wa kike elfu moja.
13 He had also seue sonnes, and three daughters.
Tena alikuwa na wana saba na binti watatu.
14 And he called the name of one Iemimah, and the name of the seconde Keziah, and the name of the third Keren-happuch.
Binti wa kwanza aliitwa Yemima, wa pili Kesia na wa tatu Keren-Hapuki.
15 In all the lande were no women found so faire as the daughters of Iob, and their father gaue them inheritaunce among their brethren.
Hapakuwepo mahali popote katika nchi ile yote palipopatikana wanawake wazuri kama binti za Ayubu; naye baba yao akawapa urithi pamoja na ndugu zao.
16 And after this liued Iob an hundreth and fourtie yeres, and sawe his sonnes, and his sonnes sonnes, euen foure generations.
Baada ya hili Ayubu akaishi miaka 140; akawaona wanawe na wana wa wanawe hata kizazi cha nne.
17 So Iob dyed, being old, and full of dayes.
Hivyo Ayubu akafa, akiwa mzee aliyekuwa ameshiba siku.

< Job 42 >