< Job 37 >

1 At this also mine heart is astonied, and is mooued out of his place.
“Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
2 Heare the sound of his voyce, and the noyse that goeth out of his mouth.
Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
3 He directeth it vnder the whole heauen, and his light vnto the endes of the world.
Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
4 After it a noyse soundeth: hee thundereth with the voyce of his maiestie, and hee will not stay them when his voyce is heard.
Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
5 God thundereth marueilously with his voyce: he worketh great things, which we know not.
Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
6 For he sayth to the snowe, Be thou vpon the earth: likewise to the small rayne and to the great rayne of his power.
Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
7 With the force thereof he shutteth vp euery man, that all men may knowe his worke.
Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
8 Then the beastes go into the denne, and remaine in their places.
Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
9 The whirlewind commeth out of the South, and the colde from the North winde.
Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
10 At the breath of God the frost is giuen, and the breadth of the waters is made narrowe.
Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
11 He maketh also the cloudes to labour, to water the earth, and scattereth the cloude of his light.
Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
12 And it is turned about by his gouernment, that they may doe whatsoeuer he commandeth them vpon the whole worlde:
Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
13 Whether it be for punishment, or for his lande, or of mercie, he causeth it to come.
Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
14 Hearken vnto this, O Iob: stand and consider the wonderous workes of God.
“Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
15 Diddest thou knowe when God disposed them? and caused the light of his cloud to shine?
Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
16 Hast thou knowen the varietie of the cloude, and the wonderous workes of him, that is perfite in knowledge?
Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
17 Or howe thy clothes are warme, when he maketh the earth quiet through the South winde?
Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
18 Hast thou stretched out the heaues, which are strong, and as a molten glasse?
je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
19 Tell vs what we shall say vnto him: for we can not dispose our matter because of darknes.
“Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
20 Shall it be told him when I speake? or shall man speake when he shalbe destroyed?
Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
21 And nowe men see not the light, which shineth in the cloudes, but the winde passeth and clenseth them.
Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
22 The brightnesse commeth out of the North: the praise thereof is to God, which is terrible.
Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
23 It is the Almightie: we can not finde him out: he is excellent in power and iudgement, and aboundant in iustice: he afflicteth not.
Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
24 Let men therefore feare him: for he will not regarde any that are wise in their owne conceit.
Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

< Job 37 >