< Job 31 >
1 I made a couenant with mine eyes: why then should I thinke on a mayde?
“Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
2 For what portion should I haue of God from aboue? and what inheritance of the Almightie from on hie?
Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
3 Is not destruction to the wicked and strange punishment to the workers of iniquitie?
Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
4 Doeth not he beholde my wayes and tell all my steps?
Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
5 If I haue walked in vanitie, or if my foote hath made haste to deceite,
“Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
6 Let God weigh me in the iust balance, and he shall know mine vprightnes.
Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
7 If my steppe hath turned out of the way, or mine heart hath walked after mine eye, or if any blot hath cleaued to mine handes,
kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
8 Let me sowe, and let another eate: yea, let my plantes be rooted out.
basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
9 If mine heart hath bene deceiued by a woman, or if I haue layde wayte at the doore of my neighbour,
“Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
10 Let my wife grinde vnto another man, and let other men bow downe vpon her:
basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
11 For this is a wickednes, and iniquitie to bee condemned:
Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
12 Yea, this is a fire that shall deuoure to destruction, and which shall roote out al mine increase,
Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
13 If I did contemne the iudgement of my seruant, and of my mayde, when they did contend with me,
“Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
14 What then shall I do when God standeth vp? and when he shall visit me, what shall I answere?
nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
15 He that hath made me in the wombe, hath he not made him? hath not he alone facioned vs in the wombe?
Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
16 If I restrained the poore of their desire, or haue caused the eyes of the widow to faile,
“Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
17 Or haue eaten my morsels alone, and the fatherles hath not eaten thereof,
kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
18 (For from my youth hee hath growen vp with me as with a father, and from my mothers wombe I haue bene a guide vnto her)
lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
19 If I haue seene any perish for want of clothing, or any poore without couering,
kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
20 If his loynes haue not blessed me, because he was warmed with the fleece of my sheepe,
ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
21 If I haue lift vp mine hande against the fatherlesse, when I saw that I might helpe him in the gate,
na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
22 Let mine arme fal from my shoulder, and mine arme be broken from the bone.
basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
23 For Gods punishment was fearefull vnto me, and I could not be deliuered from his highnes.
Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
24 If I made gold mine hope, or haue sayd to the wedge of golde, Thou art my confidence,
“Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
25 If I reioyced because my substance was great, or because mine hand had gotten much,
kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
26 If I did behold the sunne, when it shined, or the moone, walking in her brightnes,
kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
27 If mine heart did flatter me in secrete, or if my mouth did kisse mine hand,
hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
28 (This also had bene an iniquitie to be condemned: for I had denied the God aboue)
basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
29 If I reioyced at his destruction that hated me, or was mooued to ioye when euill came vpon him,
“Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
30 Neither haue I suffred my mouth to sinne, by wishing a curse vnto his soule.
lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
31 Did not the men of my Tabernacle say, Who shall giue vs of his flesh? we can not bee satisfied.
kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
32 The stranger did not lodge in the streete, but I opened my doores vnto him, that went by the way.
Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
33 If I haue hid my sinne, as Adam, concealing mine iniquitie in my bosome,
kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
34 Though I could haue made afraid a great multitude, yet the most contemptible of the families did feare me: so I kept silence, and went not out of the doore.
kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
35 Oh that I had some to heare me! beholde my signe that the Almightie will witnesse for me: though mine aduersary should write a booke against me,
(“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
36 Woulde not I take it vpon my shoulder, and binde it as a crowne vnto me?
Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
37 I will tell him the nomber of my goings, and goe vnto him as to a prince.
Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
38 If my lande cry against me, or the furrowes thereof complayne together,
“Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
39 If I haue eaten the fruites thereof without siluer: or if I haue grieued the soules of the masters thereof,
kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
40 Let thistles growe in steade of wheate, and cockle in the stead of Barley. The wordes of Iob are ended.
basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.