< Job 3 >
1 Afterward Iob opened his mouth, and cursed his day.
Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
2 And Iob cryed out, and sayd,
Kisha akasema:
3 Let the day perish, wherein I was borne, and the night when it was sayde, There is a man childe conceiued.
“Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
4 Let that day bee darkenesse, let not God regarde it from aboue, neyther let the light shine vpon it,
Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
5 But let darkenesse, and the shadowe of death staine it: let the cloude remayne vpon it, and let them make it fearefull as a bitter day.
Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
6 Let darkenesse possesse that night, let it not be ioyned vnto the dayes of the yeere, nor let it come into the count of the moneths.
Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
7 Yea, desolate be that night, and let no ioy be in it.
Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
8 Let them that curse the day, (being readie to renue their mourning) curse it.
Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
9 Let the starres of that twilight be dimme through darkenesse of it: let it looke for light, but haue none: neither let it see the dawning of the day,
Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
10 Because it shut not vp the dores of my mothers wombe: nor hid sorowe from mine eyes.
kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
11 Why died I not in the birth? or why dyed I not, when I came out of the wombe?
“Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
12 Why did the knees preuent me? and why did I sucke the breasts?
Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
13 For so shoulde I now haue lyen and bene quiet, I should haue slept then, and bene at rest,
Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
14 With the Kings and counselers of the earth, which haue buylded themselues desolate places:
pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
15 Or with the princes that had golde, and haue filled their houses with siluer.
pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
16 Or why was I not hid, as an vntimely birth, either as infants, which haue not seene the light?
Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
17 The wicked haue there ceased from their tyrannie, and there they that laboured valiantly, are at rest.
Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
18 The prisoners rest together, and heare not the voyce of the oppressour.
Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
19 There are small and great, and the seruant is free from his master.
Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
20 Wherefore is the light giuen to him that is in miserie? and life vnto them that haue heauie hearts?
“Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
21 Which long for death, and if it come not, they would euen search it more then treasures:
wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
22 Which ioy for gladnes, and reioyce, when they can finde the graue.
ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
23 Why is the light giuen to the man whose way is hid, and whom God hath hedged in?
Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
24 For my sighing commeth before I eate, and my roarings are powred out like the water.
Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
25 For the thing I feared, is come vpon me, and the thing that I was afraid of, is come vnto me.
Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
26 I had no peace, neither had I quietnesse, neither had I rest, yet trouble is come.
Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”