< Job 14 >

1 Man that is borne of woman, is of short continuance, and full of trouble.
“Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake ni chache nazo zimejaa taabu.
2 He shooteth foorth as a flowre, and is cut downe: he vanisheth also as a shadowe, and continueth not.
Huchanua kama ua kisha hunyauka; huwa kama kivuli kipitacho upesi, wala hadumu.
3 And yet thou openest thine eyes vpon such one, and causest me to enter into iudgement with thee.
Je, unamwekea jicho lako mtu kama huyo? Je, utamleta mbele yako katika hukumu?
4 Who can bring a cleane thing out of filthinesse? there is not one.
Ni nani awezaye kutoa kitu safi kutoka kitu najisi? Hakuna awezaye!
5 Are not his dayes determined? the nober of his moneths are with thee: thou hast appointed his boundes, which he can not passe.
Siku za mwanadamu zimewekewa mpaka; umekwisha kutangaza idadi ya miezi yake na kuweka mpaka ambao hawezi kuuvuka.
6 Turne from him that he may cease vntill his desired day, as an hyreling.
Hivyo angalia mbali umwache, hadi awe amekamilisha muda wake kama mtu aliyeajiriwa.
7 For there is hope of a tree, if it bee cut downe, that it will yet sproute, and the branches thereof will not cease.
“Kwa maana lipo tumaini kwa mti; kama ukikatwa utachipuka tena, nayo machipukizi yake mapya hayatakoma.
8 Though the roote of it waxe olde in the earth, and the stocke thereof be dead in ye ground,
Mizizi yake yaweza kuchakaa ardhini na kisiki chake kufa udongoni,
9 Yet by the sent of water it will bud, and bring foorth boughes like a plant.
lakini kwa kupata dalili ya maji utachipua na kutoa machipukizi kama mche.
10 But man is sicke, and dyeth, and man perisheth, and where is he?
Lakini mwanadamu hufa, na huo ndio mwisho wake; hutoa pumzi ya mwisho, naye hayuko tena!
11 As the waters passe from the sea, and as the flood decayeth and dryeth vp,
Kama vile maji yatowekavyo katika bahari, au mkondo wa mto ukaushwavyo na kuwa mkavu,
12 So man sleepeth and riseth not: for hee shall not wake againe, nor be raised from his sleepe till the heauen be no more.
ndivyo mwanadamu alalavyo chini asiamke; hadi mbingu zitakapokuwa hazipo tena, wanadamu hawataamka au kuamshwa kutoka kwenye usingizi wao.
13 Oh that thou wouldest hide me in the graue, and keepe me secret, vntill thy wrath were past, and wouldest giue me terme, and remember me. (Sheol h7585)
“Laiti kama ungenificha kaburini, na kunisitiri hadi hasira yako ipite! Laiti ungeniwekea wakati, na kisha ukanikumbuka! (Sheol h7585)
14 If a man die, shall he liue againe? All the dayes of mine appointed time will I waite, till my changing shall come.
Je, kama mtu akifa, aweza kuishi tena? Siku zote za kazi zangu ngumu nitangojea kufanywa upya kwangu.
15 Thou shalt call me, and I shall answere thee: thou louest the worke of thine own hands.
Utaniita nami nitakuitika; utakionea shauku kiumbe ambacho mikono yako ilikiumba.
16 But nowe thou nombrest my steppes, and doest not delay my sinnes.
Hakika ndipo utakapozihesabu hatua zangu, lakini hutazifuatia dhambi zangu.
17 Mine iniquitie is sealed vp, as in a bagge, and thou addest vnto my wickednesse.
Makosa yangu yatafungiwa kwa lakiri kwenye mfuko, nawe utazifunika dhambi zangu.
18 And surely as the mountaine that falleth, commeth to nought, and the rocke that is remooued from his place:
“Lakini kama mlima umomonyokavyo na kufikichika na kama vile mwamba uondolewavyo mahali pake,
19 As the water breaketh the stones, when thou ouerflowest the things which growe in the dust of ye earth: so thou destroyest ye hope of man.
kama maji yamalizavyo mawe, na mafuriko yachukuavyo udongo, ndivyo unavyoharibu tegemeo la mwanadamu.
20 Thou preuailest alway against him, so that he passeth away: he changeth his face when thou castest him away.
Humshinda mara moja kwa daima, naye hutoweka; waibadilisha sura yake na kumwondoa.
21 And he knoweth not if his sonnes shall be honourable, neither shall he vnderstand concerning them, whether they shalbe of lowe degree,
Kama wanawe wakipewa heshima, yeye hafahamu; kama wakidharauliwa, yeye haoni.
22 But while his flesh is vpon him, he shall be sorowfull, and while his soule is in him, it shall mourne.
Yeye hasikii kingine isipokuwa maumivu ya mwili wake mwenyewe, naye huomboleza kwa ajili yake mwenyewe.”

< Job 14 >