< Job 11 >
1 Then answered Zophar the Naamathite, and sayde,
Ndipo Sofari Mnaamathi alijibu na kusema,
2 Should not the multitude of wordes be answered? or should a great talker be iustified?
“Huo wingi wa maneno haupaswi kujibiwa? Mtu huyu, aliyejaa maneno mengi awe wa kuaminiwa?
3 Should men holde their peace at thy lyes? and when thou mockest others, shall none make thee ashamed?
Kujivuna kwako kunapaswa kuwafanya wengine wabaki wamenyamaza? Wakati unapoyadhihaki mafundisho yetu, hakuna awaye yote atakayekufanya wewe ujisikie mwenye aibu?
4 For thou hast sayde, My doctrine is pure, and I am cleane in thine eyes.
Kwa kuwa wewe unasema kwa Mungu, 'Imani yangu ni safi, Mimi sina waa lolote machoni pako.'
5 But, oh that God would speake and open his lippes against thee!
Lakini, laiti, Mungu huyo angesema na kufungua midomo yake dhidi yako;
6 That he might shewe thee the secretes of wisedome, howe thou hast deserued double, according to right: know therefore that God hath forgotten thee for thine iniquitie.
hivyo angekuonyesha wewe siri za hekima! Kwa kuwa yeye ni mkuu katika ufahamu. Tena tambua huyo Mungu anataka kutoka kwako kidogo kuliko uovu wako unavyostahili.
7 Canst thou by searching finde out God? canst thou finde out ye Almighty to his perfection?
Je, wewe unaweza kumfahamu Mungu kwa kumtafuta yeye? Unaweza kumtambua aliye mkuu kwa ukamilifu?
8 The heauens are hie, what canst thou doe? it is deeper then the hell, how canst thou know it? (Sheol )
Upeo uko juu kama mbingu; unaweza kufanya nini wewe? Ni wenye kina kirefu kuliko kuzimu; waweza kufahamu nini wewe? (Sheol )
9 The measure thereof is longer then the earth, and it is broader then the sea.
Vipimo vyake ni virefu kuliko nchi, na vipana kuliko bahari.
10 If hee cut off and shut vp, or gather together, who can turne him backe?
kama yeye akipita kati na kumyamazisha mtu yeyote, kama yeye akimwita mtu yeyote hukumuni, tena ni nani anayeweza kumzuia yeye?
11 For hee knoweth vaine men, and seeth iniquitie, and him that vnderstandeth nothing.
Kwa maana anawajua watu waongo; wakati anapoona uovu, hawezi yeye kuukumbuka?
12 Yet vaine man would be wise, though man new borne is like a wilde asse colte.
Lakini watu wapumbavu hawana ufahamu; wataupata wakati punda mwitu atakapozaa mtu.
13 If thou prepare thine heart, and stretch out thine hands toward him:
Lakini ikiwa umeuelekeza moyo wako kwa haki na umeunyosha mkono wako karibu na Mungu;
14 If iniquitie be in thine hand, put it farre away, and let no wickednesse dwell in thy Tabernacle.
ikiwa huo uovu ulikuwa katika mikono yako, lakini hivyo tena unauweka mbali nawe, na haukuruhusu kutokuwa mwenye haki kukaa hemani mwako.
15 The truely shalt thou lift vp thy face without spot, and shalt be stable, and shalt not feare.
Ndipo kwa hakika ungeinua juu uso wako bila ishara ya aibu; Ni dhahiri, ungethibitika na usingeogopa.
16 But thou shalt forget thy miserie, and remember it as waters that are past.
Wewe ungesahau mateso yako; ungeyakumbuka hayo tu kama maji ambayo yametiririka mbali.
17 Thine age also shall appeare more cleare then the noone day: thou shalt shine and bee as the morning.
Maisha yako yangekuwa angavu kuliko adhuhuri; japokuwa kulikuwa na giza, litakuwa kama asubuhi.
18 And thou shalt bee bolde, because there is hope: and thou shalt digge pittes, and shalt lye downe safely.
Ungekuwa salama kwa sababu kuna tumaini; ni dhahiri, wewe utapata usalama juu yako na utachukua pumziko lako katika usalama.
19 For when thou takest thy rest, none shall make thee afraide: yea, many shall make sute vnto thee.
Pia ungelala chini katika pumziko, na hakuna ambaye angekufanya wewe uogope; hakika wengi wangetafuta upendeleo wako.
20 But the eyes of the wicked shall faile, and their refuge shall perish, and their hope shalbe sorow of minde.
Lakini macho ya watu waovu yatashindwa; hawatakuwa na njia ya kukimbia; tumaini lao la pekee litakuwa pumzi yao ya mwisho ya uhai.