< Jeremiah 35 >

1 The worde which came vnto Ieremiah from the Lord, in the dayes of Iehoiakim the sonne of Iosiah King of Iudah, saying,
Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana, wakati wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda:
2 Go vnto the house of the Rechabites, and speake vnto them, and bring them into the house of the Lord into one of the chambers, and giue them wine to drinke.
“Nenda kwa jamaa ya Warekabi, uwaalike waje kwenye moja ya vyumba vya pembeni vya nyumba ya Bwana, na uwape divai wanywe.”
3 Then tooke I Iaazaniah, the sonne of Ieremiah the sonne of Habazziniah, and his brethren, and all his sonnes, and the whole house of the Rechabites,
Basi nikaenda kumwita Yaazania mwana wa Yeremia, mwana wa Habazinia, na ndugu zake na wanawe wote, yaani jamaa nzima ya Warekabi.
4 And I brought them into the House of the Lord, into the chamber of the sonnes of Hanan, the sonne of Igdaliah a man of God, which was by the chamber of the princes, which was aboue the chamber of Maaseiah the sonne of Shallum, the keeper of the treasure.
Nikawaleta katika nyumba ya Bwana, ndani ya chumba cha wana wa Hanani mwana wa Igdalia mtu wa Mungu. Kilikuwa karibu na chumba cha maafisa, ambacho kilikuwa juu ya kile cha Maaseya mwana wa Shalumu, aliyekuwa bawabu.
5 And I set before the sonnes of the house of the Rechabites, pots full of wine, and cuppes, and said vnto them, Drinke wine.
Kisha nikaweka mabakuli yaliyojaa divai na baadhi ya vikombe mbele ya watu wa jamaa ya Warekabi na kuwaambia, “Kunyweni divai.”
6 But they said, We will drinke no wine: for Ionadab the sonne of Rechab our father commanded vs, saying, Ye shall drinke no wine, neither you nor your sonnes for euer.
Lakini wao wakajibu, “Sisi hatunywi divai, kwa sababu baba yetu Yonadabu mwana wa Rekabu, alitupa agizo hili: ‘Ninyi wala wazao wenu kamwe msinywe divai.
7 Neither shall ye build house, nor sow seede, nor plant vineyarde, nor haue any, but all your dayes ye shall dwell in tentes, that ye may liue a long time in the land where ye be strangers.
Pia msijenge nyumba kamwe, wala kuotesha mbegu au kupanda mashamba ya mizabibu. Kamwe msiwe na kitu chochote katika hivi, lakini siku zote lazima muishi kwenye mahema. Ndipo mtakapoishi kwa muda mrefu katika nchi ambayo ninyi ni wahamiaji.’
8 Thus haue wee obeyed the voyce of Ionadab the sonne of Rechab our father, in all that he hath charged vs, and wee drinke no wine all our dayes, neither wee, our wiues, our sonnes, nor our daughters.
Tumetii kila kitu ambacho baba yetu Yonadabu mwana wa Rekabu alituamuru. Sisi wenyewe wala wake zetu wala wana wetu na binti zetu kamwe hatujanywa divai
9 Neither builde wee houses for vs to dwell in, neither haue we vineyard, nor fielde, nor seede,
wala kujenga nyumba za kuishi au kuwa na mashamba ya mizabibu, mashamba au mazao.
10 But we haue remained in tentes, and haue obeyed, and done according to all that Ionadab our father commanded vs.
Tumeishi katika mahema na tumetii kikamilifu kila kitu alichotuamuru baba yetu Yonadabu.
11 But when Nebuchad-nezzar King of Babel came vp into the land, we said, Come, and let vs go to Ierusalem, from the hoste of the Caldeans, and from the host of Aram: so we dwel at Ierusalem.
Lakini wakati Nebukadneza mfalme wa Babeli alipoivamia nchi hii, tulisema, ‘Njooni, lazima twende Yerusalemu ili kukimbia majeshi ya Wakaldayo na ya Washamu.’ Kwa hiyo tumeishi Yerusalemu.”
12 Then came the word of the Lord vnto Ieremiah, saying,
Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
13 Thus saith the Lord of hostes, the God of Israel, Goe, and tell the men of Iudah, and the inhabitants of Ierusalem, Will ye not receiue doctrine to obey my wordes, saith the Lord?
“Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliye Mungu wa Israeli, asemalo: Nenda ukawaambie watu wa Yuda na watu wa Yerusalemu, ‘Je, hamwezi kujifunza kutoka kwa wana wa Rekabu, na kuyatii maneno yangu?’ asema Bwana.
14 The commandement of Ionadab the sonne of Rechab that hee commanded his sonnes, that they should drinke no wine, is surely kept: for vnto this day they drinke none, but obey their fathers commandement: notwithstanding I haue spoken vnto you, rising earely, and speaking, but ye would not obey me.
‘Yonadabu mwana wa Rekabu aliwaagiza wanawe wasinywe divai, na agizo hilo wamelishika mpaka leo hawanywi divai, kwa sababu wanatii amri ya baba yao. Lakini nimenena nanyi tena na tena, lakini hamkunitii mimi.
15 I haue sent also vnto you all my seruants the Prophetes, rising vp earely, and sending, them, saying, Returne nowe euery man from his euill way, and amende your workes, and goe not after other gods to serue them, and ye shall dwel in the lande which I haue giuen vnto you, and to your fathers, but ye would not encline your eare, nor obey mee.
Tena na tena nimewatuma watumishi wangu wote manabii kwenu. Wakasema, “Kila mmoja wenu ni lazima ageuke na kuacha njia zake mbaya, na kuyatengeneza matendo yake. Msifuate miungu mingine ili kuitumikia. Ndipo mtakapoishi katika nchi niliyowapa ninyi na baba zenu.” Lakini hamkujali wala kunisikiliza.
16 Surely the sonnes of Ionadab the sonne of Rechab, haue kept the commandement of their father, which he gaue them, but this people hath not obeyed me.
Wazao wa Yonadabu mwana wa Rekabu walitimiza amri ambayo baba yao aliwapa, lakini watu hawa hawakunitii mimi.’
17 Therefore thus saith the Lord of hostes, the God of Israel, Beholde, I will bring vpon Iudah, and vpon all the inhabitants of Ierusalem, all the euill that I haue pronounced against them, because I haue spoke vnto them, but they would not heare, and I haue called vnto them, but they would not answere.
“Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Sikilizeni! Nitaleta juu ya Yuda na juu ya kila mmoja aishiye Yerusalemu kila aina ya maafa niliyotamka dhidi yao. Nilinena nao, lakini hawakusikiliza. Niliwaita, lakini hawakujibu.’”
18 And Ieremiah said to the house of the Rechabites, Thus saith the Lord of hostes the God of Israel, Because ye haue obeyed the commandement of Ionadab your father, and kept all his precepts, and done according vnto all that hee hath commanded you,
Kisha Yeremia akaiambia jamaa ya Warekabi, “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: ‘Mmetii amri ya baba yenu Yonadabu, na mmefuata mafundisho yake yote na mmefanya kila kitu alichowaamuru.’
19 Therefore thus saith the Lord of hostes, the God of Israel, Ionadab the sonne of Rechab shall not want a man, to stand before me for euer.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Yonadabu mwana wa Rekabu hatakosa kamwe kuwa na mtu wa kunitumikia mimi.’”

< Jeremiah 35 >