< Jeremiah 3 >
1 They say, If a man put away his wife, and she goe from him, and become another mans, shall hee returne againe vnto her? shall not this land be polluted? but thou hast played the harlot with many louers: yet turne againe to mee, sayeth the Lord.
“Kama mtu akimpa talaka mkewe, naye akamwacha na akaolewa na mtu mwingine, je, huyo mume aweza kumrudia tena? Je, hiyo nchi haitanajisika kabisa? Lakini umeishi kama kahaba na wapenzi wengi: je, sasa utanirudia tena?” asema Bwana.
2 Lift vp thine eyes vnto the hie places, and beholde, where thou hast not plaied the harlot: thou hast sit waiting for them in the waies, as the Arabian in the wildernesse: and thou hast polluted the lande with thy whoredomes, and with thy malice.
“Inua macho utazame miinuko iliyo kame na uone. Je, pana mahali ambapo hawajalala nawe? Uliketi kando ya barabara ukiwasubiri wapenzi, ukakaa kama yeye ahamahamaye jangwani. Umeinajisi nchi kwa ukahaba wako na uovu wako.
3 Therefore the showres haue beene restrained, and the latter raine came not, and thou haddest a whores forehead: thou wouldest not bee ashamed.
Kwa hiyo mvua imezuiliwa, nazo mvua za vuli hazikunyesha. Hata hivyo, una uso usio na haya kama wa kahaba; unakataa kutahayari kwa aibu.
4 Diddest thou not stil crie vnto me, Thou art my father, and the guide of my youth?
Je, wewe hujaniita hivi punde tu: ‘Baba yangu, rafiki yangu tangu ujana wangu,
5 Wil he keepe his anger for euer? will he reserue it to the ende? thus hast thou spoken, but thou doest euill, euen more and more.
je, utakasirika siku zote? Je, ghadhabu yako itaendelea milele?’ Hivi ndivyo unavyozungumza, lakini unafanya maovu yote uwezayo.”
6 The Lord saide also vnto me, in the daies of Iosiah the King, Hast thou seene what this rebell Israel hath done? for she hath gone vp vpon euery high mountaine, and vnder euery greene tree, and there plaied the harlot.
Wakati wa utawala wa Mfalme Yosia, Bwana aliniambia, “Umeona kile Israeli asiye mwaminifu amekifanya? Amepanda juu ya kila kilima kirefu, na chini ya kila mti uliotanda na amefanya uzinzi huko.
7 And I sayde, when shee had done all this, Turne thou vnto me: but she returned not, as her rebellious sister Iudah sawe.
Mimi nilifikiri kuwa baada ya kuyafanya yote haya angelinirudia, lakini hakurudi, naye dada yake Yuda mdanganyifu aliona hili.
8 When I sawe, howe that by all occasions rebellious Israel had plaied the harlot, I cast her away, and gaue her a bill of diuorcement: yet her rebellious sister Iudah was not afraied, but shee went also, and plaied the harlot.
Nilimpa Israeli asiye mwaminifu hati yake ya talaka, na kumfukuza kwa ajili ya uzinzi wake wote. Hata hivyo nikaona kuwa Yuda dada yake mdanganyifu hakuogopa. Yeye pia alitoka na kufanya uzinzi.
9 So that for the lightnesse of her whoredome shee hath euen defiled the lande: for shee hath committed fornication with stones and stockes.
Kwa sababu uasherati wa Israeli haukuwa kitu kwake, Yuda aliinajisi nchi kwa kuzini na mawe na miti.
10 Neuerthelesse for all this, her rebellious sister Iudah hath not returned vnto mee with her whole heart, but fainedly, sayth the Lord.
Pamoja na hayo yote, Yuda dada yake mdanganyifu hakunirudia kwa moyo wake wote, bali kwa kujifanya tu,” asema Bwana.
11 And the Lord said vnto me, The rebellious Israel hath iustified her selfe more then the rebellious Iudah.
Bwana akaniambia, “Israeli asiye mwaminifu ana haki kuliko Yuda mdanganyifu.
12 Goe and crie these woordes towarde the North and say, Thou disobedient Israel, returne, sayeth the Lord, and I will not let my wrath fall vpon you: for I am mercifull, sayeth the Lord, and I will not alway keepe mine anger.
Nenda, ukatangaze ujumbe huu kuelekea kaskazini: “‘Rudi, Israeli usiye mwaminifu,’ asema Bwana, ‘sitakutazama tena kwa uso uliokunjamana, kwa kuwa mimi ni mwenye huruma,’ asema Bwana, ‘Sitashika hasira yangu milele.
13 But knowe thine iniquitie: for thou hast rebelled against the Lord thy God, and hast scattered thy waies to the straunge gods vnder euery greene tree, but yee woulde not obey my voyce, sayeth the Lord.
Ungama dhambi zako tu: kwamba umemwasi Bwana Mungu wako, umetapanya wema wako kwa miungu ya kigeni chini ya kila mti unaotanda, nawe hukunitii mimi,’” asema Bwana.
14 O yee disobedient children, turne againe, sayeth the Lord, for I am your Lord, and I will take you one of a citie, and two of a tribe and wil bring you to Zion,
“Rudini, enyi watu msio waaminifu, kwa kuwa mimi ni mume wenu,” asema Bwana. “Nitawachagua ninyi, mmoja kutoka kwenye mji, na wawili kutoka kwenye ukoo, nami nitawaleta Sayuni.
15 And I will giue you pastours according to mine heart, which shall feede you with knowledge and vnderstanding.
Kisha nitawapeni wachungaji wanipendezao moyo wangu, ambao watawaongoza kwa maarifa na ufahamu.
16 Moreouer, when yee be increased and multiplied in the land, in those daies, saieth the Lord, they shall say no more, The Arke of the couenant of the Lord: for it shall come no more to minde, neither shall they remember it, neither shall they visite it, for that shalbe no more done.
Katika siku hizo, idadi yenu itakapokuwa imeongezeka sana katika nchi, watu hawatasema tena, ‘Sanduku la Agano la Bwana,’” asema Bwana. “Halitaingia tena kwenye mawazo yao wala kukumbukwa, hawatalihitaji wala halitatengenezwa jingine.
17 At that time they shall cal Ierusalem, The throne of the Lord, and all the nations shall be gathered vnto it, euen to the Name of the Lord in Ierusalem: and thence foorth they shall follow no more the hardnesse of their wicked heart.
Wakati huo, wataita Yerusalemu kuwa Kiti cha Enzi cha Bwana, nayo mataifa yote watakusanyika Yerusalemu kuliheshimu jina la Bwana. Hawatafuata tena ukaidi wa mioyo yao miovu.
18 In those daies ye house of Iudah shall walke with the house of Israel, and they shall come together out of the lande of the North, into the lande, that I haue giuen for an inheritance vnto your fathers.
Katika siku hizo, nyumba ya Yuda itaungana na nyumba ya Israeli, wao kwa pamoja watakuja kutoka nchi ya kaskazini hadi nchi niliyowapa baba zenu kama urithi.
19 But I sayde, Howe did I take thee for children and giue thee a pleasant lande, euen the glorious heritage of the armies of the heathen, and saide, Thou shalt call mee, saying, My father, and shalt not turne from me?
“Mimi mwenyewe nilisema, “‘Tazama jinsi nitakavyowatunza kwa furaha kama wana na kuwapa nchi nzuri, urithi ulio mzuri kuliko wa taifa jingine lolote.’ Nilidhani mngeniita ‘Baba,’ na msingegeuka, mkaacha kunifuata.
20 But as a woman rebelleth against her husband: so haue yee rebelled against me, O house of Israel, sayeth the Lord.
Lakini kama mwanamke asiye mwaminifu kwa mumewe, vivyo hivyo mmekosa uaminifu kwangu pia, ee nyumba ya Israeli,” asema Bwana.
21 A voice was heard vpon the hie places, weeping and supplications of the children of Israel: for they haue peruerted their way, and forgotten the Lord their God.
Kilio kinasikika juu ya miinuko iliyo kame, kulia na kuomboleza kwa watu wa Israeli, kwa sababu wamepotoka katika njia zao na wamemsahau Bwana Mungu wao.
22 O yee disobedient children, returne and I wil heale your rebellions. Behold, we come vnto thee, for thou art the Lord our God.
“Rudini, enyi watu msio waaminifu, nami nitawaponya ukengeufu wenu.” “Naam, tutakuja kwako, kwa maana wewe ni Bwana Mungu wetu.
23 Truely the hope of the hilles is but vaine, nor the multitude of mountaines: but in the Lord our God is the health of Israel.
Hakika zile ghasia za kuabudu sanamu kwenye vilima na milimani ni udanganyifu; hakika katika Bwana, Mungu wetu, uko wokovu wa Israeli.
24 For confusion hath deuoured our fathers labour, from our youth their sheepe and their bullocks, their sonnes and their daughters.
Tangu ujana wetu miungu ya aibu imeyala matunda ya kazi za baba zetu: makundi yao ya kondoo na ngʼombe, wana wao na binti zao.
25 Wee lie downe in our confusion, and our shame couereth vs: for we haue sinned against the Lord our God, we and our fathers from our youth, euen vnto this day, and haue not obeyed the voyce of the Lord our God.
Sisi na tulale chini katika aibu yetu, na fedheha yetu itufunike. Tumetenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wetu, sisi na mababa zetu; tangu ujana wetu hadi leo hatukumtii Bwana Mungu wetu.”