< Isaiah 61 >
1 The Spirit of the Lord God is vpon mee, therefore hath the Lord anoynted mee: hee hath sent mee to preache good tidings vnto the poore, to binde vp the broken hearted, to preach libertie to the captiues, and to them that are bound, the opening of the prison,
Roho wa Bwana Mwenyezi yu juu yangu, kwa sababu Bwana amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao;
2 To preache the acceptable yeere of the Lord, and the day of vengeance of our God, to comfort all that mourne,
kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa, na siku ya kisasi ya Mungu wetu, kuwafariji wote waombolezao,
3 To appoint vnto them that mourne in Zion, and to giue vnto them beautie for ashes, the oyle of ioye for mourning, the garment of gladnesse for the spirit of heauinesse, that they might be called trees of righteousnesse, the planting of the Lord, that he might be glorified.
na kuwapa mahitaji wale wanaohuzunika katika Sayuni, ili kuwapa taji ya uzuri badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho ya kukata tamaa. Nao wataitwa mialoni ya haki, pando la Bwana, ili kuonyesha utukufu wake.
4 And they shall builde the olde waste places, and raise vp the former desolations, and they shall repaire the cities that were desolate and waste through many generations.
Watajenga upya magofu ya zamani na kupatengeneza mahali palipoachwa ukiwa zamani; watafanya upya miji iliyoharibiwa, iliyoachwa ukiwa kwa vizazi vingi.
5 And the strangers shall stande and feede your sheepe, and the sonnes of the strangers shall be your plowmen and dressers of your vines.
Wageni watayachunga makundi yenu, wageni watafanya kazi katika mashamba yenu, na kutunza mashamba yenu ya mizabibu.
6 But ye shall be named the Priestes of the Lord, and men shall say vnto you, The ministers of our God, Ye shall eate the riches of the Gentiles, and shalbe exalted with their glorie.
Nanyi mtaitwa makuhani wa Bwana, mtaitwa watumishi wa Mungu wetu. Mtakula utajiri wa mataifa, nanyi katika utajiri wao mtajisifu.
7 For your shame you shall receiue double, and for confusion they shall reioyce in their portion: for in their lande they shall possesse the double: euerlasting ioy shall be vnto them.
Badala ya aibu yao watu wangu watapokea sehemu maradufu, na badala ya fedheha watafurahia katika urithi wao; hivyo watarithi sehemu maradufu katika nchi yao, nayo furaha ya milele itakuwa yao.
8 For I the Lord loue iudgement and hate robberie for burnt offering, and I wil direct their worke in trueth, and will make an euerlasting couenant with them.
“Kwa maana Mimi, Bwana, napenda haki, na ninachukia unyangʼanyi na uovu. Katika uaminifu wangu nitawapa malipo yao na kufanya agano la milele nao.
9 And their seede shall be knowen among the Gentiles, and their buddes among the people. All that see them, shall know them, that they are the seede which the Lord hath blessed.
Wazao wao watajulikana miongoni mwa mataifa, na uzao wao miongoni mwa kabila za watu. Wale wote watakaowaona watatambua kuwa ni taifa ambalo Bwana amelibariki.”
10 I will greatly reioyce in the Lord, and my soule shall be ioyfull in my God: for he hath clothed mee with the garments of saluation, and couered me with the robe of righteousnes: hee hath decked me like a bridegrome, and as a bride tireth herselfe with her iewels.
Ninafurahia sana katika Bwana, nafsi yangu inashangilia katika Mungu wangu. Kwa maana amenivika mavazi ya wokovu, na kunipamba kwa joho la haki, kama vile bwana arusi apambavyo kichwa chake kama kuhani, na kama bibi arusi ajipambavyo kwa vito vyake vya thamani.
11 For as the earth bringeth foorth her bud, and as the garden causeth to growe that which is sowen in it: so the Lord God will cause righteousnesse to grow and praise before all the heathen.
Kwa maana kama vile ardhi ifanyavyo chipukizi kuota, na bustani isababishavyo mbegu kuota, ndivyo Bwana Mwenyezi atafanya haki na sifa zichipuke mbele ya mataifa yote.