< Isaiah 21 >

1 The burden of the desert Sea. As the whirlewindes in the South vse to passe from the wildernesse, so shall it come from the horrible land.
Neno kuhusu Jangwa kando ya Bahari: Kama upepo wa kisulisuli unaopita katika nchi hadi kusini, mshambuliaji anakuja kutoka jangwani, kutoka nchi inayotisha.
2 A grieuous vision was shewed vnto me, The transgressour against a transgressour, and the destroyer against a destroyer. Goe vp Elam, besiege Media: I haue caused all the mourning thereof to cease.
Nimeonyeshwa maono ya kutisha: Msaliti anasaliti, mteka nyara anateka nyara. Elamu, shambulia! Umedi, izunguke kwa jeshi! Nitakomesha huzuni zote alizosababisha.
3 Therefore are my loynes filled with sorow: sorowes haue taken me as the sorowes of a woman that trauayleth: I was bowed downe when I heard it, and I was amased when I sawe it.
Katika hili mwili wangu umeteswa na maumivu, maumivu makali ya ghafula yamenishika, kama yale ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa. Nimeduwazwa na lile ninalolisikia, nimeshangazwa na lile ninaloliona.
4 Mine heart failed: fearefulnesse troubled me: the night of my pleasures hath he turned into feare vnto me.
Moyo wangu unababaika, woga unanifanya nitetemeke, gizagiza la jioni nililolitamani sana, limekuwa hofu kuu kwangu.
5 Prepare thou the table: watch in the watch towre: eate, drinke: arise, ye princes, anoynt the shielde.
Wanaandaa meza, wanatandaza mazulia, wanakula, wanakunywa! Amkeni, enyi maafisa, zitieni ngao mafuta!
6 For thus hath the Lord said vnto me, Go, set a watchman, to tell what he seeth.
Hili ndilo Bwana analoniambia: “Nenda, weka mlinzi, na atoe taarifa ya kile anachokiona.
7 And he sawe a charet with two horsemen: a charet of an asse, and a charet of a camel: and he hearkened and tooke diligent heede.
Anapoona magari ya vita pamoja na kundi la farasi, wapanda punda au wapanda ngamia, na awe macho, awe macho kikamilifu.”
8 And he cryed, A lyon: my lorde, I stand continually vpon ye watche towre in the day time, and I am set in my watche euery night:
Naye mlinzi alipaza sauti, “Mchana baada ya mchana, bwana wangu, ninasimama katika mnara wa ulinzi, kila usiku ninakaa mahali pangu nilipoamriwa.
9 And beholde, this mans charet commeth with two horsemen. And he answered and said, Babel is fallen: it is fallen, and all the images of her gods hath he broken vnto the ground.
Tazama, yuaja mtu anayepanda gari la vita pamoja na kundi la farasi. Naye anajibu: ‘Babeli umeanguka, umeanguka! Vinyago vyote vya miungu yake vimelala chini vikiwa vimevunjwa!’”
10 O my threshing, and the corne of my floore. That which I haue heard of the Lord of hostes, the God of Israel, haue I shewed vnto you.
Ee watu wangu, mliopondwa kwenye sakafu ya kupuria, ninawaambia kile nilichokisikia kutoka kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote, kutoka kwa Mungu wa Israeli.
11 The burden of Dumah. He calleth vnto me out of Seir, Watchman, what was in ye night? Watchman, what was in the night?
Neno kuhusu Duma: Mtu fulani ananiita kutoka Seiri, “Mlinzi, usiku utaisha lini? Mlinzi, usiku utaisha lini?”
12 The watchman saide, The morning commeth, and also the night. If yee will aske, enquire: returne and come.
Mlinzi anajibu, “Asubuhi inakuja, lakini pia usiku. Kama ungeliuliza, basi uliza; bado na urudi tena.”
13 The burden against Arabia. In the forest of Arabia shall yee tarie all night, euen in the waies of Dedanim.
Neno kuhusu Arabia: Enyi misafara ya Wadedani, mnaopiga kambi katika vichaka vya Arabia,
14 O inhabitants of the lande of Tema, bring foorth water to meete the thirstie, and preuent him that fleeth with his bread.
leteni maji kwa wenye kiu, ninyi mnaoishi Tema, leteni chakula kwa ajili ya wakimbizi.
15 For they flee from the drawen swords, euen from the drawen sword, and from the bent bowe, and from the grieuousnesse of warre.
Wanaukimbia upanga, kutoka upanga uliochomolewa alani, kutoka upinde uliopindwa, na kutoka kwenye joto la vita.
16 For thus hath the Lord sayd vnto me, Yet a yeere according to the yeeres of an hireling, and all the glorie of Kedar shall faile.
Hili ndilo Bwana analoniambia: “Katika muda wa mwaka mmoja, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, majivuno yote ya Kedari yatafikia mwisho.
17 And the residue of the nomber of ye strong archers of the sonnes of Kedar shall be fewe: for the Lord God of Israel hath spoken it.
Wanaume wavutao pinde walionusurika, mashujaa wa Kedari, watakuwa wachache.” Bwana, Mungu wa Israeli, amesema.

< Isaiah 21 >