< Isaiah 17 >

1 The burden of Damascus. Beholde, Damascus is taken away from being a citie, for it shall be a ruinous heape.
Neno kuhusu Dameski: “Tazama, Dameski haitakuwa tena mji bali itakuwa lundo la magofu.
2 The cities of Aroer shall be forsaken: they shall be for the flockes: for they shall lye there, and none shall make them afraide.
Miji ya Aroeri itaachwa na itaachiwa mifugo ambayo italala huko, bila yeyote wa kuyaogopesha.
3 The munition also shall cease from Ephraim, and the kingdome from Damascus, and the remnant of Aram shall be as the glory of the children of Israel, sayeth the Lord of hostes.
Mji wenye ngome utatoweka kutoka Efraimu, nao uweza wa ufalme kutoka Dameski; mabaki ya Aramu yatakuwa kama utukufu wa Waisraeli,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
4 And in that day the glorie of Iaakob shall be impouerished, and the fatnes of his flesh shalbe made leane.
“Katika siku ile utukufu wa Yakobo utafifia, unono wa mwili wake utadhoofika.
5 And it shalbe as when the haruest man gathereth the corne, and reapeth the eares with his arme, and he shall be as he that gathereth the eares in the valley of Rephaim.
Itakuwa kama mvunaji akusanyavyo nafaka na kuvuna nafaka kwa mikono yake, kama wakati mtu aokotapo masazo ya masuke katika Bonde la Warefai.
6 Yet a gathering of grapes shall be left in it, as the shaking of an oliue tree, two or three beries are in the top of the vpmost boughes, and foure or fiue in the hie branches of the fruite thereof, sayeth the Lord God of Israel.
Hata hivyo baadhi ya masazo yatabaki, kama vile mti wa mzeituni unavyopigwa, kukiachwa zeituni mbili au tatu juu ya matawi kileleni, nne au tano katika matawi yazaayo sana,” asema Bwana, Mungu wa Israeli.
7 At that day shall a man looke to his maker, and his eyes shall looke to the holy one of Israel.
Katika siku ile watu watamwangalia Muumba wao, na kuelekeza macho yao kwa yule Aliye Mtakatifu wa Israeli.
8 And hee shall not looke to the altars, the workes of his owne hands, neither shall he looke to those thinges, which his owne fingers haue made, as groues and images.
Hawataziangalia tena madhabahu, kazi za mikono yao, nao hawataheshimu nguzo za Ashera, na madhabahu za kufukizia uvumba zilizofanywa kwa mikono yao.
9 In that day shall the cities of their strength be as the forsaking of boughes and branches, which they did forsake, because of the children of Israel, and there shall be desolation.
Katika siku ile miji yao iliyo imara, ambayo waliihama kwa sababu ya Waisraeli, itakuwa kama mahali palipoachwa pa vichaka na magugu. Nayo yote itakuwa ukiwa.
10 Because thou hast forgotten the God of thy saluation, and hast not remembred the God of thy strength, therefore shalt thou set pleasant plantes, and shalt graffe strange vine branches:
Mmemsahau Mungu Mwokozi wenu, hamkumkumbuka Mwamba aliye ngome yenu. Kwa hiyo, hata ingawa mlipandikiza mimea iliyo mizuri sana na kuotesha mizabibu ya kigeni,
11 In the day shalt thou make thy plant to growe, and in the morning shalt thou make thy seede to florish: but the haruest shall be gone in the day of possession, and there shalbe desperate sorrowe.
hata kama siku ile unapoipandikiza, unaifanya iote na asubuhi ile ile unayoipanda, unaifanya ichipue, hata hivyo mavuno yatakuwa kama si kitu katika siku ile ya ugonjwa na maumivu yasiyoponyeka.
12 Ah, the multitude of many people, they shall make a sounde like the noyse of the sea: for the noyse of the people shall make a sounde like the noyse of mightie waters.
Lo! Ghadhabu ya mataifa mengi, wanaghadhibika kama bahari iliyochafuka! Lo! Makelele ya mataifa wanavuma kama ngurumo za maji mengi!
13 The people shall make a sounde like the noise of many waters: but God shall rebuke them, and they shall flee farre off, and shalbe chased as the chaffe of the mountaines before the winde, and as a rolling thing before the whirlewinde.
Ingawa mataifa yanavuma kama ngurumo za maji yanayofanya mawimbi, wakati anapoyakemea yanakimbia mbali, yanafukuzwa mbele ya upepo kama makapi juu ya milima, kama jani livingirishwapo na dhoruba.
14 And loe, in the euening there is trouble: but afore the morning it is gone. This is the portion of them that spoyle vs, and the lot of them that robbe vs.
Wakati wa jioni, hofu ya ghafula! Kabla ya asubuhi, wametoweka! Hili ndilo fungu la wale wanaotupora, fungu la wale wanaotunyangʼanya mali zetu.

< Isaiah 17 >