< Hosea 9 >
1 Rejoice not, O Israel for ioy as other people: for thou hast gone a whoring from thy God: thou hast loued a rewarde vpon euery corne floore.
Usifurahi, Israeli, kwa furaha kama watu wengine. Kwa maana haukuwa mwaminifu, umemuacha Mungu wako. Unapenda kulipa mshahara kwa kahaba kwenye sakafu zote za nafaka.
2 The floore, and the wine presse shall not feede them, and the newe wine shall faile in her.
Lakini sakafu na divai hazitawalisha; divai mpya itampungukia.
3 They wil not dwel in the Lordes lande, but Ephraim will returne to Egypt, and they will eate vncleane things in Asshur.
Hawawezi kuendelea kuishi katika nchi ya Bwana; badala yake, Efraimu atarudi Misri, na siku moja watakula chakula kichafu katika Ashuru.
4 They shall not offer wine to the Lord, neither shall their sacrifices be pleasant vnto him: but they shall be vnto them as the bread of mourners: al that eate thereof, shalbe polluted: for their bread for their soules shall not come into the house of the Lord.
Hawatamtolea Bwana sadaka za divai, wala hawatamfurahisha. Dhabihu zao zitakuwa kwao kama chakula cha matanga wote wanaolila watakuwa wamejisikia. Maana chakula chao kitakuwa chao pekee; hautakuingia nyumbani mwa Bwana.
5 What wil ye do then in the solemne day, and in the day of the feast of the Lord?
Utafanya nini siku ya sikukuu iliyowekwa rasmi, siku ya sikukuu ya Yahweh?
6 For loe, they are gone from destruction: but Egypt shall gather them vp, and Memphis shall burie them: the nettle shall possesse the pleasant places of their siluer, and the thorne shall be in their tabernacles.
Kwa maana, angalia, wamekimbia uharibifu, Misri itawakusanya, na Nofu itawazika. Maana hazina zao za pesa za fedha zitakuwa nao, na miiba itajaza hema zao.
7 The daies of visitation are come: the daies of recompence are come: Israel shall knowe it: the Prophet is a foole: the spiritual man is mad, for the multitude of thine iniquitie: therefore the hatred is great.
Siku za adhabu zinakuja; siku za kulipiza kisasi zinakuja. Waisraeli wote wajue mambo haya. Nabii ni mpumbavu, na mtu aliyevuviwa ni mwendawazimu, kwa sababu ya uovu wako mkubwa na uadui mkubwa.
8 The watchman of Ephraim shoulde bee with my God: but the Prophet is the snare of a fouler in all his waies, and hatred in the House of his God.
Nabii ndiye mlinzi wa Mungu wangu juu ya Efraimu. Lakini mtego wa ndege ni juu ya njia zake zote, na uadui umo katika nyumba ya Mungu wake.
9 They are deepely set: they are corrupt as in the daies of Gibeah: therefore he will remember their iniquitie, he will visite their sinnes.
Wamejiharibu wenyewe kama siku za Gibea. Mungu atawakumbusha uovu wao, naye atawaadhibu dhambi zao.
10 I found Israel like grapes in the wildernes: I saw your fathers as the first ripe in the figge tree at her first time: but they went to Baal-Peor, and separated themselues vnto that shame, and their abominations were according to their louers.
Bwana asema, “Nilipoikuta Israeli, ilikuwa kama kutafuta zabibu jangwani. Kama matunda ya kwanza ya msimu kwenye mtini, nimewaona baba zenu. Lakini wakaenda Baal Peori, nao wakajitoa kwenye sanamu ya aibu. Walikuwa chukizo kama sanamu waliyoipenda.
11 Ephraim their glorie shall flee away like a birde: from the birth and from the wombe, and from the conception.
Na kwa ajili ya Efraimu, utukufu wao utatoka kama ndege. Hakutakuwa na kuzaa, hakuna mimba, wala achukuaye mimba.
12 Though they bring vp their children, yet I will depriue them from being men: yea, woe to them, when I depart from them.
Ingawa wameleta watoto, nitawachukua ili asibaki hata mmoja. Ole wao nikiwaacha!
13 Ephraim, as I sawe, is as a tree in Tyrus planted in a cottage: but Ephraim shall bring forth his children to the murtherer.
Nimeiona Efraimu, kama vile Tiro, alipandwa katika mlima, lakini Efraimu atatoa watoto wake kwa mtu atakayewaua.
14 O Lord, giue them: what wilt thou giue them? giue them a baren wombe and drie breasts.
Wape, Bwana-utawapa nini? Wape tumbo lenye kuharibu mimba na matiti ambayo haitoi maziwa.
15 All their wickednesse is in Gilgal: for there doe I hate them: for the wickednesse of their inuentions, I will cast them out of mine House: I will loue them no more: all their princes are rebels.
'Kwa sababu ya uovu wao wote huko Gilgali, ndivyo nilipowachukia. Kwa sababu ya matendo yao ya dhambi, nitawafukuza nje ya nyumba yangu. Sitawapenda tena; maofisa wao wote ni waasi.
16 Ephraim is smitten, their roote is dried vp: they can bring no fruite: yea, though they bring foorth, yet will I slaie euen the dearest of their bodie.
Efraimu ni mgonjwa, na mizizi yao imekauka; hawazai matunda. Hata ikiwa wana watoto, nitawaua watoto wao wapendwa.
17 My God will cast them away, because they did not obey him: and they shall wander among the nations.
Mungu wangu atawakataa kwa sababu hawakumtii. Watakuwa watu wa kutangatanga kati ya mataifa.