< Hebrews 6 >

1 Therefore, leauing the doctrine of the beginning of Christ, let vs be led forward vnto perfection, not laying againe ye foundation of repetance from dead workes, and of faith toward God,
Kwa hiyo, tukiacha tulichojifunza kwanza kuhusu ujumbe wa Kristo, twapaswa kuwa na juhudi kuelekea kwenye ukomavu, tusiweke tena misingi ya toba kutoka katika kazi zisizo na uhai na imani katika Mungu,
2 Of the doctrine of baptismes, and laying on of hands, and of the resurrection from the dead, and of eternall iudgement. (aiōnios g166)
wala misingi ya mafundisho ya ubatizo, na kuwawekea mikono, ufufuo wa wafu, na hukumu ya milele. (aiōnios g166)
3 And this will we doe if God permit.
Na tutafanya hivi ikiwa Mungu ataruhusu.
4 For it is impossible that they which were once lightened, and haue tasted of the heauenly gift, and were made partakers of the holy Ghost,
Kwa kuwa haiwezekani kwa wale ambao waliipata nuru awali, ambao walionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa kuwa washirika wa Roho Mtakatifu,
5 And haue tasted of the good word of God, and of the powers of the world to come, (aiōn g165)
na ambao walionja uzuri wa neno la Mungu na kwa nguvu za wakati ujao, (aiōn g165)
6 If they fal away, should be renued againe by repentance: seeing they crucifie againe to themselues the Sonne of God, and make a mocke of him.
na kisha wakaanguka - haiwezekani kuwarejesha tena katika toba. Hii ni kwa sababu wamemsulubisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, wakimfanya kuwa chombo cha dhihaka hadharani.
7 For the earth which drinketh in the raine that commeth oft vpon it, and bringeth foorth herbes meete for them by whome it is dressed, receiueth blessing of God.
Kwa kuwa ardhi iliyopokea mvua inyeshayo mara kwa mara juu yake, na ikatoa mazao muhimu kwa hao waliofanya kazi katika ardhi, hupokea baraka kutoka kwa Mungu.
8 But that which beareth thornes and briars, is reproued, and is neere vnto cursing, whose end is to be burned.
Lakini ikiwa huzaa miiba na magugu, haina tena thamani na ipo katika hatari ya kulaaniwa. Mwisho wake ni kuteketezwa.
9 But beloued, we haue perswaded our selues better things of you, and such as accompany saluation, though we thus speake.
Ijapokuwa tunazungumza hivi, rafiki wapenzi, tunashawishiwa na mambo mazuri yawahusuyo ninyi na mambo yahusuyo wokovu.
10 For God is not vnrighteous, that hee should forget your worke, and labour of loue, which ye shewed toward his Name, in that ye haue ministred vnto the Saints, and yet minister.
Kwa kuwa Mungu si dhalimu hata asahau kazi yenu na kwa upendo mliouonesha kwa ajili ya jina lake, katika hili mliwatumikia waamini na bado mngali mnawatumikia.
11 And we desire that euery one of you shew the same diligence, to the full assurance of hope vnto the ende,
Na tunatamani sana kwamba kila mmoja wenu aweze kuonesha bidii ile ile mpaka mwisho kwa uhakika wa ujasiri.
12 That ye be not slouthfull, but followers of them, which through faith and patience, inherite the promises.
Hatutaki muwe wavivu, lakini muwe wafuasi wa wale warithio ahadi kwa sababu ya imani na uvumilivu.
13 For when God made the promise to Abraham, because he had no greater to sweare by, he sware by himselfe,
Kwa maana Mungu alipompa Abrahamu ahadi, aliapa kwa nafsi yake, kwa kuwa asingeliapa kwa mwingine yeyote aliye mkubwa kuliko yeye.
14 Saying, Surely I wil aboundantly blesse thee and multiplie thee marueilously.
Alisema, “Hakika nitakubariki, na nitauongeza uzao wako zaidi.”
15 And so after that he had taried patiently, he enioyed the promise.
Kwa njia hii, Abrahamu alipokea kile alichoahidiwa baada ya kusubiria kwa uvumilivu.
16 For men verely sweare by him that is greater then themselues, and an othe for confirmation is among them an ende of all strife.
Maana wanadamu huapa kwa yeye aliye mkuu kuliko wao, na kwao ukomo wa mashindano yote ni kiapo kwa kuyathibitisha.
17 So God, willing more aboundantly to shew vnto the heires of promise the stablenes of his counsell, bound himselfe by an othe,
Wakati Mungu alipoamua kuonesha kwa uwazi zaidi kwa warithi wa ahadi kusudi lake zuri lisilobadilika, alilithibitisha kwa kiapo.
18 That by two immutable things, wherein it is vnpossible that God should lye, we might haue strong consolation, which haue our refuge to lay holde vpon that hope that is set before vs,
Alifanya hivyo ili kwa vitu viwili visivyoweza kubadilika, ambavyo katika hivyo Mungu hawezi kusema uongo, sisi tulioikimbilia hifadhi tupate kutiwa moyo kushikilia kwa nguvu tumaini lililowekwa mbele yetu.
19 Which hope we haue, as an ancre of the soule, both sure and stedfast, and it entreth into that which is within the vaile,
Tunao ujasiri huu kama nanga imara na ya kutegemea ya roho zetu, ujasiri ambao unaingia sehemu ya ndani nyuma ya pazia.
20 Whither the forerunner is for vs entred in, euen Iesus that is made an hie Priest for euer after the order of Melchi-sedec. (aiōn g165)
Yesu aliingia sehemu ile kama mtangulizi wetu, akisha kufanyika kuhani mkuu hata milele baada ya utaratibu wa Melkizedeki. (aiōn g165)

< Hebrews 6 >