< Hebrews 4 >
1 Let vs feare therefore, least at any time by forsaking the promise of entring into his rest, any of you should seeme to be depriued.
Kwa hiyo, tunapaswa kuwa makini ili kwamba kati yenu asiwepo hata mmoja atakayeonekana kushindwa kufikia ahadi endelevu ya kuingia katika pumzika la Mungu.
2 For vnto vs was the Gospel preached as also vnto them: but the worde that they heard, profited not them, because it was not mixed with faith in those that heard it.
Kwani tumekuwa na habari njema kuhusu pumziko la Mungu lililotangazwa kwetu kama Waisrael walivyokuwa nayo, lakini ujumbe huo haukuwasaidia wale ambao waliusikia bila kuunganisha imani kwa hilo.
3 For we which haue beleeued, doe enter into rest, as he said to the other, As I haue sworne in my wrath, If they shall enter into my rest: although the workes were finished from the foundation of the world.
Kwa sisi, ambao tumekwisha amini-sisi ndio miongoni tutakaoingia katika lile pumuziko, Kama inavyosema, “Kama nilivyoapa kwa hasira yangu, Hawataingia katika pumziko mwangu.” Alisema hili, ingawa kazi zote alizotengeneza zilikuwa zimekamilika tangu mwanzo wa ulimwengu.
4 For he spake in a certaine place of the seuenth day on this wise, And God did rest the seuenth day from all his workes.
Kwani ameshasema sehemu fulani kuhusu siku ya saba, “Mungu alipumzika siku ya saba katika yote aliyoyafanya.”
5 And in this place againe, If they shall enter into my rest.
Tena ameshasema, “Hawataingia kwenye pumziko langu.”
6 Seeing therefore it remaineth that some must enter thereinto, and they to whom it was first preached, entred not therein for vnbeliefes sake:
Kwa sababu hiyo, tangu pumziko la Mungu bado ni akiba kwa ajili ya baadhi kuingia, na tangu Waisraeli wengi ambao walisikia habari njema kuhusu pumziko lake hawakuingia kwa sababu ya kutotii,
7 Againe he appointed in Dauid a certaine day, by To day, after so long a time, saying, as it is sayd, This day, if ye heare his voyce, harden not your hearts.
Mungu aliweka tena siku fulani, iitwayo “Leo.” Yeye aliiongeza siku hii alipozungumza kupitia Daudi, ambaye alisema kwa muda mrefu baada ya yaliyosemwa kwanza, “Leo kama mtasikia sauti yake, msifanye mioyo yenu kuwa migumu.”
8 For if Iesus had giuen them rest, then would he not after this haue spoke of an other day.
Kwani kama Yoshua aliwapatia pumziko, Mungu asingelisema juu ya siku nyingine.
9 There remaineth therefore a rest to the people of God.
Kwa hiyo bado kuna Sabato ya pumziko iliyotunzwa kwa ajili ya watu wa Mungu.
10 For he that is entred into his rest, hath also ceased from his owne works, as God did from his.
Kwani anayeingia katika pumziko la Mungu yeye mwenyewe pia amepumzika kutokana na matendo yake, kama Mungu alivyofanya katika yeye.
11 Let vs studie therefore to enter into that rest, lest any man fall after the same ensample of disobedience.
Kwa hiyo tuweni na shauku ya kuingia katika lile pumziko, ili kwamba asiwepo atakayeanguka katika aina ya uasi waliofanya.
12 For the worde of God is liuely, and mightie in operation, and sharper then any two edged sword, and entreth through, euen vnto the diuiding asunder of the soule and the spirit, and of the ioints, and the marow, and is a discerner of the thoughtes, and the intents of the heart.
Kwa maana neno la Mungu li hai na lina nguvu na linaukali kuliko upanga wowote wenye makali kuwili. Na huchoma hata kufikia kugawanya nafsi na roho, na viungo kutika uboho. Na lenye kuweza kufahamu fikira za moyo nia yake.
13 Neither is there any creature, which is not manifest in his sight: but all things are naked and open vnto his eyes, with whome we haue to doe.
. Hakuna kilichoumbwa kilichojificha katika uso wa Mungu. Badala yake, kila kitu ni dhahiri na wazi kwa macho ya mmoja ambaye ni lazima tutoe hesabu.
14 Seeing then that wee haue a great hie Priest, which is entred into heauen, euen Iesus the Sonne of God, let vs holde fast our profession.
Baadaye kuwa na kuhani mkuu aliyeingia katika mbingu, Yesu Mwana wa Mungu, kwa uimara tushikilie imani zetu.
15 For we haue not an hie Priest, which can not be touched with the feeling of our infirmities, but was in all things tempted in like sort, yet without sinne.
Kwa kuwa hatuna kuhani mkuu ambaye hawezi kuhisi huruma kwa ajili udhaifu wetu, lakini yeye ambaye kwa njia zote amekuwa akijaribiwa kama sisi, isipokuwa yeye ambaye hana dhambi.
16 Let vs therefore goe boldly vnto ye throne of grace, that we may receiue mercy, and finde grace to helpe in time of neede.
Na tuje kwa ujasiri katika kiti cha enzi cha neema, ili kwamba tupokee rehema na kupata neema ya kutusaidia wakati wa hitaji.