< Hebrews 2 >

1 Wherefore wee ought diligently to giue heede to the thinges which wee haue heard, lest at any time we runne out.
Kwa hiyo, imetupasa kuwa waangalifu sana kuhusu kile tulichosikia, ili tusije tukakiacha.
2 For if the worde spoken by Angels was stedfast, and euery transgression, and disobedience receiued a iust recompence of reward,
Kwa kuwa kama ujumbe ulionenwa na malaika ulikuwa imara, na kila uasi na kutokutii kulipata adhabu ya haki,
3 How shall we escape, if we neglect so great saluation, which at the first began to be preached by the Lord, and afterward was confirmed vnto vs by them that heard him,
je, sisi tutapaje kupona kama tusipojali wokovu mkuu namna hii? Wokovu huu, ambao mwanzo ulitangazwa na Bwana, ulithibitishwa kwetu na wale waliomsikia.
4 God bearing witnes thereto, both with signes and wonders, and with diuers miracles, and gifts of the holy Ghost, according to his owne will?
Pia Mungu aliushuhudia kwa ishara, maajabu na kwa miujiza mbalimbali, na karama za Roho Mtakatifu alizozigawa kulingana na mapenzi yake.
5 For he hath not put in subiection vnto the Angels the world to come, whereof we speake.
Mungu hakuuweka ulimwengu ujao ambao tunanena habari zake chini ya malaika.
6 But one in a certaine place witnessed, saying, What is man, that thou shouldest bee mindefull of him? or the sonne of man, that thou wouldest consider him?
Lakini kuna mahali mtu fulani ameshuhudia akisema: “Mwanadamu ni kitu gani hata unamfikiria, binadamu ni nani hata unamjali?
7 Thou madest him a litle inferiour to ye Angels: thou crownedst him with glory and honour, and hast set him aboue the workes of thine hands.
Umemfanya chini kidogo kuliko malaika; ukamvika taji ya utukufu na heshima,
8 Thou hast put all things in subiection vnder his feete. And in that he hath put all things in subiection vnder him, he left nothing that should not be subiect vnto him. But we yet see not all things subdued vnto him,
nawe umeweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Kwa kuweka vitu vyote chini yake, Mungu hakuacha kitu chochote ambacho hakukiweka chini ya mwanadamu. Lakini kwa sasa, hatuoni kwamba kila kitu kiko chini yake.
9 But we see Iesus crowned with glory and honour, which was made litle inferiour to the Angels, through the suffering of death, that by Gods grace he might taste death for all men.
Lakini twamwona Yesu, aliyefanywa chini kidogo kuliko malaika, sasa akiwa amevikwa taji ya utukufu na heshima kwa sababu alistahimili mauti, ili kwamba kwa neema ya Mungu apate kuonja mauti kwa ajili ya kila mtu.
10 For it became him, for whome are all these thinges, and by whome are all these things, seeing that hee brought many children vnto glory, that he should consecrate the Prince of their saluation through afflictions.
Ili kuwaleta wana wengi katika utukufu, ilifaa kwamba Mungu, ambaye ni kwa ajili yake na kupitia kwake kila kitu kimekuwepo, amkamilishe mwanzilishi wa wokovu wao kwa njia ya mateso.
11 For he that sanctifieth, and they which are sanctified, are all of one: wherefore he is not ashamed to call them brethren,
Yeye awafanyaye watu kuwa watakatifu, pamoja na hao ambao hufanywa watakatifu, wote hutoka katika jamaa moja. Hivyo Yesu haoni aibu kuwaita ndugu zake.
12 Saying, I will declare thy Name vnto my brethren: in the middes of the Church will I sing praises to thee.
Yeye husema, “Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; mbele ya kusanyiko nitaimba sifa zako.”
13 And againe, I will put my trust in him. And againe, Beholde, here am I, and the children which God hath giuen me.
Tena, “Nitaweka tumaini langu kwake.” Tena anasema, “Niko hapa, pamoja na watoto ambao Mungu amenipa.”
14 Forasmuch then as the children are partakers of flesh and blood, he also himselfe likewise tooke part with them, that hee might destroye through death, him that had the power of death, that is the deuil,
Basi kwa kuwa watoto wana nyama na damu, yeye pia alishiriki katika ubinadamu wao, ili kwa kifo chake, apate kumwangamiza huyo mwenye nguvu za mauti, yaani ibilisi,
15 And that he might deliuer all them, which for feare of death were all their life time subiect to bondage.
na kuwaweka huru wale waliokuwa utumwani maisha yao yote kwa sababu ya kuogopa mauti.
16 For he in no sort tooke on him the Angels nature, but hee tooke on him the seede of Abraham.
Kwa kuwa ni dhahiri kwamba hakuja kusaidia malaika, bali uzao wa Abrahamu.
17 Wherefore in all things it behoued him to be made like vnto his brethren, that hee might be mercifull, and a faithfull hie Priest in things concerning God, that he might make reconciliation for the sinnes of the people.
Kwa sababu hii ilibidi afanane na ndugu zake kwa kila hali, ili apate kuwa Kuhani Mkuu mwenye huruma na mwaminifu katika kumtumikia Mungu, ili pia apate kufanya upatanisho kwa ajili ya dhambi za watu.
18 For in that he suffered, and was tempted, he is able to succour them that are tempted.
Kwa kuwa yeye mwenyewe aliteswa alipojaribiwa, aweza kuwasaidia wale wanaojaribiwa.

< Hebrews 2 >