< Hebrews 11 >
1 Now faith is the grounds of things, which are hoped for, and the euidence of things which are not seene.
Kuwa na imani ni kuwa na hakika ya mambo tunayotumainia; kusadiki kabisa mambo tusiyoyaona.
2 For by it our elders were well reported of.
Maana wazee wa kale walipata kibali cha Mungu kwa sababu ya imani yao.
3 Through faith we vnderstand that the world was ordeined by the worde of God, so that the things which we see, are not made of things which did appeare. (aiōn )
Kwa imani sisi tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu; vitu vinavyoonekana kutoka vitu visivyoonekana. (aiōn )
4 By faith Abel offered vnto God a greater sacrifice then Cain, by the which he obtained witnes that he was righteous, God testifying of his gifts: by the which faith also he being dead, yet speaketh.
Kwa imani Abeli alimtolea Mungu dhabihu iliyokuwa bora zaidi kuliko ile ya Kaini. Kwa imani yake alikubaliwa na Mungu kuwa mwadilifu; Mungu mwenyewe alizikubali sadaka zake. Kwa imani yake ingawa amekufa, bado ananena.
5 By faith was Enoch translated, that he should not see death: neither was he found: for God had translated him: for before he was translated, he was reported of, that he had pleased God.
Kwa imani Henoki alichukuliwa na Mungu, asipate kufa. Hakuonekana tena kwa sababu Mungu alikuwa amemchukua. Maandiko yasema kwamba kabla ya kuchukuliwa kwake, yeye alikuwa amempendeza Mungu.
6 But without faith it is vnpossible to please him: for he that commeth to God, must beleeue that God is, and that he is a rewarder of them that seeke him.
Basi, pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu. Kwa maana kila mtu anayemwendea Mungu ni lazima aamini kwamba Mungu yuko, na kwamba huwatuza wale wanaomtafuta.
7 By faith Noe being warned of God of the things which were as yet not seene, mooued with reuerence, prepared the Arke to the sauing of his housholde, through the which Arke hee condemned the world, and was made heire of the righteousnes, which is by faith.
Kwa imani Noa alionywa na Mungu juu ya mambo ya baadaye ambayo hakuweza kuyaona bado. Alimtii Mungu, akajenga ile safina ambamo aliokolewa yeye pamoja na jamaa yake. Kutokana na hayo ulimwengu ulihukumiwa, naye Noa akapokea uadilifu unaotokana na imani.
8 By faith Abraham, when he was called, obeyed God, to goe out into a place, which hee should afterward receiue for inheritance, and he went out, not knowing whither he went.
Kwa imani Abrahamu alimtii Mungu alipoitwa aende katika nchi ambayo Mungu angempa iwe yake. Ingawa hakujua alikokuwa anakwenda, Abrahamu alihama.
9 By faith he abode in the land of promise, as in a strange countrey, as one that dwelt in tents with Isaac and Iacob heires with him of the same promise.
Kwa imani aliishi kama mgeni katika nchi aliyoahidiwa na Mungu. Aliishi huko katika hema kama walivyoishi Isaka na Yakobo, ambao pia walishiriki ahadi ileile.
10 For he looked for a citie hauing a foundation, whose builder and maker is God.
Maana Abrahamu alikuwa akingojea mji wenye misingi imara, mji ambao Mungu mwenyewe ndiye fundi aliyeubuni na kuujenga.
11 Through faith Sara also receiued strength to conceiue seede, and was deliuered of a childe when she was past age, because she iudged him faithfull which had promised.
Kwa imani hata Sara aliamini kwamba Mungu hutimiza ahadi zake, kwa hiyo akajaliwa kuchukua mimba ingawaje alikuwa amepita umri.
12 And therefore sprang there of one, euen of one which was dead, so many as the starres of the skie in multitude, and as the land of the sea shore which is innumerable.
Kwa hiyo, kutoka katika mtu huyo mmoja, Abrahamu, ambaye alikuwa kama amekufa, walitokea watu wengi wasiohesabika kama vile nyota za mbinguni na mchanga wa pwani.
13 All these died in faith, and receiued not the promises, but sawe them a farre off, and beleeued them, and receiued them thankefully, and confessed that they were strangers and pilgrims on the earth.
Watu hawa wote walikufa wakiwa na imani. Walikufa kabla ya kupokea mambo ambayo Mungu alikuwa ameahidi, lakini kwa mbali waliyaona, wakashangilia, na kukiri wazi kwamba wao walikuwa wageni na wakimbizi duniani.
14 For they that say such things, declare plainely, that they seeke a countrey.
Watu wanaosema mambo kama hayo, huonyesha wazi kwamba wanaitafuta nchi yao wenyewe.
15 And if they had bene mindfull of that countrey, from whence they came out, they had leasure to haue returned.
Kama wangalikuwa wanaifikiria nchi walikotoka zamani, wangalipata nafasi ya kurudi huko.
16 But nowe they desire a better, that is an heauenly: wherefore God is not ashamed of them to be called their God: for he hath prepared for them a citie.
Lakini sasa wanataka nchi iliyo bora zaidi, yaani nchi ya mbinguni. Ndiyo maana Mungu haoni haya wakimwita yeye Mungu wao, kwa sababu yeye mwenyewe amekwisha watayarishia mji.
17 By faith Abraham offered vp Isaac, when he was tryed, and he that had receiued the promises, offered his onely begotten sonne.
Kwa imani, Abrahamu alimtoa mwanae Isaka sadaka wakati Mungu alipomjaribu. Huyo Abrahamu ndiye aliyekuwa amepokea ahadi ya Mungu, lakini, hata hivyo, alikubali kumtoa dhabihu mwanae wa pekee,
18 (To whom it was said, In Isaac shall thy seede be called.)
ingawa Mungu alikuwa amemwambia: “Wazawa wako watatokana na Isaka.”
19 For he considered that God was able to raise him vp euen from the dead: from whence he receiued him also after a sort.
Abrahamu aliamini kwamba Mungu anaweza kuwafufua wafu: na kwa namna fulani kweli Abrahamu alimpata tena mwanae kutoka wafu.
20 By faith Isaac blessed Iacob and Esau, concerning things to come.
Kwa imani Isaka aliwabariki Yakobo na Esau, wapate baraka zitakazokuja baadaye.
21 By faith Iacob when he was a dying, blessed both the sonnes of Ioseph, and leaning on the ende of his staffe, worshipped God.
Kwa imani Yakobo alipokuwa karibu kufa, aliwabariki kila mmoja wa wana wa Yosefu, akamwabudu Mungu akiegemea ile fimbo yake.
22 By faith Ioseph when he died, made mention of the departing of the children of Israel, and gaue commandement of his bones.
Kwa imani Yosefu alipokuwa karibu kufa, alinena juu ya kutoka kwa Waisraeli katika nchi ya Misri, na pia akawaachia maagizo kuhusu mifupa yake.
23 By faith Moses when he was borne, was hid three moneths of his parents, because they sawe he was a proper childe, neither feared they the kings commandement.
Kwa imani wazazi wa Mose walimficha huyo mtoto kwa muda wa miezi mitatu baada ya kuzaliwa kwake. Walimwona kuwa ni mtoto mzuri, wala hawakuiogopa amri ya mfalme.
24 By faith Moses when he was come to age, refused to be called the sonne of Pharaohs daughter,
Kwa imani Mose alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mwana wa binti Farao.
25 And chose rather to suffer aduersitie with the people of God, then to enioy the pleasures of sinnes for a season,
Aliona ni afadhali kuteseka pamoja na watu wa Mungu kuliko kufurahia raha ya dhambi kwa kitambo kidogo.
26 Esteeming the rebuke of Christ greater riches then the treasures of Egypt: for he had respect vnto the recompence of the reward.
Alitambua kwamba kuteseka kwa ajili ya Masiha kuna faida kubwa zaidi kuliko utajiri wote wa nchi ya Misri, maana alikuwa anatazamia tuzo la baadaye.
27 By faith he forsooke Egypt, and feared not the fiercenes of the king: for he endured, as he that sawe him which is inuisible.
Kwa imani Mose alihama kutoka nchi ya Misri bila kuogopa hasira ya mfalme; na wala hakurudi nyuma, kwani alikuwa kama mtu aliyemwona yule Mungu asiyeonekana.
28 Through faith he ordeined the Passeouer and the effusion of blood, least he that destroyed the first borne, should touche them.
Kwa imani aliadhimisha siku ya Pasaka, akaamuru damu inyunyizwe juu ya milango, ili yule Malaika Mwangamizi asiwaue wazaliwa wa kwanza wa Israeli.
29 By faith they passed through the red sea as by drie land, which when the Egyptians had assayed to doe, they were swallowed vp.
Kwa imani watu wa Israeli walivuka bahari ya Shamu, kana kwamba ilikuwa nchi kavu; lakini Wamisri walipojaribu kufanya hivyo walikufa maji.
30 By faith the walles of Iericho fell downe after they were copassed about seue dayes.
Kwa imani kuta za mji wa Yeriko zilianguka watu wa Israeli walipokwisha zunguka kwa muda wa siku saba.
31 By faith the harlot Rahab perished not with them which obeyed not, when she had receiued the spies peaceably.
Kwa imani Rahabu aliyekuwa malaya hakuangamia pamoja na wale waliomwasi Mungu, kwa sababu aliwakaribisha wale wapelelezi.
32 And what shall I more say? for the time would be too short for me to tell of Gedeon, of Barac, and of Sampson, and of Iephte, also of Dauid, and Samuel, and of the Prophets:
Basi, niseme nini zaidi? Wakati hauniruhusu kueleza juu ya Gedeoni, Baraki, Samsoni, Yeftha, Daudi, Samweli na manabii.
33 Which through faith subdued kingdomes, wrought righteousnesse, obteined the promises, stopped the mouthes of lions,
Kwa imani hawa wote walipigana vita na wafalme, wakashinda. Walitenda mambo adili, wakapokea yale aliyoahidi Mungu. Walifunga vinywa vya simba,
34 Quenched the violence of fire, escaped the edge of the sworde, of weake were made strong, waxed valiant in battell, turned to flight the armies of the aliants.
Walizima mioto mikali, waliepuka kuuawa kwa upanga. Walikuwa dhaifu lakini walipata nguvu. Walikuwa hodari katika vita wakashinda majeshi ya kigeni.
35 The women receiued their dead raised to life: other also were racked, and woulde not be deliuered, that they might receiue a better resurrection.
Na, wanawake walioamini walirudishiwa wafu wao wakiwa wamefufuliwa. Baadhi yao walikataa kufunguliwa, wakateswa mpaka kufa ili wapate kufufuliwa na kuingia katika maisha bora zaidi.
36 And others haue bene tryed by mockings and scourgings, yea, moreouer by bondes and prisonment.
Wengine walidhihakiwa na kupigwa mijeledi, na wengine walifungwa minyororo na kutupwa gerezani.
37 They were stoned, they were hewen asunder, they were tempted, they were slaine with the sworde, they wandred vp and downe in sheepes skinnes, and in goates skinnes, being destitute, afflicted, and tormented:
Walipigwa mawe, walipasuliwa vipandevipande, waliuawa kwa upanga. Walizungukazunguka wakiwa wamevaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi, walikuwa watu maskini, walioteswa na kudhulumiwa.
38 Whom the world was not worthie of: they wandered in wildernesses and mountaines, and dennes, and caues of the earth.
Ulimwengu haukustahili kuwa na watu hao. Walitangatanga jangwani na mlimani, wakaishi katika mashimo na mapango ya ardhi.
39 And these all through faith obteined good report, and receiued not the promise,
Watu hawa wote walionekana kuwa mashujaa kwa sababu ya imani yao. Hata hivyo, hawakupokea yale ambayo Mungu aliwaahidia,
40 God prouiding a better thing for vs, that they without vs should not be made perfite.
maana Mungu alikuwa ameazimia mpango ulio bora zaidi kwa ajili yetu; yaani wao wangeufikia ukamilifu wakiwa pamoja nasi.