< Hebrews 11 >

1 Now faith is the grounds of things, which are hoped for, and the euidence of things which are not seene.
Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, na udhahiri wa mambo yasiyoonekana.
2 For by it our elders were well reported of.
Maana baba zetu wa kale walipongezwa kwa haya.
3 Through faith we vnderstand that the world was ordeined by the worde of God, so that the things which we see, are not made of things which did appeare. (aiōn g165)
Kwa imani tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, vitu vyote vinavyoonekana havikuumbwa kutoka kwa vitu vinavyoonekana. (aiōn g165)
4 By faith Abel offered vnto God a greater sacrifice then Cain, by the which he obtained witnes that he was righteous, God testifying of his gifts: by the which faith also he being dead, yet speaketh.
Kwa imani Abeli alimtolea Mungu dhabihu bora zaidi kuliko Kaini. Kwa imani alishuhudiwa kuwa mwenye haki, Mungu mwenyewe akazishuhudia sadaka zake. Kwa imani bado ananena ingawa amekufa.
5 By faith was Enoch translated, that he should not see death: neither was he found: for God had translated him: for before he was translated, he was reported of, that he had pleased God.
Kwa imani Enoki alitwaliwa kutoka maisha haya, kiasi kwamba hakuonja mauti. Hakuonekana, kwa sababu Mungu alikuwa amemchukua. Kwa kuwa kabla hajatwaliwa alikuwa ameshuhudiwa kuwa ni mtu aliyempendeza Mungu.
6 But without faith it is vnpossible to please him: for he that commeth to God, must beleeue that God is, and that he is a rewarder of them that seeke him.
Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu, kwa maana yeyote anayemjia Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko na ya kuwa huwapa thawabu wale wamtafutao kwa bidii.
7 By faith Noe being warned of God of the things which were as yet not seene, mooued with reuerence, prepared the Arke to the sauing of his housholde, through the which Arke hee condemned the world, and was made heire of the righteousnes, which is by faith.
Kwa imani, Noa alipoonywa na Mungu kuhusu mambo ambayo hayajaonekana bado, kwa kumcha Mungu alitengeneza safina ili kuokoa jamaa yake. Kwa imani yake aliuhukumu ulimwengu na akawa mrithi wa haki ipatikanayo kwa imani.
8 By faith Abraham, when he was called, obeyed God, to goe out into a place, which hee should afterward receiue for inheritance, and he went out, not knowing whither he went.
Kwa imani Abrahamu, alipoitwa aende mahali ambapo Mungu angempa baadaye kuwa urithi, alitii na akaenda, ingawa hakujua anakokwenda.
9 By faith he abode in the land of promise, as in a strange countrey, as one that dwelt in tents with Isaac and Iacob heires with him of the same promise.
Kwa imani alifanya maskani yake katika nchi ya ahadi kama mgeni katika nchi ya kigeni; aliishi katika mahema, kama Isaki na Yakobo walivyofanya, waliokuwa pia warithi pamoja naye wa ahadi ile ile.
10 For he looked for a citie hauing a foundation, whose builder and maker is God.
Kwa maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi ya kudumu ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu.
11 Through faith Sara also receiued strength to conceiue seede, and was deliuered of a childe when she was past age, because she iudged him faithfull which had promised.
Kwa imani Abrahamu, ingawa alikuwa mzee wa umri, naye Sara mwenyewe aliyekuwa tasa, alipokea uwezo wa kuwa baba kwa sababu alimhesabu Mungu aliyemwahidi kuwa mwaminifu na kwamba angetimiza ahadi yake.
12 And therefore sprang there of one, euen of one which was dead, so many as the starres of the skie in multitude, and as the land of the sea shore which is innumerable.
Hivyo kutokana na huyu huyu ambaye alikuwa sawa na mfu, wakazaliwa wazao wengi kama nyota za mbinguni na kama mchanga wa pwani usiohesabika.
13 All these died in faith, and receiued not the promises, but sawe them a farre off, and beleeued them, and receiued them thankefully, and confessed that they were strangers and pilgrims on the earth.
Watu hawa wote wakafa katika imani bila kuzipokea zile ahadi, lakini waliziona kwa mbali na kuzishangilia. Nao walikubali kwamba walikuwa wageni na wasiokuwa na maskani hapa duniani.
14 For they that say such things, declare plainely, that they seeke a countrey.
Watu wasemao mambo kama haya, wanaonyesha wazi kwamba wanatafuta nchi yao wenyewe.
15 And if they had bene mindfull of that countrey, from whence they came out, they had leasure to haue returned.
Kwa kweli kama wangekuwa wanafikiri kuhusu nchi waliyoiacha, wangalipata nafasi ya kurudi huko.
16 But nowe they desire a better, that is an heauenly: wherefore God is not ashamed of them to be called their God: for he hath prepared for them a citie.
Lakini badala yake walitamani nchi iliyo bora zaidi, yaani nchi ya mbinguni. Kwa hiyo Mungu haoni aibu kuitwa Mungu wao, kwa kuwa amekwisha kuandaa mji kwa ajili yao.
17 By faith Abraham offered vp Isaac, when he was tryed, and he that had receiued the promises, offered his onely begotten sonne.
Kwa imani Abrahamu, alipojaribiwa na Mungu, alimtoa Isaki kuwa dhabihu. Yeye aliyekuwa amezipokea ahadi za Mungu alikuwa tayari kumtoa mwanawe, aliyekuwa mwanawe pekee awe dhabihu.
18 (To whom it was said, In Isaac shall thy seede be called.)
Ingawa Mungu alikuwa amemwambia Abrahamu, “Uzao wako utahesabiwa kupitia kwa Isaki,”
19 For he considered that God was able to raise him vp euen from the dead: from whence he receiued him also after a sort.
Abrahamu alihesabu kuwa Mungu angaliweza kumfufua Isaki kutoka kwa wafu. Na kwa kusema kwa mfano, alimpata tena Isaki kutoka kwa wafu.
20 By faith Isaac blessed Iacob and Esau, concerning things to come.
Kwa imani Isaki alimbariki Yakobo na Esau kuhusu maisha yao ya baadaye.
21 By faith Iacob when he was a dying, blessed both the sonnes of Ioseph, and leaning on the ende of his staffe, worshipped God.
Kwa imani Yakobo alipokuwa anakufa, alimbariki kila mmoja wa mtoto wa Yosefu, akamwabudu Mungu akiwa ameegemea juu ya kichwa cha fimbo yake.
22 By faith Ioseph when he died, made mention of the departing of the children of Israel, and gaue commandement of his bones.
Kwa imani, Yosefu alipokaribia mwisho wa maisha yake, alinena habari za kutoka kwa wana wa Israeli huko Misri na akatoa maagizo kuhusu mifupa yake.
23 By faith Moses when he was borne, was hid three moneths of his parents, because they sawe he was a proper childe, neither feared they the kings commandement.
Kwa imani, wazazi wa Mose walimficha kwa miezi mitatu baada ya kuzaliwa, kwa sababu waliona kuwa si mtoto wa kawaida, wala hawakuiogopa amri ya mfalme.
24 By faith Moses when he was come to age, refused to be called the sonne of Pharaohs daughter,
Kwa imani, Mose alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mwana wa binti Farao.
25 And chose rather to suffer aduersitie with the people of God, then to enioy the pleasures of sinnes for a season,
Akachagua kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha kwa anasa za dhambi kwa kitambo kidogo tu.
26 Esteeming the rebuke of Christ greater riches then the treasures of Egypt: for he had respect vnto the recompence of the reward.
Aliona kushutumiwa kwa ajili ya Kristo ni utajiri mkubwa zaidi kuliko hazina za Misri, maana alikuwa anatazamia kupata thawabu baadaye.
27 By faith he forsooke Egypt, and feared not the fiercenes of the king: for he endured, as he that sawe him which is inuisible.
Kwa imani Mose aliondoka Misri bila kuogopa ghadhabu ya mfalme. Alivumilia kwa sababu alimwona yeye asiyeonekana kwa macho.
28 Through faith he ordeined the Passeouer and the effusion of blood, least he that destroyed the first borne, should touche them.
Kwa imani akaadhimisha Pasaka na kunyunyiza damu, ili yule mwenye kuwaangamiza wazaliwa wa kwanza asiwaguse wazaliwa wa Israeli.
29 By faith they passed through the red sea as by drie land, which when the Egyptians had assayed to doe, they were swallowed vp.
Kwa imani, watu walivuka Bahari ya Shamu kama vile juu ya nchi kavu; lakini Wamisri walipojaribu kufanya hivyo, walitoswa ndani ya maji.
30 By faith the walles of Iericho fell downe after they were copassed about seue dayes.
Kwa imani kuta za Yeriko zilianguka, baada ya watu kuzizunguka kwa siku saba.
31 By faith the harlot Rahab perished not with them which obeyed not, when she had receiued the spies peaceably.
Kwa imani, Rahabu, yule kahaba, hakuangamizwa pamoja na wale waliomwasi Mungu, kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi.
32 And what shall I more say? for the time would be too short for me to tell of Gedeon, of Barac, and of Sampson, and of Iephte, also of Dauid, and Samuel, and of the Prophets:
Basi niseme nini zaidi? Sina wakati wa kusema habari za Gideoni, Baraka, Samsoni, Yeftha, Daudi, Samweli na manabii,
33 Which through faith subdued kingdomes, wrought righteousnesse, obteined the promises, stopped the mouthes of lions,
ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitekeleza haki, na wakapokea ahadi za Mungu; walifunga vinywa vya simba,
34 Quenched the violence of fire, escaped the edge of the sworde, of weake were made strong, waxed valiant in battell, turned to flight the armies of the aliants.
wakazima makali ya miali ya moto, na wakaepuka kuuawa kwa upanga; udhaifu wao uligeuka kuwa nguvu; pia walikuwa hodari vitani na kuyafukuza majeshi ya wageni.
35 The women receiued their dead raised to life: other also were racked, and woulde not be deliuered, that they might receiue a better resurrection.
Wanawake walipokea watu wao waliokuwa wamekufa, wakafufuliwa. Lakini wengine waliteswa, nao wakakataa kufunguliwa, ili wapate ufufuo ulio bora zaidi.
36 And others haue bene tryed by mockings and scourgings, yea, moreouer by bondes and prisonment.
Wengine walidhihakiwa na kupigwa, hata walifungwa minyororo na kutiwa gerezani.
37 They were stoned, they were hewen asunder, they were tempted, they were slaine with the sworde, they wandred vp and downe in sheepes skinnes, and in goates skinnes, being destitute, afflicted, and tormented:
Walipigwa kwa mawe; walipasuliwa vipande viwili kwa msumeno; waliuawa kwa upanga. Walizungukazunguka wakiwa wamevaa ngozi za kondoo na mbuzi, wakiwa maskini, wakiteswa na kutendwa mabaya,
38 Whom the world was not worthie of: they wandered in wildernesses and mountaines, and dennes, and caues of the earth.
watu ambao ulimwengu haukustahili kuwa nao. Walizunguka majangwani na milimani, katika mapango na katika mahandaki ardhini.
39 And these all through faith obteined good report, and receiued not the promise,
Hawa wote walishuhudiwa vyema kwa sababu ya imani yao, lakini hakuna hata mmoja wao aliyepokea yale yaliyoahidiwa.
40 God prouiding a better thing for vs, that they without vs should not be made perfite.
Kwa kuwa Mungu alikuwa ametangulia kutuwekea kitu kilicho bora zaidi ili wao wasikamilishwe pasipo sisi.

< Hebrews 11 >