< Genesis 19 >

1 And in the euening there came two Angels to Sodom: and Lot sate at the gate of Sodom, and Lot sawe them, and rose vp to meete them, and he bowed himselfe with his face to the ground.
Malaika wale wawili wakafika Sodoma wakati wa jioni, naye Loti alikuwa ameketi kwenye lango la mji. Wakati alipowaona, aliondoka kwenda kuwalaki na kuwasujudia hadi chini.
2 And he saide, See my Lords, I pray you turne in nowe into your seruants house, and tarie all night, and wash your feete, and ye shall rise vp early and goe your wayes. Who saide, Nay, but we will abide in the streete all night.
Akasema, “Bwana zangu, tafadhali karibuni kwenye nyumba ya mtumishi wenu. Mnaweza kunawa miguu na kulala hapa kisha asubuhi na mapema mwendelee na safari yenu.” Wakamjibu, “La hasha, tutalala hapa nje uwanjani.”
3 Then he preassed vpon them earnestly, and they turned in to him, and came to his house, and he made them a feast, and did bake vnleauened bread, and they did eate.
Lakini akasisitiza kwa nguvu kwamba waingie pamoja naye nyumbani kwake. Akawaandalia chakula, mikate isiyotiwa chachu, nao wakala.
4 But before they went to bed, the men of the citie, euen the men of Sodom compassed the house rounde about from the yong euen to the olde, all the people from all quarters.
Kabla hawajaenda kulala, watu wote kutoka kila sehemu ya mji wa Sodoma, vijana kwa wazee, waliizunguka nyumba.
5 Who crying vnto Lot said to him, Where are the men, which came to thee this night? bring them out vnto vs that we may knowe them.
Wakamwita Loti wakisema, “Wako wapi wale watu ambao walikuja kwako jioni hii? Watoe nje kwetu ili tuweze kuwalawiti.”
6 Then Lot went out at the doore vnto them, and shut the doore after him,
Loti akatoka nje kuonana nao, akaufunga mlango nyuma yake,
7 And said, I pray you, my brethren, do not so wickedly.
akasema, “La hasha, rafiki zangu. Msifanye jambo hili ovu.
8 Beholde nowe, I haue two daughters, which haue not knowen man: them will I bring out now vnto you, and doe to them as seemeth you good: onely vnto these men doe nothing: for therefore are they come vnder the shadowe of my roofe.
Tazama, ninao binti wawili ambao kamwe hawajakutana kimwili na mwanaume. Acha niwatoe nje kwenu, nanyi mnaweza kuwafanyia lolote mnalotaka. Lakini msiwafanyie chochote watu hawa, kwa sababu wako kwenye ulinzi chini ya dari langu.”
9 Then they said, Away hence, and they said, He is come alone as a stranger, and shall he iudge and rule? we will nowe deale worse with thee then with them. So they preassed sore vpon Lot himselfe, and came to breake the doore.
Wakamjibu, “Tuondokee mbali.” Wakaendelea kusema, “Huyu mtu alikuja hapa kama mgeni na sasa anataka kuwa mwamuzi wetu! Tutakutenda vibaya kuliko wao.” Waliendelea kumlazimisha Loti na kusonga mbele ili kuvunja mlango.
10 But the men put forth their hand and pulled Lot into the house to them and shut to ye doore.
Lakini watu wale waliokuwa ndani wakanyoosha mkono wakamvuta Loti ndani ya nyumba na kufunga mlango.
11 Then they smote the men that were at the doore of the house with blindnes both small and great, so that they were wearie in seeking the doore.
Kisha wakawapiga kwa upofu wale watu waliokuwa mlangoni mwa ile nyumba, vijana kwa wazee, hivyo hawakuweza kuupata mlango.
12 Then the men said vnto Lot, Whom hast thou yet here? either sonne in lawe, or thy sonnes, or thy daughters, or whatsoeuer thou hast in the citie, bring it out of this place.
Wale watu wawili wakamwambia Loti, “Una mtu mwingine yeyote hapa, wakwe zako, wana au binti, ama yeyote mwingine aliye wako katika mji huu? Waondoe hapa,
13 For we will destroy this place, because the crye of them is great before the Lord, and the Lord hath sent vs to destroy it.
kwa sababu tunapaangamiza mahali hapa. Kilio kwa Bwana dhidi ya watu wa hapa ni kikubwa kiasi kwamba ametutuma kupaangamiza.”
14 Then Lot went out and spake vnto his sonnes in lawe, which maried his daughters, and said, Arise, get you out of this place: for the Lord will destroy the citie: but he seemed to his sonnes in lawe as though he had mocked.
Kwa hiyo Loti alitoka ili kuzungumza na wakwe zake, waliokuwa wamewaposa binti zake. Akawaambia, “Fanyeni haraka kuondoka mahali hapa, kwa kuwa Bwana yu karibu kuangamiza mji huu!” Lakini wakwe zake walifikiri kwamba alikuwa akitania.
15 And when the morning arose, the Angels hasted Lot, saying, Arise, take thy wife and thy two daughters which are here, lest thou be destroyed in the punishment of the citie.
Kunako mapambazuko, malaika wakamhimiza Loti, wakamwambia, “Fanya haraka! Mchukue mke wako na binti zako wawili walioko hapa, la sivyo utaangamizwa wakati mji utakapoadhibiwa.”
16 And as he prolonged the time, the men caught both him and his wife, and his two daughters by the hands (the Lord being mercifull vnto him) and they brought him foorth, and set him without the citie.
Alipositasita, wale watu wakamshika mkono wake na mikono ya mke wake na binti zake wawili na kuwaongoza salama nje ya mji, kwa kuwa Bwana alikuwa na huruma kwao.
17 And when they had brought them out, the Angel said, Escape for thy life: looke not behinde thee, neither tarie thou in all the plaine: escape into ye mountaine, least thou be destroyed.
Mara walipokwisha kuwatoa nje, mmoja wao akawaambia, “Mkimbie kwa usalama wenu! Msitazame nyuma, wala msisimame popote katika nchi tambarare! Kimbilieni milimani, ama sivyo mtaangamizwa!”
18 And Lot saide vnto them, Not so, I pray thee, my Lord.
Lakini Loti akawajibu, “La hasha, bwana zangu, tafadhalini!
19 Behold now, thy seruant hath found grace in thy sight, and thou hast magnified thy mercie, which thou hast shewed vnto me in sauing my life: and I cannot escape in the mountaine, least some euill take me, and I die.
Mtumishi wenu amepata kibali mbele ya macho yenu, nanyi mmeonyesha wema mkubwa kwangu kwa kuokoa maisha yangu. Lakini siwezi kukimbilia milimani, janga hili litanikumba, nami nitakufa.
20 See nowe this citie hereby to flee vnto, which is a litle one: Oh let me escape thither: is it not a litle one, and my soule shall liue?
Tazama, hapa kuna mji karibu wa kukimbilia, nao ni mdogo. Niruhusuni nikimbilie humo, ni mdogo sana, ama sivyo? Ndipo maisha yangu yatasalimika.”
21 Then he said vnto him, Beholde, I haue receiued thy request also concerning this thing, that I will not ouerthrow this citie, for the which thou hast spoken.
Akamwambia, “Vema sana, nitalikubali hili ombi pia, sitauangamiza mji ulioutaja.
22 Haste thee, saue thee there: for I can doe nothing till thou be come thither. Therefore the name of the citie was called Zoar.
Lakini ukimbilie huko haraka, kwa sababu sitaweza kufanya lolote mpaka ufike huko.” (Ndiyo maana mji huo ukaitwa Soari.)
23 The sunne did rise vpon the earth, when Lot entred into Zoar.
Wakati Loti alipofika Soari, jua lilikuwa limechomoza katika nchi.
24 Then the Lord rained vpon Sodom and vpon Gomorah brimstone, and fire from the Lord out of heauen,
Ndipo Bwana akanyesha moto wa kiberiti uliotoka mbinguni kwa Bwana juu ya Sodoma na Gomora.
25 And ouerthrewe those cities and all the plaine, and all the inhabitants of the cities; and that that grewe vpon the earth.
Hivyo akaiteketeza miji ile na eneo lote la tambarare, pamoja na wote waliokuwa wanaishi katika miji, hata pia mimea yote katika nchi.
26 Now his wife behind him looked backe, and she became a pillar of salt.
Lakini mke wa Loti akatazama nyuma, hivyo akawa nguzo ya chumvi.
27 And Abraham rising vp earely in ye morning went to the place, where he had stand before the Lord,
Asubuhi na mapema siku iliyofuata, Abrahamu akaamka na kurudi mahali pale aliposimama mbele za Bwana.
28 And looking towarde Sodom and Gomorah and toward all the land of the plaine, behold, he sawe the smoke of the lande mounting vp as the smoke of a fornace.
Akatazama upande wa Sodoma na Gomora, kuelekea nchi yote ya tambarare, akaona moshi mzito ukipanda kutoka kwenye nchi, kama moshi utokao kwenye tanuru.
29 But yet when God destroyed the cities of the plaine, God thought vpon Abraham, and sent Lot out from the middes of the destruction, when he ouerthrewe the cities, wherein Lot dwelled.
Kwa hiyo Mungu alipoiangamiza miji ya tambarare alimkumbuka Abrahamu, akamtoa Loti kutoka kwenye lile janga lililoharibu miji ile ambamo Loti alikuwa ameishi.
30 Then Lot went vp from Zoar, and dwelt in the mountaine with his two daughters: for he feared to tarie in Zoar, but dwelt in a caue, he, and his two daughters.
Loti na binti zake wawili waliondoka Soari na kufanya makao yao kule milimani, kwa maana aliogopa kukaa Soari. Yeye na binti zake wawili waliishi katika pango.
31 And the elder saide vnto the yonger, Our father is old, and there is not a man in the earth, to come in vnto vs after the maner of all ye earth.
Siku moja binti mkubwa akamwambia yule mdogo, “Baba yetu ni mzee na hakuna mwanaume mahali hapa atakayekutana na sisi kimwili, kama ilivyo desturi ya mahali pote duniani.
32 Come, wee will make our father drinke wine, and lie with him, that we may preserue seede of our father.
Tumnyweshe baba yetu mvinyo kisha tukutane naye kimwili ili tuhifadhi uzao wetu kupitia baba yetu.”
33 So they made their father drinke wine that night, and the elder went and lay with her father: but he perceiued not, neither whe she lay downe, neither when she rose vp.
Usiku ule walimnywesha baba yao mvinyo, alipolewa binti yake mkubwa akaingia na kukutana naye kimwili. Baba yao hakujua wakati binti yake alipoingia kulala naye wala alipotoka.
34 And on the morowe the elder saide to the yonger, Behold, yester night lay I with my father: let vs make him drinke wine this night also, and goe thou and lie with him, that we may preserue seede of our father.
Siku iliyofuata binti mkubwa akamwambia yule mdogo, “Usiku uliopita mimi nilikutana kimwili na baba yangu. Tumnyweshe divai tena, usiku huu nawe ukutane naye kimwili ili tuweze kuhifadhi uzao wetu kupitia baba yetu.”
35 So they made their father drinke wine that night also, and the yonger arose, and lay with him, but he perceiued not, when she lay downe, neither when she rose vp.
Kwa hiyo wakamnywesha baba yao mvinyo tena usiku ule, naye binti yake mdogo akaingia, akakutana naye kimwili. Kwa mara nyingine baba yao hakujua binti yake alipolala naye wala alipoondoka.
36 Thus were both the daughters of Lot with childe by their father.
Hivyo binti wawili wa Loti wakapata mimba kwa baba yao.
37 And the elder bare a sonne, and she called his name Moab: the same is the father of the Moabites vnto this day.
Binti mkubwa akamzaa mwana, akamwita jina lake Moabu; ndio baba wa Wamoabu hata leo.
38 And the yonger bare a sonne also, and she called his name Ben-ammi: the same is the father of the Ammonites vnto this day.
Binti mdogo naye pia akamzaa mwana, naye akamwita Benami; ndiye baba wa Waamoni hata leo.

< Genesis 19 >