< Galatians 3 >
1 O foolish Galatians, who hath bewitched you, that ye should not obey the trueth, to whome Iesus Christ before was described in your sight, and among you crucified?
Ninyi Wagalatia wajinga! Ni nani aliyewaroga? Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele yenu kwamba amesulubiwa.
2 This only would I learne of you, Receiued ye the Spirit by the workes of the Lawe, or by the hearing of faith preached?
Nataka nijifunze neno moja kutoka kwenu: Je, mlipokea Roho wa Mungu kwa kushika sheria, au kwa kuyaamini yale mliyosikia?
3 Are ye so foolish, that after ye haue begun in the Spirit, ye would now be made perfect by the flesh?
Je, ninyi ni wajinga kiasi hicho? Baada ya kuanza kwa Roho, je, sasa mwataka kumalizia katika mwili?
4 Haue ye suffered so many things in vaine? if so be it be euen in vaine.
Je, mlipata mateso kiasi hicho bure? Ni kama kweli yalikuwa bure!
5 He therefore that ministreth to you the Spirit, and worketh miracles among you, doeth he it through the workes of the Law, or by the hearing of faith preached?
Je, Mungu huwapa Roho wake na kufanya miujiza katikati yenu kwa sababu mnatii sheria, au kwa sababu mnaamini kile mlichosikia?
6 Yea rather as Abraham beleeued God, and it was imputed to him for righteousnes.
Kama vile “Abrahamu alimwamini Mungu na ikahesabiwa kwake kuwa haki.”
7 Knowe ye therefore, that they which are of faith, the same are the children of Abraham.
Fahamuni basi kwamba wale walio na imani, hao ndio watoto wa Abrahamu.
8 For the Scripture foreseeing, that God would iustifie the Gentiles through faith, preached before the Gospel vnto Abraham, saying, In thee shall all the Gentiles be blessed.
Maandiko yakitabiri kwamba Mungu angewahesabia haki watu wa Mataifa kwa imani, alitangulia kumtangazia Abrahamu Injili akisema kwamba, “Kwa kupitia kwako mataifa yote yatabarikiwa.”
9 So then they which be of faith, are blessed with faithfull Abraham.
Kwa sababu hii, wale wote wanaoamini wanabarikiwa pamoja na Abrahamu, mtu wa imani.
10 For as many as are of the workes of the Lawe, are vnder the curse: for it is written, Cursed is euery man that continueth not in all things, which are written in the booke of the Law, to doe them.
Kwa maana wote wanaotumainia matendo ya sheria wako chini ya laana, kwa kuwa imeandikwa, “Alaaniwe kila mtu asiyeshikilia kutii mambo yote yaliyoandikwa katika Kitabu cha Sheria.”
11 And that no man is iustified by the Law in the sight of God, it is euident: for the iust shall liue by faith.
Basi ni dhahiri kwamba hakuna mtu anayehesabiwa haki mbele za Mungu kwa kushikilia sheria, kwa maana, “Mwenye haki ataishi kwa imani.”
12 And the Lawe is not of faith: but the man that shall doe those things, shall liue in them.
Lakini sheria haitegemei imani. Kinyume chake, “Mtu atendaye matendo hayo ataishi kwa hayo.”
13 Christ hath redeemed vs from the curse of the Lawe, made a curse for vs, (for it is written, Cursed is euery one that hangeth on tree)
Kristo alitukomboa kutoka laana ya sheria kwa kufanyika laana kwa ajili yetu, kwa maana imeandikwa, “Amelaaniwa yeye aangikwaye juu ya mti.”
14 That the blessing of Abraham might come on the Gentiles through Christ Iesus, that wee might receiue the promise of the Spirite through faith.
Alitukomboa ili kwamba baraka aliyopewa Abrahamu ipate kuwafikia watu wa Mataifa kwa njia ya Kristo Yesu, ili kwa imani tupate kupokea ile ahadi ya Roho.
15 Brethren, I speake as men do: though it be but a mans couenant, when it is confirmed, yet no man doeth abrogate it, or addeth any thing thereto.
Ndugu zangu, nataka nitoe mfano kutoka maisha ya kila siku. Kama vile hakuna mtu awezaye kutangua au kuongeza kitu katika agano la mtu ambalo limekwisha kuthibitishwa, vivyo hivyo kwa hali kama hii.
16 Nowe to Abraham and his seede were the promises made. Hee saith not, And to the seedes, as speaking of many: but, And to thy seede, as of one, which is Christ.
Ahadi zilinenwa kwa Abrahamu na kwa mzao wake. Maandiko hayasemi “kwa wazao,” likimaanisha watu wengi, bali “kwa mzao wako,” yaani mtu mmoja, ndiye Kristo.
17 And this I say, that the couenant that was confirmed afore of God in respect of Christ, the Lawe which was foure hundreth and thirtie yeeres after, can not disanull, that it shoulde make the promise of none effect.
Ninachotaka kusema ni kwamba, sheria, ambayo ilitolewa miaka 430 baadaye, haitangui Agano lililothibitishwa na Mungu ili kuibatilisha ahadi ile.
18 For if the inheritance be of the Lawe, it is no more by the promise, but God gaue it freely vnto Abraham by promise.
Kwa maana kama urithi hupatikana kwa sheria, basi hautegemei tena ahadi, lakini Mungu kwa neema yake alimpa Abrahamu urithi kwa njia ya ahadi.
19 Wherefore then serueth the Law? It was added because of the transgressions, til the seed came, vnto the which the promise was made: and it was ordeined by Angels in the hande of a Mediatour.
Kwa nini basi iwepo sheria? Sheria iliwekwa kwa sababu ya makosa mpaka atakapokuja yule Mzao wa Abrahamu, ambaye alitajwa katika ile ahadi. Sheria iliamriwa na malaika kwa mkono wa mpatanishi.
20 Nowe a Mediatour is not a Mediatour of one: but God is one.
Basi mpatanishi huhusisha zaidi ya upande mmoja, lakini Mungu ni mmoja.
21 Is the Lawe then against the promises of God? God forbid: For if there had bene a Lawe giuen which coulde haue giuen life, surely righteousnes should haue bene by the Lawe.
Je basi, sheria inapingana na ahadi za Mungu? La hasha! Kwa maana kama sheria iliyotolewa ingeweza kuwapa watu uzima, basi haki ingepatikana kwa njia ya sheria.
22 But the Scripture hath concluded all vnder sinne, that the promise by the faith of Iesus Christ should be giuen to them that beleeue.
Lakini Maandiko yamefanya vitu vyote vifungwe chini ya nguvu ya dhambi, ili yale yaliyoahidiwa kwa njia ya imani katika Yesu Kristo yapate kupewa wale wanaoamini.
23 But before faith came, we were kept vnder the Law, as vnder a garison, and shut vp vnto that faith, which should afterward be reueiled.
Kabla imani hii haijaja tulikuwa tumewekwa chini ya sheria, tumefungwa mpaka ile imani ifunuliwe.
24 Wherefore the Lawe was our scholemaster to bring vs to Christ, that we might be made righteous by faith.
Hivyo, sheria ilikuwa kiongozi kutufikisha kwa Kristo, ili tupate kuhesabiwa haki kwa imani.
25 But after that faith is come, we are no longer vnder a scholemaster.
Lakini sasa kwa kuwa ile imani imekuja, hatusimamiwi tena na sheria.
26 For ye are al the sonnes of God by faith, in Christ Iesus.
Kwa maana ninyi nyote mmekuwa watoto wa Mungu katika Kristo Yesu kwa njia ya imani.
27 For all ye that are baptized into Christ, haue put on Christ.
Kwa maana wote mliobatizwa ndani ya Kristo, mmemvaa Kristo.
28 There is neither Iewe nor Grecian: there is neither bonde nor free: there is neither male nor female: for ye are all one in Christ Iesus.
Wala hakuna tena Myahudi au Myunani, mtumwa au mtu huru, mwanaume wala mwanamke, maana nyote mmekuwa wamoja ndani ya Kristo Yesu.
29 And if ye be Christes, then are ye Abrahams seede, and heires by promise.
Nanyi mkiwa ni mali ya Kristo, basi ninyi ni wa uzao wa Abrahamu na warithi sawasawa na ile ahadi.