< Ezekiel 43 >

1 Afterward he brought me to the gate, euen the gate that turneth towarde the East.
Yule mtu kisha akanileta hata kwenye lango lililokuwa linaelekea mashariki.
2 And beholde, the glorie of the God of Israel came from out of the East, whose voyce was like a noyse of great waters, and the earth was made light with his glorie.
Tazama! Utukufu wa Mungu wa Israeli ukaja kutoka mashariki; sauti yake ilikuwa kama sauti ya maji mengi, na nchi iling'aa kwa utukufu wake.
3 And the vision which I saw was like the vision, euen as the vision that I sawe when I came to destroy the citie: and the visions were like the vision that I sawe by the riuer Chebar: and I fell vpon my face.
Yalikuwa yanalingana na sura ya ono nililolona, kulingana na ono nililokuwa nimeliona wakati alipokuja kuuteketeza mji, na maono yalikuwa kama maono ambayo niliyokuwa nimeyaona Keberi Kanali nikaanguka kifudi fudi.
4 And the glorie of the Lord came into the house by the way of the gate, whose prospect is towarde the East.
Hivyo utukufu wa Yahwe ukaja kwenye nyumba ya karibu na njia ya lango lililokuwa wazi kwa upande wa magharibi.
5 So the Spirite tooke me vp and brought me into the inner court, and beholde, the glorie of the Lord filled the house.
Kisha Roho akanichukua na kunileta kwenye ua wa ndanni. Tazama! Utukufu wa Yahwe ulikuwa umeijaza nyumba.
6 And I heard one speaking vnto me out of the house: and there stoode a man by me,
Mtu alisimama karibu na mimi, na nikamsikia mtu mwingine akizungumza na mimi kutoka kwenye nyumba.
7 Which saide vnto me, Sonne of man, this place is my throne, and the place of the soles of my feete, whereas I will dwell among the children of Israel for euer, and the house of Israel shall no more defile mine holy Name, neither they, nor their Kings by their fornication, nor by the carkeises of their Kings in their high places.
Akanambia, “Mwanadamu, hapa ndipo mahali pangu pa enzi na mahali kwa ajili ya ya miguu yangu, ambapo nitaishi kati ya watu wa Israeli milele. Nyumba ya Israeli haitalikufuru tena jina langu takatifu-wao au wafalme wao katika mahali patakatifu pao.
8 Albeit they set their thresholdes by my thresholdes, and their postes by my postes (for there was but a wall betweene me and them) yet haue they defiled mine holy Name with their abominations, that they haue committed: wherfore I haue consumed them in my wrath.
Hawatalikufuru tena jina langu takatifu kwa kuweka kizingiti chao karibu na kizingiti changu, na nguzo yao ya lango karibu na nguzo yangu ya lango, bila kitu lakini ukuta kati yangu na wao. Wamelikufuru jina langu kwa matendo yao machafu, hivyo nimewala kwa hasira yangu.
9 Now therefore let them put away their fornication, and the carkeises of their Kings farre from me, and I will dwell among them for euer.
Sasa waache waondoe udanganyifu wao na maiti za wafalme wao kutoka kwangu, na nitaishi katikati yao milele.
10 Thou sonne of man, shew this House to the house of Israel, that they may be ashamed of their wickednes, and let them measure ye paterne.
Mwanadamu, wewe mwenyewe utaiambia nyumba ya Israeli kuhusu nyumba hii hivyo watajiskia aibu ya uovu wao. Wanaweza kutafakari kuhusu haya maelezo.
11 And if they be ashamed of all that they haue done, shew them the forme of the House, and ye paterne thereof, and the going out thereof, and the coming in thereof, and the whole fashion thereof, and all the ordinances thereof, and all the figures thereof, and all the lawes thereof: and write it in their sight, that they may keepe the whole fashion thereof, and all the ordinances thereof, and do them.
Kwa kuwa wameaibika kwa yote waliyoyafanya, kisha waonyeshe mchoro wa nyumba, maelezo yake, matokeo yake, maingio yake, na mchoro wake, sheria zake zote na kanuni. Kisha andika hivi chini mbele ya macho yao ili waweze kutunza michoro yote na kanuni zake zote, hivyo kama wazitiivo.
12 This is the description of the house, It shalbe vpon the toppe of the mount: all the limites thereof round about shalbe most holy. Beholde, this is the description of the house.
Hii ndiyo sheria kwa ajili ya nyumba: Kutoka kwenye kilele cha mlima hata mpaka wote unaoizunguka, patakuwa patakatifu sana. Tazama! Hii ndiyo sheria kwa ajili ya nyumba.
13 And these are the measures of the Altar, after the cubites, the cubite is a cubite, and an had breadth, euen the bottome shalbe a cubite, and the breadth a cubite, and the border thereof by the edge thereof rounde about shalbe a spanne: and this shalbe the height of the altar.
Hivi vitakuwa vipimo vya madhabahu katika dhiraa-hiyo dhiraa kuwa dhiraa ya kawaida na urefu wa kiganja. Hivyo mfereji ulio uzunguka madhabahu utakuwa dhiraa moja chini, na upana wake pia utakuwa dhiraa moja. Mpaka wa karibu uizungukayo machinjio shubiri moja. Hii itakuwa kitako cha madhabahu.
14 And from the bottome which toucheth the ground to the lower piece shalbe two cubites: and the breadth one cubite, and from the litle piece to the great piece shalbe foure cubites, and the breadth one cubite.
Usawa wa kutoka kwenye mferji hadi kwenye machinijo ya chini ya madhabahu itakuwa dhiraa mbili, na hiyo machinjio yenyewe itakuwa dhiraa moja upana. Kisha kutoka machinjio madogo hadi kwenye machinjio makubwa ya madhabahu, itakuwa dhiraa nne, na machinjio makubwa yatakuwa dhraa moja upana.
15 So the altar shalbe foure cubites, and from the altar vpward shalbe foure hornes.
Meko juu ya madhabahu kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa ni dhiraa nne juu, na kuna pembe nne zilizoelekea juu kwenye meku.
16 And the altar shalbe twelue cubites long, and twelue broade, and fouresquare in the foure corners thereof.
Meku ina dhiraa kumi na moja urefu na dhiraa kumi na mbili upana, za mraba.
17 And ye frame shalbe foureteene cubites log, and fourteene broade in the fouresquare corners thereof, and the border about it shalbe halfe a cubite, and the bottome therof shalbe a cubite about, and the steps thereof shalbe turned towarde ye East.
Mpaka wake ni dhiraa kumi na nne urefu na dhiraa kumi na nne upana pande zake zote nne, na ukingo wake ni nusu dhiraa upana. Mfereji ni dhiraa moja upana kuzuka kote pamoja na ngazi zielekeazo mashariki.”
18 And he said vnto me, Sone of man, thus saith ye Lord God, These are ye ordinances of ye altar in the day when they shall make it to offer the burnt offring thereon, and to sprinkle blood thereon.
Kisha akanambia, “Mwanadamu, Bwana Yahwe asema hivi: Hizi ndizo sheria kwa ajili ya madhabahu katika siku watakayoitengeza, kwa ajili kutoa sadaka ya kuteketezwa kwenye hiyo, na kwa jili ya kunyunyiza damu juu yake.
19 And thou shalt giue to the Priestes, and to the Leuites, that be of the seede of Zadok, which approch vnto me, to minister vnto me, saith the Lord God, a yong bullocke for a sinne offring.
Utatoa ng'ombe kutoka kwenye kundi kama sadaka ya dhambi kwa ajili ya Walawi makuhani ambao ni uzao wa Zadoki, wale wajao karibu nami kunitumikia-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
20 And thou shalt take of the blood thereof, and put it on the foure hornes of it, and on the foure corners of the frame, and vpon the border round about: thus shalt thou clense it, and reconcile it.
Kisha utachukua baadhi ya damu yake na kuiweka juu pembe nne za madhabahu na pande nne za machinjio na kuuzunguka ukingo; utaitakasa na kufanya upatanisho kwa ajili yake.
21 Thou shalt take the bullocke also of the sinne offring, and burne it in the appointed place of the house without the Sanctuarie.
Kisha chukua ng'ombe kama sadaka ya dhambi na iteketezwe katika eneneo lililotengwa la nje ya patakatifu.
22 But the second day thou shalt offer an hee goat without blemish for a sinne offring, and they shall clense ye altar, as they did clense it with the bullocke.
Kisha katika siku ya pili utatoa mbuzi dume asiyekuwa na dosari kutoka kundini kama sadaka ya dhambi; makuhani wataisafisha madhabahu kama walivyoisafisha kwa ng'ombe.
23 When thou hast made an ende of clensing it, thou shalt offer a yong bullocke without blemish, and a ram out of the flocke without blemish.
Utakapomaliza kusafisha, toa ng'ombe asiyekuwa na dosari kutoka kwenye mifugo na kondoo dume asiyekuwa na dosari kutoka kundini.
24 And thou shalt offer them before ye Lord, and the Priestes shall cast salt vpon them, and they shall offer them for a burnt offring vnto ye Lord.
Watoe mbele ya Yahwe; makuhani watanyunyiza chumvi juu yao na kuwainua juu kama sadaka ya kutekezwa kwa Yahwe.
25 Seuen dayes shalt thou prepare euery day an hee goate for a sinne offring: they shall also prepare a yong bullocke and a ramme out of the flocke, without blemish.
Utaandaa mbuzi dume kama sadaka ya dhambi kila siku kwa mda wa siku saba, na makuhani pia wataandaa ng'ombe asiye na dosari kutoka kwenye kundi na kondoo dume kutoka kwenye kundi.
26 Thus shall they seuen dayes purifie the altar, and clense it, and consecrate it.
Wataipatanisha madhabahu kwa siku saba na kuitakasa, wataitakasa kwa njia hii.
27 And when these dayes are expired, vpon the eight day and so forth, the Priests shall make your burnt offrings vpon the altar, and your peace offrings, and I will accept you, saith the Lord God.
Watamaliza hizi siku saba, na katika siku ya nane na kuendelea itakuwa kwamba makuhani wataandaa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani kwenye madhabahu, ndipo nitakapowakubali-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”

< Ezekiel 43 >