< Ezekiel 26 >

1 And in the eleuenth yeere, in the first day of the moneth, the worde of the Lord came vnto me, saying,
Hivyo ilikuwa katika mwaka wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 Sonne of man, because that Tyrus hath said against Ierusalem, Aha, the gate of the people is broken: it is turned vnto me: for seeing she is desolate, I shall be replenished,
“Mwanadamu, kwa sababu Tiro amesema juu ya Yerusalemuu, 'Aha! Malango ya watu waliovunjika! Amenigeukia; Nitajazwa kwa sababu ameharibika.'
3 Therefore thus sayth the Lord God, Beholde, I come against thee, O Tyrus, and I will bring vp many nations against thee, as the sea mounteth vp with his waues.
Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, 'Tazama! Niko juu yako, Tiro, na nitayainua mataifa mengi juu yako kama bahari iiunuavyo mawimbi yake.
4 And they shall destroy the walles of Tyrus and breake downe her towres: I will also scrape her dust from her, and make her like the top of a rocke.
Wataziharibu kuta za Tiro na kuiangusha chini minara yao. Nitafagia mavumbi yake mbali na kumfanya kama jiwe tupu.
5 Thou shalt be for the spreading of nettes in the middes of the sea: for I haue spoken it, sayth the Lord God, and it shalbe a spoile to ye nations.
Atakuwa sehemu ya kuwekea nyavu kati ya bahari, kwa kuwa nimesema hilo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-na atakuwa mateka kwa ajili ya mataifa.
6 And her daughters which are in the fielde, shall be slaine by the sworde, and they shall know that I am the Lord.
Binti zake walioko mashambani watachinjwa kwa panga, na watajua kwamba mimi ni Yahwe.'
7 For thus sayth the Lord God, Behold, I will bring vpon Tyrus Nebuchad-nezzar King of Babel, a King of Kings from the North, with horses and with charets, and with horsemen, with a multitude and much people.
Kwa kuwa hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Tazama, kutoka kaskazini namleta Nebukadreza mfalme wa Babeli, mfalme wa wafalme, dhidi ya Tiro, pamoja na farasi na magari ya farasi, na pamoja na waendesha farasi na watu wengi.
8 He shall slay with the sword thy daughters in the fielde, and he shall make a fort against thee, and cast a mount against thee, and lift vp the buckler against thee.
Atawaua binti zako katika shamba. Ataweka kazi ya boma na kujenga ulaghai dhidi ya kuta zako na kuziinua ngao dhidi yao.
9 He shall set engins of warre before him against thy walles, and with his weapons breake downe thy towres.
Ataweka vyombo vya kubomolea dhidi ya kuta zako, na vyombo vyake vitaanguka chini ya minara yako.
10 The dust of his horses shall couer thee, for their multitude: thy walles shall shake at the noise of the horsemen, and of the wheeles, and of the charets, when he shall enter into thy gates as into the entrie of a citie that is broken downe.
Farasi zake zitakuwa nyingi kwamba mavumbi yao yatawafunika. Kuta zako zitatikisika kwa mlio wa waendesha farasi, magurudumu, na magari ya farasi. Wakati atakapoingia malango yako, ataingia kama watu waingiavyo kwenye mji ambao kuta zimebomolewa.
11 With the hooues of his horses shall he treade downe all thy streetes: he shall slay thy people by the sworde, and the pillars of thy strength shall fall downe to the ground.
Kwato za farasi zake zitaikanyaga mitaa yako yote. Atawaua watu wako kwa upanga na nguzo za uweza wako zitaanguka chini.
12 And they shall robbe thy riches, and spoyle thy marchandise, and they shall breake downe thy walles, and destroy thy pleasant houses, and they shall cast thy stones and thy timber and thy dust into the middes of the water.
Watauteka nyara utajiri wako na bidhaa iliyoporwa. Watabomoa kuta zako na kuziharibu nyumba zako za kifahari. Mawe yako, mbao zako, na kokoto watazitupa kwenye maji.
13 Thus will I cause the sounde of thy songs to cease, and the sound of thine harpes shall be no more heard.
Nitaikomesha sauti ya nyimbo zako. Sauti ya vinubi haitasikika tena.
14 I wil lay thee like the top of a rocke: thou shalt be for a spreading of nets: thou shalt be built no more: for I the Lord haue spoken it, sayth the Lord God.
Nitakufanya jiwe tupu, utakuwa mahali ambapo nyavu zitasambazwa kuzikausha. Hutajengwa tena, kwa kuwa mimi, Bwana Yahwe nimesema-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
15 Thus sayth the Lord God to Tyrus, Shall not the yles tremble at the sounde of thy fall? and at the crie of the wounded, when they shall be slaine and murthered in the middes of thee?
Bwana Yahwe amwambia hivi Tiro, 'Je visiwa havitatetemeka kwa mlio wa kuanguka kwako, na pamoja na watakaogumia kwa jeraha wakati machinjio mabaya yatakapokuwa kati yako?
16 Then all the princes of the sea shall come downe from their thrones: they shall lay away their robes, and put off their broydered garments, and shall clothe themselues with astonishment: they shall sitte vpon the ground, and be astonished at euery moment, and be amased at thee.
Kisha wakuu wote wa bahari watakaposhuka kutoka kwenye viti vyao vya enzi na kuvua mavazi yao rasmi na kutupa mavazi yaliyonakshiwa. Watavaa wenyewe kwa kutetemeka, wataketi chini na kutetemeka kila wakati, na wataogopa kwa sababu yako.
17 And they shall take vp a lamentation for thee, and say to thee, Howe art thou destroyed, that wast inhabited of the sea men, the renoumed citie which was strong in the sea, both she and her inhabitants, which cause their feare to be on all that haunt therein!
Watainua maombolezo juu yako na kukwambia, umekuwaje, uliyekuwa umekaliwa na manahodha wa meli, umeharibika. Mji mashuhuri ulikuwa imara sana-sasa umetoka kwenye bahari. Wale wanaoishi ndani yake wanaotia hofu kuhusu wenyewe juu ya kila mmoja aliyeishi karibu nao.
18 Nowe shall the yles be astonished in the day of thy fall: yea, the yles that are in the sea, shall be troubled at thy departure.
Sasa fukwe zitatetemeka katika siku ya kuanguka kwako. Visiwa katika bahari vimeogofya, kwa sababu umekufa.'
19 For thus saith the Lord God, When I shall make thee a desolate citie, like ye cities that are not inhabited, and when I shall bring the deepe vpon thee, and great waters shall couer thee,
Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: wakati nitakapokufanya wewe mji kuwa ukiwa, kama miji mingine ambayo haikaliwi, wakati nitakapoviinua vilindi dhidi yako, na wakati maji makuu yatakapokufunika,
20 When I shall cast thee downe with them that descende into the pitte, with the people of olde time, and shall set thee in the lowe partes of the earth, like the olde ruines, with them, I say, which goe downe to the pitte, so that thou shalt not be inhabited, and I shall shewe my glory in the land of the liuing,
kisha nitakushusha chini kwenda kwa watu wa nyakati za zamani, kama wengingine walioenda chini kwenye shimo; kwa kuwa nitakufanya uishi katika falme za chini za dunia kama uharibifu wa nyakati za zamani. Kwa sababu hii hutarudi na kusimama katika nchi ya walio hai.
21 I will bring thee to nothing, and thou shalt be no more: though thou be sought for, yet shalt thou neuer be found againe, sayth the Lord God.
Nitaweka janga juu yako, na hutakuwepo tena milele. Kisha utatafutwa, lakini hutapatikana milele tena-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”

< Ezekiel 26 >