< Ezekiel 24 >

1 Again in the ninth yeere, in the tenth moneth, in the tenth day of the moneth, came the worde of the Lord vnto me, saying,
Katika mwaka wa tisa, mwezi wa kumi, siku ya kumi, neno la Bwana likanijia kusema:
2 Sonne of man, write thee the name of the day, euen of this same day: for the King of Babel set himselfe against Ierusalem this same day.
“Mwanadamu, weka kumbukumbu ya tarehe hii, tarehe hii hasa, kwa kuwa mfalme wa Babeli ameuzingira mji wa Yerusalemu kwa jeshi siku hii ya leo.
3 Therefore speake a parable vnto the rebellious house, and say vnto them, Thus sayth the Lord God, Prepare a pot, prepare it, and also powre water into it.
Iambie nyumba hii ya kuasi fumbo, na uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Teleka sufuria jikoni; iteleke na umimine maji ndani yake,
4 Gather the pieces thereof into it, euen euery good piece, as the thigh and the shoulder, and fill it with the chiefe bones.
Weka vipande vya nyama ndani yake, vipande vyote vizuri, vya paja na vya bega. Ijaze hiyo sufuria kwa mifupa hii mizuri;
5 Take one of the best sheepe, and burne also the bones vnder it, and make it boyle well, and seethe the bones of it therein,
chagua yule aliye bora wa kundi la kondoo. Panga kuni chini ya sufuria kwa ajili ya mifupa; chochea mpaka ichemke na uitokose hiyo mifupa ndani yake.
6 Because the Lord God sayth thus, Woe to the bloody citie, euen to the pot, whose skomme is therein, and whose skomme is not gone out of it: bring it out piece by piece: let no lot fall vpon it.
“‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ole wa mji umwagao damu, ole wa sufuria ambayo sasa ina ukoko ndani yake, ambayo ukoko wake hautoki. Kipakue kipande baada ya kipande, bila kuvipigia kura.
7 For her blood is in the middes of her: shee set it vpon an high rocke, and powred it not vpon on the ground to couer it with dust,
“‘Kwa kuwa damu aliyoimwaga ipo katikati yake: huyo mwanamke aliimwaga juu ya mwamba ulio wazi; hakuimwaga kwenye ardhi, ambako vumbi lingeifunika.
8 That it might cause wrath to arise, and take vengeance: euen I haue set her blood vpon an high rocke that it should not be couered.
Kuchochea ghadhabu na kulipiza kisasi, nimemwaga damu yake juu ya mwamba ulio wazi, ili isifunikwe.
9 Therefore thus saith ye Lord God, Woe to the bloody citie, for I will make ye burning great.
“‘Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ole wa mji umwagao damu! Mimi nami nitalundikia kuni nyingi.
10 Heape on much wood: kindle the fire, consume the flesh, and cast in spice, and let the bones be burnt.
Kwa hiyo lundika kuni na uwashe moto. Pika hiyo nyama vizuri, changanya viungo ndani yake, na uiache mifupa iungue kwenye moto.
11 Then set it emptie vpon the coles thereof, that the brasse of it may be hot, and may burne, and that the filthinesse of it may be molten in it, and that the skomme of it may be consumed.
Kisha teleka sufuria tupu kwenye makaa mpaka iwe na moto sana na shaba yake ingʼae, ili uchafu wake upate kuyeyuka na ukoko wake upate kuungua na kuondoka.
12 She hath wearied her selfe with lyes, and her great skomme went not out of her: therefore her skomme shall be consumed with fire.
Imezuia juhudi zote, ukoko wake mwingi haujaondoka, hata ikiwa ni kwa moto.
13 Thou remainest in thy filthines and wickednes: because I would haue purged thee, and thou wast not purged, thou shalt not be purged from thy filthines, till I haue caused my wrath to light vpon thee.
“‘Sasa uchafu wako ni uasherati wako. Kwa sababu nilijaribu kukutakasa lakini haikuwezekana kutakaswa kutoka kwenye huo uchafu wako, hutatakasika tena mpaka ghadhabu yangu dhidi yako iwe imepungua.
14 I the Lord haue spoken it: it shall come to passe, and I will doe it: I will not goe backe, neither will I spare, neither will I repent: according to thy wayes, and according to thy workes shall they iudge thee, sayeth the Lord God.
“‘Mimi Bwana nimesema, wakati umewadia wa mimi kutenda. Mimi sitazuia, mimi sitaona huruma wala sitapunguza hasira yangu, Utahukumiwa sawasawa na mwenendo na matendo yako, asema Bwana Mwenyezi.’”
15 Also the worde of ye Lord came vnto me, saying,
Neno la Bwana likanijia kusema:
16 Sonne of man beholde, I take away from thee the pleasure of thine eyes with a plague: yet shalt thou neither mourne nor weepe, neither shall thy teares runne downe.
“Mwanadamu, kwa pigo moja nakaribia kukuondolea kile kilicho furaha ya macho yako. Lakini usiomboleze au kulia wala kudondosha machozi yoyote.
17 Cease from sighing: make no mourning for the dead, and binde the tyre of thine head vpon thee, and put on thy shooes vpon thy feete, and couer not thy lips, and eate not the bread of men.
Lia kwa uchungu kimya kimya usimwombolezee mtu aliyekufa. Jifunge kilemba chako na uvae viatu vyako miguuni mwako, usifunike sehemu ya chini ya uso wako, wala usile vyakula vya kawaida vya wakati wa matanga.”
18 So I spake vnto the people in the morning, and at euen my wife dyed: and I did in the morning, as I was commanded.
Hivyo nikanena na watu asubuhi na jioni mke wangu akafa. Asubuhi yake nilifanya kama nilivyoamriwa.
19 And the people said vnto me, Wilt thou not tell vs what these things meane towarde vs that thou doest so?
Ndipo watu wakaniuliza, “Je, jambo hili unalofanya linamaanisha nini kwetu?”
20 Then I answered them, The worde of the Lord came vnto me, saying,
Kwa hiyo nikawaambia, “Neno la Bwana lilinijia kusema:
21 Speake vnto the house of Israel, Thus sayth the Lord God, Behold, I will pollute my Sanctuarie, euen the pride of your power, the pleasure of your eyes, and your hearts desire, and your sonnes, and your daughters whom ye haue left, shall fall by the sworde.
‘Sema na nyumba ya Israeli. Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninakaribia kupatia unajisi mahali pangu patakatifu, ngome ambayo ndani yake mnaona fahari, furaha ya macho yenu, kitu mnachokipenda. Wana wenu na binti zenu mliowaacha nyuma wataanguka kwa upanga.
22 And ye shall doe as I haue done: ye shall not couer your lippes, neither shall ye eate the bread of men.
Nanyi mtafanya kama nilivyofanya. Hamtafunika sehemu ya chini ya nyuso zenu wala hamtakula vyakula vya kawaida vya waombolezaji.
23 And your tyre shalbe vpon your heads, and your shooes vpon your feete: ye shall not mourne nor weepe, but ye shall pine away for your iniquities, and mourne one toward another.
Mtajifunga vilemba vichwani mwenu na kuvaa viatu vyenu miguuni mwenu. Hamtaomboleza au kulia, lakini mtadhoofika kwa sababu ya dhambi zenu na kulia kwa uchungu kila mtu na mwenzake.
24 Thus Ezekiel is vnto you a signe: according to all that he hath done, ye shall do: and when this commeth, ye shall know that I am the Lord God.
Ezekieli atakuwa ishara kwenu, mtafanya kama yeye alivyofanya. Wakati jambo hili litakapotokea, mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.’
25 Also, thou sonne of man, shall it not be in the day when I take from them their power, ye ioy of their honor, ye pleasure of their eyes, and the desire of their heart, their sonnes and their daughters?
“Nawe, mwanadamu, siku ile nitakapoondoa ngome yao iliyo furaha yao na utukufu wao, kitu cha kupendeza macho yao, kile kilicho shauku ya mioyo yao, wana wao na binti zao vilevile,
26 That he that escapeth in that day, shall come vnto thee to tell thee that which hee hath heard with his eares?
siku hiyo atakayetoroka atakuja kuwapasha habari.
27 In that day shall thy mouth be opened to him which is escaped, and thou shalt speake, and be no more dumme, and thou shalt be a signe vnto them, and they shall knowe that I am the Lord.
Katika siku ile kinywa chako kitamfumbukia yeye aliyenusurika, nawe utaongea wala hutanyamaza tena. Hivyo wewe utakuwa ishara kwao, nao watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.”

< Ezekiel 24 >