< Ezekiel 21 >
1 The word of ye Lord came to me againe, saying,
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 Sonne of man, set thy face toward Ierusalem, and drop thy word toward the holy places, and prophecie against the land of Israel.
“Mwanadamu, uelekeze uso wako juu ya Yerusalemu na uhubiri dhidi ya mahali patakatifu. Tabiri dhidi ya nchi ya Israeli
3 And say to the land of Israel, Thus saith the Lord, Beholde, I come against thee, and will drawe my sword out of his sheath, and cut off from thee both the righteous and the wicked.
uiambie: ‘Hili ndilo Bwana asemalo: Mimi niko kinyume nawe. Nitautoa upanga wangu kwenye ala yake na kumkatilia mbali mwenye haki na mwovu.
4 Seeing then that I will cut off from thee both the righteous and wicked, therefore shall my sworde goe out of his sheath against all flesh from the South to the North,
Kwa sababu nitamkatilia mbali mwenye haki na mwovu, upanga wangu utakuwa wazi dhidi ya kila mmoja kuanzia kusini mpaka kaskazini.
5 That all flesh may knowe that I the Lord haue drawen my sworde out of his sheath, and it shall not returne any more.
Ndipo watu wote watajua ya kuwa Mimi Bwana nimeutoa upanga wangu kwenye ala yake, nao hautarudi humo tena.’
6 Mourne therefore, thou sonne of man, as in the paine of thy reines, and mourne bitterly before them.
“Kwa hiyo lia kwa uchungu, mwanadamu! Lia kwa uchungu mbele yao kwa moyo uliopondeka na kwa huzuni nyingi.
7 And if they say vnto thee, Wherefore mournest thou? then answere, Because of the bruite: for it commeth, and euery heart shall melt, and all handes shall be weake, and all mindes shall faint, and all knees shall fall away as water: beholde, it commeth, and shall be done, saith the Lord God.
Nao watakapokuuliza, ‘Kwa nini unalia kwa uchungu?’ Utasema hivi, ‘Kwa sababu ya habari zinazokuja. Kila moyo utayeyuka na kila mkono utalegea, kila roho itazimia na kila goti litalegea kama maji.’ Habari hizo zinakuja! Hakika zitatokea, asema Bwana Mwenyezi.”
8 Againe, the word of the Lord came vnto me, saying,
Neno la Bwana likanijia, kusema:
9 Sonne of man, prophecie, and say, Thus saith the Lord God, say, A sworde, a sworde both sharpe, and fourbished.
“Mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: “‘Upanga, upanga, ulionolewa na kusuguliwa:
10 It is sharpened to make a sore slaughter, and it is fourbished that it may glitter: how shall we reioyce? for it contemneth the rod of my sonne, as all other trees.
umenolewa kwa ajili ya mauaji, umesuguliwa ili ungʼae kama umeme wa radi! “‘Je, tuifurahie fimbo ya utawala ya mwanangu Yuda? Upanga unaidharau kila fimbo ya namna hiyo.
11 And he hath giuen it to be fourbished, that he may handle it: this sword is sharpe, and is fourbished, that he may giue it into ye hand of the slayer.
“‘Upanga umewekwa tayari ili kusuguliwa, ili upate kushikwa mkononi, umenolewa na kusuguliwa, umewekwa tayari kwa mkono wa muuaji.
12 Cry, and houle, sonne of man: for this shall come to my people, and it shall come vnto all the princes of Israel: the terrours of the sword shall be vpon my people: smite therefore vpon thy thigh.
Piga kelele na uomboleze, ee mwanadamu, kwa kuwa upanga u dhidi ya watu wangu; u dhidi ya wakuu wote wa Israeli. Wametolewa wauawe kwa upanga pamoja na watu wangu. Kwa hiyo pigapiga kifua chako.
13 For it is a triall, and what shall this be, if the sworde contemne euen the rodde? It shall be no more, saith the Lord God.
“‘Kwa maana upanga huu umejaribiwa na kuhakikishwa, itakuwaje basi fimbo ya ufalme ya Yuda inayoudharau kama haitakuwepo tena, bali itakuwa imeondolewa kabisa? asema Bwana Mwenyezi.’
14 Thou therefore, sonne of man, prophecie, and smite hand to hand, and let the sworde be doubled: let the sworde that hath killed, returne the third time: it is the sword of the great slaughter entring into their priuie chambers.
“Hivyo basi, mwanadamu, tabiri na ukapige makofi. Upanga wako na upige mara mbili, naam, hata mara tatu. Ni upanga wa kuchinja, upanga wa mauaji makuu, ukiwashambulia kutoka kila upande.
15 I haue brought the feare of the sword into all their gates to make their heart to faint, and to multiplie their ruines. Ah it is made bright, and it is dressed for the slaughter.
Ili mioyo ipate kuyeyuka na wanaouawa wawe wengi, nimeweka upanga wa kuchinja kwenye malango yao yote. Lo! Umetengenezwa umetemete kama umeme wa radi, umeshikwa kwa ajili ya kuua.
16 Get thee alone: goe to the right hande, or get thy selfe to the left hande, whithersoeuer thy face turneth.
Ee upanga, kata upande wa kuume, kisha upande wa kushoto, mahali popote makali yako yatakapoelekezwa.
17 I wil also smite mine hands together, and wil cause my wrath to cease. I the Lord haue said it.
Mimi nami nitapiga makofi, nayo ghadhabu yangu itapungua. Mimi Bwana nimesema.”
18 The worde of the Lord came vnto mee againe, saying,
Neno la Bwana likanijia kusema:
19 Also thou sonne of man, appoint thee two wayes, that the sworde of the King of Babel may come: both twaine shall come out of one lande, and chuse a place, and chuse it in the corner of the way of the citie.
“Mwanadamu, weka alama njia mbili ambazo upanga wa mfalme wa Babeli utapitia, njia hizo zikianzia katika nchi hiyo hiyo. Weka kibao pale ambapo njia zinagawanyika kuelekea mjini.
20 Appoint a way, that the sworde may come to Rabbath of the Ammonites, and to Iudah in Ierusalem the strong citie.
Weka alama njia moja kwa ajili ya upanga upate kuja dhidi ya Raba ya Waamoni na nyingine upate kuja dhidi ya Yuda na Yerusalemu iliyozungushiwa ngome.
21 And the King of Babel stoode at the parting of the way, at the head of the two wayes, consulting by diuination, and made his arrowes bright: hee consulted with idoles, and looked in the liuer.
Kwa kuwa mfalme wa Babeli sasa amesimama katika njia panda, katika makutano ya njia mbili, akipiga ramli: anapiga kura kwa kutumia mishale, anataka shauri kwa sanamu zake, anachunguza maini ya wanyama.
22 At his right hand was the diuination for Ierusalem to appoint captaines, to open their mouth in the slaughter, and to lift vp their voyce with shouting, to laye engines of warre against the gates, to cast a mount, and to builde a fortresse.
Upande wake wa kuume inakuja kura ya Yerusalemu, ambapo ataweka vyombo vya kuvunjia boma, ili kuamrisha mauaji, kupiga ukelele wa vita, kuweka vyombo vya kuvunjia boma kwenye malango, kuweka jeshi kuzunguka na kufanya uzingiraji.
23 And it shalbe vnto them as a false diuination in their sight for the othes made vnto them: but hee will call to remembrance their iniquitie, to the intent they should be taken.
Itakuwa kama kupiga ramli kwa uongo kwa wale watu ambao wameapa kumtii yeye. Lakini mfalme wa Babeli atawakumbusha juu ya uovu wao na kuwachukua mateka.
24 Therefore thus sayeth the Lord God, Because ye haue made your iniquitie to bee remembred, in discouering your rebellion, that in al your workes your sinnes might appeare: because, I say, that ye are come to remembrance, ye shall be taken with the hand.
“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: ‘Kwa sababu enyi watu mmekumbusha uovu wenu kwa kuasi waziwazi, mkidhihirisha dhambi zenu katika yale yote mfanyayo, kwa kuwa mmefanya jambo hili, mtachukuliwa mateka.
25 And thou prince of Israel polluted, and wicked, whose day is come, when iniquitie shall haue an ende,
“‘Ee mtawala kafiri na mwovu wa Israeli, ambaye siku yako imewadia, ambaye wakati wako wa adhabu umefikia kilele chake,
26 Thus saith the Lord God, I will take away the diademe, and take off the crowne: this shalbe no more the same: I wil exalt the humble, and will abase him that is hie.
hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Vua kilemba, ondoa taji. Kwa kuwa mambo hayatakuwa kama yalivyokuwa. Aliye mnyonge atakwezwa na aliyekwezwa atashushwa.
27 I wil ouerturne, ouerturne, ouerturne it, and it shall be no more vntill he come, whose right it is, and I will giue it him.
Mahame! Mahame! Nitaufanya mji kuwa mahame! Hautajengwa upya mpaka aje yule ambaye ndiye mwenye haki nao; yeye ndiye nitakayempa.’
28 And thou, sonne of man, prophecie, and say, Thus saith the Lord God to the children of Ammon, and to their blasphemie: say thou, I say, The sword, the sword is drawen foorth, and fourbished to the slaughter, to consume, because of the glittering:
“Nawe, mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kuhusu Waamoni na matukano yao. “‘Upanga, upanga, umefutwa kwa ajili ya kuua, umesuguliwa ili kuangamiza na unametameta kama umeme wa radi!
29 Whiles they see vanitie vnto thee, and prophecied a lie vnto thee to bring thee vpon the neckes of the wicked that are slaine, whose day is come when their iniquitie shall haue an ende.
Wakati wakitoa maono ya uongo kwa ajili yako, wanapobashiri uongo kwa ajili yako, wanakuweka wewe kwenye shingo za watu wapotovu, wale walio waovu, wale ambao siku yao imewadia, wakati wa adhabu yao ya mwisho.
30 Shall I cause it to returne into his sheath? I will iudge thee in the place where thou wast created, euen in the land of thine habitation.
Urudishe upanga kwenye ala yake! Katika mahali ulipoumbiwa, katika nchi ya baba zako, huko nitakuhukumu.
31 And I wil powre out mine indignation vpon thee, and will blowe against thee in the fire of my wrath, and deliuer thee into the hand of beastly men, and skilfull to destroy.
Nitamwaga ghadhabu yangu juu yako na kupuliza moto wa hasira yangu dhidi yako; nitakutia mikononi mwa watu wakatili, watu stadi katika kuangamiza.
32 Thou shalt bee in the fire to be deuoured: thy blood shall be in the middes of the lande, and thou shalt be no more remembred: for I the Lord haue spoken it.
Mtakuwa kuni za kuwashia moto, damu yenu itamwagwa katika nchi yenu, wala hamtakumbukwa tena; kwa maana Mimi Bwana nimesema.’”