< Ezekiel 17 >

1 And the worde of the Lord came vnto mee, saying,
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 Sonne of man, put foorth a parable and speake a prouerbe vnto the house of Israel,
“Mwanadamu, tega kitendawili, ukawaambie nyumba ya Israeli fumbo.
3 And say, Thus saith the Lord God, The great eagle with great wings, and long wings, and ful of fethers, which had diuers colours, came vnto Lebanon, and tooke the highest branch of the cedar,
Waambie hivi, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Tai mkubwa mwenye mabawa yenye nguvu, yaliyojaa manyoya marefu ya rangi mbalimbali, alikuja Lebanoni. Akatua kwenye kilele cha mwerezi,
4 And brake off the toppe of his twigge, and caried it into the land of marchants, and set it in a citie of marchants.
akakwanyua ncha yake na kuichukua mpaka nchi ya wafanyabiashara, akaipanda huko katika mji wa wachuuzi.
5 Hee tooke also of the seede of the lande, and planted it in a fruitfull ground: hee placed it by great waters, and set it as a willowe tree.
“‘Akachukua baadhi ya mbegu za nchi yako na kuziweka katika udongo wenye rutuba. Akazipanda kama mti umeao kando ya maji mengi,
6 And it budded vp, and was like a spreading vine of low stature, whose branches turned toward it, and the rootes thereof were vnder it: so it became a vine, and it brought foorth branches, and shot foorth buds.
nazo zikaota na kuwa mzabibu mfupi, unaoeneza matawi yake. Matawi yake yakamwelekea huyo tai, mizizi yake ikabaki chini ya huo mzabibu. Kwa hiyo ukawa mzabibu na kutoa matawi na vitawi vyenye majani mengi.
7 There was also another great eagle with great wings and many feathers, and beholde, this vine did turne her rootes toward it, and spred foorth her branches toward it, that she might water it by the trenches of her plantation.
“‘Lakini kulikuwa na tai mwingine mkubwa, mwenye mabawa yenye nguvu yaliyojaa manyoya. Tazama! Huu mzabibu ukatoa mizizi yake kumwelekea huyo tai kutoka mle kwenye shamba lile ulikopandwa na kutanda matawi yake kumwelekea kwa ajili ya kupata maji.
8 It was planted in a good soyle by great waters, that it should bring forth branches, and beare fruite, and be an excellent vine.
Ulikuwa umepandwa katika udongo mzuri wenye maji mengi ili uweze kutoa matawi, kuzaa matunda na uweze kuwa mzabibu mzuri sana.’
9 Say thou, Thus saith the Lord God, Shall it prosper? shall he not pull vp the rootes thereof, and destroy the fruite thereof, and cause them to drie? all the leaues of her bud shall wither without great power, or many people, to plucke it vp by the rootes thereof.
“Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Je, utastawi? Je, hautangʼolewa na kuondolewa matunda yake, ili uweze kunyauka? Majani yake mapya yanayochipua yote yatanyauka. Hautahitaji mkono wenye nguvu au watu wengi kuungʼoa na mizizi yake.
10 Beholde, it was planted: but shall it prosper? shall it not be dried vp, and wither? when the East winde shall touch it, it shall wither in the trenches, where it grewe.
Hata kama utapandwa pengine, Je, utastawi? Je, hautanyauka kabisa wakati upepo wa mashariki utakapoupiga, yaani, hautanyauka kabisa katika udongo mzuri ambamo ulikuwa umestawi vizuri?’”
11 Moreouer, the worde of the Lord came vnto me, saying,
Ndipo neno la Bwana likanijia kusema:
12 Say now to this rebellious house, Know ye not, what these things meane? tell them, Behold, the King of Babel is come to Ierusalem, and hath taken the King thereof, and the princes thereof, and led them with him to Babel,
“Waambie nyumba hii ya kuasi, ‘Je, mnajua hii ina maana gani?’ Waambie: ‘Mfalme wa Babeli alikwenda Yerusalemu na kumchukua mfalme na watu maarufu, akarudi nao na kuwaleta mpaka Babeli.
13 And hath taken one of the Kings seede, and made a couenant with him, and hath taken an othe of him: he hath also taken the princes of the land,
Ndipo akamchukua mmoja wa jamaa ya mfalme na kufanya mapatano naye, akamfanya aape. Akawachukua pia viongozi wa nchi,
14 That the kingdome might be in subiection, and not lift it selfe vp, but keepe their couenant, and stand to it.
ili kuudhoofisha ufalme huo, usiweze kuinuka tena, ila uweze kuendelea tu chini ya mapatano yake.
15 But he rebelled against him, and sent his ambassadours into Egypt, that they might giue him horses, and much people: shall hee prosper? shall he escape, that doeth such things? or shall he breake the couenant, and be deliuered?
Lakini mfalme aliasi dhidi yake kwa kutuma wajumbe wake kwenda Misri ili kupatiwa farasi na jeshi kubwa. Je, atashinda? Je, atafanikiwa? Je, mtu afanyaye mambo kama hayo ataokoka? Je, atavunja mapatano na bado aokoke?
16 As I liue, saith the Lord God, he shall die in the middes of Babel, in the place of the King, that had made him King, whose othe he despised, and whose couenant made with him, he brake.
“‘Hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, atafia huko Babeli, katika nchi ya mfalme aliyemketisha katika kiti cha enzi, ambaye alidharau kiapo chake na kuvunja mapatano yake.
17 Neither shall Pharaoh with his mightie hoste, and great multitude of people, mainteine him in the warre, when they haue cast vp mounts, and builded ramparts to destroy many persons.
Farao na jeshi lake kubwa, na wingi wake wa watu hawataweza kusaidia chochote katika vita, wakati watakapozungukwa na jeshi ili kukatilia mbali maisha ya watu wengi.
18 For he hath despised the othe, and broken ye couenant (yet lo, he had giuen his hand) because he hath done all these things, he shall not escape.
Alidharau kiapo kwa kuvunja Agano. Kwa sababu aliahidi kwa mkono wake mwenyewe na bado akafanya mambo haya yote, hataokoka.
19 Therefore, thus sayth the Lord God, As I liue, I wil surely bring mine othe that he hath despised, and my couenant that he hath broken vpon his owne head.
“‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Hakika kama niishivyo, nitaleta juu ya kichwa chake kiapo changu, alichokidharau na Agano langu lile alilolivunja.
20 And I wil spread my net vpon him, and he shalbe taken in my net, and I wil bring him to Babel, and will enter into iudgement with him there for his trespas that he hath committed against me.
Nitautandaza wavu wangu kwa ajili yake, naye atanaswa katika mtego wangu. Nitamleta mpaka Babeli na kutekeleza hukumu juu yake huko kwa kuwa hakuwa mwaminifu kwangu.
21 And all that flee from him with all his hoste, shall fall by the sword, and they that remaine, shalbe scattered towarde all the windes: and ye shall know that I the Lord haue spoken it.
Askari wake wote wanaotoroka wataanguka kwa upanga, nao watakaonusurika watatawanyika katika pande zote za dunia. Ndipo utakapojua kuwa Mimi Bwana nimesema.
22 Thus saith the Lord God, I wil also take off the top of this hie cedar, and wil set it, and cut off the top of the tender plant thereof, and I wil plant it vpon an hie mountaine and great.
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi mwenyewe nitachukua chipukizi kutoka kwenye kilele cha juu sana cha mwerezi na kukipanda, nitavunja kitawi kichanga kutoka matawi yake ya juu kabisa na kukipanda juu ya mlima mrefu ulioinuka sana.
23 Euen in the hie mountaine of Israel will I plant it: and it shall bring forth boughes and beare fruite, and be an excellent cedar, and vnder it shall remaine all birds, and euery foule shall dwell in the shadow of the branches thereof.
Katika vilele vya mlima mrefu wa Israeli nitakipanda, kitatoa matawi na kuzaa matunda na kuwa mwerezi mzuri sana. Ndege wa kila aina wataweka viota vyao ndani yake, nao watapata makazi katika kivuli cha matawi yake.
24 And all the trees of the fielde shall knowe that I the Lord haue brought downe the hie tree, and exalted the lowe tree, that I haue dried vp the greene tree, and made the drie tree to florish: I the Lord haue spoken it, and haue done it.
Miti yote ya kondeni itajua kuwa Mimi Bwana ninaishusha miti mirefu na kuikuza miti mifupi kuwa miti mirefu. Mimi naikausha miti mibichi na kuifanya miti mikavu istawi. “‘Mimi Bwana nimesema, nami nitatenda.’”

< Ezekiel 17 >